Vita dhidi ya Corona: Mikusanyiko ya watu isiyo lazima isitishwe, misongamano idhibitiwe ili kuepusha madhara makubwa zaidi

Vita dhidi ya Corona: Mikusanyiko ya watu isiyo lazima isitishwe, misongamano idhibitiwe ili kuepusha madhara makubwa zaidi

Leo nimeangalia TBC wameonyesha makanisani watu bado wamejaa wanaendelea na sala,sala zinasaidia lakini watu wamepokea tofauti sana,tahadhari ziko wapi au ndo kusema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa,hizi sala za siku 3 ndo kama imewapa makanisa go ahead.

Hivi hili janga tunapambana nalo kwa mtindo upi,kulikuwa na haja gani ya kufunga shule na vyuo kama makanisa yanaendelea ,tuache utani kwenye vitu serious lazima tujiongezee na tusisubiri mpaka mamlaka zitangaze kufunga kwa nguvu tunatakiwa tujiongezee.

Kama unaamini hutaathirika kwa kwenda kanisani au msikitini kwanini tukifika nyumbani usiku tunafunga geti na milango kwanini tusiache tu wazi tuombe ulizi wa Mungu?.

Ni vizuri makanisa na misikiti vikapigwa stop kwanza hili janga lipite na pia tujiongezee siyo tunasubiri tu matamko.

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Hamna namna inabidi kusema tu, WAKRISTO WENGI NI WAJINGA NA WAPUMBAVU. Ilitakiwa polisi waingie makanisani watembeze bakora hadi kwa mapadri.
 
Niko wilaya mpya ya Rorya zaidi ya miezi 2 ndani ya kipindi hiki ambapo tunahaha kukwepa maambukizi ya Corona. Bado watu wanashiriki misiba kwa amri maziko yasizidi saa 4. Bado minada na magulio yanaendelea kama kawaida.

Rorya imepakana na Kenya na Ina minada kama vile Randa ambayo iko jirani kabisa na nchi jirani ya Kenya.

Kinachofanyika Ni wafanyabiashara wa huku kwetu kuvuka kimagendo na kukuza mifugo yao Kenya. Inasemekana kuwa Kenya wao wamefunga mipaka yao na shughuli zote za minada. Ila wapo wafanyabiashara wanavuka toka huku kwetu kukutana na wakenya na kufanya Biashara.

Kingine cha kushangaza sijawahi kuwaona viongozi wa kiserikali wakipita mitaani kuelemisha jamii kuhusu hilo gonjwa la Corona. Si watendaji wa vijiji au kata utadhani hawapo. Tangazo pekee nililolisikia ni kuhusu uboreshaji wa daftari la wapiga kura. Mkuu was wilaya chukua hatu toa maelekezo.

Ni wazi uchumi more umeathirika vibaya lakini kwa hali hii jitahidi kuokoa Maisha ya wananchi wako bila kusubiri matamko kutoka juu. Kwa siku ya jana mkoani kwetu Mara tumepata mgonjwa mmoja, chukua hatua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ni sawa kufanya mkusanyiko wa maombi wakati mikusanyiko yote imezuiwa? Kwa nini viongozi wetu hawatii maanani maadili ya WHO? Wanafikiri Mungu anaipenda nchi yetu zaidi au ni wapuuzi wasiojifunza toka nchi nyingine? Au ni wapuuzi wanafikiri ni mambo ya wazungu bila kujua maelfu wanakufa kila siku?
 
Hivi ni sawa kufanya mkusanyiko wa maombi wakati mikusanyiko yote imezuiwa? Kwa nini viongozi wetu hawatii maanani maadili ya WHO? Wanafikiri Mungu anaipenda nchi yetu zaidi au ni wapuuzi wasiojifunza toka nchi nyingine? Au ni wapuuzi wanafikiri ni mambo ya wazungu bila kujua maelfu wanakufa kila siku?
Hata hiyo serikali yenyewe haielewi , kipi sahihi na kipi sio sahihi. Muisamehe tuuu
 
Hivi ni sawa kufanya mkusanyiko wa maombi wakati mikusanyiko yote imezuiwa? Kwa nini viongozi wetu hawatii maanani maadili ya WHO? Wanafikiri Mungu anaipenda nchi yetu zaidi au ni wapuuzi wasiojifunza toka nchi nyingine? Au ni wapuuzi wanafikiri ni mambo ya wazungu bila kujua maelfu wanakufa kila siku?

Dah Nimejiuliza sana ili jambo nikaona ni heri nivumilie tu eti kiongozi mkubwa kabisa anakuja kusema jaman tuombe korona iondoke yan .......

Colona haiwezi ondoka kwa kuomba kama tunavyoambiwa tuombe watanzania wezangu na kama tunaamua kuomba ili corona iondoke au tunusuliwe na ili janga basi tujue tu tunaomba tukifa tuingie peponi ila sio kuomba corona isienee tanzania uku tukiwa na mikusanyiko chungu nzima, kuzembea kuchukua hatua za kujikinga na vitu kama ivo oo

Ni ujinga kuruhusu jambo ili kusimamiwa na imani zetu na sio bidii yetu katika kufanya tuelezwayo ili kujikinga .....


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
  • Thanks
Reactions: prs
Cool down! Serikali ni sirikali.
Kesho kuna maombi spesheli pale Karimjee
 
Dah Nimejiuliza sana ili jambo nikaona ni heri nivumilie tu eti kiongozi mkubwa kabisa anakuja kusema jaman tuombe korona iondoke yan .......

Colona haiwezi ondoka kwa kuomba kama tunavyoambiwa tuombe watanzania wezangu na kama tunaamua kuomba ili corona iondoke au tunusuliwe na ili janga basi tujue tu tunaomba tukifa tuingie peponi ila sio kuomba corona isienee tanzania uku tukiwa na mikusanyiko chungu nzima, kuzembea kuchukua hatua za kujikinga na vitu kama ivo oo

Ni ujinga kuruhusu jambo ili kusimamiwa na imani zetu na sio bidii yetu katika kufanya tuelezwayo ili kujikinga .....


Sent from my iPhone using JamiiForums
Afrika nzima ni nchi yetu pekee inayo kabiliana na Corona kijinga, na wajinga wengi wataenda kufanya maombi na kuambikizwa au kuambukiza. Viongozi wetu na mtazamo wao wa kishamba na kijinga eti wazungu wame over react, utawaponza wengi na wao pia, tutachekwa na kutazamwa chini kama wajinga wakati tulikuwa tunaheshimiwa Afrika mashariki yote. Hawafuatilii habari za dunia jinsi watu wanavyokufa na kuambukizwa, hawafai kuongoza.
 
Yaani tuliowapa nchi hii tulipotea sana,yaani ni wazuri midomoni kuwa wanapambana na corona kumbe hamna lolote

Maambukizi yanazidi kusambaa kwa kasi lakini serikali hii imekaa kimya haichukui hatua

Namuuunga Zitto kweli tumewakabidhi serikali watu fulani. Kwa kweli tutakufa kwa corona tuishe


Kama serikali imeshindwa total lockdown au partial lockdown au kufunga mikoa ,kwa nini isisitishe shughuli kwenye maeneo yafuatayo

1. Masoko na minada

2. Vilabu vya pombe na baa

3. Kariakoo na maeneo yenye misongamano na kwenye mialo,stend za mabasi

4. Makanisa na misikiti

5. Kwenye vivuko na usafiri wa umma

6. Harusi, sherehe na misiba

6. Vijiwe vya pulu,draft,kahawa,fukwe,migahawa,mama ntilie,na maduka makubwa yenye misongamano

7. Uchimbaji mdogo wa migodi

Mtakubaliana na mimi sasa hivi haya maambukizi ya ndani yanashika au yatashika kasi kwenye maeneo hayo

Na ukiangalia shughuli zinazoendelea kwenye maeneo tajwa wala hawana muda na corona, wanaisikia redioni.

Hapa Afrika, Tanzania tunaweza kuwa kitovu cha maambukizi na vidole kutoka kwa majirani vitaelekezwa kwetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unataka watu wafunge biashara na wasifanye shughuli zao mtawapa mahitaji matatu? Usifananishe mataifa mengine na Tanzania wenzetu wanalipwa wakiwekwa lockdown Tz hela hakuna ya kuwalipa watu ukifunga hizo biashara. [emoji41]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji15][emoji15][emoji15]
dw_kiswahili_B_PKmx5Jpd4.jpg
 
Unataka watu wafunge biashara na wasifanye shughuli zao mtawapa mahitaji matatu? Usifananishe mataifa mengine na Tanzania wenzetu wanalipwa wakiwekwa lockdown Tz hela hakuna ya kuwalipa watu ukifunga hizo biashara. [emoji41]

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa Hata kama Wakitulipa Mahitaji tutanunua wapi ilihali maduka Yamefungwa na Masoko labda Wagawe vyakula xax

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom