Vijue vijiji vitano maarufu Tanzania bara

Vijue vijiji vitano maarufu Tanzania bara

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Habari wana JF.

Leo nawaletea vijiji maarufu zaidi Tanzania bara.

1. Kolomije: Hiki kipo wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Hiki kilijipatia umaarufu kuliko vijiji vyote tangu march 2017. Hiki ni kijiji alichozaliwa Mheshimiwa Paul Makonda, RC Dar.

2. Butiama: Hiki kipo wilayani Butiama mkoani Mara. Huko ndiko alikozaliwa mwasisi wa Taifa hili Julius Nyerere.

3. Msoga: Hiki kipo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani. Huku ndipo anapoishi na nyumbani kwa Rais mstaafu Jakaya Kikwete.

4. Lupasu: Hiki kipo wilayani Masasi mkoani Mtwara. Huku ndipo alipozaliwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa.

5. Ngarash: Hiki kipo wilayani Monduli mkoani Arusha. Huku ndiko alipozaliwa Edward Lowassa.

NB: Chato sio kijiji bali ni mji na halmashauri iliyopo wilayani Chato mkoani Geita.


Nawasilisha.
 
Lupasu akifahamiki kihivyo kwani Mkapa yeye anajiita Mpare/Mchagga....na wananchi wa huko Lupasu wala hawana mpango naye kwani haonekani kabisa huko labda ashikwe tu na hamu ya kula panya then anaibukia huko ghafla kwa dakika kadhaa tu kisha anarudi kwao Lushoto na Kilimajaro.
 
Lupasu akifahamiki kihivyo kwani Mkapa yeye anajiita Mpare/Mchagga....na wananchi wa huko Lupasu wala hawana mpango naye kwani haonekani kabisa huko labda ashikwe tu na hamu ya kula panya then anaibukia huko ghafla kwa dakika kadhaa tu kisha anarudi kwao Lushoto na Kilimajaro.
aisee!
 
Umesahau Gamboshi...kijiji pekee ambacho kina uwanja wa ndege wa kimataifa na treni za umeme
 
Back
Top Bottom