Vita ya Urusi na Ukraine: Akili na malengo ya Putin nchini Ukraine

Vita ya Urusi na Ukraine: Akili na malengo ya Putin nchini Ukraine

Wengi wameziamini Propoganda dhaifu za Putin.

Urusi imepakana na nchi 5 sio 2 za NATO kwenye mpaka wa nchi kavu na Uturuki katika Black Sea.
Ngoja nikuulize, hii hofu ya Nato kwa Russia inatoka wapi? Je Nato amewahi kusema kwamba siku moja anataka aichukue Russia halafu ili iweje.

Ebu angalia mataifa mawili wanachama wa Nato kama Estonia na Latvia je hawajapakana na Russia? Kwa nini basi Russia haijawavamia kama walivyoivamia Ukraine ambayo bado hata haijawa mwanachama.?

Huyu Russia yeye nani kampa haki au uhalali wa kuyaamulia mataifa mengine mambo yao?
 
Wengi wameziamini Propoganda dhaifu za Putin.

Urusi imepakana na nchi 5 sio 2 za NATO kwenye mpaka wa nchi kavu na Uturuki katika Black Sea.
Anza kuusoma Uzi kuanzia mwanzo, maswali unayouliza au hoja unazozitoa zimejibiwa juu.

Kuuleta wakati uliyopita kwa wakati wa sasa ilihali kwa uliyopita ramani yake ilishawekwa wazi hayo ni mapungufu. Uhalali wa kuyaibua yaliyopita kwa nyakati ya sasa ni kuhoji ili fafanuzi zitolewe zaidi.

Usiturudishe nyuma tafadhali.
 
Wengi wameziamini Propoganda dhaifu za Putin.

Urusi imepakana na nchi 5 sio 2 za NATO kwenye mpaka wa nchi kavu na Uturuki katika Black Sea.
Sio kweli, hizo nchi zingine 3 za Nato zilizopakana na Russia nchi kavu ni zipi.
 
Nchi 6 zinazopakana na Russia ambazo tayari ziko NATO ni Norway, Estonia, Latvia, Lithuania, Poland na Uturuki.
Sio kweli, hizo nchi zingine 3 za Nato zilizopakana na Russia nchi kavu ni zipi.
 
Uturuki imepakana na Urusi kwenye Black Sea.

Kama Russia haitaki kuikali Ukraine lengo la mwisho la uvamizi wao ni nini?

Mwisho wa uvamizi wao ili uhasibike umefanikiwa wanataka watimize nini ndio waondoe majeshi yao Ukraine?
Ni kweli wana-share bahari, pia wana-share bahari na Ujerumani na Denmark.

Malengo yao yako wazi tu, wanataka Katiba ya Ukraine ibadilishwe ikubali na kuitambua Crimea ni sehemu ya Urusi, wanataka jamhuri za Donetsk na Lugansk kutambuliwa na Ukraine kuwa nchi huru, pia Ukraine ijitangaze kuwa nchi Neutral . Hayo yakitimia tutaona Urusi wanarudi nyumbani. Ila binafsi natilia shaka kama wataondoka maeneo ya kusini kwenye miji ya Mariupol, Berdyansk, Melitopol na Kherson.
 
Nijuze mkuu mipaka ya bahari huwekwa wapi?
Hapo sikukutajia kuwa wamepakana na Japan na Marekani kwa bahari.
Wamepakana wapi? Unajua mipaka ya bahari kati ya nchi inapowekwa?
 
Inasikitisha Sana mtu anaandika upupu na watu wanamshabikia anyway , mda utatupa majibu sahihi kama huyo Putin atawatisha NATO au watamfurumusha...!!
 
Hiyo ni sawa walikubaliana nato isijitanue lakini kwa dunia ya leo kila nchi ni huru inayo uwezo wa kuamua mambo yake bila kuingiliwa na nchi nyingine. Inachopigania ukrein ni uhuru wake wa kuamua mambo bila kuingiliwa na urusi. Kama vile urusi nayo inaamua mambo yake mwenyewe bila kuingiliwa na nchi nyingine. Mfano leo kenya na uganda wakea waamue Tanzania isijiunge na umoja fulani we unafikiri Tanzania itajisikia jee si ni bora waende vitani tuu ili wajue moja.
Kama ni hivo kwanini marekani anaweka kambi ya kijeshi kila nchi??
 

Ndio, Marekani(Jimbo la Alaska) limepakana na Russia kwa sababu umbali kati yao ni maili 55 tu na kwenye eneo la maji dogo kama hilo(maziwa na mito pia) mpaka unakuwa katikati ya maji. Huu mpaka wa Alaska na Russia hauzungumziwi sana kwa sababu ukiacha bahari bado kuna eneo kubwa la barafu lisilopitika na pia Alaska ni jimbo lilo mbali na lisilopakana kwa ardhi na jimbo lingine lolote la Marekani.

Russia imepakana na Japan bahrini na wamekuwa na migogoro ya kugombania visiwa kadhaa kati yao kwa muda mrefu.
Nijuze mkuu mipaka ya bahari huwekwa wapi?
Hapo sikukutajia kuwa wamepakana na Japan na Marekani kwa bahari.
 
Nchi 6 zinazopakana na Russia tayari ziko NATO, Hizo ni Norway, Estonia, Latvia, Lithuania, Poland na Uturuki.

Urusi akiweza kuikalia Ukraine kimabavu atakutana na nchi nyingine 5 za NATO

Sweden na Finland baada ya kuona uvamizi wa Ukraine na Georgia sasa zinafikiria kujiunga na NATO, kwa sababu ni wazi kama Ukraine isingechelewa kujiunga na NATO leo hii isengevamiwa.

Katika mazingira yote hayo hiyo buffer zone anayoitaka Russia iko wapi? Atavamia nchi zote zinazomzunguka na kuweka serikali ya kidekteta kama ya Belarus ili aweze kuipata hiyo buffer zone?
Tuelewane kidogo hii vita ni kama covid yaani dunia nzima tunateseka, kiufupi ni mwanzo wa anguko la marekani, Itafika hatua mkate utauzwa 5000 hapo watu tutasema kwa kejeli tu marekani kama super power huna msaada kwetu tupishe ndipo tutakapompokea Israel kwa shangwe atupoze.
 

Ndio, Marekani(Jimbo la Alaska) limepakana na Russia kwa sababu umbali kati yao ni maili 55 tu na kwenye eneo la maji dogo kama hilo(maziwa na mito pia) mpaka unakuwa katikati ya maji. Huu mpaka wa Alaska na Russia hauzungumziwi sana kwa sababu ukiacha bahari bado kuna eneo kubwa la barafu lisilopitika na pia Alaska ni jimbo lilo mbali na lisilopakana kwa ardhi na jimbo lingine lolote la Marekani.

Russia imepakana na Japan bahrini na wamekuwa na migogoro ya kugombania visiwa kadhaa kati yao kwa muda mrefu.
Umeeleza uzuri mkuu yoda, ila kama ingewezekana kueleza lwa mujibu wa sheria za kimataifa ingekuwa nzuri sana.
 
Na Jumaa Kilumbi,
Katika andiko hili fupi ningependa kutahadharisha kuwa hatutazungumza kiitikadi, kinafki wala kihisia, hatutazungumza mambo yanavyopaswa kuwa tutazungumza mambo yalivyo, tutazungumza kwa kuangalia ‘practical result’ na uhalisia tunaamini na tunafahamu dunia haiendeshwi kwa hisia bali kwa kanuni na misingi yenye kuleta matokeo.

VITA NI SEHEMU YA MAISHA YA MWANADAMU TANGU KALE
Vita zimekuwa ni sehemu ya maisha ya wanadamu tangu kale jamii zilikua zikivamiana kuibiana mifugo na mali na wakti mwingine kufanyana watumwa, Vita zimekuza himaya kubwa kuwahi kushuhudiwa duniani ikumbuke Dola ya Ugiriki, zimekuza chumi kubwa kumbuka uchumi wa Uingereza, zimeibua matajiri duniani unamkumbuka David Ricardo? Hivyo vita ni sehemu ya maendeleo ya mwanadamu ndio maana mpaka leo hata nchi zenye sera za ‘ki-pacifism’ bado wana kiwango fulani cha jeshi kuonesha hawapuuzi uwezekano wa vita maana ndio asili ya mwanadamu.
Ni muhimu kuelewa kuwa kwenye Vita zote kumekuwa na makundi ya aina mbili ya watu,

Moja, ni wale tunaowaita ‘Policy makers’ kundi hili wamo viongozi wa nchi wanaojua siri na misingi ya kuendesha nchi nawazungumzia Mawaziri, Waziri mkuu, Wakuu wa majeshi, wafalme na maRais wenyewe, hawa hawaongozwi kihisia, kwao nchi ndio kipaumbele chao, Usalama ndio hazina yao na watu ndio mitaji yao. Linapokuja suala la vita kundi hili litapinga au kuunga mkono kutokana na athari za vita hiyo kwa usalama wa nchi aidha ziwe hasi au chanya.

Kundi la pili, tunawaita ‘maamuma’ kundi hili lina watu wengi sana hapa wamo wananchi wa kawaida, viongozi wa dini na wote ambao hawako katika nafasi nyeti za nchi. Wao watapinga vita ikiwa wanaona watapata madhara moja kwa moja na misimamo yao inatengenezwa na ‘propaganda’ za serikali au vikundi vyenye ushawishi kwenye jamii, na wataunga mkono vita vilevile kutokana na ‘propaganda’ za watu za watu wenye ushawishi. Hawa hawaamini kuwa vita yaweza kuhalalishwa ila katika misingi ya kujilinda tu.

URUSI HAINA CHAGUO “DUMB IF THEY DUMB IF THEY DON’T”
Kama alivyowahi sema Jenerali na mwanamikamati wa Prussia Karl von Clausewitz “Vita ni muendelezo wa siasa katika namna nyingine”

Hii vita ya Ukraine na Urusi ni matokeo ya kushindwa kwa mazungumzo baina yao na nchi za Magharibi na Ukraine yenyewe. Ilipoanguka USSR miaka ya 1990 NATO waliihakikishia Urusi kuwa hawatojipanua wala kupokea wanachama wapya toka Ulaya mashariki ambapo Urusi huona ni kama kibarazani kwao. Moja ya kauli mashuhuri sana ni ile “Hata inchi moja mashariki” aliyoisema bwana James Baker (aliyekuwa katibu wa nchi wa Marekani). Ahadi zao zilikua ni maneno ya kilaghai kuwapumbaza Urusi huku wakijipatia ‘advantage’ kwa kufanya kinyume na ahadi zao.

NATO wamembana mbavu Putin, wamemuacha hana chaguo akiiacha Ukraine itajiunga NATO na akiivamia anawekewa vikwazo. Urusi hawataki NATO iwe kubwa, hawataki majirani zake wawe wanachama, hawataki kuona silaha na majeshi ya kigeni karibu na mipaka yao, hawataki kuona wanazingirwa kila pande. wanavyojisikia ni kama walivyojisikia Marekani mwaka 1962 walipowekewa nyuklia jirani kabisa pale Cuba, mpaka sasa NATO wameshawazunguka kwa upande wote wa magharibi wamebakisha Ukraine tu kumaliza mzunguko wao. Urusi wanajua hilo wamejipanga kuhakikisha kamwe halitokei na wanafanikiwa.

Madai haya ya Urusi yanawapa uhalali wa hii vita kimkakati japo vichwani mwa watu wengi kutokana na ushawishi mkubwa wa waMagharibi wanaona Urusi ni wagomvi wasio na huruma. Urusi itakua hatarini kama wataacha mambo yaende kama yalivyo, japo awali walijaribu Diplomasia kwa miaka zaidi ya 20 imeshindikana sasa ni wakti wa kutumia mabavu.

Kwenye siasa za kimataifa hii ni kawaida diplomasia inaposhindikana nguvu huwezekana, Marekani ya leo iliundwa baada ya Vita dhidi ya Uingereza na baadae ya wenyewe kwa wenyewe, Uingereza ilidumu kama kinara wa dunia kutokana na vita nyingi alizopigana ulimwenguni kote, Ujerumani isingekua hivi kama sio vita ya kuwaunganisha Wajerumani wote, Italia kamwe isingekua moja kama sio vita ya kuunganisha miji yao yote, Uhispania ingekua ya Waarabu kama sio vita Iliyopigwa Iberia kote.

Vivyo hivyo Saudia bila kupigana na Ottoman kamwe isingekua nchi tunayoijua leo, Ottomani bila umahiri wa kivita wasingeweza kutawala dunia, China bila vita wasingekuwepo walipo leo, Japan bila vita ya muda mrefu wasingefika hatua ya kuwa tishio kwa dunia, mifano iko mingi lakini ieleweke wazi kuwa maendeleo ya kisiasa kwa sehemu yamechangiwa na vita.

Hii vita kama yalivyo mambo mengine haipiganwi bila kulipia gharama, na gharama hii haiji kama fedha tu la, watu wamekufa, miundombinu inaharibika, chumi zinatetereka, vikwazo vinaongezeka na taswira ya Urusi inaharibika, ndio na hiyo ndio gharama za kuhakikisha Urusi inakuwa salama. Vita hii si tu inatuma ujumbe kwa NATO kuwa Urusi hawataki kuchezewa pia inaweka bayana wako ‘serious’ kiasi gani linapokuja suala la usalama. Watu huweza dhani wamekurupuka lakini huu ni mpango wa muda mrefu, walijua hii siku itafika na NATO walijua hii siku inakuja.

Wakati NATO na washirika wao wanaiadhibu Urusi kwa vikwazo, nchi inayoshika nafasi ya pili kwa kuwa na uchumi mkubwa duniani China ipo tayari kuisaidia Urusi kuepuka vikwazo mpaka sasa tayari wameshasaini mkataba wa ‘ushirikiano bila kikomo’ sasa bidhaa zote zilizowekewa vikwazo ulaya zitauzwa China. Madai yao na Taiwan yanakaribia kufanana na ya Urusi kule Ukraine, hivyo China inaufanyia kazi ule msemo wa kiswahili unaosema “wema hauozi”, kwa maana ndani ya muda mchache nao watakua kwenye harakati za kuichukua Taiwan na watahitaji mshirika wa kuwaunga mkono, mshirika gani bora kuliko yule anaeongoza kwa mabomu ya nyuklia?

India nchi ambayo 60% ya silaha zake zinatokea Urusi hawajalaani wala kuungana na waMagharibi kuwawekea vikwazo sababu wanaelewa waMagharibi sio watu wa kuaminika, Brazil moja ya nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi wamejitenga na vikwazo dhidi ya Urusi. Africa pia hatuko nyuma kwa kuzingatia kuwa nusu ya silaha zote Africa zinatoka Urusi tumeamua kuwa ‘neutral’ na kutoweka vikwazo kwa Urusi katika mzozo wa huu tangu 2014.

Wakati dunia inailaumu Urusi kwa kinachoendelea inasahau kua Vita hii ni kama ya Marekani kule Iraq 2003 ni kama ile ya NATO nchini Libya mwaka 2001, ni kama ya Israel kule palestina tangu mwaka 1948, ni kama ya Ufaransa Algeria miaka ya 1950. wote wanapambania maslahi ya mataifa yao wote wanahakikisha usalama wa mataifa yao japo kwenye michakato hiyo vita haikwepeki na ndio asili ya mambo, Duniani vitu vyote ni vichache upatapopata jua kuna mtu kakosa, upotezapo jua kuna mtu kapata hatuwezi kushinda wote, ni aidha unashinda au unapoteza hakuna sare katika mchezo wa maisha.

NINI HATMA YA URUSI NCHINI UKRAINE?
Kimkakati haitawezekana kwa Urusi kuikalia Ukraine kwa nguvu (occupation) kwa muda mrefu na hii ni kutokana na sababu kuu mbili;

Moja, Warusi wameshindwa kupata ‘sapoti’ ya kutosha toka kwa raia wa Ukraine wenyewe. Kama alivyosema Machiavelli baba wa sayansi ya siasa kuwa unapovamia nchi ya kigeni ni lazima uigawe ili uitawale, lazima uungane na makundi dhaifu ili kulishinda lile lilo na nguvu. Kwa muktadha wa Ukraine Urusi kaungana na watu wa Donetsk na Luhansk kuishinda serikali kyiv lakini wamekosa sapoti ya wananchi walio wengi wa Ukraine na hii imesababishwa na kushindwa kwao kutumia vyombo vya habari kuhalalisha uvamizi wao. WaMagharibi wamewapiga bao kwenye hili maana kila mtu anawaonea huruma Ukraine na kuiona Urusi ni mvamizi badala ya mkombozi kama Urusi wanavyopenda kuonekana.

Mbili, idadi ya wanajeshi wa Urusi ndani ya Ukraine haitoshi kudhibiti nchi nzima ya Ukraine na watu wake milioni 40. Jeshi la Urusi lina askari zaidi ya milioni moja na kumi na nne elfu lakini katika uvamizi wake Ukraine inakadiriwa kupeleka 150,000 tu. Idadi hii ya askari haitoshi kudhibiti miji yote ya Ukraine na watu wake takribani milioni 40. Hii inatosha kuashiria kuwa Urusi hawakusudii kuikalia Ukraine.

NI YAPI MALENGO YA PUTIN?
Kama ambavyo Putin anaiita hii vita kuwa ni ‘Oparesheni maalum’ na wala si vita kamili, Putin kaingia Ukraine akiwa na malengo yake kadhaa katika hayo kuikalia kwa nguvu si moja ya malengo.

Mosi, Wanataka Ukraine iwe ‘neutral’ isiwe chini ya ushawishi wa Ulaya, kuhakikisha hili linatokea wanalenga kuivuruga Ukraine. Wameanza kwa kuigawa 2014 walipoichukua Crimea, na sasa wamezitambua jamhuri mbili mpya za Donetsk na Luhansk ambazo inatazamiwa baadae watazichukua zijiunge na Urusi.

Pili, wanataka kupunguza uwezo wa jeshi la Ukraine (de-militarization), malengo haya ni sawa na yale yaliyowasukuma waMarekani kuivamia Iraq mwaka 2013 na ndio yaleyale yanayowasukuma Israel kuishambulia Syria kila leo. Urusi inahofia kuona Ukraine panakua nyumbani kwa makombora ya waMagharibi. Sasa dunia inafanya tafiti za kina kugundua na kuendeleza ‘Hypersonic missiles’ Ukraine kujiunga NATO kutatoa fursa kwa Marekani kuyaweka humo, itachukua dakika 7 tu kwa kombora tokea Kyiv kushambulia Moscow. Suala hili halikubaliki kwa Urusi ndio maana wanalenga kupunguza kabisa uwezo wa jeshi la Ukraine.

Tatu, Kubadili serikali Ukraine na kusimika ile itakayolinda maslahi ya Urusi. Putin anawaita waNazi akina Zelensky (rais wa Ukraine) na wenzake walio madarakani sasa na moja ya lengo lake kuingia Ukraine ni kuwafurusha waNazi wote. Tafsiri yake anataka kubadili serikali aweke ile itakayokua na maslahi nae. Malengo haya yakitimia Putin atatoka Ukraine lakini ataendelea kuitazama kwa karibu kuhakikisha hawakengeuki maslahi ya Moscow.

NAFASI YA NATO KATIKA VITA HII
Katika huu mzozo Putin ana karata ya dhahabu, NATO hawataingilia kwa kuogopa vita ya tatu ya dunia. Inaaminika tangu mwaka 1985 Urusi walitengeneza mfumo unaoitwa ‘mkono mfu’ au ‘Dead Hand’ kwa kiingereza, mfumo huu wa Urusi hutuma makombora ya nyuklia kiotomatiki kwa nchi yoyote itakayo kuwa imeishambulia Urusi hata wakiua makamanda wote wa ngazi za juu au kuangamiza makao makuu ya jeshi. Mfumo huu unaweza kutambua shambulio la Nyuklia na lilipotoka na kurudisha mashambulizi huko yaliko tokea.

Hii inaipa Urusi usalama maana NATO wanaelewa fika wakikosea hesabu kivyovyote ulaya hapatakalika.

View attachment 2140687

View attachment 2140688

View attachment 2140689

View attachment 2140690

View attachment 2140691
Mkuu mbona kuna kitu umekiacha kutolea ufafanuzi Zelensky anasema kufeli kwa mazungumzo basi vita hii itakuwa ya 3 ya dunia, Ni kwa vipi hiyo vita itatokea? nani yuko nyuma ya Ukraine kwa hiyo vita? lakini Biden kasema vita ya 3 itapigwa katika ardhi ya urusi na sio Ukraine., hemu tiririka hapa icho kitendawili kikoje?

Lakini Jana Russia ametoa masaa ili Ukraine aweze ku-surrender lakini Ukraine wamekataa jambo lenye mfano huo, tiririka hapa ni kitu gani hii hasa hawa Ukraine wanategemea kwenye hii vita? Ivi NATO tayari wapo Ukraine kwenye vita lakini hawajaonyesha baya kwenye medias kwamba wapo mzigoni?
 
Umeeleza uzuri mkuu yoda, ila kama ingewezekana kueleza lwa mujibu wa sheria za kimataifa ingekuwa nzuri sana.
Kuhusu mipaka baharini kujua umbali na mamlaka ya nchi katika maeneo hayo ya bahari inatumika United Convection Law of the Sea (UNCLOS, 1994).

Kwenye hii Convection au makubaliano ya kimataifa yamegawanya sehemu za maji na bahari kama hivi
1.Inland waters
Haya ni maji ya mito na maziwa katika nchi.

2.Territory water
Hapa nchi inatakiwa imiliki maili zisizopungua 12 kuanzia Baseline ya maji.

3.Contigious Zone
Hapa nchi uchukua eneo la maji ya bahari kuanzia Baseline na livuke territory water na lisizidi umbali wa mile 24.

4.Economic Exclusive Zone (EEZ).
Ni eneo la bahari ambalo nchi umiliki mpaka umbali usiozidi mile 200.

5. Continental Shelf
Ni eneo baada ya mile 200 kutoka usawa wa mwanzo wa maji (Baseline) ambapo nchi iliyo karibu na bahari inaweza ikatumia eneo hili kwa tafiti za kisayansi au shughuli za utumiaji wa rasilimali katika miamba.

6.High Sea
Hii ni eneo la bahari kuu na hakuna mmiliki wa eneo hili.
Huku hata nchi ambayo haijazungukwa na bahari wanaweza wakafanya shughuli zao zozote bila kusumbuliwa.

Baseline ni eneo ambalo maji yakitoka au kupwa au maji mafu(Low Tide) huanzia ndipo huo umbali au mstari huanzia.

Kutokana na makubaliano ya Umoja wa mataifa kuhusu bahari (UNCLOS) nchi sio lazima ichukue maili zote 12 za territory water na Contigious zone. Kama nchi haina uwezo wa kusimamia inaweza ikachukua hata maili 3 na kama ina uwezo ichukue hata zote 12.
 
Inasikitisha Sana mtu anaandika upupu na watu wanamshabikia anyway , mda utatupa majibu sahihi kama huyo Putin atawatisha NATO au watamfurumusha...!!
Ungekuja na hoja tungekuwa na mjadala unaojenga.
 
Kuhusu mipaka baharini kujua umbali na mamlaka ya nchi katika maeneo hayo ya bahari inatumika United Convection Law of the Sea (UNCLOS, 1994).

Kwenye hii Convection au makubaliano ya kimataifa yamegawanya sehemu za maji na bahari kama hivi
1.Inland waters
Haya ni maji ya mito na maziwa katika nchi.

2.Territory water
Hapa nchi inatakiwa imiliki maili zisizopungua 12 kuanzia Baseline ya maji.

3.Contigious Zone
Hapa nchi uchukua eneo la maji ya bahari kuanzia Baseline na livuke territory water na lisizidi umbali wa mile 24.

4.Economic Exclusive Zone (EEZ).
Ni eneo la bahari ambalo nchi umiliki mpaka umbali usiozidi mile 200.

5. Continental Shelf
Ni eneo baada ya mile 200 kutoka usawa wa mwanzo wa maji (Baseline) ambapo nchi iliyo karibu na bahari inaweza ikatumia eneo hili kwa tafiti za kisayansi au shughuli za utumiaji wa rasilimali katika miamba.

6.High Sea
Hii ni eneo la bahari kuu na hakuna mmiliki wa eneo hili.
Huku hata nchi ambayo haijazungukwa na bahari wanaweza wakafanya shughuli zao zozote bila kusumbuliwa.

Baseline ni eneo ambalo maji yakitoka au kupwa au maji mafu(Low Tide) huanzia ndipo huo umbali au mstari huanzia.

Kutokana na makubaliano ya Umoja wa mataifa kuhusu bahari (UNCLOS) nchi sio lazima ichukue maili zote 12 za territory water na Contigious zone. Kama nchi haina uwezo wa kusimamia inaweza ikachukua hata maili 3 na kama ina uwezo ichukue hata zote 12.
Nakubaliana nawe mia fil’ mia.

Mpaka wa Urusi na Uturuki ulokuwa ukieleza ni matokeo ya makubaliano ya nchi zote mbili mwaka 1978. Sababu ya makubaliano hayo ni kuwa haki za umiliki wa bahari kwa Uturuki kwenye EEZ zinafikia mpaka maji ya Urusi, wakaona wakae chini wakubaliane.

BTW umeeleza vizuri.
 
Mkuu mbona kuna kitu umekiacha kutolea ufafanuzi Zelensky anasema kufeli kwa mazungumzo basi vita hii itakuwa ya 3 ya dunia, Ni kwa vipi hiyo vita itatokea? nani yuko nyuma ya Ukraine kwa hiyo vita? lakini Biden kasema vita ya 3 itapigwa katika ardhi ya urusi na sio Ukraine., hemu tiririka hapa icho kitendawili kikoje?

Lakini Jana Russia ametoa masaa ili Ukraine aweze ku-surrender lakini Ukraine wamekataa jambo lenye mfano huo, tiririka hapa ni kitu gani hii hasa hawa Ukraine wanategemea kwenye hii vita? Ivi NATO tayari wapo Ukraine kwenye vita lakini hawajaonyesha baya kwenye medias kwamba wapo mzigoni?
Mkuu vita ya tatu ya dunia itahusisha wakubwa wa Dunia kijeshi Urusi, NATO (kama itaendelea kuwepo) na China. Nani atakua na nani dhidi ya nani hilo tulipe muda. Ila kwa hakika litakua janga kubwa sana kuwahi kutokea (Mungu atuepushe).
Kusema itapigwa kwenye ardhi ya Urusi si sawa, naamini itapiganwa Kote huku mapambano makali yakiwa Urusi, Ulaya, Marekani na China.

Ndiyo, Urusi walitoa ultimatum wakiitaka Ukraine kuisalimisha Mariupol ili Urusi wawaache wananchi na askari wa Ukraine waondoke Mariupol, Ukraine wamekataa matakwa hayo wamechagua kuendelea kupigana.

NATO hawajaingia kwenye hii vita ila wanawaunga mkono Ukraine kwa kuwatumia fedha na silaha hatari. Jeuri ya Ukraine inatoka kwa nchi za Magharibi zinazoifadhili kwa kuwapa silaha.
Matumaini waliyonayo Ukraine ni kwamba kwakuwa Urusi imewekewa vikwazo vya kiuchumi wanakadiria mpaka mwezi wa tano Urusi watakuwa wameshaishiwa rasilimali za kuendelea kufadhili hii vita hivyo itawalazimu kufikia makubaliano ya amani rahisi kwa Ukraine kuliko yalivyo sasa.
Kwahiyo wanafanya kila wanachoweza kuhakikisha wanachelewesha ushindi wa Urusi kwa kadri wanavyoweza mkuu.
 
Kwa namna nyingine una-sound kwamba:, makombora ya Urusi yanaaweza fika kokote kule aliko adui ila makombora ya US hayawezi fika Moscow bila kuwa ndani ya UKRAINE ndiyo maana US anaitaka Ukraine😂😂.
Una MAHABA japo unakata wengine wawe neutral.
 
Back
Top Bottom