Viongozi wengi wanaoamini ukimpinga unastahili kuuawa wanaongezeka, tupambane nao kwa sala kabla hatujaingiwa na roho kama zao

Viongozi wengi wanaoamini ukimpinga unastahili kuuawa wanaongezeka, tupambane nao kwa sala kabla hatujaingiwa na roho kama zao

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Tumeendelea kuwa na viongozi wengi ambao wao wakiona unakinzana na maoni au maslahi Yao wapo tayari kutumia mbinu zozote aidha wakuondoe au wakufanye unyamaze. Wao kwao siyo Kila uhai ni wa thamani, uhai kwao ni wa watoto wake, mke au Mme, wazazi na ndugu damu.

Hawa watu wanaongezeka Kwa Kasi na wanaonekana Kwa matendo. Wanaishi na kutamani watu wote waishi, wakisikia flani kapigwa utasikia chama Gani, flani katekwa utasikia chama Gani, wakisikia flani kawekwa mahabusu kinyume cha sheria swali lao ni chama Gani. Kama aliyefanyiwa hivyo siyo wa chama chake utasikia hayanihusu kila mmoja ashinde mechi zake.

Akitoka hapo anaingia msikitini au kanisani na kutoa neno au salamu akiomba amani, upendo na mshikamano. Hawa ndio binadamu wanaoendelea kupewa madaraka. Kiongozi anafikia hatua anasema chama kwanza mengine baadaye, au anasema yeyote atakayegusa maslahi ya chama changu ataondoka yeye......na watu wanapiga makofi.

Unajua tunaelekea wapi? Tunaelekea kurithisha watoto wetu hizi roho za kuthamini madaraka na chama kuliko watu. Tunaelekea kufanya ubaya unaofanywa Kwa asiye wa mrengo wetu uwe halali na anaofanyiwa wa mrengo wetu uwe hatia.

Tunapoelekea 2022 viongozi wa Dini wakiendelea kumtukuza mwandamu kuliko Mungu, wakishindwa kukemea badala yake wakasifia, wakishindwa kukataa wadhalimu kupewa nafasi kwenye nyumba za ibada tutaongeza wahalifu na hata hizo Dini hazitakiwepo Tena.

Niwaombe viongozi wa Dini mridhike na kile alichowapa Mwenyenzi Mungu na mjipe moyo mkuu wakusimamia ukweli na kukemea maovu pasipo na hofu ya kudhuriwa na wanadamu ambao ajuaye kesho Yao ni Mungu.
 
Hakika umeandika jambo la msingi sana.

Mimi napata shida sana na viongozi wa zama hizi ambao kwao kusifiwa na kuabudiwa wanaona sawa.

Naamini kabisa kuwa kiongozi mzuri atatambulika kwa kazi zake,na si kwa kusifiwa.

Vijana (hasa UVCCM) wa sasa hawawezi kushindana kwa hoja zaidi ya vitisho na mikwara mbuzi.

Hakika CCM ile tunayoijua ya kulumbana kwa hoja iliondoka na wakina Kolimba na Gama.
 
Hakika umeandika jambo la msingi sana.
Mimi napata shida sana na viongozi wa zama hizi ambao kwao kusifiwa na kuabudiwa wanaona sawa..
UVccm wamejaa wajinga walio jivika taji la uzalendo mbuzi wa kutumikia chama kuliko taifa kutwa kutisha watu sababu wametofautiana mtizamo juu ya Jambo fulani wanawaza teuzi bila kujua matokeo ya hizo harakati zao za hovyo kwa maisha yao Leo hii yuko wapi Sabaya waliye mpa sifa kwamba anakitetea chama
 
Tumeendelea kuwa na viongozi wengi ambao wao wakiona unakinzana na maoni au maslahi Yao wapo tayari kutumia mbinu zozote aidha wakuondoe au wakufanye unyamaze. Wao kwao siyo Kila uhai niwathamani...
Hiyo roho mbaya sana ilishamiri zaidi wakati wa utawala wa Magufuli.

Wengi wameathirika kwa kupotea, kubambikwa kesi za uhujumu uchumi, au kufukuzwa nyadhifa zao.

Na ni kweli, halafu alikuwa anaenda madhahabuni kusema nchi hii inataka amani na upendo, na kwamba yeye mtu wa wanyonge!
 
Chacha wangwe alipotangaza nia ya kuwania uenyekiti wa chama, sote tunajua yaliyomkuta!

Zitto kabwe alipoonyesha nia ya kuwania uenyekiti alifurushwa kwenye chama kama mbwa koko!

Tundu lisu alipoanza kuwa maarufu kuzidi wenye chama, sote tunajua yaliyomkuta!

Do we need more evidence?
 
Chacha wangwe alipotangaza nia ya kuwania uenyekiti wa chama, sote tunajua yaliyomkuta!
Zitto kabwe alipoonyesha nia ya kuwania uenyekiti alifurushwa kwenye chama kama mbwa koko!
Tundu lisu alipoanza kuwa maarufu kuzidi wenye chama, sote tunajua yaliyomkuta!
Do we need more evidence?
Akili zako bhana....

"Haiwezekani ukawa msaliti then ukasurvive, askari wanajua nini cha kufanya mmoja wao akisaliti wakiwa vitani''
2hrs later... Mtu anashonwa risasi zaidi ya 36....

ooooooh ile ile... Ni ileileee.
 
Chacha wangwe alipotangaza nia ya kuwania uenyekiti wa chama, sote tunajua yaliyomkuta!
Zitto kabwe alipoonyesha nia ya kuwania uenyekiti alifurushwa kwenye chama kama mbwa koko...
Yap maana allegation zako zimeishia njiani. Umeandika hints tu which sio evidence. Evidence ni muhim zaid
 
Chacha wangwe alipotangaza nia ya kuwania uenyekiti wa chama, sote tunajua yaliyomkuta!
Zitto kabwe alipoonyesha nia ya kuwania uenyekiti alifurushwa kwenye chama kama mbwa koko!
Tundu lisu alipoanza kuwa maarufu kuzidi wenye chama, sote tunajua yaliyomkuta!
Do we need more evidence?
Kesi ya Ugaidi inyomkabili Mbowe sasa hivi imekuja kufuta huu ujinga unaojaribu kuwapaka CHADEMA kwamba waliwashambulia wenzao kwa sababu ya madaraka na umaarufu. Mbowe yuko mahabusu karibia miezi 6 kwa sababu ya kuajiri walinzi waliokuwa Wanajeshi na kuwatumia fedha inayofikia 600,000 kujikimu.

Yaani amefadhili Ugaidi kwa 600,000??? Ingekuwaje kwake kama ndyie angekuwa amehusika kwenye shambulizi la Lissu? Ingekuwaje kama ajali ya Mh Chacha Wangwe ingekuwa na mkono wa mtu na mtu huyo akawa Mbowe au Mnyika?

Suala la Zitto Kabwe hata mtoto anayeanza kujua nini maana ya uongozi anajua, hata yeye mpaka Leo anajuta kwa alichokifanya na matokeo ya alichofanya.

Kuhusu umaarufu wa Lissu kutisha wenzake hicho ni kichekesho, Chama kinahitaji watu maarufu ili kuwa Icon. Zitto aliwahi kuwa Icon ya CHADEMA baada ya kufukuzwa bungeni kwa kutoa hadharani kashfa ya Waziri kusaini mikataba ya madini ya Tanzania hotelini Uingereza wakati kuna Ofisi za Ubalozi, umaarufu huu ndo uluomfanya akavimba na kufanya aliyofanya kinyume na taratibu za Chama.

Zitto angekuwa na Subira ndiye angekuwa mgombea wa CDM 2020 akiwa amekomaa, lakini akawa na haraka. Kila siku makosa ya watawala yanawaibua Mashujaa wa upinzani na kuwapa umaarufu.

Mbali ya jitihada binafsi na uthubutu wake lakini LISSU aliongezewa umaarufu na matamko ya Magufuli kumwita Msaliti na masaa 2 baadaye LISSU kupigwa risasi kama alivyotangaza Magufuli wakati akipokea ripoti ya madini ya Kamati ya Profesa Osollo na wenzake.
 
Chacha wangwe alipotangaza nia ya kuwania uenyekiti wa chama, sote tunajua yaliyomkuta! Zitto kabwe alipoonyesha nia ya kuwania uenyekiti alifurushwa kwenye chama kama mbwa koko! Tundu lisu alipoanza kuwa maarufu kuzidi wenye chama, sote tunajua yaliyomkuta! Do we need more evidence?
You are stupid, nicompoop,ancooth, uncivilized, and many more.

Chadema Wana intelligence Kali kuliko serikali? Mbona serikali haijabainisha Hilo na akakamatwa mhusika kwa Hilo.

Kumbe wote hatupo salama Kama serikali haiwezi kudetect tukio lolote ndani ya nchi zaidi ya maonesho ya kubeba magogo na kuvunja matofali.
 
Shida uanzia kwenye malezi.Wafrika wengi awajui malezi bora ya watoto,wanadhani kumfokea,kumtusi, viboko ndio malezi bora kumbe wanaandaa madikteta,thus tuna unakuta DC au RC anazidiwa hoja anaomba msaada police utasikia OCD kamata huyu weka ndani,akishakaa ndani halafu,ndo hoja zimejibiwa.
 
Back
Top Bottom