Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu Tetty,nimemsikiliza RC Makonda lakini kuna mahali sijaelewa mantiki yake. Pale anapotaja majina ya akina fulani lakini anashindwa kutaja majina mengine na kusema tu mmiliki wa a,b,c,d na kuendelea,maana yake ni nini? Hapa kuna tafasiri nyingi,lakini mbili tu ni kwamba mmoja aliyetajwa jina binafsi ni mhusika wa moja kwa moja na yule aliyetajwa kama mmiliki ni kuwa inawezekana katika biashara yake kuna kitu kama hicho,hivyo yeye anahitajika kama kuweka "clarification". Ni vyema ingetumika, "mmiliki wa club ya usiku na casino fulani kama ilivyotokea kwa wamiliki wengine.Siasa za Makonda ni za chuki.Wale waluosemwa na Sema kwamba wamehonga wakafutiwa mashtaka amewataja??Diamond amemtaja??Mmiliki wa zile shule zenye jina kama za wakatoliki je??Ifike mahali Tuache siasa chafu. Mnadhani Mbowe angekuwa anafanya hiyo Biashara mpaka leo angekuwepo??
Kuna siku hizi chuki zitatufikisha pabaya.Tutaishia kaka naomba nisamehe umeshaharibu sifa ya MTU.
Angewasikiliza wenye taaluma yao kuliko kuropoka.
Kumekucha!!Ni siku nyingine tena,Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa wa Dsm,ndugu Paul Makonda ataongea leo na waandishi wa habari kuhusu muendelezo wa vita ya madawa ya kulevya ktk jiji la Dsm.
Mkuu wa Mkoa atakuwa mubashara Azam Tv mara ifikapo saa 05:00 asubuhi leo hii.
Tetesi ni kuwa,mkutano huo unaweza kuwa ni kujibu tuhuma za kuwa anawakabili "dagaa" na wakati "mapapa" wa biashara hiyo wapo.Na majibu ya mkuu wa mkoa yatakuwa ni kuwataja hao mapapa na kuelezea hatua zitakazochukuliwa...
Tega usikie....(Stay Tuned)
=======
UPDATE:
=======
Ameanza kwa Kumshukuru Rais wa Jamuhuri.
Paul Makonda asema anataka wauzaji wa dawa za kulevya wajulikane hadharani na hakuna sababu ya kuficha.
Paul Makonda asema vita vya dawa za kulevya vilianza muda mrefu kwa kufutilia hali ilivyo mitaani.
'Kuna watu nilitaka nikutane nao polisi, kuna tofauti kati ya kukamatwa na kuitwa, unapoitwa unapewa nafasi ya kusikilizwa'-RC Makonda
'Kampeni hii dawa ya dawa za kulevya si ya kufanyika kimyakimya tunataka hata watoto wadogo wajue dawa hizi ni hatari kwa afya'-RC Makonda
'Asante kwa watu kama TID, nawapongeza kwa kukiri na kusema kuwa wanatambua namna walivyoingia na kuomba serikali kuwasaidia'-RC Makonda
'Tumemaliza awamu ya kwanza vita ya dawa za kulevya, sasa hii ni awamu ya pili ambayo itakuwa si nyepesi itakuwa na mawimbi mengi-Makonda
'Awamu ya 2 ya vita ya dawa za kulevya tunaianza leo na tunaianza tukiwa tumekamilika, nimekuwa kwenye operesheni usiku na mchana- Makonda
'Watu wanafanya biashara za dawa za kulevya na meli zinazokuja na mafuta'-RC Makonda
'Kuna mama kazi yake ni kusafirisha watoto wa kike ambao wanapewa dawa za kulevya, wawili wako jela China na amewatelekeza'-RC Makonda
'Tukiendelea kuvutanavutana tutapoteza lengo la kupambana na dawa za kulevya'-RC Makonda
'Tukishindwa vita hii ya dawa za kulevya, hajashindwa Makonda au Rais Magufuli tumeshindwa wote'-Rais Makonda
'Tuko na majina 65, nitahitaji kukutana nao ijumaa, wako wanaosemekana wanatumia, wako wanasemekana wanazo taarifa zitakazotusaidia-Makonda
'Nawashukuru wenyeviti wa mitaa wameanza kuleta majina ya watu ambao wanawasiwasi nao kuhusu dawa za kulevya'-RC Malone's
'Kila tunayemuita tunamfahamu kuliko mnavyofikiri kazi yetu ni kuwasikiliza'- RC Makonda
'Zile nyumba mnazozitilia shaka, hamuelewi hata kinachoendelea ni wajibu wetu wananchi kutoa taarifa na taarifa zitakuwa ni siri-RC Makonda
'Kuna ambao tuliwaita wako nje ya DSM, wapo waliotoa taarifa na watafika ila wapo waliokimbia tunawafuatilia na tutawapata wote'- RC Makonda
'Nawashukuru ndugu zangu walioko nchi mbalimbali kwa kunipigia simu na kunipa taarifa mbalimbali'-RC Makonda
Hujaona video yao?wema athibitishe vinginevyo sheria ichuke mkondo wake!
Zungu vipi mhindi maana habari zake zimevuma sana. Namba zinasomeka haswa
ina maana wote wamesingiziwa au mbowe peke yake?Siasa za Makonda ni za chuki.Wale waluosemwa na Sema kwamba wamehonga wakafutiwa mashtaka amewataja??Diamond amemtaja??Mmiliki wa zile shule zenye jina kama za wakatoliki je??Ifike mahali Tuache siasa chafu. Mnadhani Mbowe angekuwa anafanya hiyo Biashara mpaka leo angekuwepo??
Kuna siku hizi chuki zitatufikisha pabaya.Tutaishia kaka naomba nisamehe umeshaharibu sifa ya MTU.
Angewasikiliza wenye taaluma yao kuliko kuropoka.
No way!!! Mahufuli yupo serious na wapinzani et...there's no way tukapata suluhu kwa kusubiri' au maneno tuu sio kwa maufuli aseeTusubiri tuone mkuu nini hatma yetu.
Hiii Vita Makonda ametangulizwa tu, hata waliotajwa wenyewe wanajua Makonda ni mjumbe tu kwenye hili sakata.Whatever is excellent kwa anachokifanya makonda na alipo fikia hata leo akisema anaishia hapo still nitampa big up sanaaaa, wapo viongozi wengi wenye mamlaka wanaoweza kushuhulikia madawa yakule sio yeye tu na wao wafanye kwamuendelezo sio kumuachia mtu mmoja nakukaa pembeni heti tumuone atakapofikia, nachoamini MUNGU akiwa upande wake hakuna hata mmoja atakae mshinda, kaza buti makonda kwa hili la madawa umeukuna moyo wangu.
Umenena vyema nduguHuyu RC ana busara sana na anajua nini anaongea, wakati gani, namna gani kwa utaratibu upi.... Pia anajua nini kianze na kipi kifuhate..... Tumuunge mkono........ Sasa wanaopiga kelele (Wanajijua kama wana maslahi ama kwa ushabiki tu) baadaye kidogo mtaamua wenyewe kwa busara zenu kuchagua ushabiki wa kijingakijinga ama ukweli wenye faida kubwa kwa maslahi ya nchi hii kupunguza hili tatizo ama kulimaliza kabisa..... Madawa ya kulevya hayana maana kabisa anayeshabikia hii biashara ni wa kuwamwonea huruma sana sana..... Waathirika wenyewe wanaomba kusaidiwa maana ni sawa na utumwa, unakuwa mtumwa hata kama hupendi, hali ile ni mbaya kabisa, Hasara zake ni nyingi mno; inachangia uhalifu kwenye jamii, inapoteza nguvu kazi muhimu, upeo wa kufikiri unashuka chini (Elimu) Inachangia kuenea kwa magonjwa (Afya) nk ...........Big Up RC! Tuko pamoja sana
Ukiangalia suala la Lema ni 'sheria inafuata mkondo' na ukigeukia hili kuna wanaoambizana kuwa "hachomoki hapa"!Mwanawani...mbona sielewi...naunganisha nukta..kutoka kwenye blis...ninakuja..kwenye...shamba lake..ninakuja sijui kwenye madai..gani ya bank sijui..njoo sasa kwenye wabunge wake na viongozi wake walioweka ndani mpaka jana...ninamuona kamanda kwenye wakati mgumu sana..