Viongozi CHADEMA kubalini ushauri

Viongozi CHADEMA kubalini ushauri

Too bad kitaingia kwenye mifumo ile ile iliyowekwa na serikali na kitakuwa weaked, aka chadema 2.0

Until mifumo ya uchaguzi na mazingira yatakapo badilishwa for good, haijalish chama gani kipya kitakuja. Hakutakuwa na changes
Mifumo ya UCHAGUZI haiwezi kubadilika kama vyama vya siasa Ambavyo ni pinzani ni ccm b vyote
 
Mifumo ya UCHAGUZI haiwezi kubadilika kama vyama vya siasa Ambavyo ni pinzani ni ccm b vyote
Nope itaweza badilika kama vyama vya upinzani vitarudisha umoja na mshikamano. Hakuna wakati upinzani ulikuwa na capability ya kuleta changes kama kipind cha UKAWA.

Ccm know this is why wanapenyeza watu wao ili yasitokee
 
Sawa hakuna kilichobadilika, lakini hata viongozi wa dini wamefahamu mbinu chafu zinazotumika dhidi ya vyama vya upinzani. Wangesusia hizo mbinu chafu zingebaki tu kama speculation. Kususia ni njia mojawapo ya ku'disapprove' jambo, lakini si njia pekee, na pia inategemea mazingira. Hapo unasema "watu wenye akili timamu" ni wangapi wanaoiunga mkono Chadema, ukilinganisha na "wasio na akili timamu" wanaoiunga mkono Chadema pia"? Wangesusia hata hao viongozi mia kadhaa wasingepatika. Lakini tayari angalau hao wamepatikana ni starting point.
Hizo mbinu chafu zimeanza Leo?
 
OK, mkuu. Sijielewi na sina akili timamu. Tufanye hivi: weka CV yako hapa na mimi nitaweka ya kwangu, halafu wachangiaji wengine wataamua nani mwenye akili timamu na anayejitambua kati yangu na wewe. Najizuia kutumia lugha kama unayoifumia, lakini ili twende sawa tuanze na CV.
CV ya Kwanza kabisa kwa hapa JF ni hoja mnazoandika hapa!
 
Nope itaweza badilika kama vyama vya upinzani vitarudisha umoja na mshikamano. Hakuna wakati upinzani ulikuwa na capability ya kuleta changes kama kipind cha UKAWA.

Ccm know this is why wanapenyeza watu wao ili yasitokee
Kwa akili Yako unavyoona Kuna chama Cha upinzani tanzania
 
Wananchi washajionea vya kutosha Magumashi ya chafuzi chini ya CCM toka mwaka 2019, wamejionea magumashi kwenye process nzima tangu utunzi wa sheria mbovu za uchaguzi. Wananchi wanahitaji kuongozwa ili kupuuza haya maigizo ya chafuzi. Sasa unfortunately Chadema inaflip flop, mara itoe tamko la kamati kuu kuwa bila katiba mpya haitashiriki chaguzi, mara ibadili gia angani. Sasa flipflop hizi wananchi wabayumbishwa na wengine wanapoteza imani hata na CHADEMA yenyewe.
Lakini pia wananchi wenyewe hawaaminiki hata kama ni jambo linalowahusu. Nilishashiriki nikiwa Malawi kwenye kutetetea haki za wakulima wa tumbuku. Kule zao kuu la biashara ni tumbaku - matajiri na watu wakubwa wana mashamba makubwa. Sasa tulitembelea mashamba kadhaa, wakulima wakatoa malalamiko yao: malipo madogo, na yanachelewa sana hata miaka 5 mtu haijalipwa, etc. Tuliorodhesha malalamiko yao, tukawahamasisha tufanye maandamano makubwa hadi kwa mkuu wa wilaya tuliyokuwemo. Sawa kwenye maandamano walikuja kama wakulima 200 hivi. Polisi walikataza, lakini tulipuuza katazo tuakaendelea na maandamano. Tulichokifanya hata kabla polisi hawajafika kazini, tulikuwa tumeshafika ofisi ya DC, na wakulima wetu tuliwaambia wasifanye fujo yoyote, wakati wa maandamano tukae kushoto mwa barabara kuruhusu watumiaji wengine wa barabara, na hakuna kuongea na mtu au kutoa sauti inayowabugudhi wengine. Kwa hilo tulifanikiwa, hadi kufikia na tukaa chini kwa utulivu. DC alipokuja, akatuuliza "mnataka nini", tukasema tuna malalamiko tunayotaka uyasikie na uyapeleke kwa Rais. Tuliandaa risala iliyogusa maeneo yote yanayolalamikiwa. Tulikuwa pia tumewaandaa BBC wakarusha maandamano yetu hewani. Baada ya risala, DC akasema "nimesikia malalamiko yenu, nitayafanyia kazi. Rudini mlikotoka kwa amani." Tukarudi. Baada ya wiki hivi tukapokea barua (sisi waratibu), kwamba tuwapeleke viongozi kadhaa wa serikali kwenye hayo mashamba yenye malalamiko. Tukawaandaa wakulima wetu kwamba siku fulani wanatakiwa wawe mashambani kwao, maana wakuu fulani kutoka serikalini watawatembelea. Siku ya siku, hao viongozi wakaja. Tukawapeleka. Kwenye hayo mashamba hatukukuta mtu, hata baada ya kukaa muda mrefu watu wajitokeze. Hao viongozi wakatuuliza "wakulima wanaolalamika wako wapi?" Tukakosa jibu. Nao wakarudi walikotoka, na matatizo ya wakulima yakaendelea. Kwa vile wenye mashamba baadhi yao walikuwa watu wakubwa serikalini, huenda walitoa vitisho kwa tenants wao kwamba "ole wenu mtu aende kuonana na hao viongozi, nitamfukuza!" Maana tenants walikuwa wanachukuliwa kutoka mbali, sasa ukifukuzwa na una malimbikizo ya malipo unayodai hata miaka 5 au zaidi, utakubali uende kwenye mkutano kweli? Sasa hapa nimetaka nioanishe hiki walichotufanyia hawa tenants waliotupa moyo tuwapiganie wapate haki zao, lakini wakatu'disappoint' na wananchi wasiojitambua: tatizo wanaliona, lakini wameaminishwa kwamba kudai haki yao "ni kushindana na serikali...na kwamba serikali ina mkono mrefu huwezi kushindana nayo." Unaona tatizo lilipo? Hivyo, hata chama kinaweza kuibua hoja yenye public interest, lakini support ya wananchi inakuwa ndogo sana. Mfano, suala la Katiba mpya, si huwa tunasikia baadhi ya wanasiasa kutoka chama tawala wakisema "wananchi hawahitaji katiba mpya, wanachohitaji ni maji, ajira, huduma za jamii, na ona miundombinu ilivyoboreshwa, etc... Sasa katika mazingira haya, unakuta wananchi wanarudi nyuma, na kuona hao wanasiasa ndio wanaowaambia ukweli.
 
Vilikuwepo until 2015, thats when upinzani ulikufa rasmi. Ulioko sasa uko controled, waanamua washinde nafas ngapi, wapi, kwa wakati gani.
Ndio maana nakuambia haiwezekani kufanya hivyo ulivyosema sababu hamna upinzani Kuna maigizo Ili kuonekane Kuna demokrasia nchini sababu watanzania sisi ni waoga bila kuwa na chama Cha upinzani watu wachache tukianzisha maandamano tutaitwa magaidi na kupigwa risasi sababu sisi hatuna silaha ya kujibu ofopa sana uitwe gaidi halafu huna silaha ya kujibu sababu utachakaa Kwa risasi na wewe huna ya kujibu
 
Lakini pia wananchi wenyewe hawaaminiki hata kama ni jambo linalowahusu. Nilishashiriki nikiwa Malawi kwenye kutetetea haki za wakulima wa tumbuku. Kule zao kuu la biashara ni tumbaku - matajiri na watu wakubwa Wana mashamba makubwa. Sasa tulitembelewa mashamba kadhaa, wakulima wanatoa malalamiko yao: malipo madogo, na yanachelewa sana hata miaka 5 mtu haijalipwa, etc. Tuliorodhesha malalamiko yako, tukawahamasisha tufanye maandamano makubwa hadi kwa mkuu wa wilaya tuliyokuwemo. Sawa kwenye maandamano walikuja kama wakulima 200 hivi. Polisi walikataza, lakini tulipuuza katazo tuakaendelea na maandamano. Tulichojifanya hata kabla polisi hawajafika kazini, tulikuwa tumeshafika ofisi ya DC, na wakulima wetu tuliwaambia wasifanye fujo yoyote, wakati wa maandamano tukae kushoto mwa barabara kuruhusu watumiaji wengine wa barabara, na hakuna kuongea na mtu au kutoa sauti inayowabugudhi wengine. Kwa hilo tulifanikiwa, hadi kufikia na tukaa chini kwa utulivu. DC alipokuwa, akatuuliza "mnaotaka nini", tukasema tuna malalamiko tunayotaka uyasikie na uyapeleke kwa Rais. Tuliandaa risala iliyogusa maeneo yote yanayolalamikiwa. Tulikuwa pia tumewaandaa BBC wakarusha maandamano yetu hewani. Baada ya risala, DC akasema "nimesikia malalamiko yenu, nitayafanyia kazi. Rudini mlikotoka kwa amani." Tukarudi. Baada ya wiki hizi tukapokea barua (sisi waratibu), kwamba tuwapeleke viongozi kadhaa wa serikali kwenye hayo mashamba yenye malalamiko. Tukawaandaa wakulima wetu kwamba siku fulani wanatakiwa wawe mashambani kwao, maana wakuu fulani kutoka serikalini watawatembelea. Siku ya siku, hao viongozi wakaja. Tukawapeleka. Kwenye hayo mashamba hatukukuta mtu, hata baada ya kukaa muda mrefu watu wajitokeze. Hao viongozi wakatuuliza "wakulima wanaolalamika wako wapi?" Tukakosa jibu. Nao wakarudi walikotoka, na matatizo ya wakulima yakaendelea. Kwa vile wenye mashamba baadhi yao walikuwa watu wakubwa serikalini, huenda walupeleka vitisho kwa tenants wao kwamba "ole wenu mtu aende kuonana na hao viongozi, nitamfukuza!" Maana tenants walikuwa wanachukuliwa kutoka mbali, sasa ukifukuzwa na una malimbikizo ya malipo unayodai hata miaka 5 au zaidi, utamkubali uende kwenye mikutano kweli? Sasa hapa nimetaka nioanishe hiki walichotufanyia hawa tenants waliotupa moyo tuwapiganie wapate haki zao, lakini wakatu'disppoint' na wananchi wasiojitambua: tatizo wanaliona, lakini wameaminishwa kwamba kudai haki yao "ni kushindana na serikali...na kwamba serikali Ina mkono mrefu huwezi kushindana nayo." Unaona tatizo lilipo? Hivyo, hata chama kinaweza kuibua hoja yenye public interest, lakini support ya wananchi inakuwa ndogo sana. Mfano, suala la Katiba mpya, si huwa tunasikia baadhi ya wanasiasa kutoka chama tawala wakisema "wananchi hawahitaji Katiba mpya, wanachohitaji ni maji, ajira, huduma za jamii, na ona miundombinu ilivyoboreshwa, etc... Sasa katika mazingira hayo, unakuta wananchi wanarudi nyuma, na kuona hao wanasiasa ndio wanaowaambia ukweli.

Wananchi wakipata viongozi shupavu wa upinzani wa kuaminika, utaona jinsi equation itakavyochange.

Mbowe kesha flipflop sana hana imani ya umma. Watu wanamiona keshanunuliwa na Samia, kwa hiyo hata akiitisha mass action. watu wanampuuza.
 
Hizo mbinu chafu zimeanza Leo?
Hazikuanza leo. Je, wananchi do they lack awareness or consciousness? Kwa maoni yangu, wananchi wanajua, lakini shida ni kujitambua, na kujitambua kunachukua muda. Na ndilo tatizo lililo hapa kwetu.
 
Hazikuanza leo. Je, wananchi do they lack awareness or consciousness? Kwa maoni yangu, wananchi wanajua, lakini shida ni kujitambua, na kujitambua kunachukua muda. Na ndilo tatizo lililo hapa kwetu.
Kujitambua kwa sehemu kubwa tayari. Wananchi wengi kususia uchafuzi ni dalili mojawapo. Kinachokosekana ni UMOJA kuelekea kuchukua hatua stahiki
 
Ndio maana nakuambia haiwezekani kufanya hivyo ulivyosema sababu hamna upinzani Kuna maigizo Ili kuonekane Kuna demokrasia nchini sababu watanzania sisi ni waoga bila kuwa na chama Cha upinzani watu wachache tukianzisha maandamano tutaitwa magaidi na kupigwa risasi sababu sisi hatuna silaha ya kujibu ofopa sana uitwe gaidi halafu huna silaha ya kujibu sababu utachakaa Kwa risasi na wewe huna ya kujibu
Tahrir square kulifanyika maanamano ya kumuondoa rais hosni mubarak, mwaka 2011. Raia wale hawakuwa na silaha, bali walikuwa na lengo moja
Polis waliwagonga sana, hawakurudi nyuma.
Waliitwa magaid, wakafungwa na kuuwawa


Baadhi ya nchi za africa ya kati zimefanya mapinduzi majuzi hapa? What is the difference?

Jamii ya mtanzania haina umoja. Umoja wao uko kwenye baadhi ya majanga na mambo yasiokuwa serious
 
Kujitambua kwa sehemu kubwa tayari. Wananchi wengi kususia uchafuzi ni dalili mojawapo. Kinachokosekana ni UMOJA kuelekea kuchukua hatua stahiki
Mimi sioni hivyo.
1) Kujitambua bado.
2) Hali ngumu ya maisha inafanya watu wachakalike, na mtu anaona kuliko kwenda kupiga kura, ngoja nikaingize shilingi moja, maana siwezi kula siasa.
3) Mtu aliyejitambua ataona kwamba tukiwa na viongozi bora mabadiliko chanya yatatokea kuliko hali ilivyo sasa.
4) Kwa hiyo, ataweka kipaumbele kwenye kushiriki kwake, na hatakubali haki yake ipokonywe kirahisi.
5) Asiyejitambua ni rahisi sana kupokonywa haki, na anaona hana la kufanya.
 
Hao nyumbu hawawezi kukuelewa.
JamiiForums-479349169.jpg
 
Kwani wewe ndiye CHADEMA auni mali yako?

Hivi huoni unavyo jionyesha kuwa juha, au mpaka uelezwe pointi kwa point jinsi ujuha wako ulivyoi?
Huoni kuwa wewe ni zaidi ya juha,!

Wewe una akili gani kuzidi strategists wa CHADEMA hadi ung'ang'anie wafuate mawazo yako.

Mimi sio mwanachama wa CHADEMA ila nakushangaa wewe unavyodhani unaweza kuwachuuza CHADEMA .
 
Kutoshiriki uchaguzi sio ufumbuzi wa tatizo.mabadilikko yakutoka kwenye ujinga kwenda kwenye werevu na ustarabu kwa sisi waafrika sio kazi ya siku moja.Hadi sasa sisi sio kizazi cha binadamu wastarabu ndo mana mambo kama haya yakijinga bado yapo,sasa hayawezi kuisha bila kuendelea kuyaweka wazi,iko siku kitapatikana kizazi cha wenye akili tofauti nazakwetu wakaamua kubadilisha historia.Pole pole tutafika tu.
 
Back
Top Bottom