stellahchriss
Member
- Oct 8, 2013
- 29
- 7
tinna cute pole sana. mimi perfume na dawa za mswaki zilitupwa kwenye waste bin ile kufika kwa jamaa wa uhamiaji wananiuliza vipi mkuu unaenda kufundisha KISWAHILI ughaibuni? sijui nnimekaa kama mwalimu. Mwishoni akamalizia kwa kuomba hela ya Chai UHAMIAJI AIRPORT punguzen njaaa.
mimi ni kati ya wale waumini wa SABATO MASALIA, kama mnakumbuka kisa chetu cha kutaka kupanda ndege bila kuwa na TIKITI wala PASS ya kusafiria, tungefanikiwa lile zoezi, ndyo ingekuwa ni mara yangu ya kwanza kupanda ndege!
Fundi mchundo.
Ahsante kwa kufanikiwa kunichekesha.
Hahahahahah
Ahahaha mlipanic brother. Hivi Mko wapi sikuhizi?
Umetisha mkuuNamshukuru Mungu nimezaliwa kwenye familia yenye uwezo sana. Bibi yangu ana ndege mbalimbali, kuku, bata, kanga, kwale, njiwa etc
baada ya gradu yangu chuo.Tukarudi mkoa na maza. Fastjet ndo imeanza.Nı mara yetu ya kwanza wote.
1. Mama anataka kukaa akakuta juu ya siti sehemu ya mizgo kuna mtu kashaweka wake.Akatia,"wee kondaa,we kondaa wéeh,hebu njoo kwanza"
2. Nikajaribu kwenda choóni japo sijabanwa alimradi tu nione pakoje
3.Facebuk page yangu iliomba poo. Mara checkin in at JKİ Airport. Mara nitupie picha alimradi kila mtu ajue.
4. Tulivofika madreva tax wakaanza kututukana eti "hamna lolote nyie mtakuwa fastjet tu" hapo kisa ni baada ya wao wanatugombania sie hatuna time tunaenda kwny daladala.
5. Jioni napokea simu toka kwa mjomba: "ah mjomba nimeamini ushamba mzigo wa mwiba".Nkamuuliza kwanini? Akasema,"leo sina raha. mama yako kutwa nzima anantambia kwny simu kisa kapanda ndege"
kaka mwadui mining?pia nimezaliwa huko aisee..i wish to know ur real name..maana pale tulikuwa tunajuana mji mzima...
day 1 nili enjoy sanaaaa yani sanaaaa
baada ya hapo safari zilizofata ni hofu tupu as ..sipendi wakati inapoanza kuruka na wakati wa kutua. Pia hali ya hewa ikiwa mbaya safar inakuwa hovyo.
kioja changu kilikuwa kwenye pasport jamani.. nilipata ile ya muda as ilikuwa ya karatasi huyo mbio stationary kuifanyia lamination eti isiharibike. Walahi kama sio yule binti wa stationery sijui huko airport ingekuwaje ..looo!
Ombea usianzie kwenye ndege za jeshi,utajuta! But saiv naona kwaida tu kwenye ndege za aibiria na jeshi pia
Wewe wa wapi, fire, compaound, uzunguni au uhindi? Mie kw walala hoi tu MESS
umetisha mkuuMie mara ya kwanza kupanda ndege nilitoka Dsm kwenda Mwanza. Process nzima hadi niingie kwenye ndege ilikuwa 'shughuli'. Nilikaa upande wa dirishani, tulipopita Ngorongoro crater eti sikuthubutu kuchungulia nje. Kisa? Niliogopa eti nikichungulia naegemea upande mmoja hivyo nikaona kama vile ndege italalia upande ule na kuanguka! Ama kweli ushamba ni kazi!
Mara ya kwanza kusafiri nilikuwa naenda Sehemu hivi kupitia Paris. Ila siku hiyo ndege ya Air France ikawa imeharibika na hivyo ikaja ndege ya Madagascar Airlines Boeng 747, mzinga wa pipa.
Uzuri ni kuwa nilipigwa shule nyumbani nzuri sana jinsi ya kufunga mkanda, kulaza kiti na kukirudisha, kufungua headphones na kuzitumia na wapi zipo tundu za kuchomeka.
Ila nakaa, pembeni kuna Dada wa Kiganda na Mudhungu wake, akawa anahangaika jinsi ya kufunga mkanda, bwana wake akamsaidia kufunga. Sijui siku hizi anajisikiaje akikumbuka ushamba huo wa siku ya kwanza.
Kasheshe ilikuwa wakati wa kula. Ila Mungu bariki nilishaambiwa kuwa kuna vikaratasi vya kufuta uso na asubuhi mnaletewa taulo za motomoto kufuta uso pia. Msosi kufika, maajabu matupu kwani nusu ya vyakula navifahamu na nusu sivifahamu. Mie na kundi langu lote tukawa tumekubaliana tutakula kila kitu na hatubakizi hata kama watakuwa CHURA wa Kifaransa maana hawa jamaa WALA VYURA hawakawii kumlisha mtu nyama zao.
Kila kitu kilienda safi ila ikawa kasheshe kuzila OLIVE ila nikajikaza nikazila. Kulikuwa na nyama nyeusi nyeusi, sikujali ni nini, nikazila bila huruma. Mwisho vikabaki vipaketi vitatu. Kimoja kukifungua ni Sukari, nikaibugia. Kingine kufungua ni jibini, nikaila bila huruma. Cha mwisho kufungua (nilikuwa nafahamu unafungua kwa kuvunja ncha iliyochomoza) ikawa kumbe maziwa ya kwenye kahawa ambayo nilishaimaliza mapema sana bila sukari wala maziwa. Basi nikaangalia kushoto kulia hakuna anayeangalia, nikabugia. Mwisho nikasema hata kama Mjinga fulani kaniona, sijali maana hatakuja kuniona tena. Mwisho sahani yote ikawa tupu na wakaja akina dada kuchukua makasha matupu.
Kuna jamaa alikuwa anawasumbua akina dada kuagiza pombe basi ilipofika saa 9 usiku, wakamuita na kumuonyesha Friji la Pombe lilipo na wakaenda kulala. Jamaa alipofika Paris, alikuwa anatambaa kutoka ndani ya ndege.