lordchimkwese
JF-Expert Member
- Nov 16, 2015
- 1,914
- 3,356
Kingine wanawake wanapendana wananyanyuana wanapeana connection masela 80% hatupendani.....
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wanalinda brand.hata hapa wapo wengi sana,, na wako busy kupost upuuzi...mie nlipomaliza chuo nakumbuka niweka vyeti kabatini nikatoka kutafuta vibarua....tena vile vya kuvizia kwa gate.....nyapara linakuja linachagua kama 5 mnaingia ndani...ukibahatika unaambiwa kesho uingie...na kitamburo unapewa.......nilisota pale wiki.......aiseee Mungu sio athumani.....pale mimi ndio nilitoka direct......conection initik inside, kuleta vyeti nikaambiwa wewe utaenda kuwa manager wa branch mpya dsm.......hawa vijana ukiwaambia wanaona ni zuga....kubet,,,uchambuzi wasoka ....akirudi nyumbani ...ni bora kuku atataga ule yai....brake ya kwanza jikoni....duh....ila wazazi ndio tumewafikisha hapo
pisi kali kama huna mpunga wanakuona mwenzao tuu...Wanalinda brand.
Pisikali itanionaje nabebeshwa mizigo wakati inajua, mimi ni Uni Graduate laptop na movie kila time
Usiongee ili kufurahisha genge wapi unapata kazi ya ulinzi siku hiyo hiyo?Kuna kazi za ulinzi hapa Dar ukienda siku hiyo hiyo unapata kazi hata kama ni LASABA.
Mshahara mpaka Tsh 160,000.
Tena uzuri wa hizi kazi ni kukaa na kutembea tembea tu kidogo.
Kuna watu Dar hii wanabebeshwa viroba vya unga usiku mzima kwenye maviwanda na hawapati hiyo. Asubuhi kunakucha wako hoiiiii
Inapigwa sound tu na mipango kama yote.pisi kali kama huna mpunga wanakuona mwenzao tuu...
Mkuu uko wapi na ulienda kampuni zipi??Usiongee ili kufurahisha genge wapi unapata kazi ya ulinzi siku hiyo hiyo?
Binafsi nilivyomaliza chuo baada ya kudhurula na bahasha ikabidi niingie kitaa kutafuta kazi uko mtaani hakuna kazi kama mnavyosema labda kazi ya kuuza karanga,nimehangaika ktk kampuni kibao za ulinzi sijapata kazi zaidi ya kuambiwa toa elfu 80 tukupe kazi,hata saidia fundi bila connection hupati.
Ila mwisho wa siku nikaja kutusua kizali la mentali
Mkuu naomba mniunge na mm huko vikobaNi kweli kaka
Ile women empowerment imeleta matokeo chanja sana, kiukweli wanawake wanaobweteka wamebaki wachache nao hao wachache utakuta kuna sababu inayomkwamisha tu
Lakini mwanamke ukimuonyesha njia anafanya wonders, leo wanawake wanacheza vikoba, sijui upatu, kuuza vitenge karanga etc ila wanaume sijui wamepatwa na nini kabisa yani wamebaki kubeti kamari bangi na vitu vingine vibovu tu
Kuna mahali tulikuwa na kikoba watu kumi among of us 9 ni wadada na mmoja ni mkaka, uwezi amini yule kaka tulijuta kumuweka hana plan yeyote, tunakutana kila tarehe mbili ya mwezi unaleta hisa na kama una rejesho unapeleka, yule kaka siku inafika haji wala aleti pesa, siku akija awe alikuwa ana shida ya hela wala hana akisikia tu kuna hela anataka kukopa hata kama hana shida imagine anakopa anaenda kutowa watu out au basi anaenda kula tu basi tukaona huyu anatupotezea muda tukamtowA
Polen sana kwetyu huku vijana tunashindana kununua ma v8,Ni aibu sana kwakweli.
Huku uswahilini unakuta kwenye vibanda vya cd kuna vijana wadogo wamejazana hadi usiku wamenyoa viduku huku wakijifanya kina diamond,
Unajiuliza huyu kabisa muda huu ndio anarudi kwangu ananikuta mimi ndio babake anagonga anaingia kulala.. Hiiiiiiiii
Kwanini unasema nisiongee nisichokijua wakati mimi ndio niliyekuwa natafuta kazi na nimejionea.Mkuu uko wapi na ulienda kampuni zipi??
Usiongee usichokijua
na vikipewa mzigo kibao kimoja....kinawahi home wasifunge gate......Inapigwa sound tu na mipango kama yote.
Pamba zimenyooshwa, chini laba kali au four ange imepigwa kiwi halafu imewekwa juani. Machoni glasses.
Bahasha kubwa la kaki, mkononi saa na iPhone ( hata kama ya Laki used ulinunulia boom ).
Stori kama zote, kwamba kuna maboss kibao wanataka ukapige kazi, ila mshahara wa 1M haukutoshi yaani🤣🤣🤣🤣
Wengi wao wapo hapa JF, kucha kutwa kumnang'a Marehemu. Na wengi kama Erythrocyte wanahangaika kusambaza hoja za kitoto hapa JF baadala ya kufanya kazi. Hawajui huyo ni binti na anaoleka! Retired, Mshana Jr, brazaj Quinine BAK jitambueni, achana na masuala ya kusifia Chadema, piga kaziWengi Wanapenda sana kulaumu, ujuaji na ubishi.
Kuna baba mmoja alikuwa anasema vijana wengi siku hizi hawajitambui.
Mkuu labda nikupe mifano:Kwanini unasema nisiongee nisichokijua wakati mimi ndio niliyekuwa natafuta kazi na nimejionea.
Kampuni ni hizi
G4S, rampart,kk,chui,guard, giant security ,maridadi nk nyingi
Msifikirie uku mtaani kazi ni rahisi,kama wewe ulibahatika shukuru Mungu
Mada ni nzuri sana.Hili ni janga la Taifa.Habari za jumapili wana Jamii Forum
Leo naomba nizungumze kidogo na hawa wenzetu upande wa Kiume mana miaka ijayo kuna hatari ya kupoteza nguvu kazi
Siku izi ni kawaida kabisa kukuta mdada anauza matunda, anatembeza mtumba, anachoma mandazi ubuyu na juice na mengine mengi ya kuingiza kipato, huko kwenye vikoba ndo usiseme wanawake wameamua kutafuta hasa tofauti na zamani
Lakini upande wa pili kuna uvivu na kujisahau ambapo trend ikiendelea hivi kuna hatari kubwa mbeleni
Wanaume hasa hawa wanaojiita graduate mnapotea kaka zangu, najua mmesoma bodaboda mnaona si hadhi zenu tena, saidia fundi pia siyo hadhi yenu kuuza matunda siyo hadhi yenu mmebaki mnatembea na bahasha kutwa kutafuta kazi, ebu ndugu zangu acheni u brazamen wa kishamba, jichanganyeni hakuna pesa inakuja kukugongea mlango lazima tu uitolee jasho kidogo, mbona wadada wazuri tu wanajishughulisha??
Kuna mtoto wa ndugu yangu alifikia kwangu ili aende interview jamani anaamka saa tano akiamka anaamka na laptop na muvi, anakunywa chai anaendelea na muvi mchana anakula anaendelea na muvi narudi nyumbani nipo hoi bin taaban yeye hata kuoga ajaoga,saa mbili na nusu tunakula dinner ndo anamwambia dada akampashie maji ya kuoga [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] hivi huyu mtu hata akipata kazi si mzigo huu??????
Huu ni mfano lakini wanaume wa aina hii ni wengi sana
Wakati ambapo dunia ipo busy kuimpower mtoto wa kike hebu Wazazi wekeni juhudi kidogo na kwa watoto wa kiume, wajitambue na kuwafundisha kufanya kazi kwa mikono yao wenyewe.
Ni aibu sana
Baadhi ya wazazi wanaona hata ni mkosi na wako radhi kuzungusha watoto wao kwa waganga wasafishwe nyotaTatizo kubwa lipo kwenye jamii sio vijana.. yani kijana akimaliza chuo akaendesha bodaboda au kufanya Kazi ya saidia fundi watu wengi huanza kusema vibaya kumchukulia kama kitendo cha kwenda shule alipoteza muda.. na hakuna maarifa aliyo yapata ya ziada tofauti na walio baki mtaani hii kitu sio kizuri kwenye jamii yetu, na ndo kimefanya vijana wengi wajifungie majumbani.
Yani ili nchi iendelee inatakiwa tujifunze kuwasifia watu wanao kujituma kufanya Kazi kwa bidii hata kama ikiwa ni Kazi ya kuzibua choo.. na kingine pia tujifunze kwa nchi zilizo endelea.
Jamii yetu inaona kama mtu ukimaliza kusomea Uhandisi ukaenda kulima au kujiajiri katika fani tofauti unakuwa umepotea.. kwa mtazamo wangu kitu kikubwa kinacho kwamisha vijana ni majungu kutoka kwenye jamii.
Mfano niulize tu.. ni wazazi wangapi wataruhu mwanao aliesomeshwa kwa gharama mpaka chuo akawe bodaboda,saidia fundi, au hata kuwa mpishi mgahawani?? Wazazi kama mpo humu naomba mjibu kwa uwazi kabisa [emoji1488]
Mtoto wa kiume hana fursa za kuaminiwa haraka na pia jamii iliwaaminisha baadhi ya Kazi kama za mgahawa,kuuza mboga,kuchoma chapati au kuuza juice fresh au mkaa wa kupanga kwamba ni Kazi za wanawake ndio maana unaona hivyo.Hali mbaya sana kila mtu amekaa kwenye mgongo waukosefu waajira halafu watoto wakiume ndoinaonekana wanakosa sana ajira
mkuuu nenda kwa mama ntilie kaoshe vyombo uone utapewa shingapi per hour nina bro wangu alikua anipiga shule nchi za wenzetu kwenye mgahawa ila per hour alikua anachukua dau nono tu kiasi cha kuni uspport ada ya chuoHili unalolisema lina ukweli mkubwa tu. Tatizo sisi tuna tabia ya kudharau aina fulani fulani za kazi na kuziona kama ni kazi za watu fulani mf wasiosoma.
Mfano kwa nchi zilizoendelea, ni kawaida kabisa kukuta kijana lets say hawa wanaosoma vyuoni, kipindi cha likizo anaweza kuomba kazi kwenye mgahawa, bar, supermarket nk na anakua anafanya kwa masaa fulani anaingiza kipato. Hii inamjenga hata siku akimaliza chuo hakosi cha kufanya na kila mtu anaheshimu kazi ya mwenzake.
Sasa njoo hapa kwetu. Kijana wa chuo au aliemaliza chuo hata bar ya baba yake hawezi kukaa kaunta auze, anaona kama ni kujidhalilisha! Graduate hawezi kuendesha hata daladala au bajaji ya nyumbani kwao anaona anajidhalilisha, matokeo yake ndio tunakua na vijana wanakaa tu kutwa nzima hamna wanachofanya.
Mkuu, samahani, kumbe wewe ni KE?!Kuna mahali tulikuwa na kikoba watu kumi among of us 9 ni wadada na mmoja ni mkaka, uwezi amini yule kaka tulijuta kumuweka hana plan yeyote, tunakutana kila tarehe mbili ya mwezi unaleta hisa na kama una rejesho unapeleka, yule kaka siku inafika haji wala aleti pesa, siku akija awe alikuwa ana shida ya hela wala hana akisikia tu kuna hela anataka kukopa hata kama hana shida imagine anakopa anaenda kutowa watu out au basi anaenda kula tu basi tukaona huyu anatupotezea muda tukamtowA
Mtu ana comment hapa anasema hapa Dar huwezi kosa kazi ya laki mwezi afu hasemi wapi....!!Hivi ndio namna tunatakiwa tuishi na hawa vijana wenzetu! Sasa unakuta dume zima lina support malaya ila kumpa ramani mwanaume mwenzie anaona uchawi ila kwenye thread humu anashupaza koromeo ooh vijana wavivu! Watu wapo tayari kuwajibika ila kazi ziko wapi sasa?
Haingii akilini graduate ukurupuke tu kubeba jiko la kahawa na kashata! Mzazi wako anaweza kuona umeshadata ukamuua kwa presha esp. kama ndiye jembe lake analolitegemea!