Viongozi gani hao waliomuona “Dada wa Watu Nyani” na waimbaji wenzake?

Viongozi gani hao waliomuona “Dada wa Watu Nyani” na waimbaji wenzake?

alimtaja kwa majina, na baada ya kuondolewa na kupewa ubalozi, ameendelea kusema hajaridhishwa alitakiwa aachishwe kwazi kabisa na ashitakiwe. sema wameamua kumpuuza tu na yeye anaendelea kuwachafua.
Kwani huyo mwanaye alikuwa na nafasi gani katika jamii hadi TISS imuone ni mtu hatarishi kwa Usalama wa Taifa letu?

Ni siri gani nyeti alizokuwa nazo?
 
Kwani huyo mwanaye alikuwa na nafasi gani katika jamii hadi TISS imuone ni mtu hatarishi kwa Usalama wa Taifa letu?

Ni siri gani nyeti alizokuwa nazo?
of course ukimsikiliza sana mbarikiwa utakuta ni nadharia tu, hakuna uhalisia. yeye anaamini walifanya hivyo ili kumkoma yeye kwasababu ya usumbufu wake. kama walikuwa na uwezo kufanya hivyo, si wangemmaliza yeye badala ya mtoto? kwamba mbarikiwe ndio awe mtu wa muhimu sana kwa serikali kwa sababu tu ametaka kufungua kanisa? au ndio serikali iwe imemshinda kweli hadi iende kwa mwanae?, inaonyesha kidogo kama nati zimelegea kichwani kwake. ni frustrations tu.
 
of course ukimsikiliza sana mbarikiwa utakuta ni nadharia tu, hakuna uhalisia. yeye anaamini walifanya hivyo ili kumkoma yeye kwasababu ya usumbufu wake. kama walikuwa na uwezo kufanya hivyo, si wangemmaliza yeye badala ya mtoto? kwamba mbarikiwe ndio awe mtu wa muhimu sana kwa serikali kwa sababu tu ametaka kufungua kanisa? au ndio serikali iwe imemshinda kweli hadi iende kwa mwanae?, inaonyesha kidogo kama nati zimelegea kichwani kwake. ni frustrations tu.
Kwa maelezo haya, naiunga mkono Serikali kwa hatua inazochukua dhidi ya huyu hayawani Mwakipesile
 
Mpaka hapa uko sawa.

Ila ukweli halisi ni kuwa hana bifu na TISS Kwa ujumla wake bali na baadhi tu ya viongozi wake hususani aliyekuwa DG wao ambaye sasa ni balozi somewhere huko nchi za kigeni

Ndugu Huihui2 ni wazi huna taarifa sahihi na za kutosha juu ya mgogoro huu kati ya mchungaji huyu na polisi/serikali.

Iko hivi;

1. Huyu ndugu humtaja aliyekuwa DG wa TISS direct kuwa ndiye aliyeua mwanae. Kama tuhuma ziko direct kiasi hiki kwa muhusika tena akitajwa kwa jina lake, tunadhani ni kwanini mamlaka na vyombo husika havichukui hatua? Au ni haki kwa kiongozi kuua?

2. Na kabla ya hapo upo mgogoro wa kukataliwa kusajiliwa kwa taasisi/kanisa lake licha ya kufuata taratibu zote ikiwemo kuwasilisha nyaraka zote zunazotakiwa kisheria. Amefuatilia Dodoma na DSM miaka na miaka mpaka kachoka. Ameingia kila mlango wa ofisi ya serikali lakini yote imefungwa, hapati msaada na hasikilizwi. Njia pekee aliyobaki nayo kupambania haki yake ni mdomo......yaani kupiga kelele na kusema kila kitu

3. Haya yakiwa yanaendelea, akawa amefunguliwa kesi mahakama ya Mbeya. Kwa maelezo yake ni kuwa hata huko mahakamani watesi wake hapa wameshafika na wameikamata mahakama ili tu kuhakikisha hapati anachokitaka..!

## Katika mazingira haya kwanini mtu asifikiri kuwa labda yeye na watu wake wanaonekana ni manyani (wanyama) tu wasiostahili kutendewa kama wanadamu?

1. Hueleweki ndugu Huihui2. Wanamshauri kitu gani kama yule anayesemekana ameua mtoto wake yupo analindwa na kutamba mitaani? Hapa si ishu ya kishauri bali ni sheria kuchukua mkondo wake.

2. Wanafanya kiburi gani? Unataka waunyamazie na kuunyenyekea uovu na waovu?

Kama hawa watumishi wa Mungu wanachofanya ni kukemea matendo maovu, wizi, uonevu, ufisadi na kutowajibika Kwa viongozi wenye dhamana serikali unatafsiri kama "kuoneshana umwamba na serikali", basi huu umwamba Kila mpenda HAKI ni lazima auonge mkono..

Hujui usemalo na huijui historia ya kanisa wewe. Nitakupa mifano michache toka kwenye Biblia..

1. Unamjua Mfalme (Rais) wa kwanza kutawala wanadamu aliyeitwa Sauli wakati wa utumishi wa Mungu Nabii Samweli? Unajua nini kilimtokea Mfalme huyu baada ya serikali yake kuwa ya mabavu na kuonea watu huku yeye mwenyewe Mfalme akimkufuru Mungu ktk kiwango cha kutisha sana? Kama hujui, nakuambia kuwa utawala wake ulianguka na yeye mwenyewe Mfalme Sauli kufutiliwa mbali (kufa) kwa sababu ya maombi ya Nabii Samweli. [Soma kisa hiki kwenye Biblia yako kitabu cha 1 Samweli 15:1 - 35]

2. Pia soma 1 Wafalme 18:1-46 utakutana na kisa kilichorekodiwa cha mtumishi wa Mungu Nabii Eliya dhidi ya utawala wa Mfalme (Rais) Ahabu na mkewe Malkia Yezebel waliokuwa wanatawala nchi na watu kwa kutumia nguvu za miungu iliyoitwa Baali na kuleta mateso na mahangaiko kwa wananchi na watumishi wengi wa Mungu. Kanisa likiwakilishwa na Mtumishi wa Mungu Nabii Eliya lilisimama imara na kuukemea uovu huo. Utawala wa Ahabu ulianguka yeye na mkewe wakafyekelewa mbali..

3. Soma pia kisa cha Mfalme Farao [soma Biblia yako kitabu cha Kutoka sura 4 - 10 na mkazo zaidi sura ya 11] wa Misri ya kale alivyokuwa na kiburi na kutesa na kuwadharau watumishi wa Mungu Lakini kwa maombi na sala za watumishi wa Mungu, utawala wake ulianguka na kupotea mpaka leo yeye mwenyewe na jeshi lake lote na silaha zake nzitonzito kama vile, magari ya washawasha, mabomu ya machozi, bunduki na vifaru walifia na kuzikwa chini ya vilindi vya bahari ya Shamu mpaka leo.

Point hapa ni kuwa si kweli kuwa hakuna serikali iliyowahi kuangushwa na maombi ya watumishi wa Mungu BALI kinyume chake ni kuwa, hakuna serikali yoyote duniani ambayo iliwahi kupambana na kanisa la Mungu aliye hai (au sema watumishi wa Mungu) na serikali ikabaki salama, imesimama..!!

Na Tanzania mgogoro huu unaoendelea kati ya KANISA na serikali, hakika anguko la serikali liko wazi kuliko unavyofikiri..!
Mungu akubariki sana ndugu Uzima Tele .
Nilikuwa na hasira sana na mambo kadhaa yanayoendelea nchini mwetu,ila baada ya kusoma mchango wako huu juu hapo,nimejikuta narudi kwenye maandiko na hasira zote kuisha.
Ubarikiwe sana.
 
Huyo dada ni mfuasi wa Mchungaji Mwakipesile wa Isyssye Mbeya. Mchungaji huyu ana bifu na TISS. Sasa amejiingiza kushambulia serikali bila sababu akisema wamemuulia mwanaye tena Mkurugenzi wa usalama wa Taifa ndio kafanya hivyo. Jamaa hashauriki, vijana wake hao waliokamatwa hawashauriki wao wanatokana na kujiona wajuaji. Kiburi, kutojinyenyekesha, ujuaji mara nyingi huenda kwenye anguko.

Sasa kumezuka wimbi kubwa la watumishi wanaosimama na kuoneshana umwamba na serikali. Hakuna duniani mtumishi wa Mungu aliwahi ishinda dola nasi wajibu wetu ni kushauri na kuiombea mamlaka na siyo kushindana nayo
Kikinuka msebule mkuu tiss yenyewe mchumba tu
 
Habari za jumapili!

Leo nimebahatika kuusikia wimbo wa mwanadada mmoja ambaye nimemfahamu kupitia wimbo huo.

"Mnatuona Nyani" ndio jina la wimbo huo.

Huyo dada amelalama, amelalamika, ametoa dukuduku lake, ametoa yamoyoni mwake, ametoa yanayomsibu, ametoa mtazamo wake dhidi ya wale wanaomkashfu, wale wanaomtazama kama Nyani, wanaomfanyia kama Nyani.

Aaaa! Dada wa Watu Kalia. Dada wawatu kagaragara.

Hao viongozi waliomuona huyu Dada kuwa ni Nyani NI kina Nani?

Wimbo ule ulinitia huzuni, nilijikuta na ng'ata Meno, agriii! Mpaka mwisho sikusikia jina la kiongozi yeyote aliyetajwa.
Nilitaka kuwajua hao viongozi wanaomuona huyo Dada wawatu kuwa ni Nyani. Hao viongozi washughulikiwe.

Baadaye tena nasikia amekamatwa. Jamani! Embu Polisi twendeni polepole. Dada wawatu analalama, anahitaji msaada, anatoa mtazamo wake, Mbaya zaidi hakuna aliyekuwa anamjua, hata Mimi Taikon Master sikuwa namjua.
Msikilizeni, tendeni mambo Kwa utulivu, Hekima na Busara.

Hii nchi inawatu tofauti, wengine wanaona wanaonekana Nyani na watu wengine. Wengine wanawaona Nyani wengine bila ya wao kujua au Kwa kujua kupitia Matendo Yao, maneno Yao, mitazamo Yao n.k.

Nataka kujua ni viongozi gani hao waliomuona huyo Dada na waimbaji wenzake kuwa ni Nyani?

Mmemkamata ili kumsaidia awatajie hao viongozi Mtakuwa mmefanya vyema. Lakini kama ni vinginevyo mtakuwa hamtendi haki
Nilisikia

Habari za jumapili!

Leo nimebahatika kuusikia wimbo wa mwanadada mmoja ambaye nimemfahamu kupitia wimbo huo.

"Mnatuona Nyani" ndio jina la wimbo huo.

Huyo dada amelalama, amelalamika, ametoa dukuduku lake, ametoa yamoyoni mwake, ametoa yanayomsibu, ametoa mtazamo wake dhidi ya wale wanaomkashfu, wale wanaomtazama kama Nyani, wanaomfanyia kama Nyani.

Aaaa! Dada wa Watu Kalia. Dada wawatu kagaragara.

Hao viongozi waliomuona huyu Dada kuwa ni Nyani NI kina Nani?

Wimbo ule ulinitia huzuni, nilijikuta na ng'ata Meno, agriii! Mpaka mwisho sikusikia jina la kiongozi yeyote aliyetajwa.
Nilitaka kuwajua hao viongozi wanaomuona huyo Dada wawatu kuwa ni Nyani. Hao viongozi washughulikiwe.

Baadaye tena nasikia amekamatwa. Jamani! Embu Polisi twendeni polepole. Dada wawatu analalama, anahitaji msaada, anatoa mtazamo wake, Mbaya zaidi hakuna aliyekuwa anamjua, hata Mimi Taikon Master sikuwa namjua.
Msikilizeni, tendeni mambo Kwa utulivu, Hekima na Busara.

Hii nchi inawatu tofauti, wengine wanaona wanaonekana Nyani na watu wengine. Wengine wanawaona Nyani wengine bila ya wao kujua au Kwa kujua kupitia Matendo Yao, maneno Yao, mitazamo Yao n.k.

Nataka kujua ni viongozi gani hao waliomuona huyo Dada na waimbaji wenzake kuwa ni Nyani?

Mmemkamata ili kumsaidia awatajie hao viongozi Mtakuwa mmefanya vyema. Lakini kama ni vinginevyo mtakuwa hamtendi HAKI.
Nashangaa mbona mbunge wangu walikuwa wanamwita sokwe,siku moja akaamua kuwa mandonga baada ya kupigwa picha,sikuona polisi aliemsaidia.
 
Hivi DG wa TISS anamkuta wapi mtoto wa Mwakipesile mpaka amuue? Kwa kitu gani hasa.?
Una akili kweli wewe kwa kuuliza hili swali?

DG is not a person. Is an institution. Amri tu inatosha kumaliza kila kitu..

Kuhusu kanisa lake kusajiliwa, nafikiri hajakidhi vigezo vya kusajiliwa otherwise angekuwa amekwisha pewa usajili. Lakini hata mimi ningekuwa MSAJILI wa madhehebu nisingempa usajili kwa namna kichwa chake kinavyopata moto. Yule ni mgonjwa wa akili na anahitaji tiba.
Huna taarifa za kutosha na ndiyo maana "unafikiri" tu.

Kwa taarifa yako hiyo ya "kutokidhi vigezo" sio sababu hata chembe. Sababu ni kuisema na kukemea uovu na maovu ya serikali na viongozi wake serikali na hivyo kuwakera wana wa ibilisi na wao kutumia vibaya mamlaka yao kukomoa watu kama huyu..!
Kuhusu mifano ya Biblia. Nakuomba tu ushukiwe na Roho Mtakatifu ili akuwezeshe upate ufahamu mzuri wa Biblia na siyo kunukuu hovyo kama ulivyonukuu.
Haa haa 🥺🥺🥱🥱. Pole sana ndugu
Kwa hiyo wamuona huyo mwendawazimu Mwakipesile sawa na Nabii Eliah?
Si tu kumlinganisha na Nabii Eliya bali na Yesu Kristo mwenyewe kama anavyosema;

Mathayo 21:21
"....Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka..."
Na nyie Mapentekoste ndiyo mnasbabisha Waisalmu watudharau Wakristu kwa hivyo vimadhehebu uchwara vyenu.
Asimamaye katika kweli ya Mungu huwa hasubiri kuheshimiwa na watoto wa yule mwovu maana wao siku zote hupingana na haki na kweli ya Mungu.

Yesu hakuwa kuheshimiwa ktk maisha yake yote hapa duniani..
Kanisa gani litakuwa Isyesye kwenye kichochoro ndani ya pagala?
Unaelewa maana ya "kanisa?". Maana yake ni hii👇👇

1 Wakorintho 6: 19-20
"...Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu...?" Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

Mtu awe anaishi Isesye au shimoni, kijijini, milimani au mjini au kibandani au kwenye jengo lenye ghorofa, ama popote pale ili mradi ana roho mtakatifu ndani yake basi huyo ndiye kanisa na Mungu anaishi ndani yake..!!
Nyie siyo wa Mungu bali ni wa shetani tu
Haishangazi. Yesu hakuitwa wa shetani tu bali aliambiwa na watu wanafiki na wasiojua dizaini yako kuwa "ana pepo belizebuli".

Na shida yako wewe Huihui2 ni moja tu. Ni kwa sababu hujui tu. Ukijua utawajua walio wa Mungu na walio wa shetani kwa urahisi sana
Mungu akubariki sana ndugu Uzima Tele .
Nilikuwa na hasira sana na mambo kadhaa yanayoendelea nchini mwetu,ila baada ya kusoma mchango wako huu juu hapo,nimejikuta narudi kwenye maandiko na hasira zote kuisha.
Ubarikiwe sana.
Amen🙏🙏 ndugu residentura
 
Huyo dada ni mfuasi wa Mchungaji Mwakipesile wa Isyssye Mbeya. Mchungaji huyu ana bifu na TISS. Sasa amejiingiza kushambulia serikali bila sababu akisema wamemuulia mwanaye tena Mkurugenzi wa usalama wa Taifa ndio kafanya hivyo. Jamaa hashauriki, vijana wake hao waliokamatwa hawashauriki wao wanatokana na kujiona wajuaji. Kiburi, kutojinyenyekesha, ujuaji mara nyingi huenda kwenye anguko.

Sasa kumezuka wimbi kubwa la watumishi wanaosimama na kuoneshana umwamba na serikali. Hakuna duniani mtumishi wa Mungu aliwahi ishinda dola nasi wajibu wetu ni kushauri na kuiombea mamlaka na siyo kushindana nayo
Hiyo Dola inadondoshwa kutoka angani? Ni ya kutishia? au ni ya kuwatumikia wananchi?
 
Una akili kweli wewe kwa kuuliza hili swali?

DG is not a person. Is an institution. Amri tu inatosha kumaliza kila kitu..

Kuhusu kanisa lake kusajiliwa, nafikiri hajakidhi vigezo vya kusajiliwa otherwise angekuwa amekwisha pewa usajili. Lakini hata mimi ningekuwa MSAJILI wa madhehebu nisingempa usajili kwa namna kichwa chake kinavyopata moto. Yule ni mgonjwa wa akili na anahitaji tiba.
Huna taarifa za kutosha na ndiyo maana "unafikiri" tu.

Kwa taarifa yako hiyo ya "kutokidhi vigezo" sio sababu hata chembe. Sababu ni kuisema na kukemea uovu na maovu ya serikali na viongozi wake serikali na hivyo kuwakera wana wa ibilisi na wao kutumia vibaya mamlaka yao kukomoa watu kama huyu..!

Haa haa 🥺🥺🥱🥱. Pole sana ndugu

Si tu kumlinganisha na Nabii Eliya bali na Yesu Kristo mwenyewe kama anavyosema;

Mathayo 21:21
"....Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka..."

Asimamaye katika kweli ya Mungu huwa hasubiri kuheshimiwa na watoto wa yule mwovu maana wao siku zote hupingana na haki na kweli ya Mungu.

Yesu hakuwa kuheshimiwa ktk maisha yake yote hapa duniani..

Unaelewa maana ya "kanisa?". Maana yake ni hii👇👇

1 Wakorintho 6: 19-20
"...Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu...?" Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

Mtu awe anaishi Isesye au shimoni, kijijini, milimani au mjini au kibandani au kwenye jengo lenye ghorofa, ama popote pale ili mradi ana roho mtakatifu ndani yake basi huyo ndiye kanisa na Mungu anaishi ndani yake..!!

Haishangazi. Yesu hakuitwa wa shetani tu bali aliambiwa na watu wanafiki na wasiojua dizaini yako kuwa "ana pepo belizebuli".

Na shida yako wewe Huihui2 ni moja tu. Ni kwa sababu hujui tu. Ukijua utawajua walio wa Mungu na walio wa shetani kwa urahisi sana

Amen🙏🙏 ndugu residentura
Takataka tu hizi, hatuwezi kuziacha zikaendelea nchini kwetu. Lazima mamlaka zisafishe madhehebu uchwara yanayoibuka Mbeya kila uchwao
 
Back
Top Bottom