Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Kuna siku nimerudi home nimekuta Rungu la mgambo mezani sebureni, nikauliza hili rungu la nani na limefikaje? Akanijibu langu, mmh nikamuuliza umelitoa wapi? Akajibu st Mary's, umepewa? Hapana nimelichukua nimekuta mlinzi kalala nimelibeba akiamka nitampa, nikachukua Rungu hadi St Mary's maana niniapoishi nyumba inaangaliana na hiyo shule nikamkuta mlinzi anahangaika kuitafuta silaha yake ya jadi, nikamwambia leo umechukuliwa Rungu kesho atasepa na mkwasa kuwa makini...kweli kesho yake nimemkuta tena dogo yupo na mlinzi mwingine nje ya geti anamuuliza hiyo bunduki gani? Unapiga? Inauwa jambazi? Naomba nione? Nikaona sasa huyu dogo anakoelekea sio kuzuri, maana mkiwa mnatazama movie ikiwa na ngumi utaulizwa maswali hadi kero, baba, yule ndo steering? Utajibu wee na muda mwingine na challenge namwambia hapa yule ni Audi, anasema wewe baba unazeeka vibaya yule sio adui yule ni stering bada unanidanganya, akiona bunduki anastuka kabisa utamsikia enheee hili ni bonge la muvi mi ndo napendaga, dogo anazingua nilichoamua nimempeleka kijijini akake huko japo miezi kazaa ili akirudi awe na akili zingine.....na huko kwa bibiyake alipo ni kesi za utundu tuu...chakula anapenda mrenda na ugali, na Tambi, ila ni mjinga akiwa na usingizi anakuwa kama kiteja flani hivi, hapendi kulala mchana. Ana miaka mi 3 na miezi 10, nimemuanzisha chokechea, ila ilibidi nimuhamishe maana anasema mwalimu wake hamfundishi vizuri na akifanya mazoezi yake mwalimu anamkataza...mtoto wangu mazoezi pekee anayojua yeye ni push ups..na wakati huyu bingwa anaanza kutembea kipindi ana mwaka amenitia hasara sana, alikuwa anakojolea simu na ktk fridge, yaani simu inaweza kuwa kitandani akahangaika akapanda akaishusha chini akaikojolea, Keisha akaitelekeza hapo akasepa zake, na ktk fridge ukiweka chakula unaweza kula mikojo anafungua anakojolea kisha anafunga anasepa....Namshukuru mungu sasa amekua na ninateseka na mdogo wake ambae yeye ni mabundi halali usiku.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Lol, huyu bingwa kiboko hafai duuh, nimecheka sana
 
Wa kwangu kipindi ana miaka miwili mpaka mitatu aje chumbani kwetu akute mmefunga mlango balaa lake mpaka majirani watajua, hivyo kama mlango umerudishiwa akiugusa tu lazima mmoja akimbie kuufungua kabla ya hajaanzisha timbwili
 
Ndio hivyo inatakiwa wadada wakazi wawe na mioyo yao mana kila saa inabidi asafishe.

Na kuna wale wanaopenda kuchezea maji kila saa anataka maji ya kunywa kumbe anataka ayachezee. Yaani ni kazi aisee.

Ila hatuna budi kushukuru kwa yote mana hata na sisi tulipitia huko hivyo tuwavumilia wakikua wataacha.
Huyu atakuwa ana elements za amphibia....[emoji2]
 
Nimewakuta watoto mtaani nikawapa chemsha bongo kuwa kwenye pipi tano ukitoa pipi moja zitabakia pipi ngapi?

Walichonijibu sasa[emoji23]

Eti tuonyeshe kwanza hizo pipi[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
leo nimenunua maparachichi ile kuingia ndani tu yeye kayapanga kayapiga kama mpira,nimetoka maparachichi yamekua rojooo...mwenyewe anaita mama mpiraa goooo....
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Wako wawili mdogo around 5 years. Tulienda bookshop na wote wawili, huyu mdogo yeye kitabu kikiwa size ndogo akajua ni chawatoto. Akajikusanyia vitabu kadhaa vyenye size ndogo akaleta kwa cashier. .
 
Mi mwanangu akisikia simu inaita hata kama alikuwa anacheza atakimbia kuniletea,anafurahi sana akiona naongea na simu ana mwaka na nusu bado hajajua kuongea anajua haloo na neno poa.
Hahahaaaa...Kama wangu hapa!!
 
Mi wa kwangu balaa natamani akue kidogo labda nitapata zuri la kueleza, leo ni wiki ya tatu sijalala nakesha, dogo analala mchana wakati mimi nipo job, usiku halali na akilala mikononi ukimuweka kitandani tuu yani kabla hata hujakiacha kitanda kishaamka na kelele nyingi, kingine asee usikae karibu na mamaake ugomvi wake c mdogo atalia hapo hadi utashangaa, kingine tangu wiki iliyopita hajacheka sijui ndo kutabasamu hakuna. Ana miezi 4. Hataki kulazwa kama watoto wengine anapokuwa macho, yeye anataka kukaa na anakaa...huyo ni mdogo, kakayake yeye anapenda ngumi, anajua bunduki zote kwa majina, hili nimejaribu kumuonya mamayake asiwe akimuwekea movie za mapigano zaidi ya cartoon lakini sijui huyu kijana anajifunzia wapi maana hakawii kukwambia anataka awe mwanajeshi sababu hapendi majambazi, huyo Ana miaka mi 4, anajua kikorea, kajifunza wapi mi sijui...ila ana shida moja anapenda tambi tuu, vyakula vingine kula mpaka mpigizane kelele sana na husingizia anataka kukojoa akienda harudi..ana huruma sana na mamayake, mjanja mjanja sana ukikasiririka atajua jinsi ya kukufanya ucheke tuu, shida usimuache na mdogo wake peke yao, unaweza kuta mtoto analishwa ugali.
Hapa nadhani hawa wanao wakalelewe jirani na mahakama
Na ikiwezekana wakae karibu na TL manake si kwa ukatili huu
 
Mi wa kwangu balaa natamani akue kidogo labda nitapata zuri la kueleza, leo ni wiki ya tatu sijalala nakesha, dogo analala mchana wakati mimi nipo job, usiku halali na akilala mikononi ukimuweka kitandani tuu yani kabla hata hujakiacha kitanda kishaamka na kelele nyingi, kingine asee usikae karibu na mamaake ugomvi wake c mdogo atalia hapo hadi utashangaa, kingine tangu wiki iliyopita hajacheka sijui ndo kutabasamu hakuna. Ana miezi 4. Hataki kulazwa kama watoto wengine anapokuwa macho, yeye anataka kukaa na anakaa...huyo ni mdogo, kakayake yeye anapenda ngumi, anajua bunduki zote kwa majina, hili nimejaribu kumuonya mamayake asiwe akimuwekea movie za mapigano zaidi ya cartoon lakini sijui huyu kijana anajifunzia wapi maana hakawii kukwambia anataka awe mwanajeshi sababu hapendi majambazi, huyo Ana miaka mi 4, anajua kikorea, kajifunza wapi mi sijui...ila ana shida moja anapenda tambi tuu, vyakula vingine kula mpaka mpigizane kelele sana na husingizia anataka kukojoa akienda harudi..ana huruma sana na mamayake, mjanja mjanja sana ukikasiririka atajua jinsi ya kukufanya ucheke tuu, shida usimuache na mdogo wake peke yao, unaweza kuta mtoto analishwa ugali.
Hapa nadhani hawa wanao wakalelewe jirani na mahakama
Na ikiwezekana wakae karibu na TL manake si kwa ukatili huu
 
Dogo ana miaka(4.6)akigundua kuwa umedanganya,utackia anasema ACHA MANENO YAKO BWANAA huwa naenjy sana
 
Back
Top Bottom