Wakuu, dunia nzima iko katika hali mbaya na janga hili la corona
Watanzania tusisubiri serikali kukataza watu kutoka nje na kujihusisha na mikusanyiko ya aina yoyote ile, ni vema tukachukua hatua stahiki kabla ya serikali kutoa katazo na kujituliza majumbani mwetu pasipo na serikali kutangaza
Ndio, watanzania tusiwe wajinga kiasi hiki
Corona ni janga kwa sasa na hapa nchini hali na kasi ya maambukizi ni kubwa mno!
Tunahitajika kuchukua tahadhali na kujikinga na janga hili kwa kutokutoka ndani kujihusisha na mikusanyiko ya aina yoyote ile
Hali ya maambukizi ya covid-19 ikiendelea kuwa tishio nchini bado viongoz was baadhi ya makanisa wilayan Kilolo wanaendelea na utaratibu wa kawaida huku tahadhari pekee inayochukuliwa ni kunawa maji pekee.
Makanisa ya Roma kuanza sa12 asubuhi hadi sa4 wanakuwa wamemaliza ibada 2 Moja ikianzia sa12 hadi sa1.30 ingine sa2.30 hadi sa4. Madhehebu Kama ya kilokole, fpct na angliakana wameendelea kuchukua ibada Moja inayojaza watu na ibada kuchukua muda mrefu kama sa3 hadi sa7. Hali hii ipo Sana makanisa yaliyopo tarafa ya mahenge wilayan Kilolo. Swali ni je wanapuuza maagizo ya serikali?