Vijana wa zamani tukutane hapa - old school

Vijana wa zamani tukutane hapa - old school

umeshusha vitu saaana, kumbukumbu nzuri,mimi nilikuwa mpenzi wa ukuta! weekend yangu avelon sinema..
 
mimi wa shamba unanikumbusha kanda za utumbo nilipokuja kwa mjomba miaka hiyo, disko tulienda donbosko (tuliita hivyo) dj alikuwa marlon, na kibonde sijui alikuwa anahusika nn alikuwa anaharibu tu mziki na uniform zake za kino muslim!
disko lilikuwa la kufana nashangaa hujakutaja huko!
hahahahahah kibonde tena[emoji23]
 
Haaaaa haaaaaa

Tukumbushe Movie za Enzi hizo . . . .

Kulikuwa na New Chox; Empire; Empress na zipi zingine sijui . . . .
waigizaji kama fred williamson, jim kelly,mwana dada pam grier,bo sevenson, amita,hema malin,vinod,ponam walikuwa juu, sinema kama black ceaser, three the hardway,enter the dragon,black samurai,amar akbar antony,dilwale,sholay nk.
 
Dah......enzi hizo nikiwa relwe Tabora.......jamaa yangu Filipo akaniacha akahamia RTC Kagera.......kipindi ndio ule wimbo wa Sisily umetoka......acha kabisa......

Enzi hizo Supreme Fred Ndala Kasheba ndio amejiunga OSS baada ya King Kiki Kikumbi Mwanza Mpango ameondoka. Kasheba akiwa na mtindo mpya Dukuduku, nakumbuka ule wimbo, ...... Mara ya kwanza umeniomba tucheze, muziki ya kwetu siwezi kukataa, mara ya pili umerudia tena, sio kwa kucheza ila kunifinya jicho....
Uliza kwanza, kabla ya kuanza upuuzi wako bwana ee, mimi ni muke ya mtu, nimekuja kucheza, nimekuja kufurahisha mwili wangu ee, nimeshaolewa...

Vv
 
waigizaji kama fred williamson, jim kelly,mwana dada pam grier,bo sevenson, amita,hema malin,vinod,ponam walikuwa juu, sinema kama black ceaser, three the hardway,enter the dragon,black samurai,amar akbar antony,dilwale,sholay nk.

Haaaa haaaaa haaaa nimecheka kwa sauti hadi najishangaaa . . .

Really? Those were the old gold time. Will never come back now
 
Enzi hizo Supreme Fred Ndala Kasheba ndio amejiunga OSS baada ya King Kiki Kikumbi Mwanza Mpango ameondoka. Kasheba akiwa na mtindo mpya Dukuduku, nakumbuka ule wimbo, ...... Mara ya kwanza umeniomba tucheze, muziki ya kwetu siwezi kukataa, mara ya pili umerudia tena, sio kwa kucheza ila kunifinya jicho....
Uliza kwanza, kabla ya kuanza upuuzi wako bwana ee, mimi ni muke ya mtu, nimekuja kucheza, nimekuja kufurahisha mwili wangu ee, nimeshaolewa...

Vv

Daaaah . . . kweli ulikuwa mtu wa viwanja . . . . Hawa walikuwa wanatumbuiza Silent Inn Mwenge au ili ya pale Kimara (Nimesahau jina)
 
Enzi hizo ukienda Rungwe Oceanic Beach Resort ya Mzee Mwakitwange ulikuwa unakuitana na majina kama vile DJ Ngomely, DJ Pop Juice na wengine. Ukiosea jirani na hapo Rungwe, yaani Silver Sands, unakutana na kina John Peter Pantalakis, Choggy Sly na Kalikali ambaye baadaye alihamia YMCA.

Ukienda Africana ulikuwa huangalii simba aliyekuwa anafugwa hapo, bali pia DJ Mehboob, wakati ukishuka mjini hususan Motel Agip na baadaye New Africa hotel ghorofa ya saba kulikuwa na DJ Emperor (huyu Joseph Kusaga bosi wa Clouds 88.4 fmunaemjuea), Boniface kilosa a.k.a Bonny Love na DJ Jesse Malongo (wa Club Afrique, London).

Baadaye kidogo ikaja Space 1900 iliyoanzia hoteli ya Mbowe na kuhamia YMCA, na kuleta ushindani mkubwa kwenye fani ya muziki ambapo disko lilifunika kabisa muziki wa dansa. Vile vile ikazuka New Vision ambako DJ Super Deo, DJ Paul MacGhee na Joe Johnson Holela walitengeneza majina sio kawaida, huku wakimpa darasa DJ Young Millionaire ambaye sasa anatamba Star TV ya Mwanza akiwa na jina lake halisi ya Jacob Msungu, kwenye kipindi chake cha TV cha Roving DJ.Baada ya Space 1900 discotheque kuhamia YMCA, disko la RSVP Discotheque likazaliwa Mbowe na Ma DJ wake walikuwa mkongwe Saidi Mknadara a.k.a DJ Seydou, akisaidiana na DJ Yaphet Kotto.

Kwa ufupi, pamoja na kwamba DJ Eddy Sally na DJ Sweet Francis wa hoteli ya Keys mtaa wa Uhuru walikuwa juu kwa vyombo vya kwanza vya kisasa vya disko, lakini ni DJ Seydou na DJ Yaphet Kotto ambao ndio walikuwa vinara pale RSVP Mbowe. Yaani baada ya kuruka majoka kila sehemu uijuayo, lakini vijana wote wa Dar walikuwa wanakwenda Mbowe kumalizia usiku kwa DJ Seydou na DJ Kotto.Kwa ufupi huyu ndiye aliyekuwa baba wa disko Dar, sio pekee kwa uwezo usio wa kawaida wa kupanga muziki tu bali pia ngekewa ya kupata nyimbo mpya mpya kabla ya DJ yeyote nchini.

Kwa hisani ya: MATUKIO UK: NAWAKILISHA ENZI YA MIAKA YA THEMANINI (OLD SCHOOL)

My take:

Enzi hizo miaka ya 1983-1985 nilikuwa Kibaha High School (Enzi hizo tunakula Kuku na wali). na kisha JKT Ruvu. Tulikuwa kila weekend tunakuja Down Town na akina Ray Bagenda (Nadhani yuko ardhi sasa). Sometimes tunaanza Boogie (Disko la Mchana hadi majogoo.) Mbowe Hotels, YMCA; Rungwe Oceanic; Silversends, Msasani Club nk wanahusika.

Mabingwa wa Kudance wakati huo: Akina Black Moses (RIP) and the likes. Arusha Cave Disco ilikuwa ni hatari kwa kwenda mbele.
  1. Tuambie wewe enzi za ujana wako ulikuwa wapi na unakumbuka nini?
  2. Na Je; sasa hivi ma-DJ wetu hawa waliovuma wako wapi na wanafanya nini?
  3. Rafiki zako wa Ujana wako wapi na wanafanya nini?
Karibuni tukumbushane
Shimoni R chugga, sometimes 7 Floor,.....luaa intaneshno.....pia disko vumbi......na Freshaz bowl pia disko za sekondari twaletewa mademu
 
Haaaa haaaaa haaaa nimecheka kwa sauti hadi najishangaaa . . .

Really? Those were the old gold time. Will never come back now
huwezi kupata enzi hizo, hazirudi, kizazi hiki kinaona nyota tu, hakukuwa simu za mkononi,hakuna internet,hakuna matv kama sasa ila kitu kikishuka marekani hakina muda kiko dar! movie ikitoka india haina muda iko dar, tulikuwa tunapata habari za marekani,cuba na urusi ya zamani kupitia kwa vijana wa ilala( ma seamen)
 
Shimoni R chugga, sometimes 7 Floor,.....luaa intaneshno.....pia disko vumbi......na Freshaz bowl pia disko za sekondari twaletewa mademu

Haaaaa haaaa ilikuwa wapi hiyo.

Kibaha High School tulikuwa tunagiza totoz Kilakala au Vituka. Blues nyimbo za akina Lionel Richie wakati huo. Headmaster alipiga marufuku kucheza blues karibu karibu. Lazima muwe mbalimbali. Mkisogeleana anasema "Hataki Mpendane Pendane" haaaaa haaa
 
Daaaah . . . kweli ulikuwa mtu wa viwanja . . . . Hawa walikuwa wanatumbuiza Silent Inn Mwenge au ili ya pale Kimara (Nimesahau jina)

Hapana mkuu, mimi nilikuwa nifuatilia kupitia RTD enzi za David Wakati akiwa Mkurugenzi wao.

Ilikuwa ifikapo saa 9 alasiri nasikiliza kile kipindi cha Ombi Lako kilichokuwa kikiongozwa na Suleman Muhogora. Pia nilikuwa nafuatilia kupitia RTD External Service, enzi za mtangazaji nguli Stephen Lyimo.

Jumamosi kulikuwa na kipindi cha Misakato, lkn pia saa 2.30 usiku RTD Idhaa ya Biashara, Uncle J Julius Nyaisanga alikuwa na kipindi kinaitwa Philips Radio Club na kale kawimbo ka kufungulia kipindi , 'sauti safi sauti kubwa, Philips, radio club...'.

Enzi hizo nilikuwa namalizia Primary School, na nikitoka sana ni Jumamosi, tunakaa nje ya DDC Magomeni wakati bendi Juwata, au Mlimani Park wakitumbuiza.

Vv
 
Hapana mkuu, mimi nilikuwa nifuatilia kupitia RTD enzi za David Wakati akiwa Mkurugenzi wao.

Ilikuwa ifikapo saa 9 alasiri nasikiliza kile kipindi cha Ombi Lako kilichokuwa kikiongozwa na Suleman Muhogora. Pia nilikuwa nafuatilia kupitia RTD External Service, enzi za mtangazaji nguli Stephen Lyimo.

Jumamosi kulikuwa na kipindi cha Misakato, lkn pia saa 2.30 usiku RTD Idhaa ya Biashara, Uncle J Julius Nyaisanga alikuwa na kipindi kinaitwa Philips Radio Club na kale kawimbo ka kufungulia kipindi , 'sauti safi sauti kubwa, Philips, radio club...'.

Enzi hizo nilikuwa namalizia Primary School, na nikitoka sana ni Jumamosi, tunakaa nje ya DDC Magomeni wakati bendi Juwata, au Mlimani Park wakitumbuiza.

Vv

Haaaaaa haaaaa haaaaa

You really made my day.

Mzee Wakati alishafariki. Nyaisanga nadhani yuko AZAM na akina Tido.

Daaaahhh Long time sana
 
Duuh wakati huo mimi niko JKT. Bila shaka Vijana wa zamani wa Kitaa watatukumbusha zaidi . . .
Mkuu umetukumbuka na sisi kwa mada hii! Miaka ya mid /late 80's high school mujini tulikuwa na raha ni raha tuu!
 
Back
Top Bottom