Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Ilikuwa ni precision juzi juzi hapa 2013 , miez ya mwanzoni nimetoka tu chuo nikapata kijob kimoja ambacho kuna kutravel sana ndan na nje.

Safari ya kwnza Arusha, dah kiukweli nilimshangaa sana Mungu na Kiumbe wake Mzungu . Yaani dk 40 tu nipo KIA? anga linavyopendeza ajabu, na ukichangia ilikuwa asubuh nzur mlma unaonekana kwa mbali. Dah !!
After just 5 month tu ,ukawa ndo usafir wa kawaida, had sasa nina masaa mengi tu hewani na kila siku yanaongezeka.

Ashukuliwe Mungu.

Kwa hisani ya watu wa Marekani.bila kumsahau Bill gates.
 
hahaaaaaaaaa chezea kupanda ndege lol..usingizi haaukuja hata
nikisoma hii thread nacheka sana
Napenda siku moja nijaribu skydiving na wewe Mbingu duniani... Nimejitahidi sasa hivi naweza kuruka kutoka kwenye ndege mwenyewe bila kuruka na mtu... Adrenaline stunt hizo kama ni moja ya ur imaginations...
 
Nakumbuka ilikuwa Mwaka 2008 mwezi Juni nilikuwa naenda kikazi Lusaka, Zambia basi sijui hili wala lile kwenye tiketi iliandikwa saa ya ndege kuondoka mimi nikajipa kama dakika 20 hivi ndo niwe airport duuh ile kufika nikaambiwa muda umeisha daah! Nilichoka. But taratibu nikajifunza muda wa kufika airport, vitu visivyoruhusiwa kubeba kwenye ndege...HAKIKA USHAMBA MZIGO

i was with my girlfriend thnk God nothing went wrong...
 
Nakumbuka ilikuwa Mwaka 2008 mwezi Juni nilikuwa naenda kikazi Lusaka, Zambia basi sijui hili wala lile kwenye tiketi iliandikwa saa ya ndege kuondoka mimi nikajipa kama dakika 20 hivi ndo niwe airport duuh ile kufika nikaambiwa muda umeisha daah! Nilichoka. But taratibu nikajifunza muda wa kufika airport, vitu visivyoruhusiwa kubeba kwenye ndege...HAKIKA USHAMBA MZIGO

i was with my girlfriend, i had to play cool.. thnk God nothing went wrong...
 
Daah ndege balaa kuna siku nilipata trip ya kwenda New Zealand from Dar nilipanda Emirates via Dubai then Sydney mpaka New zealand safari nzima ni zaid ya masaa 48 kufika NZ nilikuwa hoi hamu yote ya ndege iliisha.
 
bukoba -mwanza.....vile vindege vidogo...hiyo siku kulikuwa na mvua sana asubuhi..wakati tunaingia kwenye ndege tukaambiwa tuzime simu zetu ila kuna watu nikawaona wanaendelea kutumia simu wakiwa ndani kabla hatujaondoka...ile tunaondoka tu airport kandege kakaanza kuyumba yumba mara pailot akarudia tangazo watu wote wazime simu...mimi simu yangu nilitoa na betri kabisaaaa..

uuuwi! Wangewambia mtoe na betri nadhan ungeenda some extra miles, ungeivunja kabisa! LOL!
 
Mara ya kwanza kusafiri nilikuwa naenda Sehemu hivi kupitia Paris. Ila siku hiyo ndege ya Air France ikawa imeharibika na hivyo ikaja ndege ya Madagascar Airlines Boeng 747, mzinga wa pipa.

Uzuri ni kuwa nilipigwa shule nyumbani nzuri sana jinsi ya kufunga mkanda, kulaza kiti na kukirudisha, kufungua headphones na kuzitumia na wapi zipo tundu za kuchomeka.

Ila nakaa, pembeni kuna Dada wa Kiganda na Mudhungu wake, akawa anahangaika jinsi ya kufunga mkanda, bwana wake akamsaidia kufunga. Sijui siku hizi anajisikiaje akikumbuka ushamba huo wa siku ya kwanza.

Kasheshe ilikuwa wakati wa kula. Ila Mungu bariki nilishaambiwa kuwa kuna vikaratasi vya kufuta uso na asubuhi mnaletewa taulo za motomoto kufuta uso pia. Msosi kufika, maajabu matupu kwani nusu ya vyakula navifahamu na nusu sivifahamu. Mie na kundi langu lote tukawa tumekubaliana tutakula kila kitu na hatubakizi hata kama watakuwa CHURA wa Kifaransa maana hawa jamaa WALA VYURA hawakawii kumlisha mtu nyama zao.
Kila kitu kilienda safi ila ikawa kasheshe kuzila OLIVE ila nikajikaza nikazila. Kulikuwa na nyama nyeusi nyeusi, sikujali ni nini, nikazila bila huruma. Mwisho vikabaki vipaketi vitatu. Kimoja kukifungua ni Sukari, nikaibugia. Kingine kufungua ni jibini, nikaila bila huruma. Cha mwisho kufungua (nilikuwa nafahamu unafungua kwa kuvunja ncha iliyochomoza) ikawa kumbe maziwa ya kwenye kahawa ambayo nilishaimaliza mapema sana bila sukari wala maziwa. Basi nikaangalia kushoto kulia hakuna anayeangalia, nikabugia. Mwisho nikasema hata kama Mjinga fulani kaniona, sijali maana hatakuja kuniona tena. Mwisho sahani yote ikawa tupu na wakaja akina dada kuchukua makasha matupu.

Kuna jamaa alikuwa anawasumbua akina dada kuagiza pombe basi ilipofika saa 9 usiku, wakamuita na kumuonyesha Friji la Pombe lilipo na wakaenda kulala. Jamaa alipofika Paris, alikuwa anatambaa kutoka ndani ya ndege.

nimecheka mpaka watu wananishangaa................ aiseeeee we acha tuu mkuu umetisha sana....
 
Mi siku ya kwanza nilikaa attention kusubiri itaanza kuyumba yumba saa ngapi tayari kwa kuanguka. Roho ilikuwa juu juu masaa manne (Dar-Addis). Mpaka tunatua nilikuwa bado siamini kuwa hatujafariki.
 
Nimecheka sana hasa issue ya paris.....me ni mwaka 2000 from dsm to mtwara with eagle air nlikuwa na dingi. Japo nlikuwa mtoto sikuogopa na dingi alinifanyia kila kitu! Ila kuna watu wanahaha
 
clasi mimi nakumbuka mara ya kwanza kupanda ndege bibi alinambia fumba macho mpaka nikikufinya ndo ufumbue, sasa mimi nkafumbua kabla sijafinywa kuja kutahamaki loh niko tandika nimezingirwa na watu wanaopiga mayowe " mchawiiiiii huyooo"
...dah ama kweli ushamba mzigo, au best ulikuwa unaongelea ndege ipi? mi yangu ilikuwa Air Ungo Jet.
 
Last edited by a moderator:
Zile ngazi za Jomo Kenyatta ni nouma sina hamu nazo kwakweli, zilinitoa ushamba na hadi leo nikikumbukaga nahisi kizunguzungu, sizipendi.....


Mi naona ndiyo nimecheka zaidi
Hasa nikikumbuka mi ngazi za Jomo Kenyatta airport zilivyonitoa nishai
nilivyoona ngazi zinatembea nikataka kurudi nilikotoka but toka mwa huo wa 1998 mpaka leo ngazi za hivyo sizipendi kabisa!!!!!!!!!!
 
naombeni mnielekez eti ndege inapita inakuwa juu ya mawingu na vpi kuhusu suala la mavi eti yanaenda kwenye mawingu ukijisaidia ukiwa ndani ya ndege . mi mwenzenu kuna mtu huwa hatulali juu ya kupanda ndege kwa sie ambao tumezoea sumry na new force tunapata sana shida kwa story za huyu jamaa. mara anasema eti hata maji ya mvua ni machafu mana ukiwa kwenye ndege unakunya mavi kwenye mawingu
 
Hana uwongo wwt..watu tumeanza kupanda ndege enzi hizo kipindi cha mwalimu..williamson diamonds mwadui walikua na ndege 4 tulikua tunapanda tu kwenda madhuleni tunashikia dar..ndege ilikua kawaida sana kama uda tu kariakoo to mwenge!

Pamoja na hayo kuna siku ya kwanza. Au kuqualify zaidi siku ya kwanza ukiwa unajitambua!

Kwani naamini kila kitu kina siku ya kwanza kama huna hiyo experience potezea. Mi ntakuja baadaye nilivyoona mabawa kuna vitu vinachezacheza na vimoshi vinatoka nikajua imeharibika kilichofuata mhh sikuwa mimi nilihisi roho imeshatoka zamaani!
 
Kuna mzee aliingia he was kinda late yeye ndo alikuwa wa mwisho, basi alipofika mbele kidogo akapayuka maneno haya nakumbuka " BASIIIIII, KWISHAAAAA, TAYARIIIII" watu tukashituka huyu dingi vipi akasema jamani nina miaka 68 leo ndo napanda ndege kwa mara ya kwanza.
 
Kuna mzee aliingia he was kinda late yeye ndo alikuwa wa mwisho, basi alipofika mbele kidogo akapayuka maneno haya nakumbuka " BASIIIIII, KWISHAAAAA, TAYARIIIII" watu tukashituka huyu dingi vipi akasema jamani nina miaka 68 leo ndo napanda ndege kwa mara ya kwanza.

dah, nimecheka sana, kama namwona huyo babu
 
Ombea usianzie kwenye ndege za jeshi,utajuta! But saiv naona kwaida tu kwenye ndege za aibiria na jeshi pia
mi nilianzia ndege za kijeshi 1990, niliona powa tu, kwasasa i dont talk about ndege kwakuwa ndege is my life.
 
Hana uwongo wwt..watu tumeanza kupanda ndege enzi hizo kipindi cha mwalimu..williamson diamonds mwadui walikua na ndege 4 tulikua tunapanda tu kwenda madhuleni tunashikia dar..ndege ilikua kawaida sana kama uda tu kariakoo to mwenge!
Umenikumbusha Mbal sn 1990's uko Dar-Mwadui na Williamson Diamonds enz iZo Ndo ilikuaga habar ya mujin enz izo dec holiday mnaenda Shinyanga kwa Bib na Bab kwel zile ndege zina historia enz za Mwalim.

Mmmmh ila kuna ndege bana yaan mpk unasikia raha ya kupanda ndege Mfn.BA, Emirates, KLM kwa wale waliopanda Air Tz lile screpa kwakwel mrudie Zoez tena au vile vindege vidogo mmmmmh.hata hamjafaudu.
 
kioja changu kilikuwa kwenye pasport jamani.. nilipata ile ya muda as ilikuwa ya karatasi huyo mbio stationary kuifanyia lamination eti isiharibike. Walahi kama sio yule binti wa stationery sijui huko airport ingekuwaje ..looo!
HaHAHAhaha umenikumbusha mbaali sana!
 
Back
Top Bottom