Nimesononeshwa sana na matokeo ya mitihani Kidato cha Nne ya Mwaka huu. Ni dhahiri kwamba kila mwaka kunakuwa na wanafunzi wanaofeli, lakini hili la 66% ya watahiniwa kufeli (kupata Division Zero) limeniuma sana.
Kuna sababu nyingi.....
kuanzia migomo ya walimu, watumishi wa umma kutishiwa nyau na serikali dhaifu, kiasi hata wengine kung'olewa meno. siasa kwenye elimu, hasa mijadala ya kishabiki ya wabunge wa ccm wanapokuwa bungeni kwa kuwa na tabia ya kusifia kila kitu kwa kauli za kijuha za 'kiwango cha ufaulu kimeongezeka ...tunaipongeza serikali' mambo yote ya namna hiyo.
lakini baya zaidi ni hili la utitiri wa vitabu vya rejea.
wakati siye tukisoma O'Level kulikuwa na vitabu dizaini moja tu. Vitabu vya Taasisi zetu adhimu...Taasisi ya Elimu Tanzania na Taasisi ya Kukuza Mitaala Tanzania. baada ya utandawazi na ubinafsishaji na nyonyaji na soko huria kumeibuka makanjanja wanaojifanya wanaandika vitabu vya maswali na majibu...moja wapo ni huyu jamaa anajiita Nyambari Nyangwine. Namshukuru Mungu sikuwahi kusoma vitabu vyake na hakika sitakuja kumshauri mtu avinunuwe. Haiwezekani kitabu kikawa na maswali na majibu tu halafu ukategemea kikusaidie kufaulu. hata kama utafaulu utakuwa bogazi tu kwa sababu huna maarifa kichwani.
Kwa kuwa waTZ tupo kama tumerogwa, basi hatuna budi tuchezee madini, tuchezee oembe za ndovu, tuchezee kila kitu, lakini TUSICHEZEE ELIMU.
vitabu vya Nyambari na makanjanja wenzake vipigwe marufuku. Walimu wapewe staha zao. Turudi kwenye mstari. Vinginevyo tunatia aibu, dunia ya leo kuwa kuzalisha wahitimu ambapo idadi ya waliofeli ni kubwa kuliko waliofaulu.
Ngw'anangwa ninaongeza moja kwenye hivyo vitabu vya maswali na majibu, majibu yaliyowekwa mengi yamekosewa. Hivi vitabu vipigwa marufuku immediately.
Nimesikia Mh Waziri TBC akisema wanaenda retreat kutafuta majibu. Nitafarijika ikiwa kuna mtu atamshahuri asihangaike na retreat anatuingiza gharama ya bure (maana najua watalipana posho kubwa). Sababu zinaeleweka na wala hazihitaji retreat. Lakini la kushangaza ni kwa nini alipinga hoja ya Mbatia ambayo ilikuwa inaomba kutafuta majibu ya matatizo haya na sasa anakuja na retreat. At least akiwa muungwana awaombe radhi watanzania.