Vijana someni Uuguzi, una fursa nyingi

"Nurse lazma afahamu tatizo LA mgonjwa na tiba yake " hapa haiko hivyo yaani huwa anaambiwa tu sio kudiagnose wala ku prescribe hio si kazi yake na wengi hawajui
 
"Nurse lazma afahamu tatizo LA mgonjwa na tiba yake " hapa haiko hivyo yaani huwa anaambiwa tu sio kudiagnose wala ku prescribe hio si kazi yake na wengi hawajui
Hapana mkuu hapo umeteleza, labda zamani lakini siku hizi.
1.Utakubaliana na Mimi nurse ndie anakaa na mgojwa muda mrefu kuliko daktari. Sasa anakaaje na mgonjwa Mwenye hypertension usiku mzima, halafu hajui hypertension ni nini?

2. Nurse huwa nao wanatoa elimu kwa jamii -anatoaje elimu kuhusiana na hypertension, au huwa wanamezeshwa nini?

Pengine hukunielewa. Nurse ni muhimu afahamu tatizo la mgonjwa na tiba yake, haimanishi kuwa nurse anaamua tiba ipi apewe mgonjwa.
 
OK atajua tu kwamba tumeadmit watu kadhaa huyu anasumbuliwa na nn na tumeambiwa tumpe dawa gan at which time na hapo hapo Hali ikibadilika wanakufuata mkuu,,, sasa sijui unazungumzia kujua kwa level ipi
 
Itabidi mtoa mada hii hoja aigeuze vise vasa ili kusudu watu wajadili vise vasa apate jibu analolitaka
 
Na nurse sio kijakazi wa MD maana naona ndo muelekeo wa jibu lako
As membe Nurse of health team, nurse ana body of knowledge, anatumia the five senses to assess his/her patient and come up with nursing diagnoses which need priorities of nursing interventions. Kwenye health team no discipline works entirely independently in isolation. There must be some points of interactions and dicasesions with other health disciplines. Kwenye hizi interaction points ndizo ambazo bwana mdogo anadhani a nurse will follow orders just because zimetolewa na dk, no discipline will follow other disciplines' orders if are not correct or needed in solving the patient's need. Nurse atakubaliana/anaafiki na maelezo ya dokta sio kufuata maagizo hata ya kijinga. Kwenye hii timu ya afya kila discipline imepewa nini cha kusomea na nini cha kufanya kwenye timu inayomzunguuka mgonjwa. Kama vile vile mchora ramani ya jengo anavyomkabidhi fundi washi ramani, na mwashi anavyomkabidhi mpauaji na mpauaji anavyomkabidhi fundi umeme na fundi umeme anavyomkabidhi fundi rangi jengo baada ya kumaliza kipande chache.

Sasa huyo dogo mvaa manati shingoni kwakuwa yeye anaanza kufanya kazi na kuwakabidhi wengine anadhani kuwa yeye ndiye wa maana kuliko wooote kwenye timu ya afya. Just nonsense like any other nonsense under the moon.
Slowly they will understandstand, unajua disciplines nyingine za afya zilichelewa Sana kuwa na graduates kwenye field compare to Medicine. Ndio maana walijiona kama vichuguu kwenye afya. But they will learn as we go up the hill when they find nurses doing their things scientifically, they drive, they do rearches, consultation works, build good houses, write books, take their children to good schools as they do or even more.
 
Ukitakujua nursing ni kipumbavu kwa tz we angalia qualification entire kwa nurse wa diploma harusiwi kusoma MD ila Co anaruhusiwa kusoma nursing wkt entrance za kusoma diploma na certificate ya nursing na clinical medicine zipo sawa

Kaka sio kweli kwa ulichosema...kozi zote za afya kwa ngazi ya diploma wanaruhusiwa kusoma kozi yoyote ya afya kwa ngazi ya bachelor (wanaita equivalent qualification) mfano...nurses anaweza soma md,,,laboratory & vice vers....kama unaitaji maelezo zaidi na evidence...njoo inbox
 
Sijui kwanin manurse huwa mnahasira hivi kama wewe,, nagombana Sana na ma nurse wangu shauri ya kunitukania wagonjwa wangu,,, Mzee kavulata fanya kazi bwana penda U nurse wako ila usidanganye kujicompare na Dr's
Natamani tungekutana siku moja halafu tuonyeshane namana kazi zetu zimesukuma mbele maisha yetu. Wewe kwavyovyote vile unaipata hela yako Kwa mateso makubwa sana ya kukosa kupunzika kwasababu ya kuzuukia vijiwe hata usiku wa manane hasa baada Mzee JPM kukaba mianya yote ya utoro.
 
Sijutii na siogopi,, usiku kwangu kama mchana toka advance na hata chuo soo kuhusu vijiwe ni kweli na hata kama na wewe unakijiwe ruksa
 
Unaongelea kipindi cha nyuma. Kwasasa kama wewe ni CO huwezi kufanya BPharm,BMLS.
 
Unaongelea kipindi cha nyuma. Kwasasa kama wewe ni CO huwezi kufanya BPharm,BMLS.

Jamaa una ham ya kubishana au unataka kuelewa
...zaman ya mwaka gani unayosema?
Mwaka jana kuna watu alisoma dploma ya uuguzi bachelor akasoma Md
Mwngne dipoloma ya maabara bachelor anasoma nursing
Mwaka huu:kuna nurse in service kachaguliwa bachelor ya maabara
 
Wacha ubishi wewe rudi katika TCU guidebook ujisahihishie mwenyeo
 
[emoji13] [emoji13] [emoji13] umevuta nadhan kasomee magar yako kama utaajiliwa ata mtaan
Mkuu akili yako bado Mgando Sana.

Nmesikitika sana kuona unashabikia kuajiliwa.

Binafsi,
Nachukulia kuajiliwa ni ukoloni mamboleo
 
Well said
 
Ni ukweli bila chenga kuwa uuguzi kote duniani ulichelewa sana kupata wahitimu wenye degree, masters na PhD. Uuguzi ulikuwa kazi ya maelekezo Tu. Udaktari Kwa muda mrefu sana ulichukua vijana werevu wenye matokeo mazuri darasani. Hivyo tangu zamani walikuwa na maprofesa wengi na watu wengi waliosoma Makerere, Uingereza, urusi, Israel, ujerumani, Italy na mwingine kwingi. Hii iliwafanya DK wawe juu kwenye sectors za afya kwakuwa ni kweli kabisa walikuwa na elimu na exposure kubwa kuliko wenzao wauguzi ambao wengi wao walikuwa darasa la saba na form IV failure. Hii ilisababisha hata viongozi wengi wa uuguzi kwenye ngazi zote wajione inferior mbele ya wenzao wa udaktari, ilikuwa vigumu kwao ku ague kwa vitu vingi hata vile vilivyowahusu wauguzi wenzao na uuguzi. Mbaya zaidi madaktari wengi walioa manesi, hii nayo ilizidi kuwafanya manesi wawaheshimu madk kama senior lakini kama waume na shemeji zao pia.

Hali hii ilisababisha vijana wenye elimu nzuri ya sayansi wengi wajiunge na udk na wauone udk ulikuwa mzuri kuliko uuguzi, na hata jamii iliamini hivyo. Kwasababu ya elimu kubwa hata kipato chao pia kilikuwa kikubwa kuliko kile cha wauguzi wasio na elimu, TNs.

Lakini mambo sasa ni tofauti, nyumbani kumenoga. Nurses sasa wanakijua kile wanachokifanya. Wanasoma na baadhi ya vile vilivyokuwa vinasomwa na MD tu. Wako manesi sasa wana degree, masters na PhD ingawa bado hawajakuwa wengi kama madk.

Baada ya kila mtoto na mzazi kutaka mtoto wake awe DK, sasa hivi vijana hao wamekuwa wengi mnooo kuliko mahitaji (saturated) baada ya vyuo vingi vya udk kufunguliwa na kuzalisha madk wengi kila mwaka. Hapa nchini tu viko vyuo vikuu vya aina hii visivyopungua 6 vinavyozalisha md 2500 kila mwaka. Hii inawafanya madk kuwaondolea ule u rare profession tena maana wapo wengi mitaani na serikari imeanza kuwapeleka kwenye vituo vya afya kabla ya kuwapeleka kwenye zahanati kule yaliko matatizo vya wananchi.

Baada ya huduma za jamii kuboreka, kupanda kwa hali za maisha, kuenea kwa preventive health services (chanjo, uzazi wa mpango, kondoms, nk) na elimu ya afya kuenea hivyo kusababisha magonjwa na wagonjwa kupungua wodini na kwenye jamii, nafasi ya udaktari nayo inazidi kuwa finyu kwakuwa magonjwa kama malaria, cholera, tb, STIs and other unhygienic diseases yanazidi kupungua kwenye jamii duniani kote. Hivyo why more dks?. Kunahitajika dk wachache Tu wenye ujuzi mkubwa kwaajili ya emergencies, na chronic non communicable diseases. Hata hapa nchini vijana walimaliza MD wakatafutiwa nafasi za waliogoma huko Kenya kuonyesha kuwa hakuna ulazima saaana wa watu hao.

Kinyume chake kutokana na nature ya kazi zao Wauguzi wanahitajika wengi Sana wodini, opd. kwenye research, mashuleni, viwandani, migodini, bandarini, jeshini, nyumba za wazee, labor ward, family planning clinics, kwenye chanjo, Kwa wakimbizi, kwenye kufundishia vyuoni, kwenye uongozi, kwenye uwandishi wa vitabu, na kwenye clinic na outreach mbalimbali. Nurses pia kama wengine wanaweza kuendesha maternity home care zao na kufanya biashara na kilimo kama wakitaka maana hawaendi kwenye viosk vya wahindi mchana kutwa kama kaka zao madk ambao usiku kucha na vimanati vyao shingoni, no time to rest with their families or even think outside the box. Kila wakati wanaongelea hadithi za wodini, wagonjwa, ccd, meconium hata wakiwa kwenye grocery za pombe na migahawa, hawana kingine wanafahamu na kusimulia isipokiwa wagonjwa hata kwenye mazishi.

Sio kwana ninasema udaktari haufai lahsha, ninachokisema kwenye uzi huu ni kwamba uuguzi unazo fursa nyingi kwenye kukabiliana na trend ya ukosefu wa ajira unaojitokeza duniani kote sasa hivi. Ni rahisi kijana kupata kazi akiwa muuguzi kuliko akiwa Dk. Washaurini watoto wenu kuhusu jambo hili. Isitoshe tafiti zinaonyesha kuwa Madk wa sasa wanafanyakazi kwa kiwango kama cha clinical officers, elimu imeshuka sana kutokana na sabababu mbalimbali zikiwemo zile za wanafunzi kuibia mitihani darasani, elimu ndogo/mbaya za shule za msingi na sekondari, idadi kubwa ya wanafunzi kuliko madarasa, walimu, sehemu ya mazoezi kwa vitendo na kushindwa kuhudhuria darasani kutokana na kushindwa kulipa ada.
 
Ha ha ha chief ulikosa chance hiyo nn maana unayoandika n ya kumpoteza alieko nje ya field,, chance bado zipo na hata private sector "vijiwe" bado saaana,,, kama huamin haya lete recommended Dr to population ratio,,,
 
Natamani niendelee na huu mchuano ila bhc ngoja niache.....kizur chajiuza kibaya chajitembeza.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…