Vita ya Clatous Chota Chama Vs Pablo mmoja kuondoka SIMBA

Vita ya Clatous Chota Chama Vs Pablo mmoja kuondoka SIMBA

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Tetesi kutoka msimbazi ni kuwa kiungo wa Simba,Clatous Chotta Chama na Kocha Mkuu Pablo Franco walirushiana maneno kwenye vyumba vya kubadilishia nguo Aprili 30, 2022 katika mchezo wa Derby ya Kariakoo dhidi ya Yanga.

Inaelezwa tukio ndilo lililisababisha Pablo kumtoa Chama na nafasi yake kuchukuliwa na Bwalya, pia katika mchezo dhidi ya Namungo FC, jana Mei 3, 2022, Chama hakuwepo hata kwenye benchi la timu hiyo.

Kutokana na hali hiyo hapo ni wazi wawili hao hawawezi kufanya kazi pamoja na mmoja lazima aondoke, inaaminika kuwa kinachombakisha Pablo mpaka sasa ni kwa kuwa kuna uwezekano wa Simba kukutana na Yanga kwa mara nyingine katika Kombe la FA.

Kama atashindwa kuingia fainali ya FA ni wazi kuwa safari yake itauwa imewadia mapema zaidi ya inavyoelezwa, pia viongozi wa Simba wanaona ameshindwa kuinua viwango vya wachezaji wengi msimu huu.
 
Tetesi kutoka msimbazi ni kuwa kiungo wa Simba,Clatous Chotta Chama na Kocha Mkuu Pablo Franco walirushiana maneno kwenye vyumba vya kubadilishia nguo Aprili 30, 2022 katika mchezo wa Derby ya Kariakoo dhidi ya Yanga...
Ondoa hapo Neno Tetesi kwani Tukio la Ukweli ambalo Binafsi nimethibitishwa Watu wangu wa karibu ambao 24/7 wako na Simba SC Kiufundi na Kiutendaji.

Kocha Pablo baada ya Msimu huu wa NBC Premier League kumaliizika Simba SC itaachana nae mazima hata hivyo kama Simba SC ikifuzu Kuifunga Pamba FC na Kutinga Nusu Fainali ya ASFC kwa Kucheza na Yanga SC na ikatokea ikafungwa na Yanga SC siku hiyo basi baada ya huo Mchezo tu Kocha Pablo atakutana na Mabegi yake na Documents zake zote pale JNIA Terminal III kusubiria Flight yake ya kwenda Madrid akatusalimie akina Raul Gonza, Andre Iniesta na Xavi Hernandez.

Na upo pia Uwezekano mkubwa Mechi ya Simba SC na Pamba FC Mafia ndani ya Simba SC Wakaichezesha ili Simba SC ifungwe na sababu ya Kumfukuza Kocha Pablo ipatikane ili Kocha Msaidizi Matola akabidhiwe Timu mpaka Mechi za mwisho ili Kupunguza Mzigo wa Kumlipa Mamilioni Kocha Mkuu Pablo ambaye hana Jipya na sana sana anaitia tu Gharama Klabu kwa Kumlipa na Kumgharamikia vingi tu.

Tunza / Tunzeni hii post yangu tafadhali.
 
Ondoa hapo Neno Tetesi kwani Tukio la Ukweli ambalo Binafsi nimethibitishwa Watu wangu wa karibu ambao 24/7 wako na Simba SC Kiufundi na Kiutendaji.

Kocha Pablo baada ya Msimu huu wa NBC Premier League kumaliizika Simba SC itaachana nae mazima hata hivyo kama Simba SC ikifuzu Kuifunga Pamba FC na Kutinga Nusu Fainali ...
Duuuuh yaan sijui simba huwa tunakutwa na nn khaaah.
 
Ondoa hapo Neno Tetesi kwani Tukio la Ukweli ambalo Binafsi nimethibitishwa Watu wangu wa karibu ambao 24/7 wako na Simba SC Kiufundi na Kiutendaji.

Kocha Pablo baada ya Msimu huu wa NBC Premier League kumaliizika Simba SC itaachana nae mazima hata hivyo kama Simba SC ikifuzu Kuifunga Pamba FC na Kutinga Nusu Fainali ya ASFC kwa Kucheza na Yanga SC na ikatokea ikafungwa na Yanga SC siku hiyo basi baada ya huo Mchezo tu Kocha Pablo atakutana na Mabegi yake na Documents zake zote pale JNIA Terminal III kusubiria Flight yake ya kwenda Madrid akatusalimie akina Raul Gonza, Andre Iniesta na Xavi Hernandez.

Na upo pia Uwezekano mkubwa Mechi ya Simba SC na Pamba FC Mafia ndani ya Simba SC Wakaichezesha ili Simba SC ifungwe na sababu ya Kumfukuza Kocha Pablo ipatikane ili Kocha Msaidizi Matola akabidhiwe Timu mpaka Mechi za mwisho ili Kupunguza Mzigo wa Kumlipa Mamilioni Kocha Mkuu Pablo ambaye hana Jipya na sana sana anaitia tu Gharama Klabu kwa Kumlipa na Kumgharamikia vingi tu.

Tunza / Tunzeni hii post yangu tafadhali.
Sisi ambao ni mashabiki wa Yanga tuushike ukweli upi?

Mwanzo mlisema ni kocha mzuri mmemtoa madrid saivi bora arudi madrid.
 
Ndani ya msimu mmoja, makocha watatu! Hakika mtakuwa mmepigwa na kitu kizito sana kichwani.

Aliondoka Kishingo, akaja Gomez! Ghafla akaletwa Pablo wa Real Madrid! Na sasa sijui mtamrudisha Julio wa Namungo!
msimu mmoja makocha wa tatu ? Acha uongo ww uto
 
Ndani ya msimu mmoja, makocha watatu! Hakika mtakuwa mmepigwa na kitu kizito sana kichwani.

Aliondoka Kishingo, akaja Gomez! Ghafla akaletwa Pablo wa Real Madrid! Na sasa sijui mtamrudisha Julio wa Namungo!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nimecheka mnooo.
Hebu tuache kwan, tuna maumivu ya kukosa ubingwa.
Huu mwaka uishe kwan, mweeeeh.
 
Back
Top Bottom