Vita ya Uganda sawa.....Rwanda hapana...Kagera tunasema hapana

Vita ya Uganda sawa.....Rwanda hapana...Kagera tunasema hapana

FOR 2015

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2012
Posts
538
Reaction score
221
Ndugu wana JF. Salaam kwenu


....'Tumevamiwa; Mwendawazimu ametuvamia, sasa tutampiga. Nia ya kumpiga tunayo, Uwezo wa kumpiga tunao na sababu ya kumpiga tunayo'.

Ndugu, hayo yalikuwa ni maneno mazito ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa tayari kuingia vitani dhidi ya Nduli Iddi Amin 'Dada'. Nimeikumbuka kauli hii baada ya takribani siku kadhaa kuwa zimepita tunaendelea kusikia Chokochoko za Wasioitakia mema Tanzania kutaka Vita na Rwanda. Hili kwa mtazamo wangu halikubaliki kwa sababu zifuatazo;

Mosi; Tanzania haina sababu hata moja ya kuivamia Rwanda, hata moja nasisitiza. Hoja za walio wengi zimelenga katika CHUKI BINAFSI dhidi ya Kagame,,basi,,hakuna sababu nyingine. Mheshimiwa Rais Kikwete alitoa ushauri kwa Kagame na Kagame akajibu mbovu, basi. Inaishia hapo, sio sababu tosha ya kutufanya tuingie vitani. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mbili; Wengi na hasa wanaoshabikia Tanzania kutaka kuingia Vitani ni watu baki, hawana maslahi hata Chembe na Mkoa wa Kagera na hawajui hata Makaburi ya Wahaya waliofariki miaka ya 1978-1980 wakati wa Vita ya Kagera yakoje. Hawakuwahi KULIA hawa; hawakuwahi kumlilia mtu aliyekufa kwa risasi, wamezoea kulilia watu wanaokufa kwa magonjwa ya kawaida. Kabla hawajaanza kushabikia mimi naita UWENDAWAZIMU huu watembee Makaburi ya Wahaya waliokufa katika Vita ya Kagera, hakika wataacha ushabiki usiokuwa na msingi. VITA YA UGANDA SAWA...VITA NA RWANDA HAPANA.

Tatu; Kiuchumi moja kati ya Mikoa iliyokuwa inaendelea kwa kasi ya ajabu baada ya kupata Uhuru ilikuwa ni Mkoa wa Kagera, baada ya Vita ya Uganda kila kitu kilienda SHAGHALABAGHALA. Unajua kwa nini? Sababu nguvu kazi kubwa (Vijana) iliuawa katika vita na wengine kukimbia makazi yao. Wala Serikali haikuwahi kufanya Juhudi Binafsi kuupa kipaumbele Mkoa wa Kagera kwa sababu ya madhara yaliyopatikana kutokana na vita hiyo. Katika vita hiyo kulikuwa na kujitolea kwingi lakini kwa sababu ya Vita yenyewe uwanja wa vita ilikuwa ni Kagera, Wahaya wengi ndio waliojitokeza. Maana ya hili ni kwamba, Endapo Serikali itataka kukidhi MIHEMKO ya WAJINGA wachache wanaopenda vita, bado Uwanja wa Vita Utakuwa Kagera. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Nne, Vifo,,Enyi mashabiki wa vita na Rwanda, jamani mnataka tena Bibi, Babu, Kaka, Dada, Shangazi, Wajomba na wadogo zetu wauawe?. Ndiyo furaha yenu? Tuambieni? Msitukumbushe mbali, msitukumbushe vilio, Simanzi na majonzi. Hapana, tunasema HAPANA. Nyie waandishi msiokuwa na Ndugu huko Bukoba mtuachie Ndugu zetu waishi maana nao wanayo haki ya kuishi kama mlivyo nyie katika maofisi yenu huko Dar es Salaam. Yaani mnaamini kuwa itakuwa ni sisi kuua tu bila kuuawa? Wahaya tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Tano, Mgawanyiko, ukijaribu kufuatilia kwa karibu unagundua kuwa kuna mgawanyiko Mkubwa sana kati ya wanaotaka vita na Rwanda na wale wasioitaka ambapo mimi naangukia katika kundi la pili. Hii kitu katika medani za vita, haiwezi kuifanya Tanzania kushinda Vita hiyo kama tunavyojitia moyo. Hakika tunajidanganya, tunafanya Propaganda za kitoto, tunacheza ngoma tukiwa uchi, tuache Ujinga. Tuache kabisa kuwaogopesha Wananchi wetu kwa maslahi ya Damu za Wahaya, Hapana hatutakubali. Wahaya kwa mara nyingine tunasema na kusisitiza VITA YA UGANDA SAWA,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mwisho, Sababu kubwa iliyotufanya tuingie Vitani na Uganda wakati huo ni Uvamizi wa Ghafla uliokuwa umefanywa na Iddi Amin kwa Tanzania akitaka kuichukua Ardhi ya Kagera. Naamini hii ni sababu kubwa sana ndio maana Mwalimu alimuita Iddi Amin MWENDAWAZIMU maana ni Mwendawazimu pekee anayeweza kuingia Nyumbani kwako, akataka kuingia hadi jikoni na hatimaye Chumbani baadaye kabatini na uvunguni. Je Rwanda na Kagame wamefanya nini?.. Kuichukua Ardhi ya Kagera kulimaanisha kuwafanya Wahaya wawe Sehemu ya Uganda, Kufanya Visiwa karibu 27 vilivyo Ziwa Victoria upande wa Kagera viwe Upande wa Uganda, Ndizi nzuri zote unazozijua Tanzania ziwe Upande wa Uganda; kiukweli hili lilikuwa halikubaliki, ndio maana tukatengeneza NIA na SABABU baada ya kuongezewa UWEZO kutoka RUSSIA. Kwa sasa Rwanda na Kagame wao hawajatukosea kitu na kwa hiyo tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Ushauri, Wale wote wanaoshabikia vita na Rwanda hasa kwa wakati huu, wangejikita zaidi katika kuhakikisha Tunajenga Uzalendo miongoni mwa Watanzania ili kuwa na Maendeleo endelevu na pia kuipenda nchi yao. Tumshauri Mheshimiwa Rais atimize wajibu wake wa Kuwaletea Watanzania Maendeleo badala ya kuja na WISH WASH ideas. Tujikite katika kuhakikisha tunakuwa na Katiba bora itakayotupa Mwelekeo Mzuri wa Taifa letu. Tumwambie Mheshimiwa Rais na washauri wake Wapeleke Huduma za Jamii kama Hospitali, Shule, Maji, Barabara kule vijijini ambapo hawajui hata Mpaka wa Tanzania na Rwanda ukoje. Tuwaambie Wabunge wajali maslahi ya Wananchi, watimize ahadi zao. Tukifanya hivyo hakika tutafika.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI KAGERA (BUKOBA)
 
JK ameshasema Tanzania haina mpango wa kuvamia nchi nyingine ila atakayevamia ardhi yetu kama atakuja na nywele ataondoka na kipara. Tuliza boli usiwe na wasi

Mkuu nadhamiria tu kuwaonya hao Mashabiki wa Vita, wanamtuhumu Kagame kuwa anapenda Vita wakati wao ndo kwa maneno yao wanaishangilia. Watanzania tuwe makini na watu hawa, wasije kuwa wanatumika kuwarainisha viongozi wetu. Kuivamia nchi ya Mwenzio ni Makosa kisheria lazima tuelewe hivyo.
 
Ni kweli hata mie sipendi vita kabisa. Ila PK na watu wake wanaropoka ovyo, wako provocative sana.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Wala serikali ya Tz haijatangaza vita na Rwanda! Acha woga ndugu yangu! Kama itabidi Rwanda tutaidunda! Pia ni dhana potofu kufikiri kuwa ni wahaya pekee ndo walikufa katika vita ya Kagera! Ni Watanzania wote walishiriki katika vita hiyo! Acha woga!
 
Nani amekwambia kuna vita? Kuwatangazia wahamiaji haram ni kuingia vitani? Wewe n moja ya watu wanaochochea mhemko wa vita hiyo. Why not keep silence? J.k kesha sema yeye ndo amir jesh, ninyi ndo akina nani?
 
Ni kweli hata mie sipendi vita kabisa. Ila PK na watu wake wanaropoka ovyo, wako provocative sana.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Ndg Maswala, Kulopoka tu hakutupi sisi Credits za kuivamia na kuipiga Rwanda, after all We are not sure of defeating him. Hatuzijui nguvu zake, tunamjaji kwa maana ya Population ya Rwanda na wala sio Idadi, Nguvu, Strategy na Teknolojia ya Jeshi lake. Watanzania tuache kupenda na kushabikia vita.
 
Ntagunga, Ndio maana nilikaa kimya kwa muda mrefu sana ila kinachoonekana ni kila kukicha Baadhi ya watu wanachochea Tanzania kuipiga Rwanda,,,Sijui wengine wameandika Safari ya Goma iishie Kigali..... Watu kama hao tusipowaambia kwamba HATUTAKI VITA wataendelea kuandika na kuzidi kuwa OGOFYA wananchi. Ni lazima tukemee hili. VITA NA RWANDA HAIKUBALIKI KATU
 
Ndugu wana JF. Salaam kwenu


....'Tumevamiwa; Mwendawazimu ametuvamia, sasa tutampiga. Nia ya kumpiga tunayo, Uwezo wa kumpiga tunao na sababu ya kumpiga tunayo'.

Ndugu, hayo yalikuwa ni maneno mazito ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa tayari kuingia vitani dhidi ya Nduli Iddi Amin 'Dada'. Nimeikumbuka kauli hii baada ya takribani siku kadhaa kuwa zimepita tunaendelea kusikia Chokochoko za Wasioitakia mema Tanzania kutaka Vita na Rwanda. Hili kwa mtazamo wangu halikubaliki kwa sababu zifuatazo;

Mosi; Tanzania haina sababu hata moja ya kuivamia Rwanda, hata moja nasisitiza. Hoja za walio wengi zimelenga katika CHUKI BINAFSI dhidi ya Kagame,,basi,,hakuna sababu nyingine. Mheshimiwa Rais Kikwete alitoa ushauri kwa Kagame na Kagame akajibu mbovu, basi. Inaishia hapo, sio sababu tosha ya kutufanya tuingie vitani. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mbili; Wengi na hasa wanaoshabikia Tanzania kutaka kuingia Vitani ni watu baki, hawana maslahi hata Chembe na Mkoa wa Kagera na hawajui hata Makaburi ya Wahaya waliofariki miaka ya 1978-1980 wakati wa Vita ya Kagera yakoje. Hawakuwahi KULIA hawa; hawakuwahi kumlilia mtu aliyekufa kwa risasi, wamezoea kulilia watu wanaokufa kwa magonjwa ya kawaida. Kabla hawajaanza kushabikia mimi naita UWENDAWAZIMU huu watembee Makaburi ya Wahaya waliokufa katika Vita ya Kagera, hakika wataacha ushabiki usiokuwa na msingi. VITA YA UGANDA SAWA...VITA NA RWANDA HAPANA.

Tatu; Kiuchumi moja kati ya Mikoa iliyokuwa inaendelea kwa kasi ya ajabu baada ya kupata Uhuru ilikuwa ni Mkoa wa Kagera, baada ya Vita ya Uganda kila kitu kilienda SHAGHALABAGHALA. Unajua kwa nini? Sababu nguvu kazi kubwa (Vijana) iliuawa katika vita na wengine kukimbia makazi yao. Wala Serikali haikuwahi kufanya Juhudi Binafsi kuupa kipaumbele Mkoa wa Kagera kwa sababu ya madhara yaliyopatikana kutokana na vita hiyo. Katika vita hiyo kulikuwa na kujitolea kwingi lakini kwa sababu ya Vita yenyewe uwanja wa vita ilikuwa ni Kagera, Wahaya wengi ndio waliojitokeza. Maana ya hili ni kwamba, Endapo Serikali itataka kukidhi MIHEMKO ya WAJINGA wachache wanaopenda vita, bado Uwanja wa Vita Utakuwa Kagera. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Nne, Vifo,,Enyi mashabiki wa vita na Rwanda, jamani mnataka tena Bibi, Babu, Kaka, Dada, Shangazi, Wajomba na wadogo zetu wauawe?. Ndiyo furaha yenu? Tuambieni? Msitukumbushe mbali, msitukumbushe vilio, Simanzi na majonzi. Hapana, tunasema HAPANA. Nyie waandishi msiokuwa na Ndugu huko Bukoba mtuachie Ndugu zetu waishi maana nao wanayo haki ya kuishi kama mlivyo nyie katika maofisi yenu huko Dar es Salaam. Yaani mnaamini kuwa itakuwa ni sisi kuua tu bila kuuawa? Wahaya tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Tano, Mgawanyiko, ukijaribu kufuatilia kwa karibu unagundua kuwa kuna mgawanyiko Mkubwa sana kati ya wanaotaka vita na Rwanda na wale wasioitaka ambapo mimi naangukia katika kundi la pili. Hii kitu katika medani za vita, haiwezi kuifanya Tanzania kushinda Vita hiyo kama tunavyojitia moyo. Hakika tunajidanganya, tunafanya Propaganda za kitoto, tunacheza ngoma tukiwa uchi, tuache Ujinga. Tuache kabisa kuwaogopesha Wananchi wetu kwa maslahi ya Damu za Wahaya, Hapana hatutakubali. Wahaya kwa mara nyingine tunasema na kusisitiza VITA YA UGANDA SAWA,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mwisho, Sababu kubwa iliyotufanya tuingie Vitani na Uganda wakati huo ni Uvamizi wa Ghafla uliokuwa umefanywa na Iddi Amin kwa Tanzania akitaka kuichukua Ardhi ya Kagera. Naamini hii ni sababu kubwa sana ndio maana Mwalimu alimuita Iddi Amin MWENDAWAZIMU maana ni Mwendawazimu pekee anayeweza kuingia Nyumbani kwako, akataka kuingia hadi jikoni na hatimaye Chumbani baadaye kabatini na uvunguni. Je Rwanda na Kagame wamefanya nini?.. Kuichukua Ardhi ya Kagera kulimaanisha kuwafanya Wahaya wawe Sehemu ya Uganda, Kufanya Visiwa karibu 27 vilivyo Ziwa Victoria upande wa Kagera viwe Upande wa Uganda, Ndizi nzuri zote unazozijua Tanzania ziwe Upande wa Uganda; kiukweli hili lilikuwa halikubaliki, ndio maana tukatengeneza NIA na SABABU baada ya kuongezewa UWEZO kutoka RUSSIA. Kwa sasa Rwanda na Kagame wao hawajatukosea kitu na kwa hiyo tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Ushauri, Wale wote wanaoshabikia vita na Rwanda hasa kwa wakati huu, wangejikita zaidi katika kuhakikisha Tunajenga Uzalendo miongoni mwa Watanzania ili kuwa na Maendeleo endelevu na pia kuipenda nchi yao. Tumshauri Mheshimiwa Rais atimize wajibu wake wa Kuwaletea Watanzania Maendeleo badala ya kuja na WISH WASH ideas. Tujikite katika kuhakikisha tunakuwa na Katiba bora itakayotupa Mwelekeo Mzuri wa Taifa letu. Tumwambie Mheshimiwa Rais na washauri wake Wapeleke Huduma za Jamii kama Hospitali, Shule, Maji, Barabara kule vijijini ambapo hawajui hata Mpaka wa Tanzania na Rwanda ukoje. Tuwaambie Wabunge wajali maslahi ya Wananchi, watimize ahadi zao. Tukifanya hivyo hakika tutafika.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI KAGERA (BUKOBA)


Tanzania inahitaji wazando wa aina ya FOR 2015, tunahitaji kuangalia miundombinu yetu kwa ujumla wake ilikuijenga tanazania bora yenye matumain hasa kwa siku zijazo.

Ngoja niwaite washabiki wa vita ambao kwao ufedhuli wa propaganda imeathili mishipa yao ya akili nakusahau madhara kama hayo hapo juu.

Manyerere Jackton , Alumbwagweumutwa , Manyerere Jackton, Mauza uza , Tambala , kidole007 , stroke , mokala1989 , [MENTION]NattyDread[/MENTION], Mwamakula , makoye78 , Lilambo , thatha , Rutunga M
 
Last edited by a moderator:
Binafsi napinga huu ujinga wa watu ambao wanakaa wanawaza kupigana hata katika mambo madogo kama haya ambayo watu wanaweza kukaa na kujadili,kama ishu ni kupigana twende tukapigane na Malawi ambao tayari wanatangaza kuchukua sehemu ya ardhi yetu na si Rwanda kwani sijaona PK akisema anahitaji kipande fulani kutoka Tz
Tuache maamuzi ya kipimbi.
 
Ukimwi, vita ya Idi Amin, MV Bukoba! Bado kuna watu wanawaza vita kwa kumuonea wivu Kagame. Hata hawajiulizi kwa nini Kagame kajibu vile! I support you
 
Binafsi napinga huu ujinga wa watu ambao wanakaa wanawaza kupigana hata katika mambo madogo kama haya ambayo watu wanaweza kukaa na kujadili,kama ishu ni kupigana twende tukapigane na Malawi ambao tayari wanatangaza kuchukua sehemu ya ardhi yetu na si Rwanda kwani sijaona PK akisema anahitaji kipande fulani kutoka Tz
Tuache maamuzi ya kipimbi.

mi naomba vita ipiganiwe Dar 'peponi' kwa Tanzania
 
Khaa!! FOR 2013 yaani wewe ni kunguru kweli. Nani katangaza vita? Unalialia tu bure. Unamaaana hata kama PK akimhit JK kama alivyoahidi basi tumuangalie tu?? Hivi kipi bora kwako kati ya Kagera kuwa sehemu ya Rwanda au Kagera kuwa battlefield ili iokolewe? Usiwe mjinga kwa kutanguliza UHAYA mbele kuliko UTANZANIA. Hata hivyo kwa akili yako kama ikitokea vita kati ya Rwanda na Tanzania unadhani itapiganiwa Mafia au Chunya au Bariadi??
 
Mkuu tz haina ubavu wa kuipiga rwanda hizi ni kelele tu maendeleo yametushinda tynalukia vingine
Ntagunga, Ndio maana nilikaa kimya kwa muda mrefu sana ila kinachoonekana ni kila kukicha Baadhi ya watu wanachochea Tanzania kuipiga Rwanda,,,Sijui wengine wameandika Safari ya Goma iishie Kigali..... Watu kama hao tusipowaambia kwamba HATUTAKI VITA wataendelea kuandika na kuzidi kuwa OGOFYA wananchi. Ni lazima tukemee hili. VITA NA RWANDA HAIKUBALIKI KATU
 
wanaoamua vita wapo dar es salaam, nyie tulizeni boli. tunaangalia maslahi ya nchi

Hapo pia ndio Hofu, Mashaka na Wasiwasi wangu umelala. Hata wanaoshabikia kutaka Tanzania Iivamie Kigali kuanzia Goma wako Dar es Salaam. Light Baba zao, Mama zao, Shangazi, Wajomba, Kaka, Dada na wadogo zao wangekuwa Kagera,,,,kidogo tungesema wana uchungu na majibu ya PK kwa JK. Vita ikiwa inaendelea huko Kagera huku wananchi wakuhangaika, mabomu yakirindima, watoto wakipoteana na wazazi wao, vyakula vikipanda bei. Wao watakuwa ama kwenye vyumba vya habari Dar wakila kiyoyozi ama vyambani mwao waki - enjoy na wapenzi wao.

 
wanaoamua vita wapo dar es salaam, nyie tulizeni boli. tunaangalia maslahi ya nchi

Munaangalia maslahi ya nchi au maslahi binafsi? Kwani uhai wa wananchi siyo sehemu ya maslahi ya nchi? Kwa hiyo watu watulie tu wakisubiri muamue wachinjwe kisa maslahi ya nchi?. Ni maslahi gani hayo yanayozidi uhai wa watu? Wananchi wanayo haki ya kulalamika maana vita ikianza victims wakubwa ni wao. Nyie wenye maamuzi munaweza kuanzisha vita na baadaye mukapanda ndege na familia zenu kwenda nchi nyingine hadi vita itakapoisha. Sijui mkirudi mtafurahi kuyakuta mafuvu na mifupa badala ya watu? Kulinda mipaka yetu ni vizuri lakini hatuna sababu ya kuchokoza vita kama hatujavamiwa na adui na zoezi hili inabidi liwe la kudumu
 
Tanzania inahitaji wazando wa aina ya FOR 2015, tunahitaji kuangalia miundombinu yetu kwa ujumla wake ilikuijenga tanazania bora yenye matumain hasa kwa siku zijazo.

Ngoja niwaite washabiki wa vita ambao kwao ufedhuli wa propaganda imeathili mishipa yao ya akili nakusahau madhara kama hayo hapo juu.

Manyerere Jackton , Alumbwagweumutwa , Manyerere Jackton, Mauza uza , Tambala , kidole007 , stroke , mokala1989 , NattyDread, Mwamakula , makoye78 , Lilambo , thatha , Rutunga M
Khaa!! wewe ndiyo umepotea kabisa. Utawezaje kufanya yote hayo kama hakuna hakuna amani? Amani ni jambo pana sana. Unataka hawa wahamiaji haramu wajazane nchini kwetu hadi baadaye waanze kudai haki za uwenyeji kama inavyosemwa?? au na wewe ni mmoja wao??
 
Khaa!! FOR 2013 yaani wewe ni kunguru kweli. Nani katangaza vita? Unalialia tu bure. Unamaaana hata kama PK akimhit JK kama alivyoahidi basi tumuangalie tu?? Hivi kipi bora kwako kati ya Kagera kuwa sehemu ya Rwanda au Kagera kuwa battlefield ili iokolewe? Usiwe mjinga kwa kutanguliza UHAYA mbele kuliko UTANZANIA. Hata hivyo kwa akili yako kama ikitokea vita kati ya Rwanda na Tanzania unadhani itapiganiwa Mafia au Chunya au Bariadi??

Kweli wewe ni rohombaya kama sura yako inavyoonyesha pamoja na uliyoyanndika hapo juu
 
Khaa!! FOR 2013 yaani wewe ni kunguru kweli. Nani katangaza vita? Unalialia tu bure. Unamaaana hata kama PK akimhit JK kama alivyoahidi basi tumuangalie tu?? Hivi kipi bora kwako kati ya Kagera kuwa sehemu ya Rwanda au Kagera kuwa battlefield ili iokolewe? Usiwe mjinga kwa kutanguliza UHAYA mbele kuliko UTANZANIA. Hata hivyo kwa akili yako kama ikitokea vita kati ya Rwanda na Tanzania unadhani itapiganiwa Mafia au Chunya au Bariadi??

Rohombaya, Nikusahihishe najulikana kama FOR 2015. Pole kwa roho yako mbaya. Nimeshauri hakuna haja ya Serikali kuwasikiliza watu wenye roho mbaya kama yako ikaingia Mkenge na kuingia vitani maana hakuna sababu ya Msingi ya kufanya hivyo kwa sasa. Nataka kukumbusha mfano wa Mwalimu alioutoa akiwa anamtania Sir George Kahama kuhusu Umimi (EGOISM) alionao Mwanadamu. Ndege ilipopata Hitilafu Sir akasema My God, hali ilipoendelea kuwa mbaya akasema Mungu Wangu, ilipokaribia kudondoka akasema MUNGU WANGE,,,huyo kajirudia zake Bukoba kuna lugha tatu hapo. Mwalimu alitaka kuonesha umuhimu wa kuwa Wazalendo. Tatizo wewe na roho mbaya yako unadhani Uzalendo ni kwa Utanzania tu, HAPANA unatakiwa kuwa Mzalendo na kwa Kabila lako. Ndio maana tunaambiwa tukajenge kwetu au mtu akifariki watu wanaanza kuuliza Mnasafirisha au...

Ni ukweli usiofichika kuwa leo hii ninyi mnaohimiza vita mnajua kwa namna yoyote HAITAWAATHIRI. Majibu mabaya ya PK kwa JK hayawi sababu tosha ya Kuanzia Goma na Kuishia Kigali. Hizo ni chuki binafsi na habari ndo hiyo. Yaani unadhani Vita ikiianza wataoathirika ni Chunya, Mafia au Bariadi,,,wala ni Kagera...Sisi tunasema YA UGANDA SAWA... RWANDA HAPANA...Peleka kule roho mbaya yako
 
Back
Top Bottom