KERO Vispika vya matangazo vimekuwa kero kubwa kwenye masoko, mamlaka ipige marufuku

KERO Vispika vya matangazo vimekuwa kero kubwa kwenye masoko, mamlaka ipige marufuku

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Hizo ni baadhi ya laana za umasikini
Nchi zinazojielewa huwezi kusikia upumbavu huo, sio kwenye mabasi wala miziki na maspika kila kona
Hata kwenye usafiri wa Umma kwenye madirisha yameandikwa heshimu wenzio unapoongea na simu
Hapo ni simu tu kuongea unaambiwa ongea taratibu
Nyie mnafurahia kelele za miziki kwenye mabasi kama sio laana ni nini?
Hao viongozi ndio kabisa utakuta nao walitoka kwenye umasikini ndio maana wanaona labda Dunia nzima wako hivyo
 
Kariakoo mitaa wanapouza vifaa vya ujenzi na umeme angalau hakuna purukushani sana
Ila kuna mitaa wanayouza nguo za wanawake kwenye meza etc aisee hatari sana wauzaji wanaimba wanapiga makofi sijui ndio mtindo gani huo wa kufanya biashara
sasa si bora hao wanaburudisha huko kariakoo kuna watu wanatembea wanauza sigara wameshika mawe wanayagonga gonga gonga kelele zinazotoka hapo ni balaa!
 
dubai ni soko kubwa sana duniani lakini hawatumii spika kufanya biashara, tanzania huwezi kumkuta mwarabu au muhindi anafanya biashara yoyote akitumia spika hii ni sisi tu ifike wakati sasa TRA ikusanye kodi ya kila spika na sisajiliwe ziwe na namba kila mwaka unalipia na kwa mwezi elfu 15000/
 
dubai ni soko kubwa sana duniani lakini hawatumii spika kufanya biashara, tanzania huwezi kumkuta mwarabu au muhindi anafanya biashara yoyote akitumia spika hii ni sisi tu ifike wakati sasa TRA ikusanye kodi ya kila spika na sisajiliwe ziwe na namba kila mwaka unalipia na kwa mwezi elfu 15000/
Acha uchawi wewe..., peleka umwinyi wako huko ndegelec.
 
Juzi niliamua kuingia soko la mitumba Karume kwa mara ya kwanza. Kweli ni sehemu nzuri ya kupata nguo nzuri za mitumba. Ila kuna kero moja isiyovumilika kwa watu tunaopenda ustaarabu.

Kila mfanyabiashara ana spika kwahiyo kelele za pale zimekuwa ni kero kubwa sijui wenyewe wanaonaje ila kwangu palinishinda. Yaani hizi spika ni kero sana.

NEMC WAZIPIGE MARUFUKU NI UCHAFUZI WA MAZINGIRA

 

Attachments

Ni uwendawazimu mtupu, wao wanafikri hiyo ndio inawavutia wateja kumbe ni kinyume chake kabisa.
 
Kaka mimi kwa mtizamo wangu nadhani pia ni nchi zote kama sio dunia nzima, ustaarabu unaendana na kipato huwezi kuishi uswahilini ukataka ustaarabu ukaeleweka

Kama una kipato cha ustaarabu usirudie tena kwenda huko karume kwenye makekele, nenda maduka makubwa makubwa

Huko Karume waichie hao ambao sio wastaarabu
Sio sahihi, huko ni kuwakera na kuwafanyia vurugu wastaarabu masikini na wenye vipato vidogo.
 
Tunaweza kuweka mifumo ya kujiendesha kistaarabu sehemu nyingi.

Tunaweza ku plan mambo yawe ya kistaarabu hata sehemu za watu wa hali ya chini.

Kwa kweli, huko ndiko tulikotokea.

Dar es salaam ulikuwa ni mji wa kistaarabu. Kuna vijana tukiwahadithia kuwa mji ulikuwa na umeme, maji, mabasi ya usafiri wa umma mpaka ya Icarus Kumbakumba, huduma za kuzoa takataka angalau mara moja za Halmashauri ya Jiji, mpaka miaka ya mwanzo ya 1980s, watu wanaona kama hadithi za kubuni.

Ni vigumu sana kuwa na ustaarabu kama kuna mfumuko mkubwa wa idadi ya watu, watu hawana kazi, wenye kazi kazi nyingi ni za "disguised unemployment" kama hizo za umachinga.

Ni vigumu sana kuwa nanustaarabu katika jamii yenye watu wenye njaa, njaa inaondoa ustaarabu. Hapo Karume hata kama mtu kalelewa kwa misingi ya heshima na kutoshikashika watu huko kijijini kwao, akija mjini na kuona ushindaninwa kibiashara ndiyo unamtaka afanye hivyo ili kufanikiwa, atafanya hivyo tu.

Njaa haina ustaarabu.

Ukitaka ustaarabu, tengeneza uchumi vizuri uondoe njaa kwanza.

Sisi tulijitahidi kuendeleza ustaarabu hata kwenye njaa ya miaka ya 1980- 1985, tukapanga foleni kwenye maduka ya kaya kununua chakula, tukisaidiwa sana na idadi ya watu kuwa ndogo. Ni vigumu sana kukosa ustaarabu kama ukiangalia kushoto unamuona mtu mnayesoma naye, ukiangalia kulia unamuona mtu mnayesali naye.

Sasa hivi, kuna njaa halafu kuna massive rural urban migration, vijana wanatoka vijijini mwao, wanakuja mijini hawamjui yeyote, wana njaa katika mji mkubwa ambao hawamjui mtu, hapo ustaarabu ni kitu cha mwisho kabisa katika mawazo yao.
Lakini pamoja na changamoto zote hizi serikali bado inaweza kuwapanga watu katika umaskini wao, mbona waliamua Wamachinga waondoke baadhi ya maeneo wakaweza,.mbona walipiga marufuku boda boda kati kati ya mji wakaweza. Hapo Karume ni kupiga marufu tu hivyo vipaza sauti kwa wote na wala hakuna mtu atakayejigusa kwa sababu kiuhalisia hata havina mchango mkubwa sana wa maana kuvutia wateja kwa hao wauzaji.

Tatizo ni kwamba serikali haitimizi wajibu wake hata katika maeneo mengine rahisi sana yasiyohitaji hata gharama kubwa za utekelezaji.
 
Back
Top Bottom