Vijana wa Bodaboda na Bajaji wana matatizo gani?

Wanaacha mizigo sana kwa ndugu mahospitalini ajali zao ni za kutisha kwa kweli wengine hufikia hata hatua ya kupoteza kumbukumbu.

Hawa watoto wanatumia mihadarati inayopelekea kuchanganyikiwa wawepo barabarani?
Una hoja ya msingi sana hapa
 

Jana nilikuwa live usiku mzima, nikiaamka nitakujibu
 
Upatikanaji wa pikipiki umekuwa mrahisi, plus ni almost hawapewi adhabu yoyote na vyombo vya sheria, ndio maana akili hawatumii na wala hawaheshim sheria za barabarani
 
Siku hiz Barabara za mwendokasi ni za kwao bodaboda na bajaji hasa njia ya kimara

Hii nchi sijui tunaelekea wap
Hii Morogoro road kuanzia pale kimara stop over zinapoanzia njia nane kuelekea mpaka kibamba ni sehemu moja hatari mnoo, Watu wanafunguka mnoo afu hawa ndugu zetu boda na bajaji wala hawaogopi
 
Maafisa Usafirishaji
 
Kwa hakika ningelikuwa na mamlaka, ningepiga marufuku boda kufanya biashara ya abiria!
Hilo si suruhisho kwa sababu,kwa Tanzania,ukiangalia utakuta ndo usafili kila mtu anaouweza. Pia,msisahau. Wale vibaka(sio wote ni madereva),wapo wakipewa elfu 5 au 10,anakimbia nayo huku unae. Hao mnadhani wataenda wapi? Kuna wale wanaohitaji kugegeda wake zenu. Nao ukipiga marufuku,watageukia kusubiria watoto wenu njiani. Kuna wale wakuagizwa makahaba. Yatakuwa yanafikaje? Bado wana umhimu sana
 
Mkuu bodaboda kuwa usafiri ambao kila mtu anauweza means tumefali kama nchi, kwanini zisiwepo tram na trains ? Vijana wapewe ajira viwandani na iwekwe miundombinu mbadala

New York na majiji makubwa mengine usafiri wa binafsi ni Taxi
 
Dah jana roho ya kijana imetoeka maeneo ya Bora, Temeke pumzika pema ndugu yangu

Wewe dereva wa hitcher popote ulipo Mungu anakuona, umemgonga ndugu yangu ukamuacha anavuja damu puani na mdomoni ukasepa so painful
 
Mkuu bodaboda kuwa usafiri ambao kila mtu anauweza means tumefali kama nchi, kwanini zisiwepo tram na trains ? Vijana wapewe ajira viwandani na iwekwe miundombinu mbadala

New York na majiji makubwa mengine usafiri wa binafsi ni Taxi
Mkuu yaani unalinganisha Bongo na New York!
 
Mkuu bodaboda kuwa usafiri ambao kila mtu anauweza means tumefali kama nchi, kwanini zisiwepo tram na trains ? Vijana wapewe ajira viwandani na iwekwe miundombinu mbadala

New York na majiji makubwa mengine usafiri wa binafsi ni Taxi
Uzuri umedumbukiamo. Viongozi wangekuwa wanajielewa,hii nchi isingekuwa inalalamika kiasi hiki. Ukiongea na watu wanaofanya kazi viwandani,utasikitika. Bora huyo anaeendesha bodaboda. Viwandani wanapigishwa kazi kama punda,mda wanaotaka wenye viwanda,mshahara kiduchu.
Wasimamizi wasingekuwa majizi,wangeset mda na mshahara. Angalau mtu ajue alienda kufanya kazi kiwandani,familia inakula,kodi analipa,na hata kiwanja anaweza kununua.

Haya yote ni matokeo ya serikali zinazothamini wawekezaji kuliko wazawa.

Sema tu watu weusi ndo hivo hatujielewi. Ingewezekana viwandani hawa wote wanaohenyeshwa wakapiga kazi chini hata wiki tu. Nchi nzima. Af hiyo serikali iruhusu wenye viwanda,wawalete raia wao. Na cha ajabu,kuna watu wameletwa viwandani huko,hawafanyi kazi,eti ni supervisor. Mshahara wake,ni kama wa wabongo 100. Kwanza unajiuliza,serikali ilishindwa kununua mashine za kuendesha viwanda hivyo yenyewe? Je,ilishindwa kuingia hata ubia?
Hivyo vifo,huo ulemavu,serikali imechangia. Tena pakubwa.
 
Mkuu yaani unalinganisha Bongo na New York!
Mkuu kwani tunataka kwenda wapi ? Serikali yenyewe inalinganisha hivo kila siku na kuna watumishi wa serikali huwa wanaenda ulaya na america kujifunza mipango miji nk

Ukweli utabaki bodaboda inabidi tuzitoe kwenye majiji yetu watu watengenezewe mazingira ya bolt
 
Hii Morogoro road kuanzia pale kimara stop over zinapoanzia njia nane kuelekea mpaka kibamba ni sehemu moja hatari mnoo, Watu wanafunguka mnoo afu hawa ndugu zetu boda na bajaji wala hawaogopi
Bodaboda na bajaji zingepigwa marufuku kwenye highways zote.
Zifanye huko mitaani...

Bandarini ziongezewe kodi kubwa ili zisizidi kuongezeka nchini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…