Black Sniper
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 32,406
- 55,148
sasa si bora hao wanaburudisha huko kariakoo kuna watu wanatembea wanauza sigara wameshika mawe wanayagonga gonga gonga kelele zinazotoka hapo ni balaa!Kariakoo mitaa wanapouza vifaa vya ujenzi na umeme angalau hakuna purukushani sana
Ila kuna mitaa wanayouza nguo za wanawake kwenye meza etc aisee hatari sana wauzaji wanaimba wanapiga makofi sijui ndio mtindo gani huo wa kufanya biashara
Siyo wanaoshinda huko tu ila hata kwa watu wengine. Hii ni culture mbaya sana tumejijengea. Bado barabarani huko, honi za magari na muziki.Huwa nawaza hatma ya hawa wanaoshinda masokoni ikoje
Daaaaahh
Usiombe ukawa na fremu jirani na fremu ya kuingiza nyimbo kwenye simu utajuta, wanamispika balaaNchi kelele kila mahali kila mahali mamiziki mziki tumekuwa taifa la wakata mauno.....
Ova
Masaki kuna tangazo limewekwa kelele marufukuNCHI HII NI KELELE KILA MAHALI
usiombe nyumba yako iwe karibu na msikiti utatamani uhamee!Usiombe ukawa na fremu jirani na fremu ya kuingiza nyimbo kwenye simu utajuta, wanamispika balaa
Kwa mimi muislam naona poa tuusiombe nyumba yako iwe karibu na msikiti utatamani uhamee!
kwa sababu wewe ni mchawi na msikiti unakuumbua kwa uchawi wakousiombe nyumba yako iwe karibu na msikiti utatamani uhamee!
Acha uchawi wewe..., peleka umwinyi wako huko ndegelec.dubai ni soko kubwa sana duniani lakini hawatumii spika kufanya biashara, tanzania huwezi kumkuta mwarabu au muhindi anafanya biashara yoyote akitumia spika hii ni sisi tu ifike wakati sasa TRA ikusanye kodi ya kila spika na sisajiliwe ziwe na namba kila mwaka unalipia na kwa mwezi elfu 15000/
Nishirikishe chimbo lako jipyaNdio boss
Karume napapenda lakini hiyo tabia ya kushikana na 'kulazimisha' niende wanakotaka wao siipendi
Juzi niliamua kuingia soko la mitumba Karume kwa mara ya kwanza. Kweli ni sehemu nzuri ya kupata nguo nzuri za mitumba. Ila kuna kero moja isiyovumilika kwa watu tunaopenda ustaarabu.
Kila mfanyabiashara ana spika kwahiyo kelele za pale zimekuwa ni kero kubwa sijui wenyewe wanaonaje ila kwangu palinishinda. Yaani hizi spika ni kero sana.
NEMC WAZIPIGE MARUFUKU NI UCHAFUZI WA MAZINGIRA
Matangazo sio lazima yawe ya kelele na usumbufu, hata ukibandika vibao vya kuonyesha bei nayo ni matangazo.kwa kweli vinakera ila sasa BIASHARA NI MATANGAZO utafanyaje sasa
Sio sahihi, huko ni kuwakera na kuwafanyia vurugu wastaarabu masikini na wenye vipato vidogo.Kaka mimi kwa mtizamo wangu nadhani pia ni nchi zote kama sio dunia nzima, ustaarabu unaendana na kipato huwezi kuishi uswahilini ukataka ustaarabu ukaeleweka
Kama una kipato cha ustaarabu usirudie tena kwenda huko karume kwenye makekele, nenda maduka makubwa makubwa
Huko Karume waichie hao ambao sio wastaarabu
Lakini pamoja na changamoto zote hizi serikali bado inaweza kuwapanga watu katika umaskini wao, mbona waliamua Wamachinga waondoke baadhi ya maeneo wakaweza,.mbona walipiga marufuku boda boda kati kati ya mji wakaweza. Hapo Karume ni kupiga marufu tu hivyo vipaza sauti kwa wote na wala hakuna mtu atakayejigusa kwa sababu kiuhalisia hata havina mchango mkubwa sana wa maana kuvutia wateja kwa hao wauzaji.Tunaweza kuweka mifumo ya kujiendesha kistaarabu sehemu nyingi.
Tunaweza ku plan mambo yawe ya kistaarabu hata sehemu za watu wa hali ya chini.
Kwa kweli, huko ndiko tulikotokea.
Dar es salaam ulikuwa ni mji wa kistaarabu. Kuna vijana tukiwahadithia kuwa mji ulikuwa na umeme, maji, mabasi ya usafiri wa umma mpaka ya Icarus Kumbakumba, huduma za kuzoa takataka angalau mara moja za Halmashauri ya Jiji, mpaka miaka ya mwanzo ya 1980s, watu wanaona kama hadithi za kubuni.
Ni vigumu sana kuwa na ustaarabu kama kuna mfumuko mkubwa wa idadi ya watu, watu hawana kazi, wenye kazi kazi nyingi ni za "disguised unemployment" kama hizo za umachinga.
Ni vigumu sana kuwa nanustaarabu katika jamii yenye watu wenye njaa, njaa inaondoa ustaarabu. Hapo Karume hata kama mtu kalelewa kwa misingi ya heshima na kutoshikashika watu huko kijijini kwao, akija mjini na kuona ushindaninwa kibiashara ndiyo unamtaka afanye hivyo ili kufanikiwa, atafanya hivyo tu.
Njaa haina ustaarabu.
Ukitaka ustaarabu, tengeneza uchumi vizuri uondoe njaa kwanza.
Sisi tulijitahidi kuendeleza ustaarabu hata kwenye njaa ya miaka ya 1980- 1985, tukapanga foleni kwenye maduka ya kaya kununua chakula, tukisaidiwa sana na idadi ya watu kuwa ndogo. Ni vigumu sana kukosa ustaarabu kama ukiangalia kushoto unamuona mtu mnayesoma naye, ukiangalia kulia unamuona mtu mnayesali naye.
Sasa hivi, kuna njaa halafu kuna massive rural urban migration, vijana wanatoka vijijini mwao, wanakuja mijini hawamjui yeyote, wana njaa katika mji mkubwa ambao hawamjui mtu, hapo ustaarabu ni kitu cha mwisho kabisa katika mawazo yao.