Vita ya Uganda sawa.....Rwanda hapana...Kagera tunasema hapana

Vita ya Uganda sawa.....Rwanda hapana...Kagera tunasema hapana

Huna point wewe


Ndugu wana JF. Salaam kwenu


....'Tumevamiwa; Mwendawazimu ametuvamia, sasa tutampiga. Nia ya kumpiga tunayo, Uwezo wa kumpiga tunao na sababu ya kumpiga tunayo'.

Ndugu, hayo yalikuwa ni maneno mazito ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa tayari kuingia vitani dhidi ya Nduli Iddi Amin 'Dada'. Nimeikumbuka kauli hii baada ya takribani siku kadhaa kuwa zimepita tunaendelea kusikia Chokochoko za Wasioitakia mema Tanzania kutaka Vita na Rwanda. Hili kwa mtazamo wangu halikubaliki kwa sababu zifuatazo;

Mosi; Tanzania haina sababu hata moja ya kuivamia Rwanda, hata moja nasisitiza. Hoja za walio wengi zimelenga katika CHUKI BINAFSI dhidi ya Kagame,,basi,,hakuna sababu nyingine. Mheshimiwa Rais Kikwete alitoa ushauri kwa Kagame na Kagame akajibu mbovu, basi. Inaishia hapo, sio sababu tosha ya kutufanya tuingie vitani. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mbili; Wengi na hasa wanaoshabikia Tanzania kutaka kuingia Vitani ni watu baki, hawana maslahi hata Chembe na Mkoa wa Kagera na hawajui hata Makaburi ya Wahaya waliofariki miaka ya 1978-1980 wakati wa Vita ya Kagera yakoje. Hawakuwahi KULIA hawa; hawakuwahi kumlilia mtu aliyekufa kwa risasi, wamezoea kulilia watu wanaokufa kwa magonjwa ya kawaida. Kabla hawajaanza kushabikia mimi naita UWENDAWAZIMU huu watembee Makaburi ya Wahaya waliokufa katika Vita ya Kagera, hakika wataacha ushabiki usiokuwa na msingi. VITA YA UGANDA SAWA...VITA NA RWANDA HAPANA.

Tatu; Kiuchumi moja kati ya Mikoa iliyokuwa inaendelea kwa kasi ya ajabu baada ya kupata Uhuru ilikuwa ni Mkoa wa Kagera, baada ya Vita ya Uganda kila kitu kilienda SHAGHALABAGHALA. Unajua kwa nini? Sababu nguvu kazi kubwa (Vijana) iliuawa katika vita na wengine kukimbia makazi yao. Wala Serikali haikuwahi kufanya Juhudi Binafsi kuupa kipaumbele Mkoa wa Kagera kwa sababu ya madhara yaliyopatikana kutokana na vita hiyo. Katika vita hiyo kulikuwa na kujitolea kwingi lakini kwa sababu ya Vita yenyewe uwanja wa vita ilikuwa ni Kagera, Wahaya wengi ndio waliojitokeza. Maana ya hili ni kwamba, Endapo Serikali itataka kukidhi MIHEMKO ya WAJINGA wachache wanaopenda vita, bado Uwanja wa Vita Utakuwa Kagera. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Nne, Vifo,,Enyi mashabiki wa vita na Rwanda, jamani mnataka tena Bibi, Babu, Kaka, Dada, Shangazi, Wajomba na wadogo zetu wauawe?. Ndiyo furaha yenu? Tuambieni? Msitukumbushe mbali, msitukumbushe vilio, Simanzi na majonzi. Hapana, tunasema HAPANA. Nyie waandishi msiokuwa na Ndugu huko Bukoba mtuachie Ndugu zetu waishi maana nao wanayo haki ya kuishi kama mlivyo nyie katika maofisi yenu huko Dar es Salaam. Yaani mnaamini kuwa itakuwa ni sisi kuua tu bila kuuawa? Wahaya tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Tano, Mgawanyiko, ukijaribu kufuatilia kwa karibu unagundua kuwa kuna mgawanyiko Mkubwa sana kati ya wanaotaka vita na Rwanda na wale wasioitaka ambapo mimi naangukia katika kundi la pili. Hii kitu katika medani za vita, haiwezi kuifanya Tanzania kushinda Vita hiyo kama tunavyojitia moyo. Hakika tunajidanganya, tunafanya Propaganda za kitoto, tunacheza ngoma tukiwa uchi, tuache Ujinga. Tuache kabisa kuwaogopesha Wananchi wetu kwa maslahi ya Damu za Wahaya, Hapana hatutakubali. Wahaya kwa mara nyingine tunasema na kusisitiza VITA YA UGANDA SAWA,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mwisho, Sababu kubwa iliyotufanya tuingie Vitani na Uganda wakati huo ni Uvamizi wa Ghafla uliokuwa umefanywa na Iddi Amin kwa Tanzania akitaka kuichukua Ardhi ya Kagera. Naamini hii ni sababu kubwa sana ndio maana Mwalimu alimuita Iddi Amin MWENDAWAZIMU maana ni Mwendawazimu pekee anayeweza kuingia Nyumbani kwako, akataka kuingia hadi jikoni na hatimaye Chumbani baadaye kabatini na uvunguni. Je Rwanda na Kagame wamefanya nini?.. Kuichukua Ardhi ya Kagera kulimaanisha kuwafanya Wahaya wawe Sehemu ya Uganda, Kufanya Visiwa karibu 27 vilivyo Ziwa Victoria upande wa Kagera viwe Upande wa Uganda, Ndizi nzuri zote unazozijua Tanzania ziwe Upande wa Uganda; kiukweli hili lilikuwa halikubaliki, ndio maana tukatengeneza NIA na SABABU baada ya kuongezewa UWEZO kutoka RUSSIA. Kwa sasa Rwanda na Kagame wao hawajatukosea kitu na kwa hiyo tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Ushauri, Wale wote wanaoshabikia vita na Rwanda hasa kwa wakati huu, wangejikita zaidi katika kuhakikisha Tunajenga Uzalendo miongoni mwa Watanzania ili kuwa na Maendeleo endelevu na pia kuipenda nchi yao. Tumshauri Mheshimiwa Rais atimize wajibu wake wa Kuwaletea Watanzania Maendeleo badala ya kuja na WISH WASH ideas. Tujikite katika kuhakikisha tunakuwa na Katiba bora itakayotupa Mwelekeo Mzuri wa Taifa letu. Tumwambie Mheshimiwa Rais na washauri wake Wapeleke Huduma za Jamii kama Hospitali, Shule, Maji, Barabara kule vijijini ambapo hawajui hata Mpaka wa Tanzania na Rwanda ukoje. Tuwaambie Wabunge wajali maslahi ya Wananchi, watimize ahadi zao. Tukifanya hivyo hakika tutafika.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI KAGERA (BUKOBA)
 
Kama itatokea Rwanda atatandikwa basi atatandikwa na majeshi ya UN na sio Tanzania.
 
Siku hizi vita zinapiganiwa kwenye mitandao mkuu, wala usifikiri kuna kunguru wa kupigana karne hii, ukiona nchi inaingia vitani ujue kuna serious case not this one from PK and JK. Kwa hiyo maoni yangu ni kuwa, nawewe unaendeleza vita kati ya Rwanda na Tanzania. Kanusha kama ni uongo mkuu FOR 2015.

Mkuu WA-UKENYENGE, Sikupenda kabisa kuanzisha hii mada, imenibidi baada ya kuona kila uchao kuna Watanzania wenzetu wachache wanachagiza ili tuone Umuhimu wa Vita. This is Crazy, nikaona ni vema nitoe ya Moyoni wasije wakadhani tuko nyuma yao. Sure ni lazima tuwe na sababu za kutosha kuingia vitani. Ni upuuzi usiokuwa kifani Kuanza kujadili habari za Bahima na kuchomekea habari za kutaka vita.

Binafsi naamini sana katika kukaa kimya hasa katika masuala kama haya maana kuyaongea ndo kunaongeza zaidi Attention na wakati mwingine katika kuongea mtu usipokuwa makini unajichanganya. To be Frank after this I won't talk anymore on this issue. Ila ujumbe umewafikia wote Wachombezaji, wapenda vita wasiokuwa na Ndugu. Na nawaambia kamwe hila zao hazitafanikiwa. WE ARE FED UP. Wanaandika ili vita ikianza walipoti na hivyo kupata Faida katika kuuza habari. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA
 
Mkuu safi sana,nimefurahi sana.vita vya maendeleo tumeshapigwa 10-0 hadi sasa hivi.eti tuingie kwenye vita.uchumi wetu ni dhaifu.Sina maana hatuna resources hapana.lakini nchi haina pesa kwani pesa inaingia kwa mafisadi wachache alafu tunataka vita.vita ni gharama .kwanini hiyo bajeti ya vita hisiende kwenye mashuleni,afya na kwenye miundo mbinu.Nakupongeza mkuu wewe ni mtu wa amani .GOD BLESS YOU
 
VITA HAIKUBALIKI. Lazima kila juhudi ifanyike kuepuka vita na kama ipo iwe ni "last last last resort" na kwa sababu ya msingi sio hili la MIPASHO BAINA YA MARAISI. Ila Ndg. FOR2105 rekebisha kidogo waliokufa kwenye mapambano ya Kagera siyo wahaya peke yao bali hata wawakilishi wa makabila mengine mengi yaliyoshiriki kwenye vita moja kwa moja. Kuna ndugu zetu wengi sana wamekufa mstari wa mbele wakipambana kumng'oa nduli Amini na ushahidi mpaka leo upo pale kwenye makaburi ya mashujaa ya kambi ya Kaboya. Ila nakubaliana na wewe kuwa Wahaya waliathirika zaidi na mimi ni mmoja wa waathirika wengi na vita kwani nilikuwa Bukoba wakati Amini akileta ndege zake kuja kulipua sehemu mbalimbali Bukoba na lilishuhudia mabomu yakidondoshwa mpaka hospitali na kuathiri wagonjwa wasiokuwa na hatia. Kwa ufupi ni kuwa Kagame siyo adui wa watanzania na HATUTAKI VITA NAYE. Serikali ielekeze kuvu zake zote kwenye mapambano na maadui zetu wa jadi ambao ni UJINGA, MARADHI NA UMASKINI. na hawa wapya ambao ni UFISADI na UHALIFU WA KIMATAIFA ikiwepo na BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA.
 
Kama itatokea Rwanda atatandikwa basi atatandikwa na majeshi ya UN na sio Tanzania.

Ndibalema, That will be more good na bila shaka watakuwa na sababu kwa wakati huo. Tusiihusishe kabisa Tanzania na watu wetu wasihusike. Na kama ikitokea Uwanja wa vita uwe hukohuko watakaoamua wenyewe. Tanzania Hapana
 
VITA HAIKUBALIKI. Lazima kila juhudi ifanyike kuepuka vita na kama ipo iwe ni "last last last resort" na kwa sababu ya msingi sio hili la MIPASHO BAINA YA MARAISI. Ila Ndg. FOR2105 rekebisha kidogo waliokufa kwenye mapambano ya Kagera siyo wahaya peke yao bali hata wawakilishi wa makabila mengine mengi yaliyoshiriki kwenye vita moja kwa moja. Kuna ndugu zetu wengi sana wamekufa mstari wa mbele wakipambana kumng'oa nduli Amini na ushahidi mpaka leo upo pale kwenye makaburi ya mashujaa ya kambi ya Kaboya. Ila nakubaliana na wewe kuwa Wahaya waliathirika zaidi na mimi ni mmoja wa waathirika wengi na vita kwani nilikuwa Bukoba wakati Amini akileta ndege zake kuja kulipua sehemu mbalimbali Bukoba na lilishuhudia mabomu yakidondoshwa mpaka hospitali na kuathiri wagonjwa wasiokuwa na hatia. Kwa ufupi ni kuwa Kagame siyo adui wa watanzania na HATUTAKI VITA NAYE. Serikali ielekeze kuvu zake zote kwenye mapambano na maadui zetu wa jadi ambao ni UJINGA, MARADHI NA UMASKINI. na hawa wapya ambao ni UFISADI na UHALIFU WA KIMATAIFA ikiwepo na BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA.

Tata, Nimekubali na nilikiri kabisa kuwa Walio-athirika wengi walikuwa Wahaya. Tushirikiane ku - discourage hawa watu wachache wapenda vita. Pole kwa masaibu ya Vita ya Kagera, una kumbukumbu nzuri, unaweza kuwa mfano bora
 
Mkuu safi sana,nimefurahi sana.vita vya maendeleo tumeshapigwa 10-0 hadi sasa hivi.eti tuingie kwenye vita.uchumi wetu ni dhaifu.Sina maana hatuna resources hapana.lakini nchi haina pesa kwani pesa inaingia kwa mafisadi wachache alafu tunataka vita.vita ni gharama .kwanini hiyo bajeti ya vita hisiende kwenye mashuleni,afya na kwenye miundo mbinu.Nakupongeza mkuu wewe ni mtu wa amani .GOD BLESS YOU

Mkuu Environmental, Ahsante sana. Inauma sana sana hasa ukienda pale Mkoani Kagera kujionea madhara ya Vita ile afu leo mtu anakuambia Peleka nchi vitani, tena Eneo la Mapambano ni lilelile, hivi inaingia akilini kweli. Mimi Hapana. Tuwaambie hawa wanaoshabikia vita HAPANA. Serikali iwe makini na watu hawa ni hatari kwa Ustawi wa Taifa letu
 
Watu wa Mkoawa Kagera nafikir kwa sasa hawahitaj Vita,napenda pia kuwataarifu watu wengine kuwa hata huo ukimwi uliathiri kikamirifu Mkoa huo kiuchumi,chanzo chake ni vita hivyo,kwana Wanajeshi ndiyo waliyouingiza Tanzania(Wanajeshi wa Tanzania waliyokuwa vitani),sijui kama mnajua hilo?Kwa sasa mkoa unajipanga ki Uchumi.Pili lazima magazeti yazingatie kuandika mambo yasiyokuwa ya kichochezi,vita si vizuri.Tatu angalia nchi tunazozita ndugu kama Kenya inachukua nafasi ya kuendesha siasa za Biashara kwa kupitisha maneno na kukoleza mgogoro ili Rwanda itumie bandari yake.
 
Gulit, Inawezekana kuwa hujaiona Point kwa sababu hujatembea ndani ya Mistari ya Mada au pengine sijaandika kwa namna inayokufurahisha wewe na pengine wewe ni Mmojawao Marafiki wa Mashaka. Ila kwa kifupi ni kuwa VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA. Njoo na hoja
 
khaa!! kumbe akili yako fupi sana. Vita huwa na sababu. Kwa akili yako unataka hata kama Rwanda wakituhit (kwani hadi sasa wanasubiria wapate fursa ya kulitekeleza hilo) basi tukae tu tukiwaimbia "eibala libi liita nyinalyo" huku tukiwapigia makofi na kuwashangilia?? Hili jingine angalau unajua kama waathirika wa kwanza wa uhamiaji haramu ni watu wa Kagera. JK hana cha kuzungumza na PK alitoa ushauri wake tu basi kuufuata au kuuacha ni haki yake PK :bored:

duh, kama unafamilia ina kaz kwel.
Leo hii Watanzania tunakosa huduma muhimu tukiwa na aman sasa tukiingia vitan itakuwaje? Vita ni very expensive interms of social and economic sectors. Unavyo onekana hili hulijui.
Vita ya kagera imechangia sana kutuporomosha kiuchumi na hadi sasa hatujarecover hayo majeraha wewe na wapuuz wenzako mnawaza vita.

Kagame hajatuvamia na hakituvamia tuna haki ya kumpiga ila kwa sasa hamna sababu ya kuingia vitan na kagame.

Kagame tushamjua ni mwendawazimu jibu zur ni kumpuuza na kulinda mipaka yetu ila huku kuendelea kujibizana nae ni sawa na kupiga sarakas tukiwa tumejifunga taulo ukilinganisha na status ya Tz dunian.

We rohombaya na blood sucker wenzako kama Jk alitoa ushaur kwa moyo mmoja kwa kagame aongee na waasi ili aman ipatikane why don't exercise that strategy with Rwanda so as to keep peace in our region?
 
Ndugu wana JF. Salaam kwenu


....'Tumevamiwa; Mwendawazimu ametuvamia, sasa tutampiga. Nia ya kumpiga tunayo, Uwezo wa kumpiga tunao na sababu ya kumpiga tunayo'.

Ndugu, hayo yalikuwa ni maneno mazito ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa tayari kuingia vitani dhidi ya Nduli Iddi Amin 'Dada'. Nimeikumbuka kauli hii baada ya takribani siku kadhaa kuwa zimepita tunaendelea kusikia Chokochoko za Wasioitakia mema Tanzania kutaka Vita na Rwanda. Hili kwa mtazamo wangu halikubaliki kwa sababu zifuatazo;

Mosi; Tanzania haina sababu hata moja ya kuivamia Rwanda, hata moja nasisitiza. Hoja za walio wengi zimelenga katika CHUKI BINAFSI dhidi ya Kagame,,basi,,hakuna sababu nyingine. Mheshimiwa Rais Kikwete alitoa ushauri kwa Kagame na Kagame akajibu mbovu, basi. Inaishia hapo, sio sababu tosha ya kutufanya tuingie vitani. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mbili; Wengi na hasa wanaoshabikia Tanzania kutaka kuingia Vitani ni watu baki, hawana maslahi hata Chembe na Mkoa wa Kagera na hawajui hata Makaburi ya Wahaya waliofariki miaka ya 1978-1980 wakati wa Vita ya Kagera yakoje. Hawakuwahi KULIA hawa; hawakuwahi kumlilia mtu aliyekufa kwa risasi, wamezoea kulilia watu wanaokufa kwa magonjwa ya kawaida. Kabla hawajaanza kushabikia mimi naita UWENDAWAZIMU huu watembee Makaburi ya Wahaya waliokufa katika Vita ya Kagera, hakika wataacha ushabiki usiokuwa na msingi. VITA YA UGANDA SAWA...VITA NA RWANDA HAPANA.

Tatu; Kiuchumi moja kati ya Mikoa iliyokuwa inaendelea kwa kasi ya ajabu baada ya kupata Uhuru ilikuwa ni Mkoa wa Kagera, baada ya Vita ya Uganda kila kitu kilienda SHAGHALABAGHALA. Unajua kwa nini? Sababu nguvu kazi kubwa (Vijana) iliuawa katika vita na wengine kukimbia makazi yao. Wala Serikali haikuwahi kufanya Juhudi Binafsi kuupa kipaumbele Mkoa wa Kagera kwa sababu ya madhara yaliyopatikana kutokana na vita hiyo. Katika vita hiyo kulikuwa na kujitolea kwingi lakini kwa sababu ya Vita yenyewe uwanja wa vita ilikuwa ni Kagera, Wahaya wengi ndio waliojitokeza. Maana ya hili ni kwamba, Endapo Serikali itataka kukidhi MIHEMKO ya WAJINGA wachache wanaopenda vita, bado Uwanja wa Vita Utakuwa Kagera. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Nne, Vifo,,Enyi mashabiki wa vita na Rwanda, jamani mnataka tena Bibi, Babu, Kaka, Dada, Shangazi, Wajomba na wadogo zetu wauawe?. Ndiyo furaha yenu? Tuambieni? Msitukumbushe mbali, msitukumbushe vilio, Simanzi na majonzi. Hapana, tunasema HAPANA. Nyie waandishi msiokuwa na Ndugu huko Bukoba mtuachie Ndugu zetu waishi maana nao wanayo haki ya kuishi kama mlivyo nyie katika maofisi yenu huko Dar es Salaam. Yaani mnaamini kuwa itakuwa ni sisi kuua tu bila kuuawa? Wahaya tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Tano, Mgawanyiko, ukijaribu kufuatilia kwa karibu unagundua kuwa kuna mgawanyiko Mkubwa sana kati ya wanaotaka vita na Rwanda na wale wasioitaka ambapo mimi naangukia katika kundi la pili. Hii kitu katika medani za vita, haiwezi kuifanya Tanzania kushinda Vita hiyo kama tunavyojitia moyo. Hakika tunajidanganya, tunafanya Propaganda za kitoto, tunacheza ngoma tukiwa uchi, tuache Ujinga. Tuache kabisa kuwaogopesha Wananchi wetu kwa maslahi ya Damu za Wahaya, Hapana hatutakubali. Wahaya kwa mara nyingine tunasema na kusisitiza VITA YA UGANDA SAWA,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mwisho, Sababu kubwa iliyotufanya tuingie Vitani na Uganda wakati huo ni Uvamizi wa Ghafla uliokuwa umefanywa na Iddi Amin kwa Tanzania akitaka kuichukua Ardhi ya Kagera. Naamini hii ni sababu kubwa sana ndio maana Mwalimu alimuita Iddi Amin MWENDAWAZIMU maana ni Mwendawazimu pekee anayeweza kuingia Nyumbani kwako, akataka kuingia hadi jikoni na hatimaye Chumbani baadaye kabatini na uvunguni. Je Rwanda na Kagame wamefanya nini?.. Kuichukua Ardhi ya Kagera kulimaanisha kuwafanya Wahaya wawe Sehemu ya Uganda, Kufanya Visiwa karibu 27 vilivyo Ziwa Victoria upande wa Kagera viwe Upande wa Uganda, Ndizi nzuri zote unazozijua Tanzania ziwe Upande wa Uganda; kiukweli hili lilikuwa halikubaliki, ndio maana tukatengeneza NIA na SABABU baada ya kuongezewa UWEZO kutoka RUSSIA. Kwa sasa Rwanda na Kagame wao hawajatukosea kitu na kwa hiyo tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Ushauri, Wale wote wanaoshabikia vita na Rwanda hasa kwa wakati huu, wangejikita zaidi katika kuhakikisha Tunajenga Uzalendo miongoni mwa Watanzania ili kuwa na Maendeleo endelevu na pia kuipenda nchi yao. Tumshauri Mheshimiwa Rais atimize wajibu wake wa Kuwaletea Watanzania Maendeleo badala ya kuja na WISH WASH ideas. Tujikite katika kuhakikisha tunakuwa na Katiba bora itakayotupa Mwelekeo Mzuri wa Taifa letu. Tumwambie Mheshimiwa Rais na washauri wake Wapeleke Huduma za Jamii kama Hospitali, Shule, Maji, Barabara kule vijijini ambapo hawajui hata Mpaka wa Tanzania na Rwanda ukoje. Tuwaambie Wabunge wajali maslahi ya Wananchi, watimize ahadi zao. Tukifanya hivyo hakika tutafika.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI KAGERA (BUKOBA)
Bila shaka wewe ni muhamiaji haramu......Rais kasema hatuna mpango wa kuivamia nchi yeyote kwa hiyo Rwanda wakiingia kwetu tucheke nao tu.....au hii operation ya kuwarudisha kwenu inawachanganya.....????
 
Mkuu unafaa kuwa kiongozi kabisaaaaaaa.wewe una hekima na busara.wewe ukiona mtu anaangalia matokeo ya vita.Hujue huyu mtu ana busara.vita sio ya siku moja kama tunavyofikiri.tumeona kule iraq,vietnam.Jamani siku hizi watu ni technology kama mkuu alivyoeleza hapo juu.Tujifunze kujenga na sio kuchochea kwa manufaa ya watoto wetu wanaokuja.Chuki tunayopandikiza sasa inaota miziz kwa kasi ya ajabu sana kwa hawa ndugu zetu,majirani wetu Rwanda.Jamani kweli watu wazima mkuu wapo hapa great thinkers website na wanaongea wana mtazamo mfupi ki akili.Vita kama unavyosema mkuu tunacheza na maisha ya ndugu zetu [wazee,watoto,akina mama].wengine kutembea hawawezi na vitu vya kuwabeba na kuwahamisha hamisha hakuna ,kwani kila mtu atakuwa anaokoa roho yake tu.Mungu hatuepushe na hili shetani la vita ambalo watu wachache wanalipenda.
 
Watu wa Mkoawa Kagera nafikir kwa sasa hawahitaj Vita,napenda pia kuwataarifu watu wengine kuwa hata huo ukimwi uliathiri kikamirifu Mkoa huo kiuchumi,chanzo chake ni vita hivyo,kwana Wanajeshi ndiyo waliyouingiza Tanzania(Wanajeshi wa Tanzania waliyokuwa vitani),sijui kama mnajua hilo?Kwa sasa mkoa unajipanga ki Uchumi.Pili lazima magazeti yazingatie kuandika mambo yasiyokuwa ya kichochezi,vita si vizuri.Tatu angalia nchi tunazozita ndugu kama Kenya inachukua nafasi ya kuendesha siasa za Biashara kwa kupitisha maneno na kukoleza mgogoro ili Rwanda itumie bandari yake.

MTU WA NJIA HII, Ni kweli kabisa watu wa Mkoa wa Kagera hawapendi vita ila kuna watu wachache nje ya Mkoa wa Kagera ambao wangependa kuona Mkoa ukianza tena kudidimia kwa kuondokewa na Nguvu kazi, maana ndio utakuwa uwanja wa Vita. Eti wanajivika Kilemba Cha Uzalendo, Uzalendo gani kwa kuwaona wenzako wanakufa na wewe Ukiwa Katika Runinga unaangalia Makombora yanavyorushwa na kuua Raia?..Hawa ndio tunaowambia kuwa VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA
 
Bila shaka wewe ni muhamiaji haramu......Rais kasema hatuna mpango wa kuivamia nchi yeyote kwa hiyo Rwanda wakiingia kwetu tucheke nao tu.....au hii operation ya kuwarudisha kwenu inawachanganya.....????

Chisango, Natambua kuwa Mheshiwa Rais keshasema hivyo, na andishi langu halikumlenga Mheshimiwa Rais, linajaribu kuwaonesha watu wanaoendelea KUCHAGIZA vita, hata baada ya Mheshimiwa Rais kusema kuwa hatuna sababu ya kuwa na Vita sio kitu cha kushabikia kama wafanyavyo hao wapenda vita pengine labda na wewe ni miongoni mwao. Hata Tamko la Mkuu wa Nchi bado wanaendelea kulijadiri tena kwa namna ya hatari. Mkuu inawezekana mimi nikawa raia mzuri tu pengine kukuzidi wewe unayekimbilia kutaka kuniita Mkimbizi. No matter what, vita hapana Chisango
 
Mkuu WA-UKENYENGE, Sikupenda kabisa kuanzisha hii mada, imenibidi baada ya kuona kila uchao kuna Watanzania wenzetu wachache wanachagiza ili tuone Umuhimu wa Vita. This is Crazy, nikaona ni vema nitoe ya Moyoni wasije wakadhani tuko nyuma yao. Sure ni lazima tuwe na sababu za kutosha kuingia vitani. Ni upuuzi usiokuwa kifani Kuanza kujadili habari za Bahima na kuchomekea habari za kutaka vita.

Binafsi naamini sana katika kukaa kimya hasa katika masuala kama haya maana kuyaongea ndo kunaongeza zaidi Attention na wakati mwingine katika kuongea mtu usipokuwa makini unajichanganya. To be Frank after this I won't talk anymore on this issue. Ila ujumbe umewafikia wote Wachombezaji, wapenda vita wasiokuwa na Ndugu. Na nawaambia kamwe hila zao hazitafanikiwa. WE ARE FED UP. Wanaandika ili vita ikianza walipoti na hivyo kupata Faida katika kuuza habari. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA

Mkuu,

Mjadara huu ulipoanza nilikasilishwa na mods na nikajifungia siku 10. Nilikuwa nimechukia sana nilipogundua watu wanashabikia vita kwa mwanvuri wa 'uzalendo'. Nilipojifungua ni kakuta mjadara ndo umepamba moto zaidi. Nimejitahidi kuwaeleza kama ulivyofanya, na ninafikiri watake wasitake wakuu wa nchi hii waiskilize sauti ya waishio Kagera. Kinyume na hapo vita ipelekwe huko waishiko sio Kagera.
 
je ni kweli Amini alikuwa wa kwanza kuvamia Tanzania? soma hapa chini ujue kile wengi hamjui
wEGQeAKmFYL9wAAAABJRU5ErkJggg==
 
Kweli kabisa ndugu! Vita vya kiuchumi vinatutesa sasa vya bunduki si itakuwa majanga!hapana kabisa!


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Wala serikali ya Tz haijatangaza vita na Rwanda! Acha woga ndugu yangu! Kama itabidi Rwanda tutaidunda! Pia ni dhana potofu kufikiri kuwa ni wahaya pekee ndo walikufa katika vita ya Kagera! Ni Watanzania wote walishiriki katika vita hiyo! Acha woga!

Jaribu kumwelewa mleta mada. He must be right.
 
[h=2]Events leading to the war[edit source | editbeta][/h]Relations between Tanzania and Uganda had been strained for several years before the war started. After Amin seized power in a military coup in 1971, the Tanzanian leader Julius Nyerere offered sanctuary to Uganda's ousted president, Milton Obote. Obote was joined by 20,000 refugees fleeing Amin's attempts to wipe out opposition. A year later, a group of exiles based in Tanzania attempted, unsuccessfully, to invade Uganda and remove Amin. Amin blamed Nyerere for backing and arming his enemies. The relationship between Uganda and Tanzania remained strained for many years.In early October 1978, dissident troops ambushed Amin at the presidential lodge in Kampala, but he escaped with his family in a helicopter.[SUP][3][/SUP] This was during a period when the number of Amin's close associates had shrunk significantly, and he faced increasing dissent from within Uganda. When General Mustafa Adrisi, Amin's Vice President, was injured in a suspicious car accident, troops loyal to Adrisi (and other soldiers who were disgruntled for other reasons) mutinied. Amin sent troops against the mutineers (which included members of the elite Simba Battalion), some of whom had fled across the Tanzanian border.[SUP][1][/SUP][SUP][3][/SUP] The rebellion spilled over into Tanzania, where Tanzania-based anti-Amin exiles joined the fighting against Amin's troops.Uganda declared a state of war against Tanzania, and sent troops to invade and annex part of the Kagera region of Tanzania, which Amin claimed belonged to Uganda.

JE NI KWELI KUWA AMINI ALIANZISHA VITA? TAFUTA KUJUA ZAIDI , MITANDAO IKO WAZI KWA WOTE , HII NI SEHEMU NDOGO TU YA HABARI YENYEWE
 
Back
Top Bottom