Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Mkuu, kwani wewe ungekua Rais wa wakati huo wa TZ ungefanya maamuzi gani? Nchi yako imevamiwa ardhi ya kagera inatangazwa ni sehemu ya Uganda na mpaka mpya unatangazwa kinyume na sheria. Wewe ungefanyaje?
Kwanini in the first place ufuge majambazi wa jirani yako sebuleni kwako?

Kwanini usiwatimue (kina M7, Okello) na kuwaambia jamani nawafukuza ondokeni sitaki shari na majirani zangu
 
Hii ni mentality ya kutokujiamini tu, kudhani kuwa sisi ni inferior kwa kila kitu. Vile vile ni kutokuelewa historia halisi

Elewa kuwa jeshi la Uganda wakati huo lilikuwa chini ya Amini, siyo kuwa Jeshi lilikuwa limegawanyika. Chanzo kikubwa cha kuelekea Amin kumpindua Obote ni kwa vile alikuwa anasuka jeshi kuwa lake na kuwa ana-sideline wasiokuwa wafuasi wake kwa kutumia hela za serikali, na Obote alipomtaka aeleze matumizi ya hela za jeshi ndipo akaamua kumpindua. Ni kikundi kidogo kilichokuwa kimebaki upande wa Obote ambacho ndicho kilikimbilia Tanzania kikiongozwa na akina Oyite Ojok na Tito Okello ambacho kiliitegemea sana Tanzania kwa miaka yote minane ya utawala wa Amini; kilikuwa hakifiki hata batallion moja. Baada ya kuangushwa kwa Amini na jeshi lote la Uganda kuvunjwa na TPDF, ndipo UPDF ilipoanzishwa na kufundishwa na TPDF, unaweza kuona hata jina lenyewe. Mvutano wa madaraka uliotokea ndani ya Uganda baada ya Amini kuwa amsheaangushwa na jeshi letu kuwa limesharudi nyumbani ndio uliosababisha Museveni aanzishe jeshi lake la msituni NRA ikiwa ni mwaka 1983. Museveni mwenyewe alipandikizwa kutokea Tanzania; wengine ni kama Dani Wadada Nabudere ambaye alikuwa anafundisha UDSM kabla ya vita.

Hata kama unaidharau Tanzania, kubali kuwa TPDF ilikuwa jeshi imara sana wakati huo. Kumbuka lilikuwa limeshapitia mapigano mabalimbali kusini mwa Afrika kwa hivyo lilikuwa na experience kubwa sana kuliko jeshi lolote Afrika ya Mashariki.
Na Mseveni alikua Mwl chuo cha Ushirika Moshi

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
Hizi ni propaganda tu ili kufunika kombe.... Anyway wewe ni mzalendo.

Kama Mwl asingewaruhusu kina Okello, M7 kutumia ardhi ya Tz kuendesha uasi wa silaha dhidi ya Uganda, basi Iddi Amin asingepata sababu ya kuanzisha Vita na Tz.
Ukikumbuka ushiriki wa Tanzania kuzikomboa baadhi ya nchi ( Mozambique, Zimbabwe, Angola, Namibia na vyama vya ukombozi vya Africa kusini)
Nchi ya Malawi chini ya Banda Kamuzu iliandaliwa kuwa chokochoko maeneo ya kusini mwa Tanzania.
Kilichofuatia ni kumshawishi Amin aanze vurugu.
Kwa hiyo nchi ikawa ina ukosefu wa Amani kusini na Kaskazini.
Vita ya kagera ndivyo ilivyo anza.
 
Nilikuwa katika mazingira ya jeshi la akiba wakati huo, na siyo kweli kuwa Jeshi la Uganda lilikuwa liko vizuri sana kuliko la Tanzania. Wale askari wetu waliokufa wengi kwa kipindi kimoja ni wale waliotumwa na Brigadia Yousufu Himid ambaye wakati huo ndiye aliyekuwa Brigade Commander wa Brigedi ya Magharibi kabla ya kuondolewa (kwa kosa hilo) na nafasi yake kukaimiwa na Kanali Kotta - baba yake na Faraja Kotta.

Brigedia huyo aliituma battalion kadhaa zivuke mto kwa mitumbwi kuingia hilo enelo lililokuwa limetekwa baada ya daraja kuvunjwa. Kwa vile upande ule uliokuwa umetekwa ni high tactical ground ndiyo maana askari wa Tanzania waligundulika na kuuwawa kwa vile walikuwa wanajiandaa kuvuka na bunduki tu, bila ya kuwa na silaha kubwa.

Askari wetu wa kwanza kuingia Uganda kukomboa ile sehemu iliyokuwa imetekwa na kusaidia ujenzi wa daraja la muda walipitia Rwanda. Ni vivyo hivyo pia kwa kupitia Rwanda ilikuwa ni rahisi wao kuingia ndani zaidi ya Uganda kwa upande wa Magharibi, hivyo hata mashambulizi makubwa ya kuingia Kampala yalitokea huko Magharibi, na ni kweli askari wetu wengine walishafika mbali karibu na Sudan kabla ya kuja kushambulia Uganda.

Kikosi Kikikubwa cha Idi Amini ni kile kilichokuwa kinaitwa Simba Batallion kilichokuwa na makazi yake pale Masaka (siyo Mbarara) ambacho baadaye kilikuja kusaidiwa na askari wa Libya wakati wa yale mapambano ya Lukaya. Kikosi kile cha Simba Batallion kilizingirwa pia na majeshi ya Tanzania kutokea Magharibi kikiongozwa na Brigadier Imran Kombe na Major General Marwa, ndipo Amini alipotuma wale askari wa Libya waje kusaidia na kufanya mapambano ya Lukaya kuwa makali sana lakini mwishowe Simba Batallion na askari wa Libya wakasalimu Amri na kuiacha Baracks ya Masaka mikononi mwa Imran Kombe. Ukishaondoa hiyo Simba batallion na Askari wa Libya, sehemu kubwa ya jeshi la Amin lilikuwa ni "maharage ya Mbeya tu"

Rangi ya nyekundu ndiyo iliyokuwa ruti ya kwanza kuingilia Uganda, halafu ruti ya kijani ndiyo ilikuwa ruti ya pili baada eneo la kaskazini mwa mto Kagera kusafishwa na daraja la muda kujengwa
View attachment 1478112
Mojawapo ya upungufu mkubwa wa nchi yetu ni kutowaruhusu watu walioshuhudia matukio muhimu ya kihistoria kuandika vitabu. Watu wengi walioshuhudia matukio muhimu wamefariki bila kacha taarifa muhimu. PhD yangu ni ya mambo ya vita na nilishawwishika sana kuandika kuhusu vita ya Kagera (mtazamo wa Tanzania) lakini Mwalimu wangu akanionya kuwa ningepata shida kupata taarifa. Ombi langu kwako ni kuhakikisha unaandika kitabu, kinafungiwa sehemu na watoto wako wakichapishe baada ya kifo chako.
 
Kwanini in the first place ufuge majambazi wa jirani yako sebuleni kwako?

Kwanini usiwatimue (kina M7, Okello) na kuwaambia jamani nawafukuza ondokeni sitaki shari na majirani zangu
Haujanijibu swali Mkuu
 
Kwanini asingedeal na hao watu? Yeye akaishambulia TZ mkoa wa kagera na kuutawala kimabavu kwa muda na kusema ni sehemu ya uganda. Je ni nchi gani duniani ingekubali sehemu ya ardhi yake kutekwa kimabavu?
Si alideal nao kwa kutuma jeshi lake nchini. Alifanya retaliation ya aggression tuliyokuwa nayo. Na retaliation mara nyingi haiwi na sababu halisi.

UN General Assembly Resolution 2624 ya mwaka 1970 inazuia kuwapa silaha au kuwasadia waasi wa nchi nyingine, hata magaidi. Tanzania tulikuwa na kiherehere na kisebusebu bila faida, ni upuuzi kuingilia maswala ya wenzako hasa kama uchumi wako ni wa kutembeza mabakuli. Hata Marekani iliingilia suala la Afghanistan na imetumia gharama kubwa sana.

Mwanzo tu tulikuwa wajinga, eti Obote amekuja kupewa hifadhi Tanzania nchi jirani na kwake. Hiyo diplomasia ya wapi? Zine Al-Abidine ben Ali wa Tunisia alikimbilia Saudi Arabia wala hakwenda Libya au Misri kwa majirani, hiyo ndio political asylum ya top leader inatakiwa kuwa. Leo hii Tanzania tumpe hifadhi mkuu wa inteligence service ya Rwanda unadhani inaleta picha gani.
 
Si alideal nao kwa kutuma jeshi lake nchini. Alifanya retaliation ya aggression tuliyokuwa nayo. Na retaliation mara nyingi haiwi na sababu halisi.

UN General Assembly Resolution 2624 ya mwaka 1970 inazuia kuwapa silaha au kuwasadia waasi wa nchi nyingine, hata magaidi. Tanzania tulikuwa na kiherehere na kisebusebu bila faida, ni upuuzi kuingilia maswala ya wenzako hasa kama uchumi wako ni wa kutembeza mabakuli. Hata Marekani iliingilia suala la Afghanistan na imetumia gharama kubwa sana.

Mwanzo tu tulikuwa wajinga, eti Obote amekuja kupewa hifadhi Tanzania nchi jirani na kwake. Hiyo diplomasia ya wapi? Zine Al-Abidine ben Ali wa Tunisia alikimbilia Saudi Arabia wala hakwenda Libya au Misri kwa majirani, hiyo ndio political asylum ya top leader inatakiwa kuwa. Leo hii Tanzania tumpe hifadhi mkuu wa inteligence service ya Rwanda unadhani inaleta picha gani.
Mkuu, Jeshi la Uganda lilivuka mpaka wa Tanzania na kushambulia kagera, kutangaza mpaka mpya kinyume na sheria na kutangaza kuwa sehemu hiyo ya kagera ni ardhi ya Uganda. Je wewe kama ungekua Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania wa wakati huo ungefanya maamuzi gani?
 
Mkuu, Jeshi la Uganda lilivuka mpaka wa Tanzania na kushambulia kagera, kutangaza mpaka mpya kinyume na sheria na kutangaza kuwa sehemu hiyo ya kagera ni ardhi ya Uganda. Je wewe kama ungekua Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania wa wakati huo ungefanya maamuzi gani?
Mimi kama amiri jeshi ningeshambulia Uganda na kuirudisha kwao kisha na kufanya assesment kama Uganda inaweza leta tafrani tena, kama ndio ningeingia mpaka kumtoa Amini na kama sio ningeishia kuwarudisha kwao.

Je kama wewe ni mwanausalama wa Uganda na jeshi la Tanzania linawapa silaha, makazi na mafunzo waasi wanaokuja kumshambulia rais wako ungefanyaje? Unajua mediation iliyofanywa na Siad Bare Rais wa Somalia na katibu mkuu wa UN, Ngo Ekangaki ilivyotukuta na hatia. Upuuzi na kiherehere tulikuwa nao
 
Mimi kama amiri jeshi ningeshambulia Uganda na kuirudisha kwao kisha na kufanya assesment kama Uganda inaweza leta tafrani tena, kama ndio ningeingia mpaka kumtoa Amini na kama sio ningeishia kuwarudisha kwao.
Sasa hii ndio Kitu kilochofanyika majeshi ya Uganda yaliondoshwa Kagera, ikafanyika assesment na kuona kuna ulazima wa kuendelea kupigana vita na kumtoa kabisa Amini.


Je kama wewe ni mwanausalama wa Uganda na jeshi la Tanzania linawapa silaha, makazi na mafunzo waasi wanaokuja kumshambulia rais wako ungefanyaje? Unajua mediation iliyofanywa na Siad Bare Rais wa Somalia na katibu mkuu wa UN, Ngo Ekangaki ilivyotukuta na hatia. Upuuzi na kiherehere tulikuwa nao
Moja, Kumbuka wale hawakua waasi kama unavyosema bali ni jeshi la Uganda lililokua na utii kwa Rais aliyepinduliwa na Amini. Ukisema wale walikua waasi nakushangaa sana. Wale walikua ni wanajeshi kamili waliokataa kuwa vibaraka.

Pili, una uthibitisho gani kwamba Jeshi la TZ liliwapa silaha?

Jeshi la Tanzania linawezaje kuwapa mafunzo Jeshi ambalo ni kamili la Uganda? Au unafikiri hao walikua mgambo?

Kuhusu makazi hao wote walikua wamepatiwa hifadhi ya kisiasa jambo ambalo linaruhusiwa kabisa. Hao walikua ukimbizini Tanzania.
 
Sasa hii ndio Kitu kilochofanyika majeshi ya Uganda yaliondoshwa Kagera, ikafanyika assesment na kuona kuna ulazima wa kuendelea kupigana vita na kumtoa kabisa Amini.



Moja, Kumbuka wale hawakua waasi kama unavyosema bali ni jeshi la Uganda lililokua na utii kwa Rais aliyepinduliwa na Amini. Ukisema wale walikua waasi nakushangaa sana. Wale walikua ni wanajeshi kamili waliokataa kuwa vibaraka.

Pili, una uthibitisho gani kwamba Jeshi la TZ liliwapa silaha?

Jeshi la Tanzania linawezaje kuwapa mafunzo Jeshi ambalo ni kamili la Uganda? Au unafikiri hao walikua mgambo?

Kuhusu makazi hao wote walikua wamepatiwa hifadhi ya kisiasa jambo ambalo linaruhusiwa kabisa. Hao walikua ukimbizini Tanzania.
Sasa unabishana na Yoweri Museveni aliyesema mwenyewe kwamba walipewa silaha na mafunzo?

Na hicho kiherehere cha kusema walikuwa jeshi halali nani kakupa. Nchi yako haina uwezo wa kujenga vyoo, mnakunya kwa msaada wa wazungu alafu bado unashobokea masuala ya nje. Yaani mtu mkeo na wanao wanakushinda kutunza na kuongoza, tena unaleta na wa jirani yako
 
Sasa unabishana na Yoweri Museveni aliyesema mwenyewe kwamba walipewa silaha na mafunzo?

Na hicho kiherehere cha kusema walikuwa jeshi halali nani kakupa. Nchi yako haina uwezo wa kujenga vyoo, mnakunya kwa msaada wa wazungu alafu bado unashobokea masuala ya nje. Yaani mtu mkeo na wanao wanakushinda kutunza na kuongoza, tena unaleta na wa jirani yako
Walipewa silaha wakati gani? Wakati wa vita vilipoanza rasmi ni kweli baadhi ya wanajeshi wa Uganda waliokua watiifu kwa Obote walijoin ili nao wapambane kumtoa Amini.

Kuhusu mafunzo ni kweli baadhi ya makamanda wengi wamewahi kupata mafunzo hapa TZ, kama Museven n.k kabla hata ya vita ya kagera.

Hao wakimbizi wa vita kutoka uganda baada ya mapinduzi ya Amin unafikiri walipenda wawe hivyo?

Ukweli utabaki ya kwamba ile vita ilikua ni lazima Tanzania ipigane ili kulinda heshima na ardhi ya nchi yetu, kutokana na uvamizi uliofanywa na majeshi ya Amin mkoani kagera.
 
Walipotea wapi; si ajabu unasikia hadithi tu; ni kweli tulipoteza wanajeshi karibu 500 ( siyo 2000 ingawa sina namba kamili) ambayo ni karibu batallion moja, na nimekuambia kuwa katika hatua za kwanza za vita kuna karibu Batallion nzima iliyopotea kwa sababu ya uamuzi mbovu wa kamanda mmoja.

Vile vile vita ya Lukaya iliua waganda na walibya wengi sana lakini pia watanzania walikufa. Mimi nilikuwa karibu sana na taarifa za mapambano yale kuanzia mwezi Octoba mwaka 1978 (siyo 1979) kabla hata Rais hajatangaza vita yenyewe kwa vile nilikuwa kwenye Brigedi ya Magharibi ambayo ndiyo iliingia vitani kwanza.

Vita iliendelea kwa miezi saba katika mazingira magumu kama niliyosema hapo, hivyo ni kweli watu walikufa. Huwezi kupigana vita ya ardhini bila askari wako kufa. Jeshi la Uganda halikuasi bali lilielemewa nguvu na jeshi la Tanzania licha ya kuwa walikuwa wanasaidiwa na askari wengi sana kutoka Libya.

Unaposema kuwa watu wetu walielemewa sana ila baada ya hapo jeshi la Uganda likaasi ndipo tukapata unafuu- ni wazi hujui vita nini- ile siyo ngoma ya mdundiko ndugu yangu, ni kazi ya kurushiana risasi za moto, sema pia ni askari wangapi wa Uganda waliokufa kama hutapatwa na ugonjwa wa moyo iwapo unaliangalia jeshi la Tanzania wakati huo katika negative lens;

Jeshi la Uganda lilikuwa kubwa sana, Amini alikuwa anawekeza sana katika jeshi kuliko sehemu nyingine yoyote, ila sasa JWTZ ilikuwa inawafuta kama sisimizi ndipo wakafikia kukata tamaa ya kuendelea na vita ile.
Shusha madini mkuu
 
Walipewa silaha wakati gani? Wakati wa vita vilipoanza rasmi ni kweli baadhi ya wanajeshi wa Uganda waliokua watiifu kwa Obote walijoin ili nao wapambane kumtoa Amini.

Kuhusu mafunzo ni kweli baadhi ya makamanda wengi wamewahi kupata mafunzo hapa TZ, kama Museven n.k kabla hata ya vita ya kagera.

Hao wakimbizi wa vita kutoka uganda baada ya mapinduzi ya Amin unafikiri walipenda wawe hivyo?

Ukweli utabaki ya kwamba ile vita ilikua ni lazima Tanzania ipigane ili kulinda heshima na ardhi ya nchi yetu, kutokana na uvamizi uliofanywa na majeshi ya Amin mkoani kagera.
Tatizo halikuanza kwenye ile vita hapa tunatafuta justification for war. Huwezi mchukua mtu aliyehasi au aliyeondolewa pale Rwanda au Uganda leo ukampa hifadhi Tanzania alafu ukapanga watu wake wakamshambulie Rais wa nchi yake wakati huo no matter yuko kikatiba au vinginevyo.

Unahisi walioasi Rwanda wakaenda South Africa ni wapumbavu, au unahisi Wakenya wenye makosa ya uhaini waliorudishwa kwao tulikosea? Hakuna nchi inafanya upumbavu kama huo, sisi eti kisa Nyerere na Obote walikuwa marafiki
 
Mkuu, unafahamu vitu hivi?

1. Hifadhi ya kisiasa
Sasa hao kina Okello, M7 n.k walipatiwa hifadhi ya kisiasa na inaruhusiwa kabisa. So kwa TZ kuwapa hifadhi hao viongozi lilikua ni jambo chanya tu.

2. Ukivusha majeshi ya taifa lako yakaingia kwenye nchi nyingine kushambulia, tayari unakua umefanya uvamizi dhidi ya nchi hiyo. Majeshi ya uganda yalivuka mpaka yakaingia Tanzania na kushambulia Kagera. Ulitegemea Jeshi letu litulie?

Sasa weka ushabiki pembeni vaa viatu vya Hayati Baba wa Taifa, ambae alikua ni Amiri Jeshi Mkuu wa wakati huo. Je wewe ndio ungekua Rais wa TZ wakati huo nchi imeshambuliwa Kivita, ungefanya nini? Kama Amiri Jeshi Mkuu.
Mpe mfano mdogo kwenye familia yake,mwanaume mmoja wa kawaida anaingia ndani kwako anampiga mke wake na watoto wake ,angefanyaje
 
Tatizo halikuanza kwenye ile vita hapa tunatafuta justification for war. Huwezi mchukua mtu aliyehasi au aliyeondolewa pale Rwanda au Uganda leo ukampa hifadhi Tanzania alafu ukapanga watu wake wakamshambulie Rais wa nchi yake wakati huo no matter yuko kikatiba au vinginevyo
Mkuu, nakukumbusha tena wale hawakuhasi bali walipinduliwa na kukimbilia ukimbizini sehemu mbalimbali ikiwemo TZ, na si kosa nchi yoyote duniani kutoa hifadhi ya kisiasa au ya ukimbizi. Kama una ushahidi kwamba wale wanajeshi watiifu wa Uganda kwa rais Obote wakati huo walipangwa ili wakamshambulie Amini uweke huo ushahidi, vinginevyo itakua ni maneno ya propaganda tu.



Unahisi walioasi Rwanda wakaenda South Africa ni wapumbavu, au unahisi Wakenya wenye makosa ya uhaini waliorudishwa kwao tulikosea? Hakuna nchi inafanya upumbavu kama huo, sisi eti kisa Nyerere na Obote walikuwa marafiki
Nchi yoyote duniani inaruhusiwa kisheria kutoa hifadhi ya kisiasa au ukimbizi kwa wahanga wowote. Pia nchi inaweza kuamua kuwarudisha au kuendelea kuwapa hifadhi wahanga kutokana na mazingira itakayoona inafaa. Sasa nakuuliza swali Je kama Amini asingevusha Jeshi lake na kuvamia Tanzania na kuteka sehemu ya ardhi ya Kagera na kusema ni sehemu ya Uganda, unafikiri (Kagera War) ingetokea?
 
Back
Top Bottom