Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

william,
jibu rahisi ni kwamba hatukuwa na sababu ya kumhifadhi obote. Hatukuwa na sababu ya kuwa na uhusiano hasimu na iddi amin. Iddi amin was the best thing that ever happened to africa and uganda. We should have loved him and not make war on him. Simply nyerere was mad to fight with amin. Tulifanya makosa makubwa sana. Nadhani hapo utaridhika. Anzisha sasa topic nyingine tumkosoe na kumdadavua nyerere. Ngoja nikusaidie; nyerere and african liberation. Big mistake. Nyerere and pan africanism: Ndoto ya mchana. Nyerere and the development of man: It will never happen. Niendelee?

mbona tuliilaani israel kuwa imemsjambulia nchi huru ya africa alipogomboa mateka wake entebe huku iddi amin akiwa adui mkubwa wetu?
 
Watanzania hakika tu watu wa ajabu sana. Kuna baadhi yetu ambao kwa bahati mbaya sana hawataki kabisa kusikia vipenzi wao wakisemwa kwa mabaya hata kama kweli mabaya hayo waliyafanya. Kama walivyo mashabiki wa CHADEMA ambao hawataki kabisa kusikia mtu kama Dr. Slaa akisemwa kwa mabaya, kuna wengine ambao hawataki hata kidogo kusikia baya likisemwa dhidi ya Nyerere. Hawa wote, ukisema baya kuhusu vipenzi vyao basi watakuja juu na kukupa majibu ya kifedhuli na kihayawani….lakini wote hawa bado wanajiita ni Greatest Thinkers!!

Sasa nirudi kwenye mada.

Ukweli bado utabaki pale pale kwamba kwa pale ilipofikia, Tanzania haikuwa na budi bali kuingia vitani dhidi ya Amin. Hata hivyo, bado ukweli unabaki paleplae kwamba point ambayo ilikuwa lazima tuingie vitani ilisababishwa na Nyerere mwenyewe.

Baada ya Amin kumpindua Obotte, Milton Obotte alipewa hifadhi na Nyerere. Kimsingi, hapakuwa na ubaya wowote kwa Nyerere kumpa Obote hifadhi hapa Tanzania. Hadi Nyerere anampa hifadhi Obote pamoja na maelfu ya wakimbizi bado Amin alikuwa hajaonesha uchokozi wa wazi dhidi ya Tanzania. Tatizo kuu lilianza pale Wakimbizi wa Uganda waliopo Tanzania walipovuka mpaka wa Tanzania na kuingia Uganga na kufanya jaribio la kumpindua Amin. Hata hivyo, jaribio hilo lilishindwa na kasha kikosi hicho kikarudi tena Tanzania.

Haya sasa, wale wanaotaka kujitia upofu kwa makusudi; watuambie ni kiongozi gani duniani angevumilia kitendo ambacho kilifanywa na Tanzania kwa kuacha Waganda waliopo nchini wavuke mpaka na kuingia Uganda kwenda kufanya jaribio la mapinduzi kasha kurudi tena nchini. Je, hapo Tanzania ilikuwa ni hifadhi ya wakimbizi au kituo cha kijeshi kwa wale waliokuwa na nia ya kumtoa Amin madarakani?! Kimsingi, hakuna jaribio la mapinduzi ambalo linaweza kufanyika pasipo na maandalizi ya kijeshi. Hata mapinduzi madogo kama yale ya Zanzibar 1964 palikuwa na mafunzo pamoja na maandalizi ya kijeshi kabla ya mapinduzi hayo kufanyika. Je, hawa wakimbizi wa Uganda ambao walitoka Tanzania na kuingia Uganda kwenda kumpindua Amin walichukulia wapi maandalizi na mafunzo ya mapinduzi amabayo walienda kuyafanya?! Je, mnataka kusema kwamba serikali ya Tanzania hawakufahamu dhamira ya Waganda ambao walikuwepo nchini?! Hivi kweli Intelligence system ya Nyerere ambahyo ilikuwa very competent haikufahamu kwamba wakimabizi wa Uganda walikuwa na nia ya kuvuka mpaka na kuingia Uganda kufanya mapinduzi?! Kwa intelligence system ya sasa inawezekana lakini sio ile ya Nyerere!!

Hivyo basi, ingawaje Amin alivamia Tanzania na kuikalia sehemu ya Mkoa wa Kagera na kudai ni ya Uganda lakini source ya chokochoko ni Nyerere mwenyewe ambae hakufurahishwa kitendo cha Amin kumpindua Obote; swahiba wa Nyerere! Aidha, ikumbukwe kwamba, hata OAU haikuiunga mkono Tanzania kwa kile kilichoonekana Tanzania kuingilia masuala ya ndani ya Uganda!! Na kwa kunoesha kwamba hawakupendezwa na suala la Tanzania kuingilia masuala ya ndani Uganda, OAU ilikataa ombi la Nyerere alilotaka kwamba OAU imlaani Amin!! Na kwa kumuumbua zaidi, Mkutano wa OAU ulifanyika Uganda ambao Nyerere alisusa kwenda kwavile tu OAU haikukubaliana na takwa lake la kuitaka jumuiya hiyo imlaani Amin.

Swali lingine linafuata hapo! Hivi kweli OAU ilikuwa na mapenzi zaidi kwa Amin kuliko Nyerere ambae alijitolea kwa ari na mali katika ukombozi wa Afrika; Kusini mwa Jangwa la Sahara?! Bila shaka, jibu ni HAPANA….sina shaka yoyote kwamba OAU ilikuwa inampenda zaidi NYerere(Tanzania) kuliko Amini lakini bila shaka walisukumwa na methali ya kiswahili isemayo “Mnyonge Mnyongeni, Haki Yake Mpeni!” Kwamba, hata kama ni kwali Amin alikuwa ni mshenzi dhidi ya Tanzania na watu wake lakini ushenz wake dhidi ya Tanzania ulisababishwa na sisi wenyewe.
Kitu kimoja ambacho alifudhu Nyerere kwenye vita hivyo ni PROPAGANDA! Alipiga propaganda za kutosha hadi akafanikiwa na kuonesha kwamba tatizo ni Amin….! Propaganda hizi zilienezwa kwa nji mbaliambali ikwemo nyimbo, machapicho na kwa njia ya muziki. Watanzania wote wakaamini kwamba Amin ni tatizo ingawaje kiini cha tatizo ulikuwa ni Nyerere mwenyewe!!

Kwa kumalizia; kama alivyosema William; kwavile Amin aliivamia Tanzania kulikuwa na ulazima gani wa kuhakikisha tunamfutilia mbali?! Jibu ni kwamba, hatukuwa na sababu hiyo! Ilitosha kabisa kumwondoa kwenye mipaka ya Tanzania na kasha kuimarisha mipaka yaetu!! Lakini kwavile lengo la Nyerere alikuwa tu kuilinda mipaka ya Tanzania, basi alihakikisha anaingia ndani kabisa ya Uganda na kumwondoa Amin madarakani!!




- Kwenye hii thread ninakukubali kwamba wewe ni Great Thinker, saafi sana nice and clear bila matusi wala jazba, ndio njia pekee ya kutoa elimu kwa sisi tusioelewa na tunaouliza, kuliko wanaojifanya wanajua kumbe maneno yao wenyewe na matatizo ya taifa yanawashitaki kwamba hawajui wanallolisema! ha! ha! ha!

William.
 
- Kwenye hii thread ninakukubali kwamba wewe ni Great Thinker, saafi sana nice and clear bila matusi wala jazba, ndio njia pekee ya kutoa elimu kwa sisi tusioelewa na tunaouliza, kuliko wanaojifanya wanajua kumbe maneno yao wenyewe na matatizo ya taifa yanawashitaki kwamba hawajui wanallolisema! ha! ha! ha!

William.

William
Amin alishageuka kansa kwa watanzania ilikuwa ni lazima aondoke; kama angekuwa na vita vya maneno tu vita visingetokea; kitendo chake cha kuvamia na kuuwa watanzania wasio na hatia hicho kilikuwa si cha kufumbia macho; Mwl. Nyerere hakuwa Raisi legelege; na lazima ukumbuke Amin alijivunia wadhamini wake Ghadaf wa Libya na alishatoa kauli ataichukua Mwanza; hizo ni kauli zake, kama ambavyo haikuwa kosa kwa Dunia kumuondoa Hitler basi pia halikuwa kosa kwa wanajeshi mahiri wa Tanzania chini ya Jemedari wao Nyerere kumuondoa Idd Amin; William hizi propaganda za kumpaka Mwl. Nyerere matope hazitafua dafu; wapo wanasiasa na majemedari wetu ambao walishiriki kikamilifu kwenye vita vile waulize watakueleza visa vya Idd Amin.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Sheria za vita haziruhusu tu kumuondoa adui kwenye ardhi yako bali kuweza pia kuondoa tishio la adui huyo na kumlazimisha kusalimu amri. Tanzania isingeweza kumuondoa Amin hadi mpakani na kuendelea kumuacha awe tishio. Katika vita - na hapa watu lazima watambue ni vita - anayeshinda ndiye anaamua terms of surrender. Tanzania haimkurudisha Obote; Obote alikuwa ni Rais wa Wauganda aliyepinduliwa na Idi Amin (kama watu wamesahau) na Obote alirudishwa kwenye nafasi yake (status quo). Sasa kama alipinduliwa tena hilo ni jingine lakini kama aliyempindua angekuwa tishio kwa Tanzania tungewajibika pia kumkung'uta.

- I mean kupiga taifa lingine na kuingilia mpaka ndani ya mipaka yake ni makosa ksiheria za kimataifa, na hadithi ya Marehemu Binaisa, kuhusu nia na madhumuni ya Mwalimu na ile vita ni tofauti kabisa na hii habari yako, betwen Lule na Binaisa, wote waliambiwa wazi kwamba nia ni kumrudisha Obote, ndio maana na wao wakamuondoa very fast kumhakikishia Mwalimu kwamba hawakubali pilcies zake kwa nchi yao.

- Kumpiga Amin mpaka ndani ya nchi yake kumetugharimu na mpaka leo bado tunalipia, ni wajibu wetu wananchi wenye uwezo wa kufikiri kuuliza kuhusu hizi failed policies!, ambazo zingine physically zinatuumiza mpaka leo, ambapo wahusika hawapo!

William.
 
mkuu unajua kati ya uganda na tanzania ni nani alikuwa mchokozi??

Je? Wajua ni kwanin? Uganda waliitandika tanzania na mpaka kuvuka mipaka??

In short.Nyerere alikuwa swaiba ake sana obote na pind idd amin alipo mpindua abote nyerere hakufurahia kabisa.Hivyo tanzania ilimuhifanyi obote na mkakati kabambe wa kumng'oa idd amin madarakan uliundwa kuna vijana waganda na watanzania walipewa mafunzo na kuanza kumletea choko choko idd amin kwa kuingia uganda na kufanya fujo walivyo fukuzwa walikimbilia tanzania choko choko zikazid wakaenda tena kufanya fujo na wakafanya uharibifu mkubwa sana uganda idd amin akakasirika akawatandika na kuwafukuza mpaka tanzania na kuingia kilomita kazaa tanzania.
Hapo ndipo nyerere alipokuwa anapataka haraka haraka akautangazia umma kwamba idd amin anataka kuitwa baadhi ya ardhi ya tz na kutangaza vita.
Je? Hapo mwenye kosa nani?? Na je? Ni nani hapo ni mchokozi wa mwenzake?

Ndio mana hata kamanda gadafi alimuunga mkono idd amin na kumsaidia kwa sababu uhuni wote alikuwa anaufahamu.

Idd Amin aliwatendea waganda mambo mengi ya kiuonevu na si waganda pekee bali hata wageni kama waAsia n.k na ndiyo maana tulipata support kubwa uganda. Amin alitangaza ardhi ya tanzania kuwa sehemu ya uganda na kuweka bendera ya uganda. Kitendo cha Gadaf kumsaidia Idd Amin kilikuwa na malengo ya kuendeleza udikteta barani Afrika.
 
William
Amin alishageuka kansa kwa watanzania ilikuwa ni lazima aondoke; kama angekuwa na vita vya maneno tu vita visingetokea; kitendo chake cha kuvamia na kuuwa watanzania wasio na hatia hicho kilikuwa si cha kufumbia macho; Mwl. Nyerere hakuwa Raisi legelege; na lazima ukumbuke Amin alijivunia wadhamini wake Ghadaf wa Libya na alishatoa kauli ataichukua Mwanza; hizo ni kauli zake, kama ambavyo haikuwa kosa kwa Dunia kumuondoa Hitler basi pia halikuwa kosa kwa wanajeshi mahiri wa Tanzania chini ya Jemedari wao Nyerere kumuondoa Idd Amin; William hizi propaganda za kumpaka Mwl. Nyerere matope hazitafua dafu; wapo wanasiasa na majemedari wetu ambao walishiriki kikamilifu kwenye vita vile waulize watakueleza visa vya Idd Amin.

Chama
Gongo la Mboto DSM

- Mkuu ulianza vizuri lakini mpaka hapo mwishoni ndio ukaanza kuonyesha makucha yako, naomba nikwambie hivi, mimi ninapokuwa na swali la msingi kwa taifa langu ninauliza bila kujali nani yupo upande wa pili, ninasikia vilio kila mahali na hii thread lakini bado inaendelea tu, sasa mntaka nini wote humu tuwe mabendera wa kufuata upepo wenu tu?

- Propaganda? wananchi wakiulzia wamefikishwaje hapa wewe unaita ni propaganda? Yaani mna hasira kweli mkiulizwa maswali ya kweli na ya muhimu kwa taifa, badala ya kutumia nafasi kuelimisha wanaouliza ni kwa sababu mnajua kwenye nyoyo zenu kwamba kuna makosa yalifanyika, lakini kwa vile mlishaamua kwamba makosa ni ya sasa tu, baaasi kila anayeuliza either sio mzima, au ana agenda, au propaganda, ila mkuliza nyinyi kuhusu serikali ya sasa basi mna hoja nzito sana mna akili sana, I mean tupo tulipo sasa kutokana na tulikotoka!

- JF sio chombo cha kuongelea mazuri isipokuwa ni chombo cha kukosoa ili kusaidia kila anayekosolewa, sasa hizi elimu zenu mlizofundishwa kukosoa tu bila kukosolewa ni elimu gani hizo? Kama hoja ni za propaganda na hazina mashiko kwa nini zinafilia kurasa zote hizi? Na kwa nini zinawavuta sana maana mimi thread ambazo naona hazina mashiko huwezi kuniona huko, sasa nyie mnaolalama kila wakati na bado mnazidi kuja kutoa maoni ya vitisho, ni nini hasa kinawasumbua?

- Mnaonekana mmezoea kuiskia nyimbo za upande mmoja tu, please tuacheni watu tukate ishus hapa, swali lipo very clear kwamba kulikuwa na ulazima gani wa kuingia mpaka ndani ya nchi na kuliacha taifa likiwa na madeni yasiyolipika? Kama ni swali la propaganda then kwa nini unakuja kujibu propaganda great thinker?

William.

William.
 
- I mean kupiga taifa lingine na kuingilia mpaka ndani ya mipaka yake ni makosa ksiheria za kimataifa, na hadithi ya Marehemu Binaisa, kuhusu nia na madhumuni ya Mwalimu na ile vita ni tofauti kabisa na hii habari yako, betwen Lule na Binaisa, wote waliambiwa wazi kwamba nia ni kumrudisha Obote, ndio maana na wao wakamuondoa very fast kumhakikishia Mwalimu kwamba hawakubali pilcies zake kwa nchi yao.

- Kumpiga Amin mpaka ndani ya nchi yake kumetugharimu na mpaka leo bado tunalipia, ni wajibu wetu wananchi wenye uwezo wa kufikiri kuuliza kuhusu hizi failed policies!, ambazo zingine physically zinatuumiza mpaka leo, ambapo wahusika hawapo!

William.

William
Kinachotugharimu leo hii si gharama ya vita vya Uganda ni ufisadi wa viongozi wetu msikwepe ukweli; silaha nyingi zilizotumika kwenye vita vilikuwa ni mkopo kutoka Russia na madeni hayo yalishasamehewa; kama unataka kujua ukweli tafuta gharama halisi ya vita na gharama ya ufisadi utaona ukweli wa maneno; gharama za ufisadi ni kubwa zaidi ya mara 10 ya vita vya Uganda.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
dah! Kupitia huu Uzi nimejifunza mengi saaaana! Sasa naanza kumwamini mwalimu wangu aw History A level mwaka 2000-2002 Ambaye kila siku akiingia class alikuwa anasema Nyerere was selfish, incompetent na asiyeambilika. Wadau endeleeni kumwaga data na Kama kuna watu wataelezea vizuri habari za villagelization ntafurahi sana kuliko kumpa Mtu sifa ambazo alikuwa hastahili mwaka 1999 tulizuiwa hata kufanya graduation za kuhitimu o level eti tukio kwenye maombolezo ya Baba aw Taifa kumbe baba mwenyewe mbinafsi
 
William
Kinachotugharimu leo hii si gharama ya vita vya Uganda ni ufisadi wa viongozi wetu msikwepe ukweli; silaha nyingi zilizotumika kwenye vita vilikuwa ni mkopo kutoka Russia na madeni hayo yalishasamehewa; kama unataka kujua ukweli tafuta gharama halisi ya vita na gharama ya ufisadi utaona ukweli wa maneno; gharama za ufisadi ni kubwa zaidi ya mara 10 ya vita vya Uganda.

Chama
Gongo la Mboto DSM

- kama unataka kuongelea ufisadi then fungua thread yake, lakini kujaribu kuingiza hoja za propaganda hapa ndio ufisadi wenyewe, siamini kwamba Russia ilitusamehe madeni ya ile Vita, ambayo wao walikuwa wanauza silaha kwetu na kwa adui at the same time, tunaambiwa tulikuwa na Viongozi genius enzi hizo, lakini walikubali tukadanganywa na Russia wao wakiuza silaha huku na kule,

- Sasa leo tunawauliza was it fair kujiiingiza kwenye ile vita mpaka kufikia madeni yote tunayolipa mpaka leo? Mnasema ni propaganda, oooh maswali ya chuki za binafsi, REALLY?

William.
 
Kwanini nchi za kiislam zilimsaidia IDDI AMINI? ukipata jawabu hapo utajuwa kwa nini Nyerere alianzisha vita na AMINI, kisha watanzania wakafanywa "wapumbavu" kutungiwa nyimbo za ajabu ajabu.

Orodhesha hapa nchi za kiislam zaidi ya Libya zilizomsaidia Amin.
 
William
Amin alishageuka kansa kwa watanzania ilikuwa ni lazima aondoke; kama angekuwa na vita vya maneno tu vita visingetokea; kitendo chake cha kuvamia na kuuwa watanzania wasio na hatia hicho kilikuwa si cha kufumbia macho; Mwl. Nyerere hakuwa Raisi legelege; na lazima ukumbuke Amin alijivunia wadhamini wake Ghadaf wa Libya na alishatoa kauli ataichukua Mwanza; hizo ni kauli zake, kama ambavyo haikuwa kosa kwa Dunia kumuondoa Hitler basi pia halikuwa kosa kwa wanajeshi mahiri wa Tanzania chini ya Jemedari wao Nyerere kumuondoa Idd Amin; William hizi propaganda za kumpaka Mwl. Nyerere matope hazitafua dafu; wapo wanasiasa na majemedari wetu ambao walishiriki kikamilifu kwenye vita vile waulize watakueleza visa vya Idd Amin.

Chama
Gongo la Mboto DSM

- Nimewahi kukaa chini na Binaisa na Lule, story zao ninaziamini sana maana zinakaribiana sana na za viongozi wetu ambazo huwa wanzitoa kwa siri sana, kwa kuogopa kuonekana wana tatizo na Mwalimu.

- Binaisa anasema aliambiwa wazi kwamba yeye ni RC tu wa Uganda sio rais, yaani Mkuu wa mkoa wa Tanzania wakati ule, Lule alipojaribu kuwa objective anasema aliwekwa under house arrest, halafu mnakuja watu wazima hapa mnataka kutudanganya na kututisha na maneno mengi uongo uongo as if wote hapa ni watoto wadogo, kama mmezidiwa hoja ni kukaa pembeni tu! Mnatutisha na mavitabu yaliyoandikwa na ma-compromise, mtu unasoma kitabu ukurasa wa kwanza tu umeshaelewa kila kitu kitabu gani hicho?

- Waliotyaka kuandika vitabu vya ukweli si walufukuzwa au hujui? I mean wakuu wacheni tujadili taifa letu kama kawa!


William.
 
Fikra zangu zilikuwa Kama za w malecela wakati niko form .2 ila baada ya kusoma sana na kutafakari kwa kina nikagundua Nyerere alikuws sahihi katika jambo hili.tumvumilie huyu malecela kwani akili zake bado ni za form 2
O

- REALLY? Umekuja kwenye thread iliyoandikwa na mtu mwenye akili za darasa la 10? ha! ha! ha!

William.
 
Naomba kuuliza. Hivi ni watanganyika tu wanaowajibika na PAN-AFRICANISM?
 
mkuu unajua kati ya uganda na tanzania ni nani alikuwa mchokozi??

Je? Wajua ni kwanin? Uganda waliitandika tanzania na mpaka kuvuka mipaka??

In short.Nyerere alikuwa swaiba ake sana obote na pind idd amin alipo mpindua abote nyerere hakufurahia kabisa.Hivyo tanzania ilimuhifanyi obote na mkakati kabambe wa kumng'oa idd amin madarakan uliundwa kuna vijana waganda na watanzania walipewa mafunzo na kuanza kumletea choko choko idd amin kwa kuingia uganda na kufanya fujo walivyo fukuzwa walikimbilia tanzania choko choko zikazid wakaenda tena kufanya fujo na wakafanya uharibifu mkubwa sana uganda idd amin akakasirika akawatandika na kuwafukuza mpaka tanzania na kuingia kilomita kazaa tanzania.
Hapo ndipo nyerere alipokuwa anapataka haraka haraka akautangazia umma kwamba idd amin anataka kuitwa baadhi ya ardhi ya tz na kutangaza vita.
Je? Hapo mwenye kosa nani?? Na je? Ni nani hapo ni mchokozi wa mwenzake?

Ndio mana hata kamanda gadafi alimuunga mkono idd amin na kumsaidia kwa sababu uhuni wote alikuwa anaufahamu.

Hizo zilikuwa propaganda za amin ili ku justify uvamizi wake kwa TZ na alifanikiwa kumuingiza mkenge gadaffi ambaye alimuunga mkono lakini gadaffi alikuja kugundua badae kuwa amin was a liar na ndo maana gadaffi alimtaka radhi nyerere vilevile nyerere alimrudishia gadaffi mateka wote wa kilibya na gadaffi alifarijika kwa kuipa TZ mafuta mengi buree!
 
- Nimewahi kukaa chini na Binaisa na Lule, story zao ninaziamini sana maana zinakaribiana sana na za viongozi wetu ambazo huwa wanzitoa kwa siri sana, kwa kuogopa kuonekana wana tatizo na Mwalimu.

- Binaisa anasema aliambiwa wazi kwamba yeye ni RC tu wa Uganda sio rais, yaani Mkuu wa mkoa wa Tanzania wakati ule, Lule alipojaribu kuwa objective anasema aliwekwa under house arrest, halafu mnakuja watu wazima hapa mnataka kutudanganya na kututisha na maneno mengi uongo uongo as if wote hapa ni watoto wadogo, kama mmezidiwa hoja ni kukaa pembeni tu! Mnatutisha na mavitabu yaliyoandikwa na ma-compromise, mtu unasoma kitabu ukurasa wa kwanza tu umeshaelewa kila kitu kitabu gani hicho?

- Waliotyaka kuandika vitabu vya ukweli si walufukuzwa au hujui? I mean wakuu wacheni tujadili taifa letu kama kawa!


William.

William
Wewe ni msomi kila uandishi una agenda na kila agenda utumika kama propaganda machine; kama uliwahi kuongea na Binaisa na Lule hilo hatuwezi kulithibitisha wote ni marehemu (R.I.P) ukweli wa hilo unalijua wewe binafsi; labda nikuulize tu mbona umelitoa leo hii na si jana; "halafu mnakuja watu wazima hapa mnataka kutudanganya na kututisha na maneno mengi uongo uongo as if wote hapa ni watoto wadogo, kama mmezidiwa hoja ni kukaa pembeni tu"! Hapa hatutishani tunadebate kutafuta ukweli wa hoja; katika mada yako unadai vita vimetugharimu hadi leo ninachotaka kukwambia tu kabla Mwl. Nyerere hajaachia madaraka alifanya kazi kubwa ya kuhakikisha madeni yetu na Urusi na China yanasamehewa kitu ambacho alifamikiwa kwa kiasi kikubwa; nimegusia ufisadi ili ujue nini kinachotugharimu watanzania umejaribu kuhusisha gharama vita ndio inayotugharimu umejaribu kukwepa ukweli watanzania wanajua nini kinachowagharimu; Mkuu unapo debate ni wigo mkubwa yataingia yaliyomo na yasiyokuwamo umesoma hilo kwenye humanities; nimesema hizo ni propaganda za wazi najua unaelewa vyema siasa na propaganda vinamix bila matatizo. HIZI NI PROPAGANDA KWANI ULIANZA NA BIAFRA NA SASA VITA NA IDD AMIN HIVI WEWE KAMA MTANZANIA HUNA HATA MOJA ZURI LA KUMJADILI NYERERE? NAAMINI YAPO MENGI SANA ALIYOYAFANYA NYERERE AMBAYO YALIKUNUFAISHA NA YANAENDELEA KUKUNUFAISHA HADI LEO HII. Tuendelee na hoja

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
mbona tuliilaani israel kuwa imemsjambulia nchi huru ya africa alipogomboa mateka wake entebe huku iddi amin akiwa adui mkubwa wetu?
ninalokumbuka ni kuwa Nyerere alilaan Islael kwa kuiteka na kuikalia palestina.
 
- Nimewahi kukaa chini na Binaisa na Lule, story zao ninaziamini sana maana zinakaribiana sana na za viongozi wetu ambazo huwa wanzitoa kwa siri sana, kwa kuogopa kuonekana wana tatizo na Mwalimu.

- Binaisa anasema aliambiwa wazi kwamba yeye ni RC tu wa Uganda sio rais, yaani Mkuu wa mkoa wa Tanzania wakati ule, Lule alipojaribu kuwa objective anasema aliwekwa under house arrest, halafu mnakuja watu wazima hapa mnataka kutudanganya na kututisha na maneno mengi uongo uongo as if wote hapa ni watoto wadogo, kama mmezidiwa hoja ni kukaa pembeni tu! Mnatutisha na mavitabu yaliyoandikwa na ma-compromise, mtu unasoma kitabu ukurasa wa kwanza tu umeshaelewa kila kitu kitabu gani hicho?

- Waliotyaka kuandika vitabu vya ukweli si walufukuzwa au hujui? I mean wakuu wacheni tujadili taifa letu kama kawa!


William.

Mkuu William,

Sijakaa na Binaisa au Lule. Lakini nachofahamu kuwa vita vya kukomboa Kagera na kumuondoa Idd Amin vilichukua kama miezi sita (October 1978 - April 1979). Vilikuwa ni vita fupi.

Baada ya vita Tanzania ilichukua jukumu la kukaa Uganda kwa miaka miwili. Na miongoni mwa majukumu ya miaka miwili hiyo ilikuwa ni mikakati ya kurudisha Obote.

Nyerere alikuwa ana deni kubwa na Obote. Mwaka 1971 kulikuwa na harakati za kupindua serikali ya Obote. Hivyo Obote hakutaka kwenda kwenye mkutano wa jumuia za madola uliofanyika Singapore. Nyerere akamshawishi kwenda na matokeo yake Obote kupinduliwa. Tanzania ilimpokea na kumwifadhi kama rais. Na juhudi zilifanyika kumrudisha.

Uwezekano mkubwa kama tulivyoona vita vya Iraq, gharama kubwa zilikuja katika juhudi za kumrudisha Obote madarakani na sio kwenye vita vya kukomboa eneo la Kagera au Kumuondoa Iddi Amini.

Kumrudisha Obote ilikuwa ni kazi kubwa. Kwanza alikuwa hakubaliki na waganda wenyewe. Na kwenye uchaguzi hakufanya vizuri.
 
- Wakuu JF heshima mbele sana, naomba kuuliza tena hivi kulikuwa ana ulazima wa kupiagana Vita na Idd Amin mpaka kumuondoa kwenye madaraka nchini mwake? Yeye alivunja sheria za kimataifa kwa kutuingilia ndani ya mipaka yetu, je na sisi kwa kuvuka mipaka yake pia mbona kama tulijivua nguo kama yeye, yaani tukawa two wrongs!

- I mean kumuondoa tu kwenye ardhi yetu ndio sheria za kimataifa zinavyosema, lakini kwenda mpaka kumuondoa kwenye uongozi wa Taifa lake mbona kama we went too far, na historia ikaishia kutusuta maana tukamuweka Obote, akaishia kuondolewa tena na mwingine, au Great Thinkers mnasema je?

- Na wale mabingwa wa Conspiracy Theories karibuni sana!!



William.

Jipu haliwezi kupona bila kutolewa ile mbegu iliyo kwa ndani...
 
- I mean kupiga taifa lingine na kuingilia mpaka ndani ya mipaka yake ni makosa ksiheria za kimataifa, na hadithi ya Marehemu Binaisa, kuhusu nia na madhumuni ya Mwalimu na ile vita ni tofauti kabisa na hii habari yako, betwen Lule na Binaisa, wote waliambiwa wazi kwamba nia ni kumrudisha Obote, ndio maana na wao wakamuondoa very fast kumhakikishia Mwalimu kwamba hawakubali pilcies zake kwa nchi yao.

- Kumpiga Amin mpaka ndani ya nchi yake kumetugharimu na mpaka leo bado tunalipia, ni wajibu wetu wananchi wenye uwezo wa kufikiri kuuliza kuhusu hizi failed policies!, ambazo zingine physically zinatuumiza mpaka leo, ambapo wahusika hawapo!William.
Asolutely wrong Bill. Baada ya Amin alifuata Lule ambaye aliondolewa na kurithiwa na Binaisa.
Binaisa alikuwa 'arrested' na akina Tito Okello.
Ndani ya serikali ya Binaisa Museveni alikuwa waziri wa Ulinzi na kisha kuhamishwa wizara hiyo.
Kabla ya Obote kushinda uchaguzi, uganda ilikuwa inaongozwa na kamati ya muda.

Aliyemondoa Obote ni Majeshi yake. Hadi hapo Lule na Binaisa walikuwa hawana uwezo dhidi ya Obote.
Kusema ya kuwa Binaisa na Lule walimuondoa Obote ili kumkomoa mwalimu na siasa zake si kweli na nadiriki kusema ni upotoshaji wa 'short cut' ili hukumu ipatikane hata kwa mashitaka ya kuunga unga.

Obote aliporudi mara ya pili alifanya mauaji ya raia wengi hasa jimbo la kati. Hata alipotorka na kufika mpakani mwa Kenya, Nyerere hakukubali arudi Tanzania.

Sababu kubwa ya Amin kuvamia Kagera kwa mujibu wake ni madai kuwa Kagera ni sehemu ya Uganda. Alipofanikiwa kupora mali, kuvuruga maisha ya watu wa Kagera, Amin alipandisha bendera ya Uganda na kumteua mkuu mpya wa Wilaya ya Kagera.

Vita ya Kagera inaweza kuwa ni 'failed policy' kama unavyodai. Ni vema basi utueleze ingekuwa wewe upo katika nafasi ya kutoa maamuzi unadhani nini ungefanya wananchi wako wakiwa wameuawa na kufukuzwa katika eneo lao na kipande cha nchi kuchukulia?
 
William
Wewe ni msomi kila uandishi una agenda na kila agenda utumika kama propaganda machine; kama uliwahi kuongea na Binaisa na Lule hilo hatuwezi kulithibitisha wote ni marehemu (R.I.P) ukweli wa hilo unalijua wewe binafsi; labda nikuulize tu mbona umelitoa leo hii na si jana; "halafu mnakuja watu wazima hapa mnataka kutudanganya na kututisha na maneno mengi uongo uongo as if wote hapa ni watoto wadogo, kama mmezidiwa hoja ni kukaa pembeni tu"! Hapa hatutishani tunadebate kutafuta ukweli wa hoja; katika mada yako unadai vita vimetugharimu hadi leo ninachotaka kukwambia tu kabla Mwl. Nyerere hajaachia madaraka alifanya kazi kubwa ya kuhakikisha madeni yetu na Urusi na China yanasamehewa kitu ambacho alifamikiwa kwa kiasi kikubwa; nimegusia ufisadi ili ujue nini kinachotugharimu watanzania umejaribu kuhusisha gharama vita ndio inayotugharimu umejaribu kukwepa ukweli watanzania wanajua nini kinachowagharimu; Mkuu unapo debate ni wigo mkubwa yataingia yaliyomo na yasiyokuwamo umesoma hilo kwenye humanities; nimesema hizo ni propaganda za wazi najua unaelewa vyema siasa na propaganda vinamix bila matatizo. HIZI NI PROPAGANDA KWANI ULIANZA NA BIAFRA NA SASA VITA NA IDD AMIN HIVI WEWE KAMA MTANZANIA HUNA HATA MOJA ZURI LA KUMJADILI NYERERE? NAAMINI YAPO MENGI SANA ALIYOYAFANYA NYERERE AMBAYO YALIKUNUFAISHA NA YANAENDELEA KUKUNUFAISHA HADI LEO HII. Tuendelee na hoja

Chama
Gongo la Mboto DSM

Chama,

Vita viliingiza gharama kubwa sana kiuchumi. Katika Hotuba ya mwisho wa mwaka 1979, Nyerere alisema kuwa itachukua miezi 18. Baada ya mwaka akasema miaka 18.

Kuhusu madeni ya Urusi na China sina uhakika nayo. Lakini sehemu kubwa matumizi ya jeshi haipo kwenye zana za kivita. Warusi na wachina walitudai kwenye zana za kijeshi.

Lakini wakati wa vita vya Kagera na Uganda, serikali ilibidi iongeze idadi ya wanajeshi. Na vita vilipokwisha wote walipewa nafasi katika majeshi ya ulinzi na usalama. Hivyo kulipa mishahara pekee yake ilikuwa ni kazi kubwa.

Vilevile majeshi ya Tanzania yalikaa Uganda kwa miaka miwili. Gharama za kukaa kule zilikuwa za kwetu. Vilevile zana zingine za kivita zilitoka katika nchi nyingine kama Yugoslavia. Hivyo hoja ya kuwa tulisamehewa haina mpango.

Vilevile manunuzi mengine ya zana na mahitaji ya kivita yalitumia reserve na mikopo ambayo ilitakiwa kutumika kwenye shughuli za maendeleo. Hivyo misamaha ya warusi na wachina haikutoa unafuu wowote hule.
 
Back
Top Bottom