Vita ya Uganda sawa.....Rwanda hapana...Kagera tunasema hapana

Vita ya Uganda sawa.....Rwanda hapana...Kagera tunasema hapana

Mkuu,

Mjadara huu ulipoanza nilikasilishwa na mods na nikajifungia siku 10. Nilikuwa nimechukia sana nilipogundua watu wanashabikia vita kwa mwanvuri wa 'uzalendo'. Nilipojifungua ni kakuta mjadara ndo umepamba moto zaidi. Nimejitahidi kuwaeleza kama ulivyofanya, na ninafikiri watake wasitake wakuu wa nchi hii waiskilize sauti ya waishio Kagera. Kinyume na hapo vita ipelekwe huko waishiko sio Kagera.

Mkuu Mutakyamirwa, Naamini kwa dhati hawa mashabiki, wapambe wa vita wataisikia Sauti hii ya Watanzania. Binafsi nilifanya hivyo pia kumbe ulikuwa ni mwanya wa hawa jamaa kuendelea na UASI na UCHOCHEZI wao. Kamwe Serikali isiingie Mkenge. Wana Ajenda yao hao. Wana Kagera wanataka kuchapa kazi. Majanga ya Mv. Bukoba, Vita na Uganda, UKIMWI vyote vilihusisha vifo na hivyo kupunguza Nguvu kazi ya Taifa na Mkoa wa Kagera kwa Ujumla. Sasa nyie Blood Suckers mnataka nini tena jamani? Mbona yako mengi ya kuandika? Wagonjwa wanakufa mahospitalini, watoto wanasomea chini ya miti? hakuna walimu wa kutosha?bidhaa muhimu bei juu, Wauza Madawa ya kulevya kibao? Utoroshaji wa fedha nje ya nchi ndo usiseme? yaani mmeona KUCHAGIZA vita tu. HAKIKA NI WA KUPUUZWA
 
Ni kweli hata mie sipendi vita kabisa. Ila PK na watu wake wanaropoka ovyo, wako provocative sana.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
halafu kule Rwanda ili ujue yuko kivita zaidi kimaandalizi nasikia kila jengo refu keshaweka vifaa vya kutungulia ndege, njia zote za kwenda nyumbani kwake zimewekwa miiba. Sasa hivi mtanzania ukipata shida bahati mbaya imekukutia Rwanda usitegemee kabisa kupata msaada unaohitajika hata kama utakwenda polisi sanasana watakuchania hato document zako watakazohitaji kama vielelezo. Ndio ujue mioyo ya watu wa visasi ilivyo migumu hata akikuchekea.
 
Events leading to the war[edit source | editbeta]

Relations between Tanzania and Uganda had been strained for several years before the war started. After Amin seized power in a military coup in 1971, the Tanzanian leader Julius Nyerere offered sanctuary to Uganda's ousted president, Milton Obote. Obote was joined by 20,000 refugees fleeing Amin's attempts to wipe out opposition. A year later, a group of exiles based in Tanzania attempted, unsuccessfully, to invade Uganda and remove Amin. Amin blamed Nyerere for backing and arming his enemies. The relationship between Uganda and Tanzania remained strained for many years.In early October 1978, dissident troops ambushed Amin at the presidential lodge in Kampala, but he escaped with his family in a helicopter.[SUP][3][/SUP] This was during a period when the number of Amin's close associates had shrunk significantly, and he faced increasing dissent from within Uganda. When General Mustafa Adrisi, Amin's Vice President, was injured in a suspicious car accident, troops loyal to Adrisi (and other soldiers who were disgruntled for other reasons) mutinied. Amin sent troops against the mutineers (which included members of the elite Simba Battalion), some of whom had fled across the Tanzanian border.[SUP][1][/SUP][SUP][3][/SUP] The rebellion spilled over into Tanzania, where Tanzania-based anti-Amin exiles joined the fighting against Amin's troops.Uganda declared a state of war against Tanzania, and sent troops to invade and annex part of the Kagera region of Tanzania, which Amin claimed belonged to Uganda.

JE NI KWELI KUWA AMINI ALIANZISHA VITA? TAFUTA KUJUA ZAIDI , MITANDAO IKO WAZI KWA WOTE , HII NI SEHEMU NDOGO TU YA HABARI YENYEWE

WAKABAMBEE, Hiyo kitu nilishaisoma siku nyingi mno. I have it in ma head. Strongly nasema Nduli Idd Amin 'Dada' alivamia Ardhi ya Tanzania na hilo andiko linasema. Hilo ndio lilikuwa kosa lake, aliingizwa katika Mtego akategeka na hivyo akachakazwa, Ilikuwa ni haki ya Mwalimu kumuondoa na kisha kumuadhibu, hata hivyo the Story is Contrary to this Issue and I take it as History. Hoja yangu nimeijenga kwa wapenda vita ingawa wewe kimsingi pia hukupenda Uchokozi wa Tanzania kwa Uganda that time. Na mimi sipendi tuwe wachokozi
 
Ntagunga, Ndio maana nilikaa kimya kwa muda mrefu sana ila kinachoonekana ni kila kukicha Baadhi ya watu wanachochea Tanzania kuipiga Rwanda,,,Sijui wengine wameandika Safari ya Goma iishie Kigali..... Watu kama hao tusipowaambia kwamba HATUTAKI VITA wataendelea kuandika na kuzidi kuwa OGOFYA wananchi. Ni lazima tukemee hili. VITA NA RWANDA HAIKUBALIKI KATU

Nakuunga mkono. Vita na Rwanda haikubaliki ng'o. Tushughulike na kuinua uchumi na elimu ya watoto wetu na siyo vita. Vita huwa havina mshindi. Hata kama tukisema tulimshinda Nduli Idd Amin Dada bado tuliathirika sana kiuchumi na sidhani kama tumesha-stabilize tangu wakati ule. Tukatae vita kwa sababu yo yote ile.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
halafu kule Rwanda ili ujue yuko kivita zaidi kimaandalizi nasikia kila jengo refu keshaweka vifaa vya kutungulia ndege, njia zote za kwenda nyumbani kwake zimewekwa miiba. Sasa hivi mtanzania ukipata shida bahati mbaya imekukutia Rwanda usitegemee kabisa kupata msaada unaohitajika hata kama utakwenda polisi sanasana watakuchania hato document zako watakazohitaji kama vielelezo. Ndio ujue mioyo ya watu wa visasi ilivyo migumu hata akikuchekea.

Rubi, Hicho ndicho kinachotuponza Watanzania na pengine Wanyarwanda walio nchini mwao, KUSIKIA...Kuna Wanyarwanda pia wanaamini Wanyarwanda wakija Tanzania wananyanyaswa. Sasa wewe Rubi kama Mtanzania hebu tujadili hapa umesikia wapi kesi ya Mnyarwanda kunyanyaswa hapa Tanzania?. Kama hakuna then It is the same Story kwa Watanzania huko Rwanda. Yaani ni kukuza tuu mambo mradi wafanikishe mambo yao.

Kuongea ni Hulka ya Mtu ndio maana Wakenya wakienda Dukani wanasema NATAKA kilo moja ya Sukari wakati Mtanzania akienda atasema Naomba Kilo moja ya Sukari, ila wote wanachotaka ni kuhudumiwa. Tuache UMIMI, Tuache UBINAFSI
 
Ni kweli hata mie sipendi vita kabisa. Ila PK na watu wake wanaropoka ovyo, wako provocative sana.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

mbona hueleweki so kama wanaropoka ndo wanyaamazishwe kwa vita? nyani wale wadogo wakiona msitu unaungua hukaa juu ya mawe ng'ambo na kuchekelea bila kujua kama hayo ni makazi yao.....roho zenu za chki zishindwe kwa jina la yesu...we nani kumchukia binadam mwenzako...kagame na wanyarwanda walifanya nini hadi uwachukie hivo?unapoteza muda kushabikia ujinga wakati ni mlala hoi wa kawaida tu utakachoambulia ni njaa,hakuna madawa,shule ndo hivo mwisho za kata ila manufaa ya vita kama yapo hutanusa ng'o.....vita unayostahili kupigana kwa gharama yoyote ni ile ya madawa ya kulevya ufisadi na civic education...hiyo ndo vita ya mtz
 
Nakuunga mkono. Vita na Rwanda haikubaliki ng'o. Tushughulike na kuinua uchumi na elimu ya watoto wetu na siyo vita. Vita huwa havina mshindi. Hata kama tukisema tulimshinda Nduli Idd Amin Dada bado tuliathirika sana kiuchumi na sidhani kama tumesha-stabilize tangu wakati ule. Tukatae vita kwa sababu yo yote ile.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

Mkuu Kinauche, Nakushukuru, huu ni muda wa kuijenga nchi yetu sio Propaganda zisizo kuwa na kichwa wala miguu. Hao wapenda vita tuwashauri wabadili muelekeo. VITA HAILIPI kwa Tanzania. It only pays to US,UK,France, Russia na ni kwa sababu wanapata mwanya wa kuuza siraha na kamwe wasingependa itokee katika nchi zao. Blood Suckers andikeni Articles za Kuhusu Katiba Mpya ya Kuwasaidia Watanzania miaka 50 au pengine hata 100 ijayo sio kushabikia vita.
 
Wanaotaka vita hivi ni CCM ili wapate kisingizio kuwa tumeshindwa kuwapa maisha bora kwa kila Mtanzania kwa sababu tulichokozwa tukapigana vita. Hivyo hakuna kitu tena tuna kofia na khanga na wali mkavu tu. Tuchagueni tena muone furaha ya kushinda vita jamanie.....???
 
mbona hueleweki so kama wanaropoka ndo wanyaamazishwe kwa vita? nyani wale wadogo wakiona msitu unaungua hukaa juu ya mawe ng'ambo na kuchekelea bila kujua kama hayo ni makazi yao.....roho zenu za chki zishindwe kwa jina la yesu...we nani kumchukia binadam mwenzako...kagame na wanyarwanda walifanya nini hadi uwachukie hivo?unapoteza muda kushabikia ujinga wakati ni mlala hoi wa kawaida tu utakachoambulia ni njaa,hakuna madawa,shule ndo hivo mwisho za kata ila manufaa ya vita kama yapo hutanusa ng'o.....vita unayostahili kupigana kwa gharama yoyote ni ile ya madawa ya kulevya ufisadi na civic education...hiyo ndo vita ya mtz

Ruzibiza, Wasamehe bure ila naamini Serikali pia watu wanaoichochea inawaona. Watu hawa ni ajabu kwelikweli they like Human Blood, sijui kwa nini. Ingawa naamini ni kwa sababu Ndugu, Jamaa na Marafiki zao hawataathirika kwa namna yoyote. TUWAKEMEE, na vyombo vya dola viwaonye
 
Wanaotaka vita hivi ni CCM ili wapate kisingizio kuwa tumeshindwa kuwapa maisha bora kwa kila Mtanzania kwa sababu tulichokozwa tukapigana vita. Hivyo hakuna kitu tena tuna kofia na khanga na wali mkavu tu. Tuchagueni tena muone furaha ya kushinda vita jamanie.....???

mgt software. Vita ikianza hakuna CCM, hakuna CHADEMA, hakuna CUF wala baba yake na NCCR, TLP wala UDP. Na kwa taarifa sio kwamba tutakuwa na uhakika wa kushinda. Ni vema kama kuna hizo NOTIONS basi vyama vyote bila kujali Itikadi vikakemea hawa watu wachache wasituingize katika Vita isiyo na kiuno wala kiwiliwili. HATUTAKI
 
na mie sitaki vita kabisa maana nguvu ilitumika Kagera iliharibu kila kitu, wenye magari makubwa kama Kugis, na wengine waliathilika sana maana magari yao yalikuwa yakikamatwa na kuamlisha kupeleka vikozi uwanja wa vita, wahindi wote waliondoka na mali nyingi, BCU ilifilisika kutokana na kugawa magari na pesa kwa ajiri ya vita. Kiwanda cha sukari na majani ya chai yaliaribiwa. Mifugo ilikosa madawa ikafa. Kwa kweli kilikuwa kilio cha kusaga meno na pia ndio ulikuwa mwisho wa usomi kwa wahaya, maana shule nyingi zilifungwa walimu walipelekwa kupigana.
 
Its true kwamba vita sio nzuri hata mimi sikubalian nalo ila rais anapaswa kuwa makini katka maamuz juu ya hili,maana siku zoye anaemaliza huwa anaonekana sie alienza!
 
Ndugu wana JF. Salaam kwenu


....'Tumevamiwa; Mwendawazimu ametuvamia, sasa tutampiga. Nia ya kumpiga tunayo, Uwezo wa kumpiga tunao na sababu ya kumpiga tunayo'.

Ndugu, hayo yalikuwa ni maneno mazito ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa tayari kuingia vitani dhidi ya Nduli Iddi Amin 'Dada'. Nimeikumbuka kauli hii baada ya takribani siku kadhaa kuwa zimepita tunaendelea kusikia Chokochoko za Wasioitakia mema Tanzania kutaka Vita na Rwanda. Hili kwa mtazamo wangu halikubaliki kwa sababu zifuatazo;

Mosi; Tanzania haina sababu hata moja ya kuivamia Rwanda, hata moja nasisitiza. Hoja za walio wengi zimelenga katika CHUKI BINAFSI dhidi ya Kagame,,basi,,hakuna sababu nyingine. Mheshimiwa Rais Kikwete alitoa ushauri kwa Kagame na Kagame akajibu mbovu, basi. Inaishia hapo, sio sababu tosha ya kutufanya tuingie vitani. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mbili; Wengi na hasa wanaoshabikia Tanzania kutaka kuingia Vitani ni watu baki, hawana maslahi hata Chembe na Mkoa wa Kagera na hawajui hata Makaburi ya Wahaya waliofariki miaka ya 1978-1980 wakati wa Vita ya Kagera yakoje. Hawakuwahi KULIA hawa; hawakuwahi kumlilia mtu aliyekufa kwa risasi, wamezoea kulilia watu wanaokufa kwa magonjwa ya kawaida. Kabla hawajaanza kushabikia mimi naita UWENDAWAZIMU huu watembee Makaburi ya Wahaya waliokufa katika Vita ya Kagera, hakika wataacha ushabiki usiokuwa na msingi. VITA YA UGANDA SAWA...VITA NA RWANDA HAPANA.

Tatu; Kiuchumi moja kati ya Mikoa iliyokuwa inaendelea kwa kasi ya ajabu baada ya kupata Uhuru ilikuwa ni Mkoa wa Kagera, baada ya Vita ya Uganda kila kitu kilienda SHAGHALABAGHALA. Unajua kwa nini? Sababu nguvu kazi kubwa (Vijana) iliuawa katika vita na wengine kukimbia makazi yao. Wala Serikali haikuwahi kufanya Juhudi Binafsi kuupa kipaumbele Mkoa wa Kagera kwa sababu ya madhara yaliyopatikana kutokana na vita hiyo. Katika vita hiyo kulikuwa na kujitolea kwingi lakini kwa sababu ya Vita yenyewe uwanja wa vita ilikuwa ni Kagera, Wahaya wengi ndio waliojitokeza. Maana ya hili ni kwamba, Endapo Serikali itataka kukidhi MIHEMKO ya WAJINGA wachache wanaopenda vita, bado Uwanja wa Vita Utakuwa Kagera. VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Nne, Vifo,,Enyi mashabiki wa vita na Rwanda, jamani mnataka tena Bibi, Babu, Kaka, Dada, Shangazi, Wajomba na wadogo zetu wauawe?. Ndiyo furaha yenu? Tuambieni? Msitukumbushe mbali, msitukumbushe vilio, Simanzi na majonzi. Hapana, tunasema HAPANA. Nyie waandishi msiokuwa na Ndugu huko Bukoba mtuachie Ndugu zetu waishi maana nao wanayo haki ya kuishi kama mlivyo nyie katika maofisi yenu huko Dar es Salaam. Yaani mnaamini kuwa itakuwa ni sisi kuua tu bila kuuawa? Wahaya tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Tano, Mgawanyiko, ukijaribu kufuatilia kwa karibu unagundua kuwa kuna mgawanyiko Mkubwa sana kati ya wanaotaka vita na Rwanda na wale wasioitaka ambapo mimi naangukia katika kundi la pili. Hii kitu katika medani za vita, haiwezi kuifanya Tanzania kushinda Vita hiyo kama tunavyojitia moyo. Hakika tunajidanganya, tunafanya Propaganda za kitoto, tunacheza ngoma tukiwa uchi, tuache Ujinga. Tuache kabisa kuwaogopesha Wananchi wetu kwa maslahi ya Damu za Wahaya, Hapana hatutakubali. Wahaya kwa mara nyingine tunasema na kusisitiza VITA YA UGANDA SAWA,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Mwisho, Sababu kubwa iliyotufanya tuingie Vitani na Uganda wakati huo ni Uvamizi wa Ghafla uliokuwa umefanywa na Iddi Amin kwa Tanzania akitaka kuichukua Ardhi ya Kagera. Naamini hii ni sababu kubwa sana ndio maana Mwalimu alimuita Iddi Amin MWENDAWAZIMU maana ni Mwendawazimu pekee anayeweza kuingia Nyumbani kwako, akataka kuingia hadi jikoni na hatimaye Chumbani baadaye kabatini na uvunguni. Je Rwanda na Kagame wamefanya nini?.. Kuichukua Ardhi ya Kagera kulimaanisha kuwafanya Wahaya wawe Sehemu ya Uganda, Kufanya Visiwa karibu 27 vilivyo Ziwa Victoria upande wa Kagera viwe Upande wa Uganda, Ndizi nzuri zote unazozijua Tanzania ziwe Upande wa Uganda; kiukweli hili lilikuwa halikubaliki, ndio maana tukatengeneza NIA na SABABU baada ya kuongezewa UWEZO kutoka RUSSIA. Kwa sasa Rwanda na Kagame wao hawajatukosea kitu na kwa hiyo tunasema VITA YA UGANDA SAWA,,,VITA NA RWANDA HAPANA.

Ushauri, Wale wote wanaoshabikia vita na Rwanda hasa kwa wakati huu, wangejikita zaidi katika kuhakikisha Tunajenga Uzalendo miongoni mwa Watanzania ili kuwa na Maendeleo endelevu na pia kuipenda nchi yao. Tumshauri Mheshimiwa Rais atimize wajibu wake wa Kuwaletea Watanzania Maendeleo badala ya kuja na WISH WASH ideas. Tujikite katika kuhakikisha tunakuwa na Katiba bora itakayotupa Mwelekeo Mzuri wa Taifa letu. Tumwambie Mheshimiwa Rais na washauri wake Wapeleke Huduma za Jamii kama Hospitali, Shule, Maji, Barabara kule vijijini ambapo hawajui hata Mpaka wa Tanzania na Rwanda ukoje. Tuwaambie Wabunge wajali maslahi ya Wananchi, watimize ahadi zao. Tukifanya hivyo hakika tutafika.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI KAGERA (BUKOBA)
Hivi kwa historia ya mtu kama Kagame akikuambia ataku-hit, unadhani anamaanisha nini?
 
Wacha uwoga kwanza waliokufa siyo wahaya tu kwa taarifa yako, yale makaburi 619 yaliyopo Kaboya sijui Kyaka ni ya Watanzania kutoka mikoa yote ya Tanzania bara na visiwani.Tukichokozwa tutampiga PK maana nia ya kumpiga tutakuwa nayo, sababu ya kumpiga tutakuwa nayo na uwezo wa kumpiga mpaka navosema sasa hivi saa tano usiku huu tunao tena kwa 100%
 
Rubi, Hicho ndicho kinachotuponza Watanzania na pengine Wanyarwanda walio nchini mwao, KUSIKIA...Kuna Wanyarwanda pia wanaamini Wanyarwanda wakija Tanzania wananyanyaswa. Sasa wewe Rubi kama Mtanzania hebu tujadili hapa umesikia wapi kesi ya Mnyarwanda kunyanyaswa hapa Tanzania?. Kama hakuna then It is the same Story kwa Watanzania huko Rwanda. Yaani ni kukuza tuu mambo mradi wafanikishe mambo yao.

Kuongea ni Hulka ya Mtu ndio maana Wakenya wakienda Dukani wanasema NATAKA kilo moja ya Sukari wakati Mtanzania akienda atasema Naomba Kilo moja ya Sukari, ila wote wanachotaka ni kuhudumiwa. Tuache UMIMI, Tuache UBINAFSI
ndugu jaribu kutembelea rwanda uone kama hujawahi fika uone ili uamini uambiwacho. siku hizi si za zamni au jaribu kutafuta waTZ waliotoka rwanda hivi karibuni upate yanayojiri kivitendo sio kimacho.
 
Ushauri alioutoa JK kwa PK unaonyesha wazi jinsi rais wetu asivyopenda limwagike hata tone moja la damu ya mhanga mwingine wa ukanda wa maziwa makuu! Aliutoa ushauri huo ikiwa tayari askari wetu wakiwa tayari Kongo kuitikia wito wa UN. Aliutoa ushauri huo kama ni sehemu ya kuwajibika kwake kulinda maisha ya askari wetu na vilevile kuwapa nafasi wadau wengine (wanaojifichaficha) kusaidia ku'diffuse tense atmosphere' iliyokuwepo wakati huo! Rais wetu aliwajibika kikamilifu lakini wapenda vita wakaona KUTUTISHIA NYAU ni solution! Hamna mtu anaetaka vita Tanzania na wapenda vita halisi wameumbuka na wanaona haya!
 
Back
Top Bottom