Uchaguzi 2020 Viongozi wa CHADEMA hatua mlizochukua zitawatia aibu kubwa

Uchaguzi 2020 Viongozi wa CHADEMA hatua mlizochukua zitawatia aibu kubwa

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Hii ni dalili kuwa hamlitakii mema taifa letu na ipo siku mtaliletea janga kubwa. Ndio maana aliyekuwa mbunge wa Temeke kupitia CCM aliwahi kutoa ombi kuwa Chadema ni chama cha wapenda vurugu hivyo kinastahili kufutwa.

Baada ya kushindwa uchaguzi kwenye box la kura na wananchi kuichagua Ccm sasa mnataka kuiaminisha jumuia ya kimataifa kuwa hapa Tanzania kuna ukiukwaji wa haki za binadamu. Je mbona mlipokuwa wabunge hizi propaganda zenu hatukuzisikia?

Sasa hivi mmezua mchezo mchafu eti mnatafuta hifadhi kama wakimbizi wa kisiasa kuwa kuna tishio la kuuliwa na vyombo vya dola. Mnachotaka tu ni kuchafua taswira ya nchi yetu kuwa hakuna amani na kuna ukiukwaji wa haki za binadamu. Je kama kuna ukiukwaji wa haki za binadamu mbona UN wapo kimya na wana ofisi hapa Tanzania.

Kama vyombo vya dola vilitaka kumuua G Lema wangemuacha yupo salama wiki zote hizi mbili tangu uchaguzi uishe? L Nyalandu anatafuta kick kuwa anakimbia kuuliwa hivi mwanasiasa ambae unataka kuuliwa watu watakuacha hizi siku zote upo salama?

Godbless Lema alipokuwa mbunge alikumbana na kesi nyingi sana,na mpaka alikaa mahabusu miezi minne mbona alipotoka mahabusu hakukimbilia Kenya kwenda kuomba hifadhi kama mkimbizi wa kisiasa?

Kwa ujumla ni kutokubali matokeo ndio sababu ya kutaka kuchafua taswira ya nchi yetu. Na kukosa ubunge ambao kwenu mlidhania nia ajira za kudumu ndio sababu mnataka kwenda kujifanya wakimbizi.

Na hii propaganda mlioamua kuitumia itabuma na mtaaibika zaidi na huu ndio unaenda kuwa mwisho wenu mbaya kisiasa. Maana watanzania wana akili na hawadanganywi kitoto.

Nota bene : Kila propaganda mlizoanzisha zote zilibuma,kumbukeni wakati wa Covid-19 mlipata aibu kubwa,amabayo imewanyima kura.
 
Chagu wa malunde mbona unaoonekana kukerwa na mtu kutafuta usalama wa maisha yake?
Au wewe ni mmoja wa wanaotumwa kuua viongozi wa chadema?

Mmevuruga nchi alafu mnataka muonekane wasafi mbele ya jumuiya ya kimataifa
 
Kama mmeshindwa kumuhakikishia Lissu ulinzi wake mpaka leo, unataka wafanyeje? unaweza kukaa sehemu usiyo na amani?

Upinzani sio uadui, fungueni akili zenu.
Amefanya kampeni miezi miwili kuna mtu alimgusa? Nchi hii inafuata misingi ya sheria. Anaogopa nini?
 
Hivi kuna aibu kubwa kama alichofanya CCM na Bwana yule kuiba kura na kuua watu ili atawale Kwa nguvu? Au hujui aibu maana yake? Shame on you na vizazi vyenu
Kura ziliibiwa wapi? Mnatengeza clip za uongo kuaminisha watu upuuzi! Kama waliiba si mfungue kesi na sio kwenda nje kuwa wakimbizi.
 
Rais amesema leo Dodoma hatafanya uteuzi zaidi ya Baraza Mawaziri. Labda mtoa mada waweza kupata nafasi kwenye Baraza, kwa wakuu wa mikoa, wilaya na Ma - DED, DAS na RAS hafanyi mabadiliko.
Uteuzi unahusika vipi? Jadili mada iliyopo mezani.
 
mataga punguza jazba.
sio mimi niliyesitisha maswala ya uteuzi bali ni mwenyekiti wa chama chako.
Mimi nafanya shughuli zangu, njoo Segese uone tunavyopambana. Habari za uteuzi ni za kishamba na washamba kama wewe ndio wanazifikiria.
 
Hii ni dalili kuwa hamlitakii mema taifa letu na ipo siku mtaliletea janga kubwa. Ndio maana aliyekuwa mbunge wa Temeke kupitia CCM aliwahi kutoa ombi kuwa Chadema ni chama cha wapenda vurugu hivyo kinastahili kufutwa....
Acha porojo. Kuna watu walipigwa risasi 16. Wewe unajua mpaka mtu akimbie nyumba na biashara zake ni mchezo siyo? Tena mwanaume? Shut up.
 
Yetu tunasubiri yenu tayari mnayo.
Sasa hivi Tz ni sawa na mtetea anaepulizwa na upepo...
Sawa na kauli aliyowahi kutoa Selelii.
Hata wakati wa Covid -19 mlikuwa wabishi,matokeo mmeyaona kwenye box la kura.
 
Back
Top Bottom