Vijana wa Kitanzania waibuka kidedea Mashindano ya TEHAMA Nchini China

Vijana wa Kitanzania waibuka kidedea Mashindano ya TEHAMA Nchini China

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-05-27 at 15.50.05_782c2e8e.jpg
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, amewapongeza vijana watatu wa Tanzania - Dickson Mram, Matimu Mahimbo na James Amos - kwa kuibuka washindi katika mashindano ya TEHAMA duniani ya Huawei yaliyofanyika Mei 23-26,2024 Shenzhen, China.

Vijana hao wenye ujuzi katika uhandisi wa kompyuta, IT na mawasiliano ya simu waliambatana na Mhadhiri msaidizi kutoka Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Mhandisi Jumanne Ally ambapo wanafunzi zaidi ya 470 kutoka nchi 49 duniani walishiriki mashindano hayo.

Waziri Nape amesema kuwa ushindi huu unaonyesha uwezo uliopo miongoni mwa vijana wetu wa kitanzania katika fani muhimu za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.

Vijana hao watarudi Tanzania tarehe 28 Mei, 2024 na wanawatarajiwa kupokelewa kwa shangwe na kupongezwa kwa kuwa mfano wa kuigwa na vijana wengine wa kitanzania.

Waziri Nape ameuzungumzia ushindi huo kuwa mwanzo mzuri wa kujenga taifa lenye ubunifu katika fani za TEHAMA.
 
Teknolojia ndio nguzo kubwa ya uchumi kwa nchi nyingi zilizo piga hatua kubwa duniani kwa sasa, kama kungekua na mipango mizuri na uwekezaji wa kutosha inawezekana ingetuinua watanganyika lakini tatizo ccm iko pale
 
Mmmmhh niwe tu muwazi hiyo post sijaelewa walichokuwa wanashindania ni kipi Hadi hao wa tz washinde kwenye technology Tena Kuna nchi 30+ zimeshiriki na china yenyewe ikiwepo,

half mbona hiyo picha ni kama vile picha ya kuomba kupiga ukiwa umeshika kikombe na Sio unakabidhiwa

Ngoja ninyamaze ila.......... 🤣🤣🤣
 
Hizi ndizo habari tunapenda kusikia na kuona syo kila siku tu habari za wakata mauno. Nape hawa uwakaribishe Bungeni kama wageni rasmi

Ova
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, amewapongeza vijana watatu wa Tanzania - Dickson Mram, Matimu Mahimbo na James Amos - kwa kuibuka washindi katika mashindano ya TEHAMA duniani ya Huawei yaliyofanyika Mei 23-26,2024 Shenzhen, China...
Hongera kwao ila je wakirudi watatumika? Wenzetu lengo la mashindano haya ni kutafuta bright student of them all and wana waajiri kwenye taasisi zao.
 
Niliona hayo mashindano UD yalikuwa mazuri sana
Hope yatafungua njia ya uwekezaji katika elimu yetu hasa katika SoMo la computer
 
Back
Top Bottom