Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna channel YouTube inaitwa davista mata media naona ndio anafanya kipindi na huyo jamaa Musa chesa.Kuna jamaa mmoja alikua mharifu sana jambazi musa chesa uyu wa kigoma polisi walimshindwa uyu mpaka alipo okoka na kukabizi bunduki alikua anatumia madawa haya ya kuto onekana na alijizndka sana kumshka ilikua ishu siku is mchungaji ila kigoma kwa ndumba sio mchezo
Acha ubishi, Ujiji ndo sehemu iliyodumaa kimaendeleo katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji.Alikumabia kuwa ujiji hakuna nyumba nzuri ni nani, unafananisha na wapi?
Alafu mamba huwa anameza baada ya kutafuna so haiwezi kutokea umezwe na Mamba na upone!Kuna gahawa nyingi humu....mtu anamezwa na mamba!
Unaandika na kujijibu mwenyewe!!!!!Napokea vitisho toka juzi.najitahidi but nakuwa na wakati mgumu. Na wengine mpaka wanaandika mambo ya kipuuzi. Kama unaona nimetunga achana na story. Na wala silazimishi mtu aamini.mi silipwi chochote kile na sihitaji pesa yà mtu.watu wajiheshimu hamjui changamoto za ku reveal haya mambo. Na msidhani wanapenda yajulikane
View attachment 1689137
Watu watasema machizi wameenda kumtembelea chizi mwenzao🤣🤣Anaepajua anapoishi Chizi Maarifa aseme tukafanye fujo nyumban kwake [emoji35][emoji35][emoji35]
Duuuuh kumbe issue ya mtoto wa mkubwa ili trend sana na kuna msanii aliwahi kuimba.PART VI
Maisha mwenzangu alikuwa ameyapatia.ana gari zuri tu.mimi sikuwa hata na wazo la kununua gari kwa muda huo. Sikuwa na uwezo huo.
Abdul alinielezea biashara za madawa ya kulevya alinielezea kuwa kama naweza nijiunge naye.hofu yangu ilikuwa ni kuwa hiyo ni biashara kharamu.
Abdul alinihakikishia sipaswi kuwa na mashaka sababu ni biashara ambayo anaifanya na watu wakubwa mmoja wapo ambaye anajua alikuwa mtoto wa kiongozi mkubwa sana wa nchi na mwingine mtoto wa mkuu wa polisi jiji flani (huyu mkuu wa polisi alikuja uawa baada ya mtoto wake kukamatwa china akiwa na mtoto wa kiongozi mkubwa halafu mtoto wa kiongozi mkubwa alimtoa mwanawe akamwacha mtoto wa huyu mkuu wa polisi.huyu mkuu alitaka akaharibu kila kitu.akawahiwa akauawa)
Abdul alinielezea mambo makubwa na mazito ambayo sitayaandika hapa kwa sababu kadhaa.lakini jambo moja ambalo alinihakikishia ni kuwa alikuwa pia ameshaenda sana Kigoma kupikwa.
Abdul alikuwa anaenda Kigoma Ujiji kwa mzee mmoja ambaye alikuwa anamweka kwenye pipa la maji na kuchanganya na dawa ambazo baada ya hapo Abdul anakuwa haonekani.
Hizi dawa zipo. Unatakiwa zile nguo ambazo unatakiwa uzitumie siku hiyo uzivae. Halafu unawekwa kwenye pia na maji yanachemshwa kiasi flani. Unazama mwili mzima.ukiwa na viatu na kila kitu.
Ukitoka hapo huonekani labda kwa mtu ambaye ana supernatural power pia.lakini hawa wakawaida huonekani.
Mnakumbuka kisa cha yule kijana mmoja mbezi kama sikosei ambaye alikuwa anatembea na wake za watu kimazingara? Haya mambo yapo. Mtu anakuww haonekani ila anaweza fanya chochote kile kama kufungua mlango na ukaona mlango unafunguka. Au ukasikia mtu anatembea ila ukigeuka humwoni.
Kwa Kigoma Ujiji na mpakani mwa kigoma na Kongo,Kigoma na Burundi ni maeneo ambayo nafahamu hizi dawa zipo sana.
Na dawa za mazonge ambazo unaweza ukawa unaona kitu wewe tu wenzako hawaoni. Kukutia uchizi. Kama kuna mtu aliwahi kaa Kigoma miaka flani pale sokoni na karibu na Stesheni alikuwepo chizi mmoja ambaye alikuwa akitembea anakimbiza hewan Ubooh wake. Anasema anaona ubooh unakimbia hewani.
Huyu inasemekana alipenda sana onesha urijali na akatembea na mke mdogo wa Mzee Mmoja alikuwa akifahamika kama Mkataamkali kama sikosei.
Akawa ametiwa hayo mazonge anatembea anakimbiza Ubooh hewani.ikawa ndo basi tena. Mwishowe akawa Kichaa kabisa.
Kigoma watu walikuwa wanaogopa hata kuibiana.sijui siku hizi maana na kule nako ukionesha tu una mafanikio ukarudi kwenu unaweza usirudi tena Mjini.
Abdul alikuwa na pesa. Amebadilika sana ndani ya muda mfupi. Alinishawishi sana lakini sikuweza kubaliana naye. Akawa ananambia kina safari anaifanyia kazi ya kwenda South Africa na China. Huko ndo maisha ataya win hasa.
Mimi nlikuwa njia panda.nikifahamu athari za madawa ya kulevya.nikifahamu kuwa ikitokea nakamatwa kifungo nitakipata tu. Abdul alikuwa akijiamini. Ingawa anasema bado hakuwa mfanyabiashara mkubwa sana lakini alikuwa na connections na watu walishaanza mwona kuwa ni potential.
Nlirudi kwangu tukaendelea kuonana na Abdul na kupeana salamu. Mwishowe akachoka.
Mimi nliendelea na kazi yangu ya ufundi.siku moja nimechukua gari ya mteja nikawa nmeenda Ilala pale Shaurimoyo kununua spare.ile gari kuna mteja alileta itengenezwe na unajua sisi mafundi huwa tunatumia usafiri huo huo unaoletwa na wateja.
Basi narudi nipo surrender kwenye kifoleni ghafla nligongwa na gari Range Rover nyeusi. Gari nliyokuwa nayo haikuumia sana.
Kwenye ile Range alitoka kijana mmoja mweupe hivi mwembamba.akaniuliza gharama ya kutengeneza ile gari itakuwa tsh ngapi? Yule kijana alinishtua sana. Mwili ulinisisimka sana. Sijawahi kutana na mtu mwili ukasisimka kama vile. Nlimtizama sidhani kama alikuwa binadamu wa kawaida maana nliona kama wakati flani anataka kupotea then anakuwepo.
Nlitamka milion 1. Hakujibu kitu.akaingia kwenye gari akachukua pesa na kuja nipa. Sikuhesabu.nikabeba hadi kwenye gari nikawa naondoka.kucheck zile pesa nikajiwa na hamu ya kuhesabu.
Nliingia pale mbele barabara ya kushoto kama naelekea makaburini.nikapark gari. Kuhesabu ilikuwa tsh 1,700,000. Sikuamini. Nikahesabu tena.nikahesabu mara tano. Ili 1,700,000.
Repair ya ile gari ilikuwa haizidi tsh 50,000. Nlishangaa sana. Why yule bwana mdogo anipe pesa zote hizo.
Katika ulimwengu wa roho. Msiamini kama humu duniani tupo peke yetu. Kuna majini mengi yapo njiani.mitaani kwa namna mbalimbali.hili nlihakikishiwa kabisa na mzee na siku moja alitaka nipaka dawa usoni nione.nlimgomea. alinambia nione viumbe vilivyopo duniani. Sikuafiki...
Siku zote hizi nlianza pata mawazo ya kumtafuta Ahmed.sasa nlikuwa na nauli ya kwenda Mwanza kumtafuta Ahmed.maana nliambiwa Ahmed yupo mwanza anafanya biashara ya uvuvi na ni tajiri kweli kweli...
Itaendelea.....
Yap namfatilia pale kila sikuKuna channel YouTube inaitwa davista mata media naona ndio anafanya kipindi na huyo jamaa Musa chesa.
wewe unamfahamu vizuri Musa chesa?
Ya kusadikika.Mtanisamehe kwa hati mbaya
Kuna point nimekutana nazo Mkuu wanao kupinga bado watoto wadogo kwenye mambo haya
binafsi nakumbuka mwaka 2005 kuna sehemu mtaani jamaa mmoja mtu wa kigoma huko mwenye mali za masharti
kuna siku nilienda kutatua short ya umeme nyumbani kwake yeye hakuwepo alikuwa mpangaji mmoja tu ndio anaamia.
Chakushangaza zaidi nyumba kubwa inavyumba kumi na mbili lakini wapangaji wote wameama
Nilipanda juu ya dali kwa kusoma dua sana kwa sisi waislamu (naas,falaq,ikhaalas ) mara tatu tatu
nikafanya kazi nimemaliza ile kushuka chini mwenye nyumba na mkuta kukasirika sana ana mwambia yule mpangaji huyu fundi(kijana jr) simjui nikakaa kimya wakasemana na mpangaji wake pale mm nikakaa kimya
Mwisho nikamwambia mzee juzi tu simekufungia feni pale dukani kwako mzee mbona leo unasema unijui
mzee akaendelea kukataa sikujui kabisa na sijawahi kukuona hapa mtaani
.akatoa simu na kupiga kisha huyo kasepa nikabaki mimi na yule mpangaji
ambaye anaamia nikaanza kumlaumu
kwanini umenidanganya kuwa umeshaongea na mwenye nyumba mimi nifanye kazi yule mpangaji akabaki ameduwaa tu kijana jr nimeongea nae na nikamwambia ni wewe akasema uje urekebishe na shangaa anasema kwamba hakujui. mimi nikasepa zangu home kesho yake nikaanza kuumwa moyo na kifua nikigeuka upande siwezi napata maumivu makali ya moyo kwa ndani nikikoa au kuongea ni maumivu per day kazi yangu ni kulala chali nikapelekwa mnazi mmoja kupiga x-lay nikaambiwa sina tatizo lolote kwenye moyo nikaandikiwa sindano tano za powercef aiseee sindano kali zinaumaaaa balaaa nikachomaa after five day nikamaliza ila maumivu ya moyo yapo pale pale kazi yangu ikawa ni kulala kuna siku bimkubwa akanifata kijana jr mara ya mwisho ulifanya kazi nyumba gani nikawa sina kumbukumbu vizuri kumbe yule mpangaji wa yule mzee alikuja home kuniulizia akaambiwa amelala anaumwa ndio akamwambia bi mkubwa yote yaliotokea Fasta tu bimkubwa wakanipeleka kwenye rukya(maombi ya kiislamu) ndio nikakaa sawa yule mzee nikikutana nae anashtuka sana mkuu wanao kupinga ndio hao hao wazee wa Ndago . mwaka jana mwishoni nyumba ameivunja amejenga kanisa baada ya ile nyumba kukosa wapangaji na siri mtaani kuvuja mauza uza ya mule ndani jamaa ana vx kali anauza kiduka anavaa ndala amegeuza za rangi tofauti
Asante kwa kushindwa kujibu hojaAcha ubishi, Ujiji ndo sehemu iliyodumaa kimaendeleo katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji.
Nami Ni mfuatiliaji Sana.Yap namfatilia pale kila siku
Wewe hautaonekana ila pesa ukizishika tu na kuzibeba zitaonekana hapo ndipo shida itakapoanziaAisee hiyo ndumba ni nzuri nikiipata na ingia benki mchana kweupe na jichotea mkwanza kiulaiiiini!!
Mamba wa kichawi sio sAlafu mamba huwa anameza baada ya kutafuna so haiwezi kutokea umezwe na Mamba na upone!
Alafu hata risasi akipigwa aingii mwilini zinadundaAisee hiyo ndumba ni nzuri nikiipata na ingia benki mchana kweupe na jichotea mkwanza kiulaiiiini!!
Liberatus. Ballow wa MwanzaKwa maelezo hayo naamini kweli kuna watu wanamtisha
Liberatus. Ballow wa MwanzaKwa maelezo hayo naamini kweli kuna watu wanamtisha