Vijana wa sasa hawana busara na maadili mema, hawajieshimu, hawaoni ukweli na hawajui historia yetu

Vijana wa sasa hawana busara na maadili mema, hawajieshimu, hawaoni ukweli na hawajui historia yetu

Ukitoa marekani Tz ni nchi isiyo na tamaduni wala maadili, matunda yake tutayaona
 
Na hao wazee wa zamani mpaka leo bado wameng'ang'ania madaraka hawataki kabisa kustaafu maana nje ya serikali wanahisi hawawezi kusurvive.
Mtu kawa raisi, lakini mpaka leo eti anajengewa mjumba kama wote. Wakati ana maslahi makubwa, hakatwi kodi, anatunzwa na serikali lakini eti hadi nyumba najengewa.
Haya masuala ni mazito sana
 
haijalishi una busara kiasi gani yaani pasipo connection utaishia kuwa mshauri wa familia.
 
Ukiambiwa Dr Salim Ahmed Salim aliteuliwa balozi nchini Misri akiwa na miaka 22 halafu ukalinganisha na vijana wetu wa leo wenye elimu na umri huo utaona km vile tunarudi nyuma badala kwenda mbele.

Na ukiambiwa miaka ya 70 hadi 90 nchi yetu ilikuwa na vyama vya ushirika kila mko vyenye nguvu kabisa vya kuweza kununua mazao ya wakulima bila matatizo halafu ukalinganisha na Sacco's za sasa hivi za wasomi utaona tunarudi nyuma badala ya kwenda mbele.

Ukiambiwa zamani nchi yetu bila wasomi ilikuwa na viwanda Mutex mwatex kiltex urafiki nk na mashirika ya umma yenye mafanikio makubwa sana lkn baada wasomi kuyaongoza ndo yamefilisika kabisa lazima utakuwa na mashaka na elimu za vijana wetu.
Kwako nin maana ya msomi?
Je una ushahidi gani kuwa wasomi wamechangia pakubwa kufeli kwa hayo uliyozungumza?
Taja shirika/chama kilichofanikiwa miaka hiyo na majina ya viongozi wake pamoja na elimu zao ili kuthibitisha hayo uliyoyasema.

Mwisho nakushauri mshale wako ulipouelekeza umekosea shabaha,huwezi kumlaumu mtoto kwanini amezaliwa nje ya ndoa wakati yeye ni matokeo ya zinaa ya wazazi.
@Asiyejua maana haambiwi maana
 
Kwako nin maana ya msomi?
Je una ushahidi gani kuwa wasomi wamechangia pakubwa kufeli kwa hayo uliyozungumza?
Taja shirika/chama kilichofanikiwa miaka hiyo na majina ya viongozi wake pamoja na elimu zao ili kuthibitisha hayo uliyoyasema.

Mwisho nakushauri mshale wako ulipouelekeza umekosea shabaha,huwezi kumlaumu mtoto kwanini amezaliwa nje ya ndoa wakati yeye ni matokeo ya zinaa ya wazazi.
@Asiyejua maana haambiwi maana
Majibu yote yapo kwenye thread, soma vizuri kwa uelewa.
 
Na hao wazee wa zamani mpaka leo bado wameng'ang'ania madaraka hawataki kabisa kustaafu maana nje ya serikali wanahisi hawawezi kusurvive.
Mtu kawa raisi, lakini mpaka leo eti anajengewa mjumba kama wote. Wakati ana maslahi makubwa, hakatwi kodi, anatunzwa na serikali lakini eti hadi nyumba najengewa.
Na kiuhalisia, hata hana shida nayo. Mazingira yanawekwa ili aliyeko sasa naye aporomoshe lake na akihojiwa aseme na waliomtangulia pia wamepewa.
 
Ukitoa marekani Tz ni nchi isiyo na tamaduni wala maadili, matunda yake tutayaona
Marekani inahusika kivipi?

Alafu marekani kufananisha na sisi ni sawasawa kumfananisha tembo na ndama.
 
Back
Top Bottom