Visa na Mikasa vya kusaka kwangu Utajiri toka Kigoma mpaka Kongo

Visa na Mikasa vya kusaka kwangu Utajiri toka Kigoma mpaka Kongo

PART VI


Maisha mwenzangu alikuwa ameyapatia.ana gari zuri tu.mimi sikuwa hata na wazo la kununua gari kwa muda huo. Sikuwa na uwezo huo.

Abdul alinielezea biashara za madawa ya kulevya alinielezea kuwa kama naweza nijiunge naye.hofu yangu ilikuwa ni kuwa hiyo ni biashara kharamu.

Abdul alinihakikishia sipaswi kuwa na mashaka sababu ni biashara ambayo anaifanya na watu wakubwa mmoja wapo ambaye anajua alikuwa mtoto wa kiongozi mkubwa sana wa nchi na mwingine mtoto wa mkuu wa polisi jiji flani (huyu mkuu wa polisi alikuja uawa baada ya mtoto wake kukamatwa china akiwa na mtoto wa kiongozi mkubwa halafu mtoto wa kiongozi mkubwa alimtoa mwanawe akamwacha mtoto wa huyu mkuu wa polisi.huyu mkuu alitaka akaharibu kila kitu.akawahiwa akauawa)

Abdul alinielezea mambo makubwa na mazito ambayo sitayaandika hapa kwa sababu kadhaa.lakini jambo moja ambalo alinihakikishia ni kuwa alikuwa pia ameshaenda sana Kigoma kupikwa.

Abdul alikuwa anaenda Kigoma Ujiji kwa mzee mmoja ambaye alikuwa anamweka kwenye pipa la maji na kuchanganya na dawa ambazo baada ya hapo Abdul anakuwa haonekani.

Hizi dawa zipo. Unatakiwa zile nguo ambazo unatakiwa uzitumie siku hiyo uzivae. Halafu unawekwa kwenye pia na maji yanachemshwa kiasi flani. Unazama mwili mzima.ukiwa na viatu na kila kitu.

Ukitoka hapo huonekani labda kwa mtu ambaye ana supernatural power pia.lakini hawa wakawaida huonekani.

Mnakumbuka kisa cha yule kijana mmoja mbezi kama sikosei ambaye alikuwa anatembea na wake za watu kimazingara? Haya mambo yapo. Mtu anakuww haonekani ila anaweza fanya chochote kile kama kufungua mlango na ukaona mlango unafunguka. Au ukasikia mtu anatembea ila ukigeuka humwoni.

Kwa Kigoma Ujiji na mpakani mwa kigoma na Kongo,Kigoma na Burundi ni maeneo ambayo nafahamu hizi dawa zipo sana.

Na dawa za mazonge ambazo unaweza ukawa unaona kitu wewe tu wenzako hawaoni. Kukutia uchizi. Kama kuna mtu aliwahi kaa Kigoma miaka flani pale sokoni na karibu na Stesheni alikuwepo chizi mmoja ambaye alikuwa akitembea anakimbiza hewan Ubooh wake. Anasema anaona ubooh unakimbia hewani.

Huyu inasemekana alipenda sana onesha urijali na akatembea na mke mdogo wa Mzee Mmoja alikuwa akifahamika kama Mkataamkali kama sikosei.

Akawa ametiwa hayo mazonge anatembea anakimbiza Ubooh hewani.ikawa ndo basi tena. Mwishowe akawa Kichaa kabisa.

Kigoma watu walikuwa wanaogopa hata kuibiana.sijui siku hizi maana na kule nako ukionesha tu una mafanikio ukarudi kwenu unaweza usirudi tena Mjini.

Abdul alikuwa na pesa. Amebadilika sana ndani ya muda mfupi. Alinishawishi sana lakini sikuweza kubaliana naye. Akawa ananambia kina safari anaifanyia kazi ya kwenda South Africa na China. Huko ndo maisha ataya win hasa.

Mimi nlikuwa njia panda.nikifahamu athari za madawa ya kulevya.nikifahamu kuwa ikitokea nakamatwa kifungo nitakipata tu. Abdul alikuwa akijiamini. Ingawa anasema bado hakuwa mfanyabiashara mkubwa sana lakini alikuwa na connections na watu walishaanza mwona kuwa ni potential.

Nlirudi kwangu tukaendelea kuonana na Abdul na kupeana salamu. Mwishowe akachoka.

Mimi nliendelea na kazi yangu ya ufundi.siku moja nimechukua gari ya mteja nikawa nmeenda Ilala pale Shaurimoyo kununua spare.ile gari kuna mteja alileta itengenezwe na unajua sisi mafundi huwa tunatumia usafiri huo huo unaoletwa na wateja.

Basi narudi nipo surrender kwenye kifoleni ghafla nligongwa na gari Range Rover nyeusi. Gari nliyokuwa nayo haikuumia sana.

Kwenye ile Range alitoka kijana mmoja mweupe hivi mwembamba.akaniuliza gharama ya kutengeneza ile gari itakuwa tsh ngapi? Yule kijana alinishtua sana. Mwili ulinisisimka sana. Sijawahi kutana na mtu mwili ukasisimka kama vile. Nlimtizama sidhani kama alikuwa binadamu wa kawaida maana nliona kama wakati flani anataka kupotea then anakuwepo.

Nlitamka milion 1. Hakujibu kitu.akaingia kwenye gari akachukua pesa na kuja nipa. Sikuhesabu.nikabeba hadi kwenye gari nikawa naondoka.kucheck zile pesa nikajiwa na hamu ya kuhesabu.

Nliingia pale mbele barabara ya kushoto kama naelekea makaburini.nikapark gari. Kuhesabu ilikuwa tsh 1,700,000. Sikuamini. Nikahesabu tena.nikahesabu mara tano. Ili 1,700,000.

Repair ya ile gari ilikuwa haizidi tsh 50,000. Nlishangaa sana. Why yule bwana mdogo anipe pesa zote hizo.

Katika ulimwengu wa roho. Msiamini kama humu duniani tupo peke yetu. Kuna majini mengi yapo njiani.mitaani kwa namna mbalimbali.hili nlihakikishiwa kabisa na mzee na siku moja alitaka nipaka dawa usoni nione.nlimgomea. alinambia nione viumbe vilivyopo duniani. Sikuafiki...

Siku zote hizi nlianza pata mawazo ya kumtafuta Ahmed.sasa nlikuwa na nauli ya kwenda Mwanza kumtafuta Ahmed.maana nliambiwa Ahmed yupo mwanza anafanya biashara ya uvuvi na ni tajiri kweli kweli...

Itaendelea.....
 
PART I

Katika harakati za kutafuta maisha kuna mengi sana ambayo wanaume tunapitia. Leo ntawaelezea visa na mikasa ambayo nlipitia toka nimemaliza kidato cha nne mwaka 1995. Mambo haya yametokea nikiyaona na pia nikihusika.

Mimi ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto 7. Nikiwa na dada watano na mdogo wa kiume mmoja.

Nakumbuka mwaka 1995 mara baada ya kumaliza masomo nikawa home mara nyingi na vijana wenzangu.mpaka matokeo yametoka nlikuwa na division 2 hivyo nlipaswa niendelee na masomo.

Mzee hakuwa ametaka niendelee na masomo kwa kuwa hakuwa na pesa na pia mama alikuwa akiumwa mara kwa mara hivyo ikawa tunauza ng'ombe na mawese ili mama atibiwe.tukiwa na mahangaiko hayo mdogo wangu wa nne naye alishikwa na ugonjwa wa ajabu sana.

Akawa kama ana mashetani yakimpanda anatoka jasho jingi sana huku akitetemeka. Kipindi hicho anaishi Ujiji kwa Bamdogo. Ikabidi aletwe home kuja kuugua. Hapo ikabidi aitwe ustaadhi ayasikilize na kuyatuliza.tulihangaika sana. Dada zangu kuumwa umwa chanzo kilikuwa hao dada zangu kiukweli walikuwa warembo sana. Kila mtu pale kijijini aliwapenda. Wazee wengi walitamani kuoa kwetu.

Baba yangu alioa mwanamke wa mpakani na Burundi.alikuwa mzuri sana.

Pale alipokuwa anaishi sister Mzee mmoja alitaka mwoa huyu dada kama mke wa nne kipindi hicho mdogo tu.mzee alikataa. Kumbe yule mzee akamrushia majini ili yamsumbue asiolewe. Kwa hiyo ikawa shughuli hasa pale home.

Mama anaumwa sister anaumwa. Mi naendaje shule? Hali ile iliniumiza sana.nikatamani ngesoma ili niwaondoe wazee pale kijijini na akili nlikuwa nayo sana.shuleni ni wawili tu ambao tulipata division 2 wengine wote walipata 3,4 na 0.

Basi baada ya kuhangaika sana kutafuta pesa ili nikasome tulishauriana na jamaa zangu wengine wawili.

Hawa walikuwa nao wanataka pesa wamechoka maisha ya umaskini. Ahmed na Abdul. Ahmed yeye alikuwa ameishia darasa la saba akaamua kuwa mvuvi.

Jamaa alikuwa angalau anapata pata vijicent kidogo lakini hakuridhika.kila mara alikuwa ananipa mikasa ya ziwa tanganyika kwa mambo ya ushirikina.

Akisimulia jinsi ambavyo kuna siku ilikuwa wavuvi wenzie wamtoe kafara ili wapate samaki wengi.(hiki kisa ntakisimulia siku moja) Ahmed alikuwa akinikataza kupenda kupanda mitumbwi ya watu. Alinambia jinsi ambavyo kuna shangazi yake mtoto wake alianza umwa ghafla baada ya kupakizwa kwenye mtumbwi uliokuwa umepark ufukweni. Ikaja onekana yule mtoto aliguswa na misukule kwenye mtumbwi. Yule mtoto alianza kuumwa ghafla na kutokwa na udenda.walimuwahi kwa mganga ndo kupona kwake.

Basi Ahmed akawa anasisitiza sana kuwa tuvuke tuingie kongo kuna pesa nyingi sana.binafsi nlikuwa nasita maana sikuwa mzuri sana ziwani.nilikuwa na woga sababu nlishawi mezwa na mamba nikiwa mdogo lakini mzee alimng'amua kuwa alikuwa mzee jirani(mzee luyaga) akamkemea. Yule mamba alinitapika mzima kabisa.nikawa mwoga sana wa maji.

Basi tulishauriana sana baadaye tukaamua jioni moja tuondoke twende kongo.

Basi nyumbani mimi nliwaaga kuwa kuna tajiri mmoja kaomba nimsindikize kasulu kuna mambo anataka nimsaidie.mzee alihoji sana lakini akaniruhusu.

Siku hiyo ilikuwa jioni giza limeingia. Tukapanda boat tukiwa wengi kidogo kila mtu akiwa kimya.

Tulikutana na misuko suko mingi sana ziwani.nakumbuka kuna sehemu tulifika ile boat ikazima.halafu ikawa inazunguka pale pale yaani kama mtu anaizungusha hivi. Wakati huo inazunguka kwa kasi inatengeneza kama shimo kwenda chini.wale waongozaji walikuwa watatu.walipambana sana wakinyunyizia dawa n.k mwishowe wakakubaliana kuwa pale lazima tuache mtu mmoja.

Sikuelewa maana yake mpaka Ahmed alipofafanua.kuwa hatutoki pale mpaka tumtose mtu mmoja. Wakati natafakari mle ndani tupo kama 10 hivi wale jamaa wakawa kama wanashauriana jambo ila kwa kunong'onezana. Wakaanza kuuliza kila mtu aliondokaje.mimi nikajikuta nasema nliaga kuwa naenda kongo ktk wale watu mmoja akasema ye alitoroka tu hamna anayejua yupo wapi.

Wakati huo bado tunazungushwa pale pale na kuna shimo kuelekea chini ya maji kama unavyoona kimbunga.wale jamaa wakashauriana.ghafla wakamkamata yule jamaa na kumtupia kwenye maji pale shimoni. Alipogusa tu maji ni kama alivutwa chini halafu kikatokea kitu kama moshi mweusi ukamnyonya/mpokea kumshusha chini. Kukawa kimya.

Ziwa likawa limetulia sana.hapo mimi moyo unadunda sana.wale jamaa wakasema mmeona kilichotokea.tukatikisa vichwa. Wakasema hakijatokea kitu na tulivyo ndivyo tulivyotoka nchi kavu.hakuna mtu kuongelea hilo jambo kwa mtu yeyote.

Nlitetemeka sana.nilikuja shtuka tumefika ukingoni.walikuja kama migambo hivi pale pembezoni mwa maji.wakaongea na wale jamaa watatu wakapewa mshiko wakatwambia tutawanyike haraka sana wao wanaenda kusini sisi twende magharibi.

Safari ikaanza tukiongozwa na ahmad.ahmad alitutembeza sana kama masaa matatu mpaka tulipofika sehemu tukakuta kuna nyumba mbavu za mbwa na watu wanaota moto.akauliza kama tunaweza fika kwa mzee Shangai.wale jamaa wakatutizama kwa mshangao sana na kugundua tumetoka kigoma.wakahoji sana why tunataka enda mwona huyo mzee. Ahmed alisema tu kuwa kuna mwenzetu ana shida ndo tumemsindikiza.wakatuelekeza.

Ahmed alitaka tuendelee kutembea usiku huo huo. Tulitembea kama mwendo wa masaa 4. Tukifuata tu hiyo njia.mpaka kuja fika nyumba moja imezungukwa na miti.

Ile nyumba tuliifikia shida ikawa kuvuka kizingiti cha majani kwenda uwanja nyumba husika. Ilikuwa tunavuka tunakanyaga majani yametandikwa chini ila hatufiki kwenye nyumba.tulihangaika sana.hebu fikiria umbali wa kurusha jiwe kuanzia sijui saa tisa ile mpaka tunasikia jogoo hatuwezi fika hiyo sehemu. Alipowika jogoo tukagundua kumekuchwa sasa maana ilikuwa tunakaa baada ya muda tunajaribu tena.

Safari hii tukaweza vuka bila shida.tumefika karibu na mlango ahmed anaita babu, babu,babuu. Akatokea paka. Akaja akatuangalia...halafu akarudi ndani.baada ya dk moja akatokea mbabu flani hivi anatabasamu.

Akatukaribisha akitaka kwanza tujimwagie dawa miguuni.akatupa kila mtu kibuyu.tukaosha miguu. Akatwambia mmechoka laleni.

Mi nakumbuka nlikuja shtuka saa saba au nane hivi tukiwa tumelala kwenye ngozi kwenye kakibanda kengine nyuma ya nyumba.nlifikaje sikumbuki.

Tukajieleza sana.yule mzee akatwambia ngoja atueleze zaidi akatuambia tabia zetu na mambo mbalimbali ya ukweli.akamwambia Abduli wewe shida yako unapenda sana wasichana. Abdul alikataa kabisa kuwa si kweli.Mzee Shangai akawa anacheka tu.

Baadaye tumekaa akaja binti kutuletea chakula. Alikuwa binti mzuri sana.sana mzee hakutuambia kitu.basi tumemaliza kura mzee akatwambia yule binti atatupeleka kutembea shambani tuchume matunda.

Kiufupi tulimwambia mzee tunataka dawa ya utajiri.alituhoji sana hasa akisema tatizo la Abdul ni mademu.tukae naye siku tatu tufikirie kama bado tunataka dawa atatupeleka sehemu kama tumebadili mawazo ataturuhusu turudi.

Tuliona kama anatuchelewesha sana.ila hatukuwa na namna. Basi yule bint mzuri akawa anatupeleka kwenye matunda.

Abduli alishaonekana kumtaka yule demu.hivyo akawa amekaa mbele kabisa ana mdadisi dadisi bint. Mwishowe akaanza mwimbisha.yule bint alikataa sana.

Abdul akamwimbisha sana bint akasema basi tukirudi sababu mzee shangai atatoka kwenda porini mpaka kesho yake basi wataonana.

Abdul alikuja tusimulia huku anafuraha sana. Akidai anaenda kumla yule binti jioni mtoni.

Tulimtaka sana aachane na hizo issue baadaye akaanza sema ni wivu tu unatusumbua.

Kweli. Jioni mzee akaaga kuwa anaenda porini kuna watu anaenda kutana nao wanajeshi waasi.atatuacha na yule bint.

Baada kama ya kutoka masaa mawili abduli akatoka na yule bint.baadaye tumekaa chini ya mti tunaota moto abdul alirudi anapiga kelele sana

Kumuuliza tatizo nini akatujibu haoni sehemu zake za siri.mimi na Ahmed tulicheka sana tukijua jamaa anatudanganya .hapo Abdul aliangua kilio kikatushtua. Kweli Ahmed akaenda papasa.jamaa hakuwa na Ub**. Kabisa. Abdul akazidisha kulia.

Wakati tunatafakari hayo yule bint akarudi mbio naye.akaingia ndani. Abdul akawa anamwambia amwite babu shangai.bint anasema tusubiri kesho.ktk hali ya kuhangaika Ahmed akaenda mletea maji ya kunywa Abdul.

Hapo nlishindwa jizuia kucheka kuwa anamleteaje maji ya kunywa wakati jamaa hatoweza kojoa? Abduli akazidi kulia sana.nadhani akakumbuka akinywa maji hatoweza kojoa.

Nikawaza jamaa atakuwa anajisaidia kama kuku vyote vinatokea kwa nyuma.nikajikuta nacheka mpaka machozi yananitoka.

Abduli siku hiyo alikesha. Asubuhi sana akaja mzee Shangai.akaelezwa hali ile.alicheka sana.akasema Abdul tatizo lako wewe unapenda sana wanawake. Huyo ni mke wangu mi nlitaka nikuone tu je kweli ulivyokuwa unakataa.akampaka masizi kichwani. Akampiga mgongoni Abdul akalala. Alikuja amka anashika mashine.imerudi. Alifurahi sana aisee akaanza ruka ruka. Ndi kutueleza kweli alitaka kumla yule binti ila ndo akagundua yupo flat.

Na pia usiku alienda kukojoa haja ndogo ikatokea nyuma maji mengi sana. Tulijikuta tunacheka sana.

Baada ya siku tatu mzee akatwambia sasa muda umefika kama tupo tayari jioni tutaondoka wote.

Nakumbuka tulibeba maji tu kwenye vibuyu. Tulitembea sana tukipanda milima na kushuka,vijito na mito hatimaye tukafika kwenye mti mkuuuubwa sana. Mzee akatwambia tumefika tutulie hapo atuelekeze mambo ambayo yanaenda tokea.....

Nitaendelea.
Hiyo PART II, III, etc, iweke hapahapa mkuu. Nimescroll sana lakini sijaiona. Unganisha na hii PART I
 
IMEENDELEA
Kumbe mwamba kapanga na walee warombo wezake wanekabee mitaa ya mbelee waniibie simu na pesa,saa tumetembea Kama atua 30 hivi jamaa angu akawa Kama anajisaidia,mi Niko mbele Mara paaap nikapigwa robaa,katika kufurukuta jamaa akawa ameshika t-shirt kanifunika usoo...asee nilikua na vimazoezi vya shotokani walijuta Yule wambelee yangu Nika mpiga finger printi ya macho nilikua nitoboe macho akaachia t-shirt,analia Nika mgeukia Yule mwingine Niki weka stensi Nika mpiga washgelii mojaaa ya maana,baada ya hapo niliwaachia t-shirt na kutoka nduki mpaka camp

Wakuu salama?
Na dawa ya NIMRCAF nimenunua asee hii dawa ni kiboko sana, nje na kuponya mafua pia inasaisaidia kule 6x6 kwa bed yani nakula mzigo bila kutoa wazungu.

Dawa hii inamchanganyiko wa Tangawizi, kotunguu swaumu, kitunguu maji, limao na pilipili. Dawa hii sahvi ni adimu inapatikana kwa connection na ipanda bei daily. [emoji119][emoji119]View attachment 1698567

Jamani mm nimechoka kusubiri🤫 huyu maarifa huenda marifa yake ya utunzi yamekomea hapa😆😆, byeeee. "Kila nikitaka kuandika naumwa sanaaa"👈👈👈👈🤣🤣🤣🤣

Haijasaidia. Till today hujajibu. Tukubaliane hapa kuwa hata wewe una kiburi na majivuno.

Usiwanyooshee vidole wenzio. Unatapika sana maneno yasiyofaa. Sitojali kama utatukana hapa.......na wala hizo PM usijibu tena maana HUFAI.
Pathetic.

Mwanzisha simulizi usiporudi kuendelea watu watauana humu[emoji849]

naona jamaa karogwa

Chizimaarifa njoo utulize upepo maana huku watu wanaanza kutwangana makonde

Bampa to bampa, nayo nayo

Nhiiiiiiiiii bhagoshaa
 
Back
Top Bottom