Vijana wengine waibukia hospitalini Dodoma kutaka kuuza figo

Vijana wengine waibukia hospitalini Dodoma kutaka kuuza figo

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1678709888659.png

Siku chache baada ya uongozi wa Hospitali ya Bugando Mwanza kuelezea kadhia wanayoipata kutokana na vijana kuulizia iwapo wananunua figo, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Benjamin Mkapa Dk Alphonce Chandika naye leo Jumatatu Machi 13, 203 ameeleza kuwepo na wimbi la vijana wanaopiga simu hospitalini hapo kuuliza ikiwa wanaweza kuuza figo zao.

Dk Chandika amesema hadi sasa amepokea simu zisizopungua nne kutoka kwa vijana hao wakidai kutaka kuuza figo hali aliyoieleza kuwa ni kutokana na changamoto za maisha.

"Hili suala lipo unakuta vijana maisha yana changamoto halafu anajua Benjamin Mkapa wanapandikiza figo, wamekuwa wakipiga simu. Niwaombe huo utaratibu haupo na sheria zetu haziruhusu biashara ya uuzaji wa viungo na hata tukigundua kuna biashara imefanyika tunasitisha mara moja," alisema Chandika.

Dk Chandika ameyasema hayo leo Machi 13, 2023 wakati akizungumza kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka mitano ya huduma ya upandikizaji figo iliyoanza kutolewa hospitalini hapo mwaka 2018.

Aidha Chandika amesema katika kipindi hicho wamekutana na changamoto ya ukosefu wa elimu kwa baadhi ya ndugu na kushindwa kutoa figo wakihofia kufariki dunia.

Akizungumzia huduma hiyo Faraji Shabani aliyepandikizwa figo aliyopewa na mtoto wake amesema huduma hiyo imesaidia kuokoa maisha yake kutokana na kuugua muda mrefu.

Aidha Shabani amewaasa wananchi kujiunga na huduma ya Bima ya Afya kwa Wote kwani baadhi ya huduma katika upandikizaji wa figo hufidiwa kwa mgonjwa mwenye bima.

Naye Neema Sweti aliyempa figo kaka yake alisema alipata ujasiri huo baada ya kupata semina ya huduma hiyo mara kwa mara na sasa anaendelea vizuri baada ya miaka mitano tangu atoe figo yake.

MWANANCHI
 
Ni nikajua wameisha mtafta watu kama 100 hiv kumbe wa4 tu.
Wakiruhusu figo zitanyofolewa sana na mauaji yatakuwa mengi
Wafanye mtu akifa viungo vyake ni vizima vihifadhiwe na kupewa wagonjwa ila iwe hiari kwa mgonjwa
Kuna nchi mmoja niliona wao hadi leseni zao za udereva zinampa mtu ruhusa ya kuonesha kiungo atakacho donate ikitokea kafa kwa ajari
 
Wakiruhusu figo zitanyofolewa sana na mauaji yatakuwa mengi
Wafanye mtu akifa viungo vyake ni vizima vihifadhiwe na kupewa wagonjwa ila iwe hiari kwa mgonjwa
Haviingiliani kirahisi ndo maana unaona watu wapo ambao hukosa kabisa figo.

Kuna mswada uko njiani kuruhusu viungo vyako viendelee kutumika
 
Haviingiliani kirahisi ndo maana unaona watu wapo ambao hukosa kabisa figo.

Kuna mswada uko njiani kuruhusu viungo vyako viendelee kutumika

Watulipe hela sasa
 
Haviingiliani kirahisi ndo maana unaona watu wapo ambao hukosa kabisa figo.

Kuna mswada uko njiani kuruhusu viungo vyako viendelee kutumika
Kwanini viendelee kutumika nikiwa mfu wakati kuna uwezekano wa kuiuza nikiwa hai na nikaendelea kusurvive na hiyo moja huku nimejipatia mkwanja
 
Mkuu vipi ukisikia wanahitaji kununua vichwa unishtue..
Maana mimi kichwa changu sikielewi kabisa...kama mteja yupo nicheki tafadhali.
 
 
Mkuu vipi ukisikia wanahitaji kununua vichwa unishtue..
Maana mimi kichwa changu sikielewi kabisa...kama mteja yupo nicheki tafadhali.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Biashara ya viungo imekuwa wazi wordiwaid, kukataa kuifanya nikukimbiza pesa kwa vijana.
Ikiruhusiwa iwe hovyo hovyo kutakuwa mauaji ya kutisha. Watu watauawa na kunyofolewa figo zao.
 
Back
Top Bottom