Vita dhidi maambukizi ya corona Tanzania, kampuni ya Total Tanzania mfano wa kuigwa!. Ukifika lazima unawe, upimwe na mashine ndipo uruhusiwe kuingia!

Vita dhidi maambukizi ya corona Tanzania, kampuni ya Total Tanzania mfano wa kuigwa!. Ukifika lazima unawe, upimwe na mashine ndipo uruhusiwe kuingia!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Katika kusaidia kudhibiti Maambukizi ya virusi vya Corona, kukitokea any good practice, lets share ili na wengine waige.

Leo nimetembelea makao makuu ya kampuni ya mafuta ya Total, Total Tanzania, ukifika pale
  1. Hatua ya kwanza ni lazima unawe na maji moto tiririka hapo nje na sabuni, wamejenga kabisa sink la kunawia na liko permanent. Wewe hugusi chochote, ukiweka mkono sink lina sense maji tiririka ya moto yanatoka, ukiweka mkono kwenye sabuni sabuni nayo inatoka. System hii niliiona Kempinski na Serena. Ukimaliza unaingia kwenye blow drier kukausha mikono, na kumalizia kwa sanitizer.
  2. Hatua ya pili baada ya kunawa, unakutana na wahudumu wawili wa kike na kiume, wameshika mashine kama zile la traffic kupimia pombe madereva, unapimwa joto na mashine kwa kukupima maeneo mawili, kwenye paji la uso na kwenye mshipa mkubwa wa damu wa mkono huku umekunja ngumi. Kipimo cha joto la kichwa kisipotally na joto la mkono, safari yako kuingia Total inaishia hapo. Ukiwa fit, unaingia hatua ya tatu.
  3. Ukimaliza unapewa hand gloves unavaa, kisha unapewa face mask unavaa.
  4. Hatua ya nne ni kupewa escort, haushiki chochote, milango ni kufunguliwa ndipo unaingia ndani na kumsubiri mwenyeji wako kwenye chumba maalum sanitized. Unakaa kwenye kiti, mwenyeji wako akifika, anakaa umbali wa mita 1.5, kama umeleta barua yoyote au kitu chochote kinapokelewa na kupotishwa kwenye sterilisar tray ndio inapokelewa kama barua za ubalozi wa Marekani au UK!.
  5. Ukimaliza yule askari aliyekuleta anakusindikiza hadi pale nje, zile gloves na face mask ni zako, nje kuna dust bin ya kukanyaga inafunguka unavua na kutupa, au unaweza ku sepa nazo.
My Take
Huu ni utaratibu mzuri sana, sijui ile mashine inauzwa kiasi gani, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu angetangaza public corporations zote zinazotembelewa na watu, zaidi ya kunawa mikono, zinunue mashine hizo na asubuhi wafanyakazi wote wapimwe, na wageni wote wapimwe, wapewe face mask bure na zinunue sterile cabinets barua zote ziwe sterilised kabla ya kupokelewa.

Najua it's a cumbersome procedure lakini kwa wenzetu wanaojali, it's worth to spend little on prevention than much on cure.

Hongera sana Total Tanzania kuonyesha mfano, nadhani kwa sababu hii ni kampuni ya kimataifa, vikampuni vyetu locals, let's learn mambo mazuri kwa wenzetu waliotutangulia, Corona inazuilika.

Paskali
 
Hii kweli Paskali, mabenk makubwa yote yana uwezo nazo, hata kumbi mbalimbali za mikutanao wana uwezo huo borawaende kule Total wapate mafunzo
 
Pascal Mayalla,

Paskali bana, kweli ww ni msukuma, ukiona tukio kama linakukosha na kukupa hamasa mpaka unaona na sisi tujue lililokusimsimua! Ni hivi, hilo uliloiona hapo Total Ni mbwembwe tu, na wala haliwezi kufanya kazi kwenye mikusanyiko mikubwa, ambako ndio kwenye hatari kubwa ya maambukizi.

Pata picha watu watumie mtindo huo kwenye masoko, kisha uone kama kuna litakaloendelea. Anyway, ngoja tukupongeze kwa kwenda kwenye ofisi za total, na si ajabu umevuta chochote ili uje umwage hili promo humu jukwaani.
 
Hao wafanyakazi wa hapo nje ya ofisi yao wanajilinda vipi? Hawapigi chafya na kukooa, ingawaje wanatakiwa kufunika pua na midomo yao? Ila inasaidia kwa kiasi chake.
Ni mwendo wa mask na gloves full time
P
 
Paskali bana, kweli ww ni msukuma, haliwezi kufanya kazi kwenye mikusanyiko mikubwa, ambako ndio kwenye hatari kubwa ya maambukizi. Pata picha watu watumie mtindo huo kwenye masoko, kisha uone kama kuna litakaloendelea.
Process nzima ya kunawa na kupimwa hardly takes less than 2 minutes. Mkiwa wengi mnasimama one meters apart. Kama maonyesho ya sababa wali scan watu wote, what this and it is threat to life?.
P
 
Pascal Mayalla, Bei ya vifaa hivyo unless viwe subsdized na serikali. Wiki jana niliingia hotel moja ya nyota za kutosha maarufu sana mjini, mlangoni kuna mtu anakupa sanitizerz kwenye lift pia ila niliwasikia nafikir alikua floor manager akiwagombeza wafanyakazi wake pale mapokezi kuwa dumu la lita 5 sijui elfu 80000 linaishaje siku moja nyie mnatumiaje.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Process nzima ya kunawa na kupimwa hardly takes less than 2 minutes. Mkiwa wengi mnasimama one meters apart. Kama maonyesho ya sababa wali scan watu wote, what this and it is threat to life?.
P

Pata picha hiyo process ukaifanyie hapo kariakoo. Anyway, ngoja nisiharibu furaha na hamasa yako.
 
Back
Top Bottom