Vijana waliopo CCM wanalo la kujifunza hapa

Inaonyesha vijana wa CCM wengi hawajasoma vizuri. Chadema ilifanya kampeni vyuoni na kubeba vijana wengi sana na ndiyo hao akina Silinde and company ambao ni mawaziri na sasa hao waliokuwa wamebaki wameukwaa uDC. CCM ibadili mwelekeo wa kurecruit vijana or else viongozi wao wataendelea kuchukua vijana wa upinzani.
 
Hao ulowataja tayari ni wanachama watiifu wa CCM. Nilitarajia unitajie hata mmoja alotoka direct upinzani
Hawakuwa ccm na wala hawakutumwa cdm. Kilichotokea ni njaa tu ya matumbo yao ndiyo ilifanya wakisaliti chama kilichowatoa mbali!!!
 
Una hakika gani kama hao wapinzani walioteuliwa DCs na ambao tayari ni viongozi kuwa hawakuwa katika mission maalum na wameshahitimisha? Wapinzani wote chimbuko la asili ni CCM. Na walioteuliwa awali walikuwa CCM na wengine ni kutoka Kule Kwa walio gizani tusiowaona Ila wako kazini. Usoni na maneno Yao ni uoinzani Ila akigeuza kisogo yuko kazini na boss anapata taarifa sahihi. Upinzani bado Sana Tanzania maana mapandikizi bado yameshikilia Kasi. CCM hamtuwezi😎😎😎😎
 
Inaelekea hujui maana ya chama. Chama ni hoja na ushawishi na CCM kwenye hilo hawamo.
Wao ni chama dola, ukiwatenga na dola tuu wamekufa na kupotea kabisa.
Ndugu hujui chama; usitafute ugomvi na wana CCM.

Sijui wewe ila sisi tunapowachokoza vijana wao hakina Mwigulu, Nape and so forth tunajua mipaka yetu.

Nyuma yao kuna chama na ndio watu ambao tunaowakosoa provided unafanya kistaarabu and you do not want to mess with them.

CCM aijali kukosolewa tatizo lenu matusi mnataka kuwatukana watu kwa lugha ambazo amuwezi kuongea na wazazi wenu; ilhahi hao watu mnaowatukana wamelingana au kuwazidi umri wazazi wenu.

Nyofoa tu kucha mpate adabu
 
Yaani hao vijana wote walioko CCM hawana uwezo ndiyo maana mama kawaacha? Haingii akilini. Mi naona hapo ni shule tu ndiyo imebeba wapinzani.
 

mbna simwoni lazaro nyalandu, sumaye na lowasa
 
Halafu Mataga yana miaka kibao yapo CCM yakitarajia kupata vyeo, mwisho wa siku vyeo vimekuwa vya wapinzani tu na si Mataga, yaani mtu anatoka upinzani leo,kesho anakuwa DC,na Kuliacha Taga likipayuka Lumumba bila mwelekeo, haya majitu ni shenz taipu sana!

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
CCM ndiyo mnavyojidai kuwa upinzani wote umeanzia kwenu. Hao vijana tuliwekewa picha zao hapa wakati wamechukuliwa na CDM na kuanza siasa. Walikuwa choka mbaya!!! CDM imewanoa na wakapendeza. Rushwa ni hatari sana sana. Vijana wamechepukia CCM kwa sababu ya matumbo tu!!! Tusubiri 2025 kama bado mtawapitisha. Kwanza 2020 wote hawakupita. Kama walikuwa vijana wenu kwanini mliwatosa? Hao wote asante mwendazake! Mama alijinasibu kuwa yeye na mwendazake ni kitu kimoja. Kweli mambo ya utawala na jinsi anavyotawala anamuiga sana mwendazake. Tofauti ni moja tu! Mambo ya kibinadamu mama yuko juu. Hii ya bajeti ya ajabu mwendazake asingekubali wananchi tulipie kupitia vocha na luku. Tena mtu angepoteza uwaziri fasta. Hii ndiyo tofauti yao!!! Mwendazake na ubaya wake wote alikuw na very good points zilizomfanya awe tofauti na viongozi wengine!!!
 
Yaani hao vijana wote walioko CCM hawana uwezo ndiyo maana mama kawaacha? Haingii akilini. Mi naona hapo ni shule tu ndiyo imebeba wapinzani.
Akili zako zinakutosha mwenyewe

Hakuna kada wa chama cha mapinduzi mwenye ndoto za nafasi za ukuu wilaya and so forth

Makada wa CCM awategemei nothing zaidi ya kuomba nafasii za ridhaa kwa wananchi na kupata ushindani; hizo za kiserakali zikitokea ni majaaliwa tu.
 
Maana yake ni kwamba, hao in ccm kabla hawajajijunga hadema, waliwekwa cdm kwa shughuli maalum wakisimamiwa na mwenyekiti.
Ni miongoni mwa assuptions za kizembe sana hizi, mara nyingi wazembe wa kufikiri hua wanatafuta sababu za kujitetea kama hi. Nasari angeakua mwana ccm kificho asingetishwa vile, kanusurika KIFO two times, akigombea mara ya kwanza ubunge wa Arumeru baada ya naibu waziri kufariki, chopper yake hadi ikadakwa na matawi ya miti, wakaua mbwa wake walivyo vamia nyumba yake ili wampeleke mbele za HAKI. Wana ccm kificho hawafanyiwagi hayo mkuu, mtazame yule sultani wa act, pamoja na mawe anayotupiaga huko chamani (Lumumba ) but hajawahi hata kulala walau siku 2 police, hanaga hata kesi moja mahakamani. Funguka mkuu, use your brain to think, halafu jaribu pia kua mtunzaji mzuri wa historia, itakusaidia sana ku reason mambo
 
Si kweli unachoongea. Hakuna mtu asiyetaka mabadiliko. Wewe unakuwa katibu wa kata unalipwa elfu kumi kila mwenzi halafu unaambiwa uwe mkuu wa wilaya ulipwe milioni tatu unakataa!!!! Akili utakuwa nazo kweli!!!! Kutaka maendeleo ni hulka ya binadamu. Kama mtu hataki maendeleo basi huyo atakuwa zombie na ni wa kumkimbia kama ukoma!!! Hafai kabisa kuwa rafiki yako maana hatakupa changamoto yeyote.
 
Yaani hii miccm haijui kufikiri ndiyo maana inaachwa kwenye teuzi Isitoshe shule yao ndogo na mwendazake alikuwa anaangalia sana shule. Teuzi zake zote ni wasomi sasa huyu kafuata nyao na alituambia yeye na mwendazake ni kitu kimoja. Tutegemee teuzi za kimwendazake tu yaani kuangalia shule na kuendelea na rushwa iliyofanywa na mwendazake. hao walioteuliwa kuna walivyoahdiwa ndiyo maana walidefect!!!
 
There u are brother.
 
Inaelekea hujui maana ya chama. Chama ni hoja na ushawishi na CCM kwenye hilo hawamo.
Wao ni chama dola, ukiwatenga na dola tuu wamekufa na kupotea kabisa.
Kwa kweli CCM nje ya kwapa za vyombo vya dola haipumui siku mbili
 

"Nyofoa tu kucha mpate adabu"?
Kumbe tunajadili na mtu mwenye akili za kizamani za Magufuli?
Pole sana
 
Ndugu CCM kama chama hakina ahadi ya kumtoa mtu yoyote kimaisha. Isipokuwa kinauwezo wa kuwapa watu nafasi za uongozi kama taasisi ya chama cha siasa.

Sasa ukisema uende CCM ukidhani ndio njia ya kukimbia umaskini; itakula kwako.

CCM ni taasisi tu yenye agenda ya kuwaletea watanzania maendeleo na mwanachama yeyote mwenye kadi na sifa ya kushika na nafasi sahihi ya uongozi anaweza teuliwa huo ndio uhalisia.

Onyesha thamani yako kama mwanachama CCM aiwezi kukuacha miaka 800.
 
Ccm ianze ku recruit vijana talent's na smart kutoka vyuoni huko na kuwapa nafasi ili kuleta mabadiliko chanya kwa nchi na chama Chao, shida vijana vilaza , majambazi ndo hukimbilia huko na kupewa nafasi au hao vijana kutukana upinzani ndio ilikuwa kigezo Cha kupata vyeo matokeo Yao ubunifu una washinda.
 
Sidhani ka huwa ni mission waliyotumwa huwezi lingamisja vijana wa upinzani na uvccm kujenga hoja kwa mstakabali wa nchi hao ni vitu viwili tofaut. Huko upinzani huwa ni platform inayo wafanya wajulikane hyo ya mission nakupinga kabisa ukikaa na uvccm hata ufikiri wao ni mdogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…