Zakayomfupi
JF-Expert Member
- Mar 11, 2024
- 281
- 320
Issue ni kwamba mpaka Leo Al Qaeda wanasaidiwa na Marekani na wana silaha za kisasa ambazo ni wachache sana wanazo.Naifahamu historia ya Al-Qaeda vizuri sana mkuu, Al-Qaeda ilichipukia kutoka makundi ya Mujahideen yaliyokuwa yanapambana kuuondoa uvamizi wa USSR nchini Afghanistan miaka ya 1980 na kipindi hicho yalikuwa yanapewa msaada wa silaha, pesa na intelligence kutoka US kupambana na uvamizi wa USSR, tatizo USSR na ujamaa walipong'olewa Afghanistan Al-Qaeda walienda rogue na full extremists.
It has nothing to do with Sunni, Sadam ni Sunni na alikuwa ni rafiki mkubwa Wa wakristo Middle East, same kwa Pan Arab leaders wengine kama Kina Yaser Arafat. Haya makundi yanayofadhiliwa na west na Marekani ndio yanayoua wakristo Middle East. Divide and Conquer kuhakikisha kila kundi linapigana na mwenzake wao wachote Mafuta kirahisi.Waasi wa Syria ni washenzi, Assad ameweza kuishi bila kuwanyanyasa wakristo ambao wengi wanaishi Allepo. Lakini waasi wanauwa kwa kuwakata vichwa. Hata Lebanon wakristo waliungana na Shia dhidi ya Suni katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Suni ni hatari sana kwa ukristo.
Ww jamaa bwana ,sasa hao marafiki ambao hutaki awe nao sindo wamemfanya awe madarakani mpaka sasa na kuinusuru Syria kuangukia kwenye makundi maovu?Namkubali sana Assad, tatizo lake ni moja tu ambalo umeshalitaja.
Kwa maoni yangu, ingewezekana wale waasi wange stopishwa tu, sema ndiyo vile anaponzwa na marafiki
Mkuu, unataka kumaanisha kwamba washia ndio wagomvi?Malysia, Indonesia na Brunei ni mataifa ambayo majority ni Wasuni, Bangladesh huwa kuna machufuko ya mara kwa mara kati ya Waislamu na Wahindu na Wabudha pia katika baadhi ya maeneo.
Upo sahihi kabisa ....Ukiangalia kwa undani makundi ya waasi yanayopigana dhidi ya utawala wa dikteta Bashir Al-Assad nchini Syria hayatoi matumaini mema kwamba endapo yatafanikiwa kumng'oa Assad siku za usoni za Syria zitakuwa njema chini ya utawala wao mpya, makundi yanayompinga Assad ukuondoa Wakurdi nusu yake ni makundi ya kijihadi yenye msimamo mkali. Haya makundi yakishika madaraka ina maana Syria itageuzwa taifa la kidini rasmi na inaweza kugeuka changamoto nyingine kubwa si kwa raia wa ndani tu bali hata nchi majirani ikiwemo Israel.
Familia ya Assad ambayo ni alawites , tawi la Washia lenye msimamo tofauti na sehemu kubwa ya Waislamu ikiwemo kuruhusu matumizi ya pombe na kutoamini kabisa wanawake kuvaa hijabu ni takwa la lazima la dini wameiendesha Syria kama taifa jumuishi la imani zote kwa muda mrefu japo chini ya utawala wa chama kimoja cha Baath, hakuna uhakika kama waasi watakoingia kumrithi Assad watadumisha taifa jumuishi la Syria lisilo la kidini au lenye mrengo wa upande mmoja zaidi wa kidini na hapo ndipo migogoro itapozidi na kuharibu mambo kabisa.
Ni kweli kihistoria Syria chini ya utawala wa familia ya Assad haujawahi kuwa rafiki sana wa Israel lakini pia haijawahi kuwa utawala wa uadui wa kiwendawazimu sana kuipasua kichwa Israel, mara nyingi imejizuia au imejiepusha kuingia katika migogoro isiyo ya lazima na Israel. Mtihani mkubwa ni kwamba Syria ya Assad imekuwa kibaraka wa Iran wakati wote ambaye ni adui mkubwa wa Marekani na Israel.
Na vurugu ni kama zilianza wakati mmojaWaarabu huwa wanashindwa kupiga mahesabu ya kina aisee.
Badala mkubali kukaa chini ya bendera moja ya utawala mujenge taifa mnaleta utofauti unaowagawanya na kuharibu nchi na kuipasua kipande kipande.
Hili la Syria na Libya halina tofauti sana.
Inakuwaje sasa nchi zenye wasunni wengi zina amani na washia, wakiongozwa na Iran ndio wanaonekana wana vurugu?Wasuni ndio huwa wagomvi zaidi mkuu wanapokutana na Washia kwa sababu wanawaona wenzao Washia kama sio Waislamu kamili au Waislamu waliopotoka.
Mbona Marekani, Uingereza, Ufaransa,na Ujerumani huwaweki kwenye list ya waliokuwa wapeleka silaha wakubwa kwa waasi?Upo sahihi kabisa ....
Kipindi mgogoro upo kwenye kilele chake nchi kama Qatar, Saud Arabia, Uturuki zilimwaga fedha na silaha nyingi mno kwa Kila aliyekuwa anapigana na Assad mwishowe hizo silaha ziliangukia kwa makundi ya kijihadi kama Isis na Al nusra (HTS).
Kwa Sasa Syria imegawanyika mno na kuiunganishe tena sio kazi rahisi isitoshe nchi zote kubwa zimejihusisha na hivi vita na zina askari wake humo, hili linaongeza ugumu wa kuiunganisha nchi.
Fikiria hadi sasa kundi linaloongoza mashambulizi na kuteka maeneo huko Allepo na Hama ni wanajihadi wa HTS, nadhani hili limefanya hata Marekani na wamagharibi kuachana na sera Yao ya kutaka Assad aondoke maana hawajui atakayerithi atakuaje maana hata wale waasi wanaowafadhili kwa kuwaita 'moderate' ni dhaifu mno kuweza kuwashinda wanajihadi.
Nchi zenye Wasuni wengi wanatumia mabavu kuwatiisha Washia, kuna malalamiko makubwa sana ya kukandamizwa na kutengwa kwa Washia nchini Saudi Arabia,. Iran pia ndio taifa kubwa lenye Washia wengi lakini linazungukwa na mataifa yenye Wasuni wengi kwa hiyo kila mmoja anachochea vurugu upande mwingine.Inakuwaje sasa nchi zenye wasunni wengi zina amani na washia, wakiongozwa na Iran ndio wanaonekana wana vurugu?
Wapuuz hao wapigwe tu hao waasiWaasi wanajaribu kuiteka Hamma tokea jana wamerudishwa nyuma na wamezungukia upande wa pili wa Mji reinforcement inapelekwa kundi kubwa la Waasi linaelekea huko.
Kiongozi wao Abu Mohamed Al Jolaani kasema baada ya Hama ni Homs,na baada ya Homs ni Damascus yenyewe, wakati huohuo maelfu ya Wanamgambo wa Kishia wanazidi kumiminika kutoka Iraq na Beyond ili kuja kuisaidia Regime ya Assad.
View attachment 3167515
Al Jolaani anasema kaachana na Al Qaida lakini anataka Taliban Style Government.
Nawaonea huruma Wanawake wa Syria Arab Republic.
MWENYEZI MUNGU alilinde na kulitunza kanisa la SyriaIt has nothing to do with Sunni, Sadam ni Sunni na alikuwa ni rafiki mkubwa Wa wakristo Middle East, same kwa Pan Arab leaders wengine kama Kina Yaser Arafat. Haya makundi yanayofadhiliwa na west na Marekani ndio yanayoua wakristo Middle East. Divide and Conquer kuhakikisha kila kundi linapigana na mwenzake wao wachote Mafuta kirahisi.
Hii ni speech Ya Michael Aoun raisi wa Lebanon aliopita Akielezea situation ya Wakristo Middle East.
"We chose this long-term political option, because we knew that the interests of the West do not lie with us. Its interests lie with Israel, on one hand, and with the oil, on the other hand. We are not included among its interests at present. The only thing it cares about is resolving the problem of Israel at our expense, through the naturalization of the Palestinians in Lebanon, and pleasing the oil-producing countries, because its material interests lie there. Therefore, we had to choose a policy of coordination with all elements of Lebanese society, and with our neighboring countries, in order to build strong, solid, and mutual relations. Lebanese society in general, and the Christians in particular, are not used to this, and therefore, it has aroused fear and concern. However, our confidence in ourselves, in the choice we made, and in our views have made it possible for us to stand before you, and to ask you to give the efforts we are undertaking a chance. A short while ago, in Doha, we saw the results. All the Christians in the Middle East, all the Christians in the Middle East are fleeing, while the Christians of Lebanon are returning. The forecasts of the entire world. For 25–35 years, we have been reading that the Christians in the Middle East are becoming extinct. Western policies have led the Christians in the Middle East towards extinction. Western policies have not left a single Christian in Palestine and the holy places. Western policies have not left a single Christian in Iraq. They intended to get rid of us by marginalizing us, and by treating us as a superfluous element in society."[117]
Dah maisha haya hawo jamaa wanaenda kufa au kuponaKataib Hezbollah na Vikundi vingine vya Kishia vimeanza kuingia Syria kama Nzige, vinatokea Iraq and Beyond👇
View: https://youtu.be/MeBckllq07w?si=UKdRx3wpMxZoZK9k
Mambo yanazidi kuwa Motomoto.