Vikwazo dhidi ya Israel vinavyowekwa na Marekani vinatuma ujumbe gani kwa mashabiki wa vita ya Gaza?

Vikwazo dhidi ya Israel vinavyowekwa na Marekani vinatuma ujumbe gani kwa mashabiki wa vita ya Gaza?

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Kwa mara ya kwanza tangu kuundwa kwa Taifa la Israel mnamo 1948, serikali ya Marekani ambayo imekuwa mshirika mkuu wa siasa na harakati za Israel pale Mashariki ya Kati, imeeleza kusudio lake la kuweka vikwazo kwa kikosi maalumu cha Jeshi la IDF kilichofanya oparesheni zake upande wa ukingo wa Magharibi unaokaliwa kimabavu na masettler wa Israel

Vikwazo hivyo vinahusu kikosi hiko kuwekewa vikwazo maalumu ikiwemo kutotumia fedha zozote zinazotokana na ufadhili wa Marekani.
Screenshot_20240421_114556_Chrome.jpg


Mimi binafsi msimamo nilionao ni kutounga mkono vita aina yeyote ile. Sababu kuu zinazonisukuma kuwa na msimamo huo ni pamoja na
  1. Athari za vita kwa maisha ya wanadamu hususan waathirika wakuu watoto na wanawake
  2. Athari kwa mazingira, hakuna vita inayoacha salama mazingira ambapo pamoja na uharibifu mkubwa unaoonekana, bali kemikali za silaha zinazotumika na masalia vitaendelea kuwa tishio kwa mazingira na hali ya hewa sambamba na viumbe tegemezi kwa mazingira hayo
  3. Mahusiano baina ya raia kati ya pande za vita kuvunjika na hatimaye kuzaliwa kwa doctrine ya chuki, kubaguana na kuviziana
  4. Athari za kiuchumi kwa wahusika na wasiohusika na vita hizo
Serikali ya Marekani inatoa ujumbe gani kwenye hii U-turn ya vuu bin ghafla dhidi ya Israel?

Source: www.timesofisrael.com
 
Israel itafanya kila linawezekana kujilinda na maadui zake hata bila msaada wa marekani
 
  • Nzuri
Reactions: 511
Marekani usimwamini Kwa asilimia 100 baada miezi kadhaa utashangaa hivyo vikwazo zimeisha na maisha ya hao settlers yataendelea kama kawaida.
Angalia Jana USA wamepitisha Bill ya dollar billion 16 kwenda Israel kwajil ya ulinzi Tu.
 
Israel itafanya kila linawezekana kujilinda na maadui zake hata bila msaada wa marekani
Ni mjinga ataamin hao wapumbavu marekani wataacha kuisaidia israel. Tulishazoea hizo propaganda na uongo wa marekan na israel.
 
Kwa mara ya kwanza tangu kuundwa kwa Taifa la Israel mnamo 1948, serikali ya Marekani ambayo imekuwa mshirika mkuu wa siasa na harakati za Israel pale Mashariki ya Kati, imeeleza kusudio lake la kuweka vikwazo kwa kikosi maalumu cha Jeshi la IDF kilichofanya oparesheni zake upande wa ukingo wa Magharibi unaokaliwa kimabavu na masettler wa Israel

Vikwazo hivyo vinahusu kikosi hiko kuwekewa vikwazo maalumu ikiwemo kutotumia fedha zozote zinazotokana na ufadhili wa Marekani.
View attachment 2969818

Mimi binafsi msimamo nilionao ni kutounga mkono vita aina yeyote ile. Sababu kuu zinazonisukuma kuwa na msimamo huo ni pamoja na
  1. Athari za vita kwa maisha ya wanadamu hususan waathirika wakuu watoto na wanawake
  2. Athari kwa mazingira, hakuna vita inayoacha salama mazingira ambapo pamoja na uharibifu mkubwa unaoonekana, bali kemikali za silaha zinazotumika na masalia vitaendelea kuwa tishio kwa mazingira na hali ya hewa sambamba na viumbe tegemezi kwa mazingira hayo
  3. Mahusiano baina ya raia kati ya pande za vita kuvunjika na hatimaye kuzaliwa kwa doctrine ya chuki, kubaguana na kuviziana
  4. Athari za kiuchumi kwa wahusika na wasiohusika na vita hizo
Serikali ya Marekani inatoa ujumbe gani kwenye hii U-turn ya vuu bin ghafla dhidi ya Israel?

Source: www.timesofisrael.com
Vita zote ni mbaya lakini huwezi ukavamiwa tu na wewe ukamuachia adui akufanyie anavyojisikia kufanya.
 
Kwenye hii Operation naona Israel wapo sahihi ni katika suala zima la kulinda usalama wa taifa lake na watu wake
 
Back
Top Bottom