Vijana wa HALAIKI huwa wananufaika na kipi baada ya mafunzo na shughuli ya kiserikali kupita?

Vijana wa HALAIKI huwa wananufaika na kipi baada ya mafunzo na shughuli ya kiserikali kupita?

Vyeti wavipeleke wapi ? Waende kuombea kazi au kutambulika ili iweje ka tukio kenyewe ni kadogo sana. Sasa mtu si atajikuta ana vyeti 200. Cheti kitolewe kwenye kitu ambacho ni outstanding siyo hiyo michezo ambayo kila mtu anaweza kufanya. Siku hizi hata vyeti vya computer hizi basic skills Kama word na excel havitumiki tena sembuse hiyo michezo

Ma tukio ya namna hii ni mengi mno nchini hata simba day na Yanga say yanafanyika tena kutumia watoto au vijana hao hao kutoka mashule mbali mbali . Vyeti hapo ni unnecessary
Hayo matukio ya simba na yanga huandaliwa miezi mitatu?
Naona cheti ni muhimu kwa sababu wanaochaguliwa ni wachache, kama hakukuwa na umuhimu wa hayo mafunzo si wangeshiriki watoto wote?
Hao waliochaguliwa wapewe vyeti vya kushiriki hayo mafunzo.
 
Sasa wapeww vyeti watavifanyia kazi gani

Hapa naona kuna kosa hufanyika, huwezi wafanyisha watoto kazi ya malipo, lakini mkono wa pongezi kwa watoto ingekuwa Bora zaidi plus hayo matruck suit
Wewe cheti cha kuzaliwa umefanyia kazi gani? Hao machipukizi ya ccm kadi hawana? Ni za nini kama ni watoto
 
Ngoja nikuambie kitu.
Hata wakipewa vyeti havitawasaidia kitu katika maisha yao yote mpaka kifo
Shule kuna vikundi vya pccb, KUELIMISHA UKIMWI, SCOUT n.k ambapo huwatunukia vyeti lakini havijawahi kuwasaidia lolote katika harakati zao za kusaka ajira na harakati zingine.
Kwani wakipewa inagharimu nini?
 
Hujui umuhimu wa cheti cha kuzaliwa?
Nimekujibu kwa hoja yako cheti ni chanini kwa watoto ndio nimekuuliza kwani cheti cha kuzaliwa kwa mtoto ni chanini? Kwamba watoto hawastahili vyeti? Unatukana
 
Hayo matukio ya simba na yanga huandaliwa miezi mitatu?
Naona cheti ni muhimu kwa sababu wanaochaguliwa ni wachache, kama hakukuwa na umuhimu wa hayo mafunzo si wangeshiriki watoto wote?
Hao waliochaguliwa wapewe vyeti vya kushiriki hayo mafunzo.
Angalia simba day ndo utaona maandalizi siyo ya wiki moja au mbili,zile pattern zilizochorwa pale uwanjani ndo utajua walikuwa na maandalizi ya kutosha na yanachukua muda. Na pia suala siyo miezi mitatu au minne suala ni lengo lake ni nini . Na usiyaite mafunzo hayo siyo mafunzo kwamba yana qualify kupewa cheti, ni event tu imeandaliwa basi ikiisha imeisha ikija event nyingine itahitaji set up nyingine. Sasa huwezi kuita shule nzima lazima kuchagua wachache sababu ile siyo haki ya kila mtu ni tukio tu limejitokeza unachukua watoto wachache basi wanafanya linaisha. Ni mambo ya kawaida sana kama unavyoona watoto wanatengeneza nyimbo na michezo Kwa ajiri ya kusherehesha kaka au dada zao kwenye graduation Kwa shule husika. Sasa watoto wakiandaa wimbo au mchezo kwa zaidi ya mwezi Kwa ajiri ya graduation tena Kwa kusimamiwa na walimu wao huwezi Sema wapewe vyeti. Ni mambo ya kawaida kabisa. Tulikuwa na michezo mashuleni na tulijiandaa kwa muda mrefu na kilikuwa kipindi pendwa kwa wanafunzi. Mechi tu ya shule na shule wanafunzi wanapiga zoezi miezi kadhaa sembuse hako katukio kadogo kwamba ndo wapewe cheti 😂😂. Sasa mtu si atamaliza chuo amejaza kabati la vyeti

Pitia hizi picha za simba day hapa chini angalia watoto hapo na ukiwauliza wana enjoy sana matukio kama haya ni sehem muhimu sana kwa mtoto kuliko mwaka mzima unamlisha vita ya majimaji na kina kinjekitile Ngwale . Ni basi tu shule nyingi hazina facility za kufanya mambo kama haya na budget zao ni ndogo ila ni muhimu mno katika kumjenga mtoto
 

Attachments

  • IMG_7593.jpeg
    IMG_7593.jpeg
    77.3 KB · Views: 3
  • IMG_7592.jpeg
    IMG_7592.jpeg
    121.5 KB · Views: 3
Angalia simba day ndo utaona maandalizi siyo ya wiki moja au mbili,zile pattern zilizochorwa pale uwanjani ndo utajua walikuwa na maandalizi ya kutosha na yanachukua muda. Na pia suala siyo miezi mitatu au minne suala ni lengo lake ni nini . Na usiyaite mafunzo hayo siyo mafunzo kwamba yana qualify kupewa cheti, ni event tu imeandaliwa basi ikiisha imeisha ikija event nyingine itahitaji set up nyingine. Sasa huwezi kuita shule nzima lazima kuchagua wachache sababu ile siyo haki ya kila mtu ni tukio tu limejitokeza unachukua watoto wachache basi wanafanya linaisha. Ni mambo ya kawaida sana kama unavyoona watoto wanatengeneza nyimbo na michezo Kwa ajiri ya kusherehesha kaka au dada zao kwenye graduation Kwa shule husika. Sasa watoto wakiandaa wimbo au mchezo kwa zaidi ya mwezi Kwa ajiri ya graduation tena Kwa kusimamiwa na walimu wao huwezi Sema wapewe vyeti. Ni mambo ya kawaida kabisa. Tulikuwa na michezo mashuleni na tulijiandaa kwa muda mrefu na kilikuwa kipindi pendwa kwa wanafunzi. Mechi tu ya shule na shule wanafunzi wanapiga zoezi miezi kadhaa sembuse hako katukio kadogo kwamba ndo wapewe cheti 😂😂. Sasa mtu si atamaliza chuo amejaza kabati la vyeti
Achana na michezo, naongelea ishu ya matukio ya kiserikali mkuu.
 
Nilikua chipikizi mwaka 1987, baada ya kua mkubwa aiseeee nilijiona bonge la fala sana nikiwaza walivyo tufanya wapuuzi wakati wao watoto wao walikua wakisoma Kenya na Uganda miaka hiyo
 
Achana na michezo, naongelea ishu ya matukio ya kiserikali mkuu.
Kwa mtoto There is no difference , iwe shughuli za kiserikali iwe shule iwe ya tukio lolote lile faida Kwa mtoto ni zile zile maana wao si viongozi wala si wanasiasa wao wanasherehesha tu. Wakitoka hapo wanachokumbuka ni michezo Yao tu huwezi kumuuliza kilichohutubiwa akakumbuka. Kwa hiyo regardless ni nani muandaaji Kwa mtoto it’s the same thing
 
Back
Top Bottom