Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wakuu kesho tena nakwea SOUTH AFRICA AIRWAYS nakwenda SYDNEY yaani hapa sijalala nafikria sijui itakuaje maana nasikia huko ni mbali kweli kweli, zaidi ya masaa 16 angani, daah sasa nikisikia kukata GOGO inakuaje? daah mpaka najiogopa Aisee! SHIKAMOO MZUNGU
Duh, hii ni nouma. Yaan kama ni muuza chips anakuuliza "niweke kila kitu?"
ndege kitu kingine aisee mimi nikiwa nasafiri kwa ndege silali siku 2 nzima nawazia safari ya dar-mwanza na fastjet. Outing weekend naendaga airport japo nifaid kwa macho tu
Poa Mkuu nitaku-PM nakuja mkutanoni japo ngeli lenyewe la kuunga unga nitalisongesha hivyo hivyo hope wazungu watanielewa. Daah ila sasa hii ya kukaa angani muda wote huo ndo sijielewi kwa mfano Napata tumbo la kuhara nafanyaje? maaana Dar mpaka Johannesburg nasikia masaa 3 hiyo sina shida, sasa hiyo Johannesburg -Sydney daah masaa 16 na dakika 25, ni hatari tupu.
Mimi sikumbuki vizuri,ila nina zaidi ya masaa laki moja hewani