Vita vya Syria vina mchanganyiko sana, ila dikteta Assad ni uovu wenye afadhali (lesser evil) kuliko waasi Wanajihadi

Vita vya Syria vina mchanganyiko sana, ila dikteta Assad ni uovu wenye afadhali (lesser evil) kuliko waasi Wanajihadi

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Ukiangalia kwa undani makundi ya waasi yanayopigana dhidi ya utawala wa dikteta Bashir Al-Assad nchini Syria hayatoi matumaini mema kwamba endapo yatafanikiwa kumng'oa Assad siku za usoni za Syria zitakuwa njema chini ya utawala wao mpya, makundi yanayompinga Assad ukiondoa Wakurdi nusu yake ni makundi ya kijihadi yenye msimamo mkali. Haya makundi yakishika madaraka ina maana Syria itageuzwa taifa la kidini rasmi na inaweza kugeuka changamoto nyingine kubwa si kwa raia wa ndani tu bali hata nchi majirani ikiwemo Israel.

Familia ya Assad ambayo ni alawites , tawi la Washia lenye msimamo tofauti na sehemu kubwa ya Waislamu ikiwemo kuruhusu matumizi ya pombe na kutoamini kabisa wanawake kuvaa hijabu ni takwa la lazima la dini wameiendesha Syria kama taifa jumuishi la imani zote kwa muda mrefu japo chini ya utawala wa chama kimoja cha Baath, hakuna uhakika kama waasi watakoingia kumrithi Assad watadumisha taifa jumuishi la Syria lisilo la kidini au lenye mrengo wa upande mmoja zaidi wa kidini na hapo ndipo migogoro itapozidi na kuharibu mambo kabisa.

Ni kweli kihistoria Syria chini ya utawala wa familia ya Assad haujawahi kuwa rafiki sana wa Israel lakini pia haijawahi kuwa utawala wa uadui wa kiwendawazimu sana kuipasua kichwa Israel, mara nyingi imejizuia au imejiepusha kuingia katika migogoro isiyo ya lazima na Israel. Mtihani mkubwa ni kwamba Syria ya Assad imekuwa kibaraka wa Iran wakati wote ambaye ni adui mkubwa wa Marekani na Israel.
 
Waarabu huwa wanashindwa kupiga mahesabu ya kina aisee.

Badala mkubali kukaa chini ya bendera moja ya utawala mujenge taifa mnaleta utofauti unaowagawanya na kuharibu nchi na kuipasua kipande kipande.

Hili la Syria na Libya halina tofauti sana.
 
Waarabu huwa wanashindwa kupiga mahesabu ya kina aisee.
Badala mkubali kukaa chini ya bendera moja ya utawala mujenge taifa mnaleta utofauti unaowagawanya na kuharibu nchi na kuipasua kipande kipande.
Hili la Syria na Libya halina tofauti sana.
Siasa za mashariki ya kati ni ngumu sana na zina historia ndefu ya mchanganyiko usio na afya wa dini, ukabila na rasilimali za kiuchumi.
 
Siasa za mashariki ya kati ni ngumu sana na zina historia ndefu ya mchanganyiko usio na afya wa dini, ukabila na rasilimali za kiuchumi.
Yani Kuna muda hadi unasikitika mkuu.

Kama ukisema ni uislam mbona Malaysia,Indonesia,Brunei waislam wengi na hayo hayatokei!?

Bangladesh Kuna waislam wengi na dini zingine kibao ila wanaungana chini ya bendera moja ya nchi.

Hata Sheikh Hasinah alipopinduliwa na wananchi waislam,wakristo kwa wapagani waliungana chini ya kauli moja.

Sijui waarabu wana nini kichwani kiasi hawana umoja!?
 
Yani Kuna muda hadi unasikitika mkuu.
Kama ukisema ni uislam mbona Malaysia,Indonesia,Brunei waislam wengi na hayo hayatokei!?
Bangladesh Kuna waislam wengi na dini zingine kibao ila wanaungana chini ya bendera moja ya nchi.
Hata Sheikh Hasinah alipopinduliwa na wananchi waislam,wakristo kwa wapagani waliungana chini ya kauli moja.
Sijui waarabu wana nini kichwani kiasi hawana umoja!?
Malysia, Indonesia na Brunei ni mataifa ambayo majority ni Wasuni, Bangladesh huwa kuna machufuko ya mara kwa mara kati ya Waislamu na Wahindu na Wabudha pia katika baadhi ya maeneo.
 
Familia ya Assad ambayo ni alawites ,
Kwa upande mwingine Alawites wanaitwa "Waislamu Poa", na hawa Waasi wanataka Taliban Style Government. Na huenda Syria Arab Republic ikabadilishwa jina na kuitwa Islamic Emirate of Sham and Levant ngoja tuone, yetu macho.

Tatizo la Assad ni kule kuwaachia Wairan njia ya kupitisha Silaha kwenda Lebanon ya Hezbola.
 
Malysia, Indonesia na Brunei ni mataifa ambayo majority ni Wasuni, Bangladesh huwa kuna machufuko ya mara kwa mara kati ya Waisalumu na Wahundu na Wabudha katika baadhi ya maeneo.
Bangladesh ni kwa uchache sana,vurugu za Bangladesh ndogo sio za kuitikisa amani ya nchi.
Mkuu huko uarabuni sunni ndio majority ila ona kinachotokea.
 
Kwa upande mwingine Alawites wanaitwa "Waislamu Poa" na hawa Waasi wanataka Taliban Style Government. Na huenda Syria Arab Republic ikabadilishwa jina na kuitwa Islamic Emirate of Sham and Levant ngoja tuone yetu macho.

Tatizo la Assad ni kule kuwaachia Wairan njia ya kupitisha Silaha kwenda Lebanon ya Hezbola.
Iran ya Washia ndio wanaoiimarisha familia ya Assad madarakani Syria wasiondolewe na Wasuni, bila msaada wao ingekuwa vigumu sana kina Assad kudumu madarakani huo muda wote kwa sababu Shia na Alawites ni minorities.
 
Waarabu huwa wanashindwa kupiga mahesabu ya kina aisee.

Badala mkubali kukaa chini ya bendera moja ya utawala mujenge taifa mnaleta utofauti unaowagawanya na kuharibu nchi na kuipasua kipande kipande.

Hili la Syria na Libya halina tofauti sana.
Tatizo hatufuatilii mambo,jumatatu netanyahu alisema assad anacheza na moto, jumatano isis wakaanzisha mashambulizi syria,miezi miwili nyuma palikua na habari marekani kukusanya waasi Syria,leo kimenuka na waasi wako wengi kinyama
Jana,duru za kijasusi israel zimenukuliwa zikisema vita syria itawafanya hizbullah wakasaidie na kaskazini israel kupata utulivu
 

Attachments

  • Screenshot_2024-11-29-19-14-17-834.jpg
    Screenshot_2024-11-29-19-14-17-834.jpg
    433.8 KB · Views: 7
Waarabu huwa wanashindwa kupiga mahesabu ya kina aisee.

Badala mkubali kukaa chini ya bendera moja ya utawala mujenge taifa mnaleta utofauti unaowagawanya na kuharibu nchi na kuipasua kipande kipande.

Hili la Syria na Libya halina tofauti sana.
Tatizo hatufuatilii mambo,jumatatu netanyahu alisema assad anacheza na moto, jumatano isis wakaanzisha mashambulizi syria,miezi miwili nyuma palikua na habari marekani kukusanya waasi Syria,leo kimenuka na waasi wako wengi kinyama
Jana,duru za kijasusi israel zimenukuliwa zikisema vita syria itawafanya hizbullah wakasaidie na kaskazini israel kupata
 
Unaonaje Syria kiuchumi ilikuaje tangu itawaliwe na hao minorities?
Syria haijawahi kuwa na uchumi mzuri sana katika historia yake yote kwa sababu ya sera mbaya za uchumi na ufisadi uliopitiliza katika sekta ndogo ya mafuta iliyokuwa inategemewa, umasikini umekuwepo mkubwa, raia wake wengi wamekuwa wakiishi kwa misaada na wachache kutoka familia ya Assad na machawa wao wakineemeka na mapato ya nchi. Pia ukiacha miaka michache ya baada uhuru utawala wote wa Syria umekuwa wa Alawites, familia ya Assad wamekuwa watawala kwa miaka takribani 50.
 
Tatizo hatufuatilii mambo,jumatatu netanyahu alisema assad anacheza na moto, jumatano isis wakaanzisha mashambulizi syria,miezi miwili nyuma palikua na habari marekani kukusanya waasi Syria,leo kimenuka na waasi wako wengi kinyama
Jana,duru za kijasusi israel zimenukuliwa zikisema vita syria itawafanya hizbullah wakasaidie na kaskazini israel kupata utulivu
Waarabu hawamuwezi Muisraeli, wao wenyewe kwa wenyewe hawapendani, na ni rahisi sana kuwagawa.

Sasa hivi Netanyahu anakula Popcorn huku anaangalia Magaidi yanavyochinjana😁😆
 
Ukiangalia kwa undani makundi ya waasi yanayopigana dhidi ya utawala wa dikteta Bashir Al-Assad nchini Syria hayatoi matumaini mema kwamba endapo yatafanikiwa kumng'oa Assad siku za usoni za Syria zitakuwa njema chini ya utawala wao mpya, makundi yanayompinga Assad ukuondoa Wakurdi nusu yake ni makundi ya kijihadi yenye msimamo mkali. Haya makundi yakishika madaraka ina maana Syria itageuzwa taifa la kidini rasmi na inaweza kugeuka changamoto nyingine kubwa si kwa raia wa ndani tu bali hata nchi majirani ikiwemo Israel.

Familia ya Assad ambayo ni alawites , tawi la Washia lenye msimamo tofauti na sehemu kubwa ya Waislamu ikiwemo kuruhusu matumizi ya pombe na kutoamini kabisa wanawake kuvaa hijabu ni takwa la lazima la dini wameiendesha Syria kama taifa jumuishi la imani zote kwa muda mrefu japo chini ya utawala wa chama kimoja cha Baath, hakuna uhakika kama waasi watakoingia kumrithi Assad watadumisha taifa jumuishi la Syria lisilo la kidini au lenye mrengo wa upande mmoja zaidi wa kidini na hapo ndipo migogoro itapozidi na kuharibu mambo kabisa.

Ni kweli kihistoria Syria chini ya utawala wa familia ya Assad haujawahi kuwa rafiki sana wa Israel lakini pia haijawahi kuwa utawala wa uadui wa kiwendawazimu sana kuipasua kichwa Israel, mara nyingi imejizuia au imejiepusha kuingia katika migogoro isiyo ya lazima na Israel. Mtihani mkubwa ni kwamba Syria ya Assad imekuwa kibaraka wa Iran wakati wote ambaye ni adui mkubwa wa Marekani na Israel.
Sasa hao Israel ndio wanafadhili hayo makundi,

Siku zote nawaambia humu Huyo Israel ndio adui yenu na sio hao viongozi wa hizo nchi, na ndio maana unaona Wakristo WA lebanon wameamua kufadhili Hezbollah wa nafahamu nini kitawapata ikiwa Israel atakua na influence za Hio Nchi.

Hao Al Qaeda Wa Syria wana full Silaha za Marekani na wakiumia kutibiwa ni Israel.

Syria chini ya Assad kabla ya 2011 makundi mengi yaliexist pamoja, yes ana mabaya yake ila kama unavyosema ni lesser evil.

Same kwa Sadam na viongozi wengine wa huo ukanda.
 
Back
Top Bottom