Vijana wa Kiume badilikeni

Vijana wa Kiume badilikeni

Habari za jumapili wana Jamii Forum

Leo naomba nizungumze kidogo na hawa wenzetu upande wa Kiume mana miaka ijayo kuna hatari ya kupoteza nguvu kazi

Siku izi ni kawaida kabisa kukuta mdada anauza matunda, anatembeza mtumba, anachoma mandazi ubuyu na juice na mengine mengi ya kuingiza kipato, huko kwenye vikoba ndo usiseme wanawake wameamua kutafuta hasa tofauti na zamani

Lakini upande wa pili kuna uvivu na kujisahau ambapo trend ikiendelea hivi kuna hatari kubwa mbeleni
Wanaume hasa hawa wanaojiita graduate mnapotea kaka zangu, najua mmesoma bodaboda mnaona si hadhi zenu tena, saidia fundi pia siyo hadhi yenu kuuza matunda siyo hadhi yenu mmebaki mnatembea na bahasha kutwa kutafuta kazi, ebu ndugu zangu acheni u brazamen wa kishamba, jichanganyeni hakuna pesa inakuja kukugongea mlango lazima tu uitolee jasho kidogo, mbona wadada wazuri tu wanajishughulisha??

Kuna mtoto wa ndugu yangu alifikia kwangu ili aende interview jamani anaamka saa tano akiamka anaamka na laptop na muvi, anakunywa chai anaendelea na muvi mchana anakula anaendelea na muvi narudi nyumbani nipo hoi bin taaban yeye hata kuoga ajaoga,saa mbili na nusu tunakula dinner ndo anamwambia dada akampashie maji ya kuoga [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] hivi huyu mtu hata akipata kazi si mzigo huu??????

Huu ni mfano lakini wanaume wa aina hii ni wengi sana

Wakati ambapo dunia ipo busy kuimpower mtoto wa kike hebu Wazazi wekeni juhudi kidogo na kwa watoto wa kiume, wajitambue na kuwafundisha kufanya kazi kwa mikono yao wenyewe.

Ni aibu sana

Umeandikanukweli
 
Hapa kwetu kuna Kijana ana shahada ya uzamili kakosa Kazi mama yake ni mama ntilie amejoini nae wanafanya Kazi Kijana anapita maofisini kuuliza wanaotaka chakula na anawaletea. Wana maisha mazuri hadi watu wanashangaa. Nachotaka kusema ni kwa vijana wajitambue wafanye Kazi yoyote itakayopatikana. Kusoma ni kuondoa ujinga siyo kuajiliwa maana wengi ni Mizigo kusoma, kujieleza, kuandika barua za Kazi hawawezi!
Kweli kabisa,wengi tunafanya biashara kimazoea,kuigana... Msomi wangu amebuni kitu kipya,sikuwa na mawazo. Ameshauri tusichukue faida,yeye anapata hela kidogo sana (sh 30,000/mo)...anachukua chakula kwangu(anajipikia)... Pasaka hii alifanya tukio (live band),,hadi tukaomba ulinzi wa polisi maana ilifana sana sana... Ni biashara ndogo ya pombe/ kwa sasa imekua ndani ya muda mfupi,kwa gharama ndogo. Naona kuna faida,lakini ameshauri nisichukue pesa,,inajiendesha.. Pesa anaweka kwenye a/c, amenishauri tufanye hesabu kila mwisho wa wiki.
 
Vijana wa kiume wanapenda usharobaro,anaona akijichanganya kubeba zege mademu watamcheka.

Mama samia afanye haraka kuinstall mfumo wa elimu ya ufundi katika ngazi za awali,mtu akimaliza hata darasa la 7 awe na ujuzi tu mzuri ambao utamuwezesha kujiajiri.
 
Umegonga penyewe...kuna graduate nilimkuta mahali,akagongea msosi...tukachoma nyama,kilo za kutosha....wakati tunapata hilo dona la nguvu,kachumbari...tukashushia kwa maji ya mende(yeye hatumii)..akaniambia kuna mchongo anausikilizia mahali...nikamchana... Kesho yake akanitafuta tena,akiomba mwongozo wa maisha ya mtaani. Nikamwachia goli asimamie...na masharti kibao. Baada ya mwezi tukafanya hesabu...alinifaa sana sana..amekuwa partner
Hivi ndio namna tunatakiwa tuishi na hawa vijana wenzetu! Sasa unakuta dume zima lina support malaya ila kumpa ramani mwanaume mwenzie anaona uchawi ila kwenye thread humu anashupaza koromeo ooh vijana wavivu! Watu wapo tayari kuwajibika ila kazi ziko wapi sasa?

Haingii akilini graduate ukurupuke tu kubeba jiko la kahawa na kashata! Mzazi wako anaweza kuona umeshadata ukamuua kwa presha esp. kama ndiye jembe lake analolitegemea!
 
Vijana wa kiume wanapenda usharobaro,anaona akijichanganya kubeba zege mademu watamcheka.

Mama samia afanye haraka kuinstall mfumo wa elimu ya ufundi katika ngazi za awali,mtu akimaliza hata darasa la 7 awe na ujuzi tu mzuri ambao utamuwezesha kujiajiri.
Umelipa million zaidi ya kumi kugharamia elimu kisha uishie kubeba zege my friend? Na hao droputs wafanye nini?

Kwanini msishawishi watu kufanya mega projects kupitia kampuni? Watu waji organize wafungue kampuni zao maisha yaanzie huko! Kwa hili hata mzazi atashawishika!
 
Hivi ndio namna tunatakiwa tuishi na hawa vijana wenzetu! Sasa unakuta dume zima lina support malaya ila kumpa ramani mwanaume mwenzie anaona uchawi ila kwenye thread humu anashupaza koromeo ooh vijana wavivu! Watu wapo tayari kuwajibika ila kazi ziko wapi sasa?

Haingii akilini graduate ukurupuke tu kubeba jiko la kahawa na kashata! Mzazi wako anaweza kuona umeshadata ukamuua kwa presha esp. kama ndiye jembe lake analolitegemea!

Ni kweli mkuu mzazi anaweza akafa kwa presha ghafla akiangalia fedha aliyotoa kuanzia kwenye efemu akademia zile za kina emmy.
 
Umelipa million zaidi ya kumi kugharamia elimu kisha uishie kubeba zege my friend? Na hao droputs wafanye nini?

Kwanini msishawishi watu kufanya mega projects kupitia kampuni? Watu waji organize wafungue kampuni zao maisha yaanzie huko! Kwa hili hata mzazi atashawishika!

Hahaha kubeba zege ni kwa wale wenye elimu ya hapa na pale yaani ile ya kuunga unga la 6 B.
 
Ni kweli mkuu mzazi anaweza akafa kwa presha ghafla akiangalia fedha aliyotoa kuanzia kwenye efumu akademia zile za kina emmy.
Hahaha mzazi kalipia efuem academia million za kutosha! Kaja mpaka chuo kalipia around 20M halafu eti kirahisi tu dogo umwambie unaenda Jangwani kununua kashata na jiko la kahawa unaanza kupuyanga unatafuta sh.100/100
 
Hahaha kubeba zege ni kwa wale wenye elimu ya hapa na pale yaani ile ya kuunga unga la 6 B.
Eeh yani mwamba aliona mwalimu wa nidhamu anamzingua akamtia ndonga akala cheti cha kuingia mtaa! Hao sasa ndio wazee wa hustle hard! Zege twende, Kuokota makopo twende, kupiga debe twende!

Sasa utamlinganisha na mtoto aliozoea kucheza play station na kucheki movies mpaka anafika form6!
 
Hahaha mzazi kalipia efuem academia million za kutosha! Kaja mpaka chuo kalipia around 20M halafu eti kirahisi tu dogo umwambie unaenda Jangwani kununua kashata na jiko la kahawa unaanza kupuyanga unatafuta sh.100/100
Inasikitisha sana aiseee mtu una "nyuzi" yako uanze kutembea na beseni la mihogo/karanga/matango? Hii kiukweli ni kwa wenye elimu ya hapa na pale.
 
Inasikitisha sana aiseee mtu una "nyuzi" yako uanze kutembea na beseni la mihogo/karanga/matango? Hii kiukweli ni kwa wenye elimu ya hapa na pale.
Mzee kwa wadhifa wake lazma aumwe pressure! Unless otherwise ufanye biashara proper kwenye eneo rasmi, mazingira mazuri ya kuridhisha ile kidijitali kabisa!

Tatizo linaanzia hapo sasa, project tu ya kufanya branding na kadhalika inataka 10M kabla ya mtaji!😂😂😂 who is willing to give you that money! Utaambiwa anza chini maanake ukaanze kutembeza kahawa sasa au sio 😂😂😂
 
Inasikitisha sana aiseee mtu una "nyuzi" yako uanze kutembea na beseni la mihogo/karanga/matango? Hii kiukweli ni kwa wenye elimu ya hapa na pale.
Hizo wanazofaulu kirahisi ni mademu sababu wengine wanagongwa na hao hao wateja ambao baadae wanageuka ma sponyoo! Unaskia alianzaga na chupa 2 za uji tu sahizi anamiliki mgahawa wake kinondoni😂😂😂

Kazi pekee ambayo vijana wa kiume wanafaulu ni ya kupaka rangi wanawake wa maboss tu😅 na kubeba malaya kuwapeleka magesti wakakazwe!
 
dah nmesoma comment zote kwenye huu uzi but sitopenda kudhihaki pande yoyote kati ya ke au me.

jambo la muhimu napnda mleta thread atambue ni kwamba maisha ni safari na mpngaji ni mungu hivyo kama safari yako imeanza usimseme mwenzio ambae hajaanza kwa kumuona mzembe,hii itakusaidia sana endapo ndani yasafari yko ukaanguka

nashukuru kwa nilipofikia mungu ni mkubwa mapambano yaendelee
 
Hizo wanazofaulu kirahisi ni mademu sababu wengine wanagongwa na hao hao wateja ambao baadae wanageuka ma sponyoo! Unaskia alianzaga na chupa 2 za uji tu sahizi anamiliki mgahawa wake kinondoni😂😂😂

Kazi pekee ambayo vijana wa kiume wanafaulu ni ya kupaka rangi wanawake wa maboss tu😅 na kubeba malaya kuwapeleka magesti wakakazwe!
Hahahahaaa mama wa kibubu shamim zeze aliwaingiza cha kiume baada ya kusema alianza na mtaji wa elfu 10 kumbe sponsor anauza dona.
 
Back
Top Bottom