Vita vya Kagera: Historia yangu - Sehemu ya kwanza


Matusi hayafai mwezi mtukufu!

Jina zuri!
Tabia sasa!
Lahaula!
 
Kwa kweli Story za hii vita Vya Kagera huwa zinanisisimua sana tu, Nimesoma kile kitabu cha War In Uganda cha Martha Honey na Tony Avirgan yaani utapenda km unaangalia movie vile. Kuna picha mle za akina Ben Msuya, Mti Mkavu, Oyite Ojok huyu alikuwa kamanda ktk jeshi la ukombozi wa Uganda waliopigana bega kwa bega na majeshi yetu. Nakumbuka vita hivi vinapiganwa mie nilikuwa km na 4yrs tulikuwa Songea, kule kuna kambi kubwa za jeshi basi ikasemekana ndege za Nduli zaweza fika na kupiga kule, mji mzima kila family tukachimba mahandaki ya kujificha, mbaya zaidi mzee wangu alikuwa Polisi upande wa upelelezi, dah nilikuwa naomba mungu tusiambiwe mzee kapelekwa mstari wa mbele! ndege zikipita angani watu wanakimbia kujificha. nakumbuka baada ya vita kwisha askari wengi walirudi Songea mjini basi walikuwa km wamechanganyiiwa hivi na watu waliaswa kutowachokoza. siku moja niko na bro wangu tunakwenda town si nikagongana na soldier akasimama akaniambi mtoto Kaa chonjo kule saa mbaya i nearly did in my pant! hahahaha. Mkuu simulizi zako ziendelee huwa napensa sana jinsi mashujaa wetu walivyomtosa Nduli na kumchakaza vibaya!
 
Aksante sana RUVUMAN umeongea maneno mazuri sana na ushauri mzuri kwangu nilikuwa najibu tu swali aliloniuliza kuwa ni kitu gani nakikumbuka sana katika Vta hiyo,Najua sana vitani kuna mambo mengine yanatendeka huko si mazuri kwa jamii lakini nitajitahidi sana na staadhiri USALAMA WA TAIFA nitakuwa naongelea tu hali halisi iliyotokea nashukuru kwa maoni yako.
 
Mkuu Echolima,

Nashukuru kwa majibu yako murua, nadhani imefika wakati kuandika kitabu, nadhani kitafanya vizuri.
 
Last edited by a moderator:
Wakati naleta uzi huu nilikuwa naelezea tu kumbukumbu zangu baada ya kuangalia TBC Wakati wanaonyesha siku ya mashujaa lakini kwa kuwa hapa ni kwa GT Mmenipandikizia wazo hili zuri la kutunga kitabu nawashukuru sana wote walionitia moyo katika sehemu hii ya kwanza,Naongea na jamaa ili lengo hilo litimie la kutengeneza kitabu Nimeona kweli kitapendeza sana lakini shukrani nyingi zitakuwa kwenu GT.
Mkuu Echolima,

Nashukuru kwa majibu yako murua, nadhani imefika wakati kuandika kitabu, nadhani kitafanya vizuri.
 
Last edited by a moderator:
Echolima,

..umesema ulikwenda vitani ukitokea chuo cha maafisa wa kijeshi monduli.unaweza kutupa historia fupi ya chuo hiki? kilianzishwa mwaka gani? wakuu waliopata kukiongoza etc etc. je, ni kweli kilianzishwa kwa msaada wa wachina??
 
Last edited by a moderator:
 
Mkuu Echolima,

Ni kweli unachosema hujue Tanzania hakuna vitabu vya kumbukumbuku vya historia yetu, mfano ukitaka kusoma historia ya Tanganyika mpaka utafute vitabu vya wazungu kina Judith Listowel, John Iliffe na wengine.

Angalia watu kama kina Shigongo leo matajiri kwa kuandika vitabu vya udaku tu.

Kwa nini wewe usipate utajiri kupitia kitabu chako ambacho kina facts tupu, takupa mfano mmoja.

Wanajeshi wa Marekani wale wote waliopigana vita vya Vietnam wote waliandika vitabu mpaka wale wapishi, achilia mbali hawa waliopigana vita Iraq, Libya.

Kuna vitabu maarufu vya vita vya Vietnam, kama Things The Carried, The Bettle That Changed, A Rumor of War, The Quiet American, vipo vingi sana na vinaendelea kusomwa duniani kote.

Kuna vizazi vipya havijuhi chochote kuhusu vita vya Kagera, hata hao waliokuwepo wakati wa vita bado walikuwa wanaitaji kujua mengi.

Anzisha Project hii mapema kama una kumbukumbu za wanajenshi wenzako jipange kaka, kitabu chako kikiwa na matoleo mawili moja la Kiingereza lingine la Kiswahili mbona utapumzika vizuri.



CC; JokaKuu,
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hebu hii history andika kitabu,najua kweli sio mwandishi omba msaada kwa waandishi wakusaidie,nadhani watu kama nyinyi ni watu muhimu katika history ya nchi yetu,
Watoto wetu leo hata mashuleni sidhani kama wanafundishwa habari za vita ya kagera wala kujua tu majina ya mashujaa wetu,
Khofu yangu miaka 20 ijayo nchi itakuwa imepoteza history yake yote,
 
Kuna mtu ameni-PM na kuniuliza vyeo alivyokuwa anaitwa AMIN kipindi hicho kwa faida ya wengine alikuwa anaitwa LIFE PRESDENT,FIELD MARSHAL,DR.IDD AMIN DADA VC,MC,DSO and CBE.Vyombo vyote vya habari nchini Uganda walipokuwa wanatangaza habari za Amin Lazima wataje vyeo hivyo vyote.labda tu nielezee kirefu cha vifupisha vya vyeo vyake hivyo.VC-Victoria Cross,MC-Military cross.DSO-Distinguished Service Order.CBE-Coqueror Of the British Empire.
 

sembuse dogo kagame mdeki barabara na kujiona kashakuwa superpower!
 
Mkuu wa Kaya alikuwa amemaliza UDSM miaka minne kabla ya vita, na katika viongozi maarufu wanaoonekana karibu na high table wakati mwalimu Nyerere akihutubia wananchi kuhusu nia, sababu na uwezo wa kumpiga Amin, ni JK na Mkapa tu. Psychologically walionyesha special type ya concentration, excitement na labda ukaribu na Mwalimu. Wote wanaotangaza nia ya kugombea sasa hivi wenye umri unaofanana na akina JK au Mkapa hawaonekani. Tafakari...........
 
Mkuu Echolima

mbali na majeshi ya miguu mlitumia pia majeshi ya majini katika vita hii??

Vipi kuhusu majeshi ya anga nayo yalitumika sana au hatukua wazuri sana upande wa anga??
 
Last edited by a moderator:

Kwa hiyo unataka kusema nini??

Ili iweje??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…