Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 78,790
- 128,275
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naomba unipatie majibu ya maswali yangu haya ma4, ili kuthibitisha kauli zako hizo mbili.Kiuhalisia ile vita haikuwa na Ulazima
Watanzania walikufa wengi sana kuliko Waganda.
Ukikutana na wanaoijua ile vita vizuri watakueleza.
Nyie madogo wa 2000s hata akili hamna kabisa. Yaani unaandika vitu kama hivi bila hata kufikiriaKumbe unakubaliana na maelezo yangu kuwa mchele wa Tailendi umeanza kuingia Bongo baada ya vita ya Uganda.
Halafu, weka jazba pembeni. Kuweka record ni kuwa IDD Amin alivamia mpakani mwa Uganda na TZ (akaingia maeneo ya Kagera)
Unakubali kuwa vita haikua na ulazima?
Kwamba ilikua inatosha kumwondoa adui mpakani arudi kwake, tubaki tukilinda mipaka yetu.
Kulikua na haja gani kwenda mpaka Kampala hadi Sudani huko na kuyaacha majeshi yakilinda usalama huku yakiendelea kutumia rasilimali za Tanzania?
Kwanini baada ya kumkimbiza Amini pale Kagera wasingerudi na kubaki kulinda mipaka tu na kuwaacha Waganda wapambane na uongozi wao?
Nilikuwa katika mazingira ya jeshi la akiba wakati huo, na siyo kweli kuwa Jeshi la Uganda lilikuwa liko vizuri sana kuliko la Tanzania. Wale askari wetu waliokufa wengi kwa kipindi kimoja ni wale waliotumwa na Brigadia Yousufu Himid ambaye wakati huo ndiye aliyekuwa Brigade Commander wa Brigedi ya Magharibi kabla ya kuondolewa (kwa kosa hilo) na nafasi yake kukaimiwa na Kanali Kotta - baba yake na Faraja Kotta.
Brigedia huyo aliituma battalion kadhaa zivuke mto kwa mitumbwi kuingia hilo enelo lililokuwa limetekwa baada ya daraja kuvunjwa. Kwa vile upande ule uliokuwa umetekwa ni high tactical ground ndiyo maana askari wa Tanzania waligundulika na kuuwawa kwa vile walikuwa wanajiandaa kuvuka na bunduki tu, bila ya kuwa na silaha kubwa.
Askari wetu wa kwanza kuingia Uganda kukomboa ile sehemu iliyokuwa imetekwa na kusaidia ujenzi wa daraja la muda walipitia Rwanda. Ni vivyo hivyo pia kwa kupitia Rwanda ilikuwa ni rahisi wao kuingia ndani zaidi ya Uganda kwa upande wa Magharibi, hivyo hata mashambulizi makubwa ya kuingia Kampala yalitokea huko Magharibi, na ni kweli askari wetu wengine walishafika mbali karibu na Sudan kabla ya kuja kushambulia Uganda.
Kikosi Kikikubwa cha Idi Amini ni kile kilichokuwa kinaitwa Simba Batallion kilichokuwa na makazi yake pale Masaka (siyo Mbarara) ambacho baadaye kilikuja kusaidiwa na askari wa Libya wakati wa yale mapambano ya Lukaya. Kikosi kile cha Simba Batallion kilizingirwa pia na majeshi ya Tanzania kutokea Magharibi kikiongozwa na Brigadier Imran Kombe na Major General Marwa, ndipo Amini alipotuma wale askari wa Libya waje kusaidia na kufanya mapambano ya Lukaya kuwa makali sana lakini mwishowe Simba Batallion na askari wa Libya wakasalimu Amri na kuiacha Baracks ya Masaka mikononi mwa Imran Kombe. Ukishaondoa hiyo Simba batallion na Askari wa Libya, sehemu kubwa ya jeshi la Amin lilikuwa ni "maharage ya Mbeya tu"
Rangi ya nyekundu ndiyo iliyokuwa ruti ya kwanza kuingilia Uganda, halafu ruti ya kijani ndiyo ilikuwa ruti ya pili baada eneo la kaskazini mwa mto Kagera kusafishwa na daraja la muda kujengwa.
View attachment 1478112
Uwongo !!Niliwahi ambiwa na Mzee mmoja kuwa mdogo wake alipigana Ile vita
Ni kwamba wanajeshi wa jwtz walizingilwa na kuwekwa Kati halafu amri ikatolewa na na jeshi la Uganda kuwa walale kifudifudi halafu kifaru kikapita kina wakanyaga na kuwaua kabisa. Basi waliofanikiwa kukimbikia wakarudi na kusema yaliyo tokea yote. Wale waliokuwa wanaambiwa kilichotokea wakaadhibiwa Kwa kupigwa viboko 10 Kila mwana jeshi halafu wanaambiwa wasonge mbele.
Wale walio nusurika kufa wakaambiwa ninyi pandeni kwenye gari hili mrudi uraiani.
Kweli wakapanda lkn mmoja wao akawaambiwa wenzeke jamani kama tulio wasimulia kilichotokea wamepigwa vibokona kuambiwa wasonge mbele je sisi tunaenda kufanywaje? Akasema Mimi naenda vitani huko tunaenda kunyongwa kabisa!!
Ikabidi washuke na kwenda kujiunga na wenzao.
Je hili Lina ukweli wowote au ilikuwa chai yenye kwamba ndani yake?
Asante kwa elimu wengine tunapita kujifunza.Pumba kabisa wewe kwani kumbe unaongea mambo usiyoyajua bali ya kuhadithiwa tu. Hata hujui kuwa mahindi ya Yanga yalikuja kutoka wapi halafu unakuja hapa kupiga kelele.
Kwa vile mimi ni mwalimu nitakufundisha ifuatavyo. Mahindi ya Yanga yaliingia Tanzania mwaka 1975 kutokana na ukame uliokuwa umeikumba nchi mwaka 1973 na 1974 ikiwa ni muda mfupi sana baada ya opereshini vijiji ambayo ilivuruga kilimo cha asili na kuacha watu hawana chakula; na ulikuwa ni msaada ulioidhinishwa na Rais Jimmy Carter wa Marekani kupitia USAID.
Ule mchele wa Jasmine kutoka Thailand haukutolewa msaada kwa ajili ya vita, bali ulianza kuagizwa kuingia nchini wakati wa utawala wa rais Mwinyi na wafanya biashara binafsi baada ya Liberalization; hiyo ni pamoja na mafuta yakupikia ya OKI kutoka Singapore, ambayo ilikuwa ni kwa sababu za kibiashara kushindana sokoni tu. Kama unazungumza unga wa Yanga baada ya vita ni kuwa hukuwepo na wala hujui hali halisi ya wakati ule, kwani tuliokula unga ule mpaka mwaka 1977 hatusemi vile.
Vita iliaza mwaka 1978 wakati nchi haina unga wa yanga tena. Kwa upande wa pili; ni kweli kuwa uchumi wa nchi ulivurugika sana kwa sababu Tanzania ililazimika kununua silaha kali za kupambana na Amin kwa muda mfupi ambazo hazikuwa kwenye bajeti ya nchi; na ikatumia hela za kukopa zinazokaribia bajeti ya miaka miwili au mitatu hivi ya nchi ili kupata mitambo ya Balllistic misiles (BM40) mingi kuliko uwezo wake wakati ule kwa sababu amini alikuwa ameuza migodi yote ya Shaba kwa Urusi kusudi apatiwe vifaru vingi; na alikuwa na vifaru vingi sana ambavyo jeshi letu lilivivunjavuvunja kama chungu ambacho hakikupita kwenye tanuru. Kitu ambacho Tanzania tunashukuru tena kwnye vita ile ni kuwa baada ya vita kuanza, Urusi nayo ikaivamia Afghanstani kipindi hicho hicho na hivyo ikawa iko bize kupambana na Mujahedeen, ikaacha kupelea vifaru kwa Uganda tena.
Wewe bado hujui lolote kuhusu vita. Vita sio nzuri lakini nia na kusudi la vita linakusukuma kupigana. Kauli mbiu ya vita popote ni kupigana hadi tone la mwisho la damu hasahasa linapokuja suala la hadui kukuvamia na kuchukua nchi yako. Mvamizi akifanikiwa kukuteka na kutwaa ardhi yako kinachofuatia ni kukufanya mtumwa wewe na wanao na wazazi wako na wake zako? Sasa wewe usiyejielewa je huko tayari kufanywa mtumwa? Idd Amini aliweka wazi kuwa mkoa wa Kagera ni mali yake na akishautwaa atatwaa tena Mwanza na eneo looote la ziwa Victoria upande wa Tanzania mali yake. Na akasema 'by saa nne kesho chai atainywea Dar es Salaam' na kweli ndege za Amini zilifika hadi Dar kabla ya kulazimishwa kutua na kutekwa na jeshi letu. "The is nothing good in war except it is ending". Wee unaongelea hasara kwa upande wa Tanzania, ulishawahi kuwaza hasara ya Uganda? Kwanza kile kitendo cha kupigwa, na kiongozi wako wa nchi kukimbia, na nchi ngeni ikakukalia kwa muda kadhaa, ni kitendo cha AIBU MPAKA KESHO. Tanzania tulishawahi kuitawala Uganda! Na kuanzia hapo tukamuweka Rais tunayemtaka na anatawala mpaka sasa!Vita hiyo tulipoteza sana kuliko faida tuliyopata Watanzania.
Hili lilikuwa kaburi refu la uchumi wetu hadi leo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwenye vita kuna kitu kinaitwa tactical manuvers, hizi ni muhimu sana,, adui huwa anajipanga sana kwenye njia rahisi. hivyo utapoteza watu wengi hapo, lakin inakuwa ngumu kwa adui kujua njia zako na ni rahis kumpiga.Tulizunguka sana. Arua, Kasese, portfot na kwingine kabla ya kufika Kampala. Swali ni kwanini tulizunguka sana badala ya kukatisha tu na kufika hapo kampala na kumtimua huyu nduli?
Hiyo ni kweli kuna story azisemwi hadi leo mzee wangu alikuwa rubani wa kuvulumisha mabomu enzi hizoKwa taarifa yako majeshi ya Uganda yalikuwa vizuri sana kabla ya uasi.
Vita ilipoanza tulipoteza wanajeshi wengi mno japo taarifa zilifichwa, binamu yangu amepigana na amesimulia mengi mno ambayo serikali haikuweka na haitaweka wazi.
Hivyo unaposema kwani tulizunguka, unafikiri hao jamaa walikuwa dhaifu kiasi hicho?
Vita ina mbinu nyingi, moja wapo ni kumzunguka adui wakati yeye anapambana na wale waliom face... ghafla anashangaa anashambuliwa eneo ambalo hakutegemea.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kupoteza askari katika vita ni jambo la kawaida! Hiyo ni vita sio harusi! Lakini kinachoangaliwa mwisho wa vita nani kashinda? Kama Tanzania tungehamua kuwaua askari mateka wa Uganda na Sudani ingejuwa "massacre". Tanzania ilipokuwa inakamata askari ilikuwa inawaweka mateka (ilikuwa haiwahui)
Wee mwehu nini? Nyerere vita ilimshinda kivipi? Idd Amini alipigwa na kukimbia! Tukaweka uongozi tunaoutaka mpaka leo na kesho!Unaweza ukanipa straight fact (sio porojo) kwamba kwa nini immediately after Kagera War uchumi wa TZ ulishuka mpaka negative 3% (rejea mahindi ya Yanga kutoka Marekani na mchele wa Thailand)
Unaweza kutaja sababu moja plain (usipige story) kwamba kwa nini Nyerere baada ya kuona vita inamshinda, aliamuru Migambo Wote wa mitaani wapelekwe frontline vitani kupigana vita. Wanajeshi walikua hawatoshi?
Kwa hiyo gazeti likiandikwa unaamini Tu! Afadhali ingekuwa kitabuNi kwa sababu alipofukuzwa Amin akawa kiongozi ni Yusuf Lule mwislamu lakini Nyerere kuona huyu siye anayemtaka akaleta mizengwe ya kumrudisha Mkatoliki mwenzake Obote ambaye waganda walikuwa hawamtaki.
Gazeti la Reporter la Kenya la tarehe 20/6/1963 lilitangaza katika ukurasa wake wa mbele: "KUIBADILI AFRIKA YA MASHARIKI KUWA KATIKA DINI YA ROMANI CATHOLIC". Ndani ya gazeti hilo ukurasa wa 18 liliwataja waliopewa dhamana ya kufanikisha jambo hilo kuwa ni: Uganda - Kiwanuka, Kenya - Mboya na Tanganyika Mheshimiwa Nyerere.
Sheikh wangu umevuliwa nguo.jisitiri.acha hili lipite. Tutafute hoja nyingine.hii jamaa ameshinda kwa busara na uelewa. Wala usihamaki na kughadhibika. Kichuguu anaonekana ni msomi.Kwa nini wewe ushindwe kumuandikia na kumpigia simu akupe hiyo context uliyoitaja ???au huna context unafoka na kumwaga povu tu ??
Sina hakika kama unaakili zilizo sawaVita hiyo tulipoteza sana kuliko faida tuliyopata Watanzania.
Hili lilikuwa kaburi refu la uchumi wetu hadi leo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kasome vizuri historia yako kama sivyo nwalimu wako alikudanganyaKiufupi hii vita ilikuwa ya kijinga na kiwendawazimu iliyotugharimu Hadi leo.nyerere alimchokiza idd amini Kwa lengo la kumrudisha Obote Kwa kuwa alipinduliwa na iddi amini baada ya uchumi kuwa hoi.Nyerere alimfadhili Obote na baadhi ya waganda wakafany uvamizi Uganda na kuishia kupigwa vibaya sana na majeshi ya amini(hapo ilikuwa ni kabla ya kutangazwa vita)Alipoona Hivyo iddi amini ndiyo akaamua na yeye kuiteka kagera na ndiyo ikawa mwanzo wa vita rasmi.kiufupi Nyerere alikuwa mchokozi na tungekuwa na mkuu wa majeshi mwenye kujitambua asingemkubalia Nyerere.
Hawa vijana sijui wamedanganywa na walimu wao wa history huko shuleni !? Maana kama kweli aliifatilia ile vita vizuri hawezi kusema haikuwa na ulazimaWatoto wa 2000 wanapojaribu kuzaliwa 1960
Mdogo wangu vita haikuwa ya ulazima wakati Nduli Iddi Amini Dada alivamia Mkoa wa Kagera kwa madai ya kwamba ile ni sehemu ya uganda lazima aichukue.
Kwa hiyo mwl. JKN angewaachia..!?
Tugawane za kwakoSina hakika kama unaakili zilizo sawa
Zangu zitakupasua ubongo maana ninyingi sana kwako hazitoshi hata nikikupa 0.0000125%Tugawane za kwako