Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere?

Kama spika Ndugai angechukua uamuzi wa kujiuzuru angejijengea heshima kubwa,kinyume anakanusha akidai amenukuliwa vibaya.Kimsingi matamshi yawe yamenukuliwa vibaya au yawe ndiyo maneno halisi aliyoyatamka anapaswa kupisha
Maamuzi magumu kama hayo yanaweza kuchukuliwa na watu kama Lowasa, kwanza wana uchumi wa kutosha.

Huyo mgogo kama si mabilioni ya serikali kutumika kwa ajili ya matibabu yake India angekuwa ameshakufa siku nyingi kabla hata ya Mwendakuzimu.

Kwahiyo usitarajie kitu cha namna hiyo kwa mtu ambaye bado anatamani kuhudumiwa na serikali.

Mtaani kugumu usione hivi.
 
Mi naamin Prof Asad alikuwa sahihi kuhusu viongoz tuliokuwa nao. Alikuwa sahihi pia kuhusu bunge tulilonalo maana nilimsikia Ndungai akilalamikia bunge kupitisha vitu sivyo. Yeye akiwa Spika. Tatu. ukimsikiliza hii kauli alivyosema nimekosa mimi nimekosa sana utajua amelazimika tu kuomba msamaha ila ndan yake hayuko sawa. Mwisho. Mi nadhan viongoz wengi wamepatikana kwa kujipendekeza au unafiki au kujuana so ukiangalia hakuna mfumo wa uandaaji viongoz so hakuna mzalendo zaid sana wapo washakaji kwa hiyo hakuna wa kuwajibika. Na hili lipo mpka kwa wananch wa kawaida.
 
Duh! Inafikirisha sana !!
 
1.Anaomba msamaha so kwasababu kakosea bali anajua nguvu ya Rais mfalme anayelindwa na KATIBA mbovu. Japo yeye ni kiongozi wa mhimili wenye nguvu unaopaswa kuisimamia serikali lkn anajua , Rais anaweza fanya lolote. Ukizingatia anaangalia future yake. Tafsir yake Ni kila mwenye nafasi anajitahidi kulinda kitumbua chake hata kwa kujifedhehesha.

2.Hawezi kuwajibika/kujiwajibisha kwa sababu hata kwa kutofanya hivyo pia Hakuna wa kumwajibisha. Hakuna wa kuwajibika na Hakuna wa kumwajibisha. Mwenye mamlaka ya kumwajibisha akijaribu kufanya hivyo anajikuta anajiwajibisha na yeye pia.

Yote haya Ni matokeo ya Katiba mbovu.
 
Huo utamaduni kwa sasa haupo.Tungeweza kua na huo utamaduni kama tungeuweka kikatiba.ila kwa porojo za mdomo na kuoneana aibu usitegemee ilo kutokea.sasa hivi madaraka ni fursa sio utumishi tena.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Sijaona kosa la Ndugai mimi. Yeye alikuwa anajenga hoja ya kwa nn tozo zikawepo. Na anasema upende usipende utakatwa tu kwa vile tumezidi mikopo. Anasema ni heri tukatwe tozo kuliko kwenda kunyenyenyekea watu huko na deni likizidi kupaa. Yeye main point yake ilikuwa kuelezea umuhimu wa tozo. Wakatokea wapuuzi flani wakatwisti ajenda. Ila amefanya mistake sana kuomba msamaha
 
Ndugai amevuna alichopanda...ila kwa hili tukio la kuomba msamaha je huu mhimili utaweza kweli kuisimamia serikali ipasavyo.? Au ndio umesalimu amri kwa mhimili mwingine?
 
Naona Pasco unataka kuutikisa mhimili wa bunge tena, shauri yako mkuu achana na haya mambo
 
Binafsi naona ni kosa kubwa alilolifanya Spika la kuomba radhi hadharani. Angeomba radhi ndani ya proper channel bila ya media.

Alichokifanya amedhihirisha mhimili wa bunge hauna nguvu ya kuikosoa serikali na wananchi wanapata sababu ya kudai katiba mpya.

Hata upande wa serikali ungelinyamazia tuu kuliko kuibuka makada kumjibu spika. Lingeisha tuu na ndani ya vikao wangeombana radhi
 
Huyu ajiuzulu tu..kamchana Rais parefu mnoo.. hakuna namna tena.
 
Sasa kama hajafanya kosa kwanini kasema "NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA SANA?"
 
Blaza Jumapili naenda kuitolea sadaka hii thread. Barua ya kujiuzulu ya mzee Mwinyi imenikosha sana. Mzee alikuwa muungwana sana tangu akiwa kijana...

Ahsante sana kwa huu uzi mujarab
 
Kwani hizoTrillioni 1.3 zimejenga madarasa tu au zimefanya na kazi nyingine Kama zilivyoombwa?
 
Kabisaa hapa tunataka majibu na si blah blah,
Na Makato ya tozo ni mlima
 
Mkuu atakulia tena taimingi bungeni, hujakoma tu "kudhalilisha" mhimili?😀
 
Hahaaaa!!!!nadhan unataka kuitwa tena ktk ile kamati
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…