Vipi kauli ya Kagame kuwa Rwanda ingekuwa na bandari kama ya Dar, huduma zote Rwanda zingekuwa bure?

Mkuu..Reli ni kila kitu

Na reli inahujumiwa na wenye malori

Kama unakumbuka Hanspope alimkashifu sana Minister Magufuli kipindi akiwa ujenzi...alipopiga stop malori yenye uzito unaozisi
Ni suala la muda tu. Hayo malori ya akina Hans Pope yatakuja kuwa kama chai maharage. Baada ya Hiace na Coaster kuingia kwa wingi walienda shamba bila kufukuzwa.

Malori lazima yafanye kazi sehemu inakoishia reli. Gharama za nafaka ni kubwa kwa sababu ya malori. Ingekuwa ni usafiri wa reli, ingekuwa nafuu sana.
 
Uko sahihi mkuu....Tunahitaji reli ndio msingi wa maendeleo na usafirishaji usio na wasiwasi

Mfano hata dar...solution ilikuwa ni Reli ...haya magari piga stop kuingia mjini...mji unakuwa msafiiiiii

Hivi gesi ya mtwara si ilishaanza kutoka....Mbona bei ya umeme haijashuka?

Tulitegemea gesi hii ingeweza kutumika hata kwa electric train
 
Kagame alikubali kuitwa dikteta kwa ajili ya maendeleo ya nchi yake hapa kwetu JMP kaanza tayari baadhi wanaleta maneno oh huyo ni udikteta
Kwa maana hiyo kakame na magufuli sasa wapo sahihi kufanya mazuri ya nchi yao

Waafrica tunahitaji "development dictatorship". Na hili naliunga mkono..Hata hivyo Mbona bado magufuli sio dictator? anatekeleza sheria alizozikuta..hajatunga sheria mpya...kazitoa sheria kabatini. Hilo ndo alifanyalo..Tatizo watanzania tulizoea business as usual. Aidha hatuwezi kumlinganisha na Kagame katika suala la kile kinachoitwa "udikteta" hususani katika masuala ya pure politics..Shortly Go magufuli, go, go, go..Hata patakapohitaji kukaza buti kwa sheria mpya tunga tu ili mradi zinalenga kuleta "Development DIctatorship"
 
Labda tumwachie Kagame kwa miaka mitano tuone kama hayo aliyoyasema ni ya kweli au porojo tu.
 
Tanzania Ina rasilimali za kuweza kuifanya itoe huduma buree au kwa gharama nafuu kwa watu wake...
Lakini tatizo la msingi lipo kwenye Elite Capture!
Ukitaka ujue nasema nini rejea:
1. Matumizi ya anasa ya viongozi na wateule
2. Kodi na tozo kandamizi
3. Mifumo isiyoendelevu
4. Roho mbaya, chuki, fitina dhidi ya wananchi
 
Mkuu, kwani wewe hupendi viongozi wako waishi vizuri? Hupendi kuwaona viongozi wako wakitumia mav8 ya maana ambayo hata Mawaziri wa vinchi kama Sweden na Denmark hawana?

Jisikie fahari kiongozi wako kuishi kifahari!

Unajua kuwakilishwa nako ni heshima? Iko hivi, kiongozi wako akitumia gari la kifahari, anakuwa amefanya hivyo kwa niaba yako, kwa hiyo ni wewe ndiye uliyetumia.
 

KWELI. Ni fahari sana asee! Tunafurahi 😭😭😭
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…