Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata iwe ni wezi hakuna justification ya kuua watu ambao hawana silaha. Jaribu kuingia YouTube usikiliza maelezo ya huyo kaka mtu ndiyo utajua ni mauaji ya kinyama. Wanasema polisi walikuwa wanafanya doria tangu mchana na walishawakamata na kuwaweka chini ya ulinzi. wakaanza kuwapiga risasi za miguuni na baadae mwilini tena mbele za watu. Mimi ndiyo maana huwa nasema watanzania tuko kama manyumbu. Mtu anaua na watu wanaona ni sawa tu.
Sijui kwanini watu hawaoni huu upande, mtu anachukuliwa mke na bodaboda, kijana wa bodaboda anauliwa unaambiwa alikuwa Panyaroad.Mahakama zimewekwa za nini? Utajua fulani ni mwizi bila kumfikisha mahakamani? Huoni utaratibu wa aina hii unatoa mwanya kwa polisi kuua mtu yeyote kwa kisingizio kuwa ni mwizi? Hivi kama mna ugomvi na mtu, na huyo mtu akampa polisi fedha nyingi ili akupige risasi kwa kisingizio cha kuwa wewe ni mwizi huoni unaweza kuuawa bila sababu?
Kama ni polisi hawezi kumua mtu bila sababu from no where..kutakuwa na jambo limejificha nyuma ya pazia