Vijana wa Kitanzania, mna deni kubwa kwa Lissu

Vijana wa Kitanzania, mna deni kubwa kwa Lissu

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
2,428
Reaction score
3,937
Kwa tathmini yangu, kama kuna kundi ambalo future yao imeharibiwa sana na sera, maamuzi na mienendo ya serikali ya Magufuli, basi kundi hilo ni la vijana.

Kwanza, tukianzia kwenye sheria kandamizi zinazotingwa kila siku ambazo zinafunga mianya hata ile midogo iliyokuwa imebaki ya vijana kuweza kutoboa. Sheria za mitandao kwa mfano.

Tukija kwenye maamuzi ya kiuchumi na kifedha. Pesa nyingi iliyotapanywa kinyume cha sheria na serikali katika kufanya manunuzi yasiyo na tija ingeweza kutumika kuboresha elimu na mazingira ya vijana kuweza kutoboa kimaisha.

Tatu, maamuzi ya kuminya uhuru wa kuongea una athari zaidi kwa vijana. Kina Mdude, Tito, Kabendera, Saanane wanawakilisha alama ya vijana victims wa serikali hii.

Ujana ndiyo kipindi mtu anakuwa huru zaidi, spirit yake inataka kujaribu vitu tofauti, inajenga uwezo wa kuangalia mambo kwa mitazamo mipya na kukosoa. Ni miaka ya kuwa rebellious. Ndiyo miaka tunawakosoa hadi wazazi wetu. Ni natural process katika makuzi ya binadamu. Magufuli na serikali imenyima fursa hiyo kwa kizazi hiki cha sasa na itaenda kuwaathiri katika maisha yao yote.

Tundu Lissu, baada ya masaibu yake, angeweza kutulia zake huko Ulaya akala maisha yake fresh tu. Wengi tusingemlaumu.

Ila kwa mapenzi yake ya dhati kwa taifa hili, ameamua kurudi kuwapambania nyie vijana na future yenu. Tafadhali msimuangushe. Mnahitaji kuongeza juhudi kusimama naye na muwe mstari wa mbele kulinda kura na kupinga mbinu zozote zile za kuharibu zoezi la kura. Future yenu inategemea sana matokeo ya uchaguzi huu.

Mwisho nawahusia vijana, chagueni Tundu muweze kutoboa!
 
Umeandika hoja nzito sana Mkuu.

Vijana tumekubali kuburuzwa kwa UPUMBAVU WETU VIJANA WENGI WA HII NCHI NI MBUMBUMBU KABISA.
Tunaiga upumbavu wa wazee wetu mfano. Huyo Mukaruka mzee hajui hata anachokitetea zaidi ya upumbavu tu.

Vijana tugutuke nchi hii inahitaji mabadiriko makubwa.

Kwa kifupi system inawatumia kipindi kifupi na vijana wanatukika kweli wengine nasikia wanalipwa hadi buku 7
 
Jamaa ameandika pumba sana lakini akaenda mbali zaidi na kuandika pumba za pumba zake kwa kusema vijana wanatakiwa waachiwe wafanye chochote kwani umli wao wa kujaribu kila kitu. Mleta mada lazima anatatizo la kisaikolojia au akili. Yaani anamaana vijana waachiwe kufanya lolote hata kama ni la uvunjifu wa sheria jamaa vipi. Ndiyomana wanajaribu hata kuwa mashoga kama mtetezi alivyokuja
 
Saaaasa kwa hiyo ukiuza ngada, usipo lipa kodi ndio unawakilisha vijana? kazi kweli kweli.
 
Vijana wote watamchagua TAML,tar 28.
Cha muhimu hapa tuhamasishane jinsi ya kulinda kura zetu tu.
 
Uko sahihi mkuu Keynez. Vijana wanajitahidi, wanayumbishwa na propaganda uchwara. Laiti vijana wangeelewa falsafa ya Haki, Uhuru na Maendeleo ya Watu, wasingefanya makosa panapo 28 Oct.

Ni imani yangu kuwa watu walio na akili sawa sawa wameelewa hii falsafa na wako tayari kuikomboa nchi. Sijawahi sikia maccm yanataja popote na wakati wowote ule neno HAKI. mara hii tuyafundishe
 
Back
Top Bottom