Vita kati ya majangili na askari wa hifadhi za wanyama pori

Vita kati ya majangili na askari wa hifadhi za wanyama pori

Rufiji dam

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2020
Posts
4,107
Reaction score
9,671
Kuna vita mbaya sana ipo lakini watu hawajui, hii vita kati ya Jangili na Askari wa kulinda na kutunza Wanjama katika hifadhi za Wanyama.
Hii ni zaidi ya vita hawa wakigumiana hakuna majadiliano ni vyuma tu vinatembea. Kwa sisi tuliokulia Selou Game reserve tunajua hii vita.

Kuna siku tupo porini hatua chache kutoka pale lilipo treini ndani ya Selou tukakatiza sehemu kuna mti upo katikati ya barabara uligoma kutolewa.

Mbele tukagumiana na mvuvi haramu jamaa alijichochea kwenye bwawa lina mamba kibao nikauliza sasa itakuwaje mzee mmoja Ranger akanijibu hao ndio maadui zetu na huyo hawezi kuliwa na hao mambo Wandenge wanauchawi sana.

Tukaenda mbele mida ya usiku mwingi tukaona moto kwa mbali unawaka tukajichochea ile tumefika tu tukakuta jamaa walikuwa wanabanika samaki. Nikajisemea hii dunia kuna mtu anaogopa kutoka ubungo mpaka mbezi kwa miguu. Wakati kuna jangili anakatika selou usiku mwingi bila hofu.

Siku hiyo tukakosa mawindo yetu nilikuwa katika mafunzo kwa vitendo. Huyu mzee akaniambia humu ni msutuni kina NguruMbili ama makucha(Simba) na Abeid Mziba(Nyati mzee wa Vichwa) na binadamu Jangili mzee akasema bora ukutane na Wanyama kuliko Jangili. Akasisitiza ni vita kali ambayo haina kelele.
 
Siku nafanya zangu boat na wageni ziwa manze pale selous mgeni akaona mtu kichakani kwa mbali,alivyonitonya kuchukua binocular nikaona njema kama tano hivi zimelala na gobole zao standby asee nileguza chap boat camp.

Sikukumbuka hata kama nina radio call
Baadae tukio hili lilikuja kuniletea tatizo pale kazini
 
Kuna vita mbaya sana ipo lakini watu hawajui, hii vita kati ya Jangili na Askari wa kulinda na kutunza Wanjama katika hifadhi za Wanyama.
Hii ni zaidi ya vita hawa wakigumiana hakuna majadiliano ni vyuma tu vinatembea. Kwa sisi tuliokulia Selou Game reserve tunajua hii vita.
Yani natamanigi Sana mazali kama haya yakukutana na majangili porini huko tena usiku. Huo mkono nitakaoutembeza nitaacha historia na alama ya kudumu.

Asante mleta mada Lazima sasa hivi nizame chaka niitendee haki black belt yangu.
 
Upo sawa ila mwandiko wako ndio shida. Mwaka jana mwezi julay kama si August, kuna game wawili waliuliwa kikatili japo mmoja hakuonekana. Ilikuwa kwenye milima ya Udzungwa hapo maeneo ya Mangula.

Inasemekana hao walizi wa wanyama pori walikuwa na pikipiki. Inasemwa kwamba walikutana na majangili wakawateka na kisha kuwachukuwa wao na pikipiki yao mpaka kwenye mto. Wakawaamuru wavue nguo na kisha kulazimishwa kuingia kwenye maji na kulazimishwa kuzama. Aisee jmaa wakafa maji. Majangili yale yakatokomea na kuacha ile pikipiki na zile nguo pale.

Baada ya msako mkali wa kuwatafuta akapatikana mmoja. Mwingine hakuonekana. Kwenye lile tukio unaweza kudhani kwamba jamaa walipaki pale kusudi waoge, kwa jinsi zile nguo na pikipiki zilivyokutwa. Msiba ule ulikuwa mgumu kwa familia zao haswa kwa familia ya yule mmoja ambaye hakupatikana.

Hii vita kati ya jangili na game anayemwahi mwinzie anamla kichwa. Hata hivyo hawa magame ni wakatili sana.
 
Kwaio unataka kusema bora iwe ivi kuliko majangiri mkuu?
thewildlife_tz-20211126-0001.jpg
 
Tatizo ma game wengi mnajifanya mna huruma sana kwa wanyama, mkiwa bush mnajiona wenyewe ndo mshakua matarzan na kuusahau ubinadamu.

Hao wanyama mmewafata porini na kujimilikisha kama wenu, na roho mbaya ndio imewatawala sijui nani kawalisha sumu hiyo.

Naongea haya kwakua kuna dogo aliahawah pigwa nusu kufa kwasababu alikutwa na manati akiwa ameshika ndege mmoja aliyemuwinda
 
[emoji3][emoji3]
Ukipata muda tupia story yoyote inayomhusu kichaa wa pori a.k.a nyati.
Najua unaifaham

Sent using Jamii Forums mobile app
Nyati msikie tu, bora ukitane na pride ya simba ila sio nyati nakumbuka miaka hiyo nilipokuwa nafanya tafiti katika mbuga ya Serengeti ile wakati wa kufanya darting kuna mzungu mmoja alikoswa koswa kupigwa pembe..
 
Hawajamuona Simba au wanazuga!

Upo sawa ila mwandiko wako ndio shida. Mwaka jana mwezi julay kama si August, kuna game wawili waliuliwa kikatili japo mmoja hakuonekana. Ilikuwa kwenye milima ya Udzungwa hapo maeneo ya Mangula.
Ila askali wa wanyamapoli ndio makatili... Kuna moja nilisikia walimtoa mtu ngozi ya kwenye unyayo yote yaani walimchuna miguu yote bila ganzi na kumruhusu aondoke,, dah so sad ila na hao majangili hawajawahi kusikia kila siku ni mambo yale yale.
 
Back
Top Bottom