Vitabu vyangu bora vya nyakati zote. Vipi vyako?

Vitabu vyangu bora vya nyakati zote. Vipi vyako?

Nitumie namba nikutumie hicho kitabu unachotaka hapo juu alafu mimi nimetafsiri vitabu vingi sina

Vipo kwenye mfumo wa hard copy na soft copy
Mkuu hongera sana kwa
Kutafsiri vitabu.

Binafsi ningependa kusoma vitabu
Ulivyotafsiri. Kama hutajali waweza kunitumia?
 
Nilisahau kitabu kimoja cha muhimu sana, ambacho kimekuwa niko mtoto.

WHEN THERE IS NO DOCTOR cha DAVID WERNER.

Mama yangu alikuwa nesi, hiki kitabu alikuwa nacho nyumbani. Ni kitabu ambacho kinatoa muongozo wa magonjwa mbalimbali yale ya 'muhimu', dalili zake na matibabu yake. Kilitolewa miaka ya 1990 mwanzoni kabisa na David Werner, ambaye ni mtaalamu wa Afya ya jamii, ambaye kwa miaka mingi amefanya kazi ya kuelimisha jamii kuhusu masuala ya afya akiwa zaidi vijijini katika nchi zaidi ya 50 'maskini'. Nchi hizi, kwa ambao tumekaa vijijini, tunajua zina sifa moja, kumpata Daktari ni sawa na kutafuta sindano porini. Nadhani kwa uzoefu huu, ndipo Werner aliona umuhimu wa kuandika kitabu ambacho mtu anaweza kujitazama dalili zake na kujua nini hasa anachoumwa na afanye nini ili walau kupata ahueni ya haraka huku zikifanyika jitihada za kusafiri kwenda kumtafuta Daktari, ambayo kwa kawaida ni nje ya kijiji. Pia amependekeza dawa ambazo mtu anaweza zitumia. Lakini pia amependekeza dawa ambazo ni za kawaida katika mazingira ya nyumbani. Mfano, kutumia mchanganyiko wa maji ya vuguvugu na chumvi, kusukutua ili kutibu fizi iliyovimba. Nimekua na hardcopy, ila teknolojia ishukuliwe, sasa kuna softcopy.

Screenshot_20210731-100202.jpg
View attachment Where There Is No Doctor A Village Health Care Handbook by David Werner, Jane Maxwell, Carol T...pdf
 
Paula Paul nilikuwa impressed na idea yako ya kureview walau kitabu kimoja nilichosoma na kukipenda katika mwezi. I'm doing it now!.

Mwezi huu, nimesoma vitabu vitatu, viwili sikuvimaliza nadhani nitavisoma kwa muda mrefu zaidi, ila kimoja ndio nimekimaliza, nilipoanza sikutaka kukiweka chini. Hii hapa nimejaribu kufanya mapitio ya kitabu hicho.

Kitabu kinaitwa SECURING DEMOCRACY; MY FIGHT FOR PRESS FREEDOM AND JUSTICE IN BOLSONARO'S BRAZIL. cha GLEN GREENWARD.

Kitabu hiki kimetoka mwezi wa nne mwaka huu, 2021. Ukiniuliza nawezaje kukielezea kitabu hiki kwa sentensi moja, jibu langu ni hili; Jinsi gani vyombo vya haki vinaweza tumika kutimiza malengo ya kisiasa.

Screenshot_20210731-124127.png

0c49bf113b71af39a808d5cddabc7f41061772ef.jpeg


Mwaka 2014, wakati Edward Snowden anapuliza kipyenga na kuibua jinsi gani vyombo vya usalama vya Marekani (National Security Agency) na Uingereza Government Communications Headquarters (GCHQ) vinavyotumika, kinyume na sheria, kuwapeleleza raia wake, raia na viongozi wa nchi mbalimbali duniani, kama Brazil. Snowden, alipotaka kutoa habari hizi, alimtafuta Glenn Greenwald, aliyekuwa ni correspondent wa gazeti la the Guardian la Uingereza, mwaka 2013. Pengine swali, kwanini Greenwald?

Greenwald, ni Mmarekani, mwandishi wa Habari, ambaye kabla alikuwa na kampuni yake ya kisheria ambayo ilikuwa inajihusisha na mashtaka ambayo yamejikita kwenye haki zinazopatikana kutokana na mabadiliko ya kwanza ya katiba ya Marekani (First US Constitution Amendment, ya mwaka 1791, ambayo yaliweka masharti ambayo yanaikataza bunge la Marekani kutunga sheria ya kuanzisha dini maalumu ya taifa, au kutunga sheria itayozuia uhuru wa kuabudu, kuzuia uhuru wa maoni au habari; uhuru wa Wamerekani kukusanyika kwa amani). Baadae aliacha na kujikita kwenye uandishi wa habari ambao kimsingi ulikuwa ni zenye mlengo wa kupigania uhuru wa kisiasa, maoni na kuabudu. Kwa misingi hii, Snowden aliona huyu ni mtu sahihi, kumpa habari zake 'Snowden Files'. Mwaka 2014, alitoa kitabu kiitwacho No Place to Hide kuelezea mkasa mzima wa Snowden. Hapo ndipo nilipomfahamu na kuvutiwa sana na uandishi wake. Ambapo, kufuatia issue hii ya Snowden, ndipo ilipoanzishwa chombo cha Habari kiitwacho The Intercept, kikiwa na waandishi 'wa kweli' kama Jeremy Scahill, na Mehdi Hasan (kwa sasa hayupo), kikiwa na lengo la kufanya uandishi wa habari za Kichunguzi, bila kuwa na upande - Adversarial Journalism. Baada ya issue hii ya Snowden, Greenward alipata mtifuano mkubwa na serikali ya Uingereza na Marekani, na kuamua kusettle zaidi Brazil. Ambapo huko alianzisha tawi la intercept (Intercept Brazil). Na pia, alikutana na David Miranda na kufunga naye ndoa, in the course of life David, alikuja kuwa Diwani na hatimaye mbunge nchini Brazil.

Mwaka 2018, aliunganishwa na rafiki yake, Mbunge aitwaye Manuela, kuwa kuna mtu amehack mawasiliano ya mtandao wa Telegram (uliokuwa ukitumiwa na kuaminiwa na vigogo wa Brazil kuwa hauwezi kiwa hacked) ya mawaziri wa masuala ya katiba ya Brazil, Sergio Moro na Mwendesha Mashtaka Deltan Dellagnol. Katika Mawasiliano hayo ya zaidi ya miaka mitano, yanaonyesha ni jinsi gani, Moro na Dellagnol walivyokuwa wakiendesha operation kubwa katika historia ya Brazil, ya kupambana na rushwa iliyoitwa Operation Car wash. Uvujishaji huu, ni wa muhimu sana, sababu umetoa elimu na onyo kubwa sana kwenye jamii, juu ya tahadhari inapokuja suala la vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa masuala ya Rushwa au madawa ya kulevya n.k!

Brazili ni nchi ambayo kwa sababu za kihistoria (ukoloni), na baadae miaka ya 1960 , kuchangiwa na Marekani kufanya mapinduzi nchini humo na kuweka utawala wake, wa chama kimoja, wa kidikteta na kijeshi, ulifanyw tabaka la weupe ambao ni wachache kuwa ndio wamiliki wa kila kitu nchini humo, siasa, uchumi, biashara, vyombo vya habari, vyombo vya dola na mtandao wa biashara ya madawa ya kulevya. Wasio weupe (non-whites) ambao ndio wengi ni tabaka tawaliwa kwa miaka mingi. Kutokana na misingi ya utawala wa kijeshi, udiktea, maisha ya Brazil katika nyanja zote yametawaliwa na ubabe na rushwa katika kila eneo. Hali hii ilipotamalaki, wabrazil walichoshwa na tabaka la watawala - elite establishment. Na yeyote ambaye alikuwa akihubiri na kupambana na tabaka hilo, wabrazil walimuhusudu na kumpa support mtu huyo.

Falsafa hii ya kisiasa, ndio iliwatawala wabrazil; 'Anyone who is hated by the political system that we despise and the elites who control it, and who promises to burn it and them down to the ground, is on our side.'

Ndipo ilipotokea mwaka 2014, ilipoanzishwa Operesheni ya kupambana na wala rushwa, wakwepa kodi na watakatishaji fedha. Chini ya aliyekuwa Jaji katika mji wa Curitiba, Sergio Moro, (Jaji wa mahakama hii, unaweza mfananisha na Hakimu katika mahakama ya Kisutu hapa nchini kwetu kutokana na unyeti wa kesi zinazopelekwa pale). Kiongozi wa Operesheni hii alikuwa ni Mwendesha Mashtaka Deltan Dellagnol, na iliitwa Operation Car wash [emoji3]. Mamia ya watu walikamatwa, Mamilioni ya dola zililipwa mfano wakuu wa Shirika la mafuta Brazil, Petrobas walilipa takribani $ Mil 700, vigogo walifungwa, na hatimaye kigogo mkubwa zaidi alifungwa, Luiz Inácio Lula da Silva. Huyu alikuwa Rais wa Brazil mwaka 2003 hadi mwaka 2010. Wananchi waliiunga mkono Operesheni hii sababu 'maadui zao'-wala rushwa walikuwa wanaburuzwa mahakamani na Jaji Moro alikuwa ni shujaa wa taifa na 'Mungu Mtu'-kwa lugha yetu, tungesema aliupiga Mwingi.

Kwa sura ya nje, Operesheni hii, ilikuwa ni jambo la kitakatifu. Lakini, ambacho wabrazil hawakujua ni kuwa, hii ilikuwa ni harakati ya kisiasa, ya kumzuia Rais Mstaafu Lula, asiweze gombea uchaguzi wa 2018-ambaye ndiye alikuwa na 'uhakika' wa kushina na chama chake cha Mrengo wa kushoto cha Workers Party. Kufungwa kwake, kulimpa nafasi Jairo Bolsonaro, ambaye chama chake hakikuwa na nguvu, ambaye kihulka ni dikteta mwenye siasa kali za mrengo wa kulia. It went right, Bolsonaro mwaka 2019 alishinda Urais wa Brazil.
thumbs_b_c_936d2d79d414e2e3d830c6bdaa7c7105.jpg


Alipoingia Madarakani Bolsonaro, mwaka 2019, alimpa Moro nafasi ya waziri wa katiba na Usalama wa Taifa. Huyu ndiye alikuwa waziri, pengine, mtu mwenye mamlaka na wa kutisha zaidi brazil, sababu ya vyombo vilivyokuwa chini yake. Investigation, law enforcement, policing, domestic intelligence, financial monitoring, and electronic surveillance.

3006.jpg


Wakati nasoma kitabu hiki, nilipata mawazo pia, kama nia ilikuwa ni ya kisiasa, haiathiri ukweli kuwa walifanya makosa ya rushwa, seems I was too quick to conclude. Faili alizozitoa mdukuzi huyu kwa Greenwald, ziliibua mambo yafuatayo;

1. Dallagnol alikamata 'vidagaa' ambao walishinikizwa kutoa ushahidi dhidi ya Vigogo, ambao hatimaye walitiwa hatiani. Mfano, Vigogo wa Shirika la Petrobas.

2. Mwendesha Mashtaka (MM) na Jaji walishirikiana kuandaa Ushahidi dhidi ya washatakiwa ambao waliwalenga, na hatimaye jaji mwenyewe kuwafunga.

3. Tatu, walighushi nyaraka ambazo ziliwasilishwa kama ushahidi wa mashtaka.

4. MM na jaji walitengeneza jumbe za kughushi kwa lengo la kumchafua Rais Lula.

5. MM aliharibu ushahidi ambao ungetumiwa na washtakiwa kwenye utetezi wao.

6. MM na jaji walikuwa na mawasiliano wakati wote juu mwendendo wa kesi ambao ni kinyume na Sheria na maadili ya majaji.

Kimsingi, Jaji Moro hakuwa tu anashirikiana na Mwendesha Mashtaka, bali yeye ndiye alikuwa kiongozi, Bosi na Mchora mipango mkuu, wa kuwatia hatiani vigogo ambao mwishoni watamtia hatiani Lula; walifanikiwa. Na hatimaye Lula alifungwa miaka 9. Maana yake hakuweza shiriki uchaguzi, na lengo kuu la kisiasa lilifanikiwa- Bolsonaro alishinda Urais.

Ukipause hapa ukavuta kumbukumbu na kutafakari, unaweza kuona ni jinsi gani hata hapa nchini mwetu, yapo mashataka au Operesheni ambazo licha ya kuonekana zinafanya jambo sahihi lakini zimekuwa na malengo ya kisiasa nyuma yake-hii kwa nchini mwetu iko hasa ndani ya Chama Tawala, si kwa sababu wapinzani ni 'Malaika', bali hawana resources za kufanikisha.

Kisheria, jaji anapaswa awe huru na asiwe na upande wowote (When the judge loses impartiality, he ceases to be a judge.). Pili, Mashtaka yanapaswa yasaidiwe na ushahidi ambao haupaswi kuwa wa kughushi, udanganyifu au umepatikana kwa shurti. Haya yote ukiyaweka kwenye Muktadha unaona kuwa Operesheni hii, ilikuwa ni batili na waliofungea hawakufungwa kihalali. Na ilipaswa punde baada ya taarifa hii kutika, Moro kama waziri alipaswa kuwa amejiuzuru na kushtakiwa. Lakini kwa Brazil ni tofauti, a mafia state. Greenwald alipata mashambulizi ya kila namna, kutoka kwenye Serikali ya Rais Bolsonaro, Bolsonaro mwenyewe, wanaye ambao ni viongozi wakubwa wa kisiasa na propagandists wake, Waziri moro mwenyewe na vyombo vyake anavyo viongoza. Ilichukua zaidi ya mwaka, ndipo Moro alipojiuzuru (kutokana kuibuka hali ya kutiaminiana kisiasa kati yake na Rais Bolsonaro) na na Dellagnol (akitoa sababu ya afya ya familia yake).

Kwenye kitabu hiki, kuna mafunzo mawili makubwa, ambayo yote mawili ni tadhali/angalizo.

1. Operesheni zinazofanywa na vyombo vya dola, zinapswa sana kuwa na mazingira ya kuweza kumulikwa, ili kuhakikisha utii wa sheria.

2. Jamii, inapokuwa ina kiu kubwa ya mabadiliko, inahitaji iwe makini, sababu kuna uwezekano mkubwa wa harakati za kisiasa kutumia fursa hiyo kutimiza azma za kisiasa-madaraka.

Haki huchelewa, lakini baadae hupatikana, Rais Lula alitumia mwaka mmoja na nusu gerezani, na baadae mahakama kumuachia huru.

Nakusihi kisome kitabu hiki katika sura zake zote 9, kina mafunzo makubwa kuhusu mazingira ya uhuru wa vyombo vya habari duniani hasa nchi za Uingereza, Marekani na Brazil, Historia ya Brazil kisiasa-hada jinsi gani Marekani alivyosaidia kuwekwa misingi ya udikteta, ukatili, kutokuheshimu sheria (Sura ya 2), hali ya sasa ya kisiasa na kijamii ya Brazil chini ya Rais Bolsonaro na kumfahamu yeye mwenyewe binafsi (sura ya 5). Ila kama una 75% ya muda wako, basi soma Sura ya Tatu, ya nne, ya sita na ya saba (ambazo ndio hasa zimeelezea kuhusu Ubakaji huu wa misingi ya haki). Kama Una 50% ya muda wako, basi soma sura ya tatu ja ya sita. Kama una muda mchache zaidi, na unataka kupata picha ya jumla, lakini inayojitosheleza, basi soma sehemu ya Utangulizi (Preface), ametoa summary ambayo imeelezea maudhui na story yote kwenye sakata hili. Ila kwa ujumla, ni kitabu chepesi kusoma, kina kurasa 280 tu, na kilivyoandikwa, ni kama unatazama filamu ya kusisimua ya kipelelezi kuhusu siasa.

Red Giant I hope you will this too!
 
Paula Paul nilikuwa impressed na idea yako ya kureview walau kitabu kimoja nilichosoma na kukipenda katika mwezi. I'm doing it now!.

Mwezi huu, nimesoma vitabu vitatu, viwili sikuvimaliza nadhani nitavisoma kwa muda mrefu zaidi, ila kimoja ndio nimekimaliza, nilipoanza sikutaka kukiweka chini. Hii hapa nimejaribu kufanya mapitio ya kitabu hicho.

Kitabu kinaitwa SECURING DEMOCRACY; MY FIGHT FOR PRESS FREEDOM AND JUSTICE IN BOLSONARO'S BRAZIL. cha GLEN GREENWARD.

Kitabu hiki kimetoka mwezi wa nne mwaka huu, 2021. Ukiniuliza nawezaje kukielezea kitabu hiki kwa sentensi moja, jibu langu ni hili; Jinsi gani vyombo vya haki vinaweza tumika kutimiza malengo ya kisiasa.

View attachment 1875113
View attachment 1875114

Mwaka 2014, wakati Edward Snowden anapuliza kipyenga na kuibua jinsi gani vyombo vya usalama vya Marekani (National Security Agency) na Uingereza Government Communications Headquarters (GCHQ) vinavyotumika, kinyume na sheria, kuwapeleleza raia wake, raia na viongozi wa nchi mbalimbali duniani, kama Brazil. Snowden, alipotaka kutoa habari hizi, alimtafuta Glenn Greenwald, aliyekuwa ni correspondent wa gazeti la the Guardian la Uingereza, mwaka 2013. Pengine swali, kwanini Greenwald?

Greenwald, ni Mmarekani, mwandishi wa Habari, ambaye kabla alikuwa na kampuni yake ya kisheria ambayo ilikuwa inajihusisha na mashtaka ambayo yamejikita kwenye haki zinazopatikana kutokana na mabadiliko ya kwanza ya katiba ya Marekani (First US Constitution Amendment, ya mwaka 1791, ambayo yaliweka masharti ambayo yanaikataza bunge la Marekani kutunga sheria ya kuanzisha dini maalumu ya taifa, au kutunga sheria itayozuia uhuru wa kuabudu, kuzuia uhuru wa maoni au habari; uhuru wa Wamerekani kukusanyika kwa amani). Baadae aliacha na kujikita kwenye uandishi wa habari ambao kimsingi ulikuwa ni zenye mlengo wa kupigania uhuru wa kisiasa, maoni na kuabudu. Kwa misingi hii, Snowden aliona huyu ni mtu sahihi, kumpa habari zake 'Snowden Files'. Mwaka 2014, alitoa kitabu kiitwacho No Place to Hide kuelezea mkasa mzima wa Snowden. Hapo ndipo nilipomfahamu na kuvutiwa sana na uandishi wake. Ambapo, kufuatia issue hii ya Snowden, ndipo ilipoanzishwa chombo cha Habari kiitwacho The Intercept, kikiwa na waandishi 'wa kweli' kama Jeremy Scahill, na Mehdi Hasan (kwa sasa hayupo), kikiwa na lengo la kufanya uandishi wa habari za Kichunguzi, bila kuwa na upande - Adversarial Journalism. Baada ya issue hii ya Snowden, Greenward alipata mtifuano mkubwa na serikali ya Uingereza na Marekani, na kuamua kusettle zaidi Brazil. Ambapo huko alianzisha tawi la intercept (Intercept Brazil). Na pia, alikutana na David Miranda na kufunga naye ndoa, in the course of life David, alikuja kuwa Diwani na hatimaye mbunge nchini Brazil.

Mwaka 2018, aliunganishwa na rafiki yake, Mbunge aitwaye Manuela, kuwa kuna mtu amehack mawasiliano ya mtandao wa Telegram (uliokuwa ukitumiwa na kuaminiwa na vigogo wa Brazil kuwa hauwezi kiwa hacked) ya mawaziri wa masuala ya katiba ya Brazil, Sergio Moro na Mwendesha Mashtaka Deltan Dellagnol. Katika Mawasiliano hayo ya zaidi ya miaka mitano, yanaonyesha ni jinsi gani, Moro na Dellagnol walivyokuwa wakiendesha operation kubwa katika historia ya Brazil, ya kupambana na rushwa iliyoitwa Operation Car wash. Uvujishaji huu, ni wa muhimu sana, sababu umetoa elimu na onyo kubwa sana kwenye jamii, juu ya tahadhari inapokuja suala la vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa masuala ya Rushwa au madawa ya kulevya n.k!

Brazili ni nchi ambayo kwa sababu za kihistoria (ukoloni), na baadae miaka ya 1960 , kuchangiwa na Marekani kufanya mapinduzi nchini humo na kuweka utawala wake, wa chama kimoja, wa kidikteta na kijeshi, ulifanyw tabaka la weupe ambao ni wachache kuwa ndio wamiliki wa kila kitu nchini humo, siasa, uchumi, biashara, vyombo vya habari, vyombo vya dola na mtandao wa biashara ya madawa ya kulevya. Wasio weupe (non-whites) ambao ndio wengi ni tabaka tawaliwa kwa miaka mingi. Kutokana na misingi ya utawala wa kijeshi, udiktea, maisha ya Brazil katika nyanja zote yametawaliwa na ubabe na rushwa katika kila eneo. Hali hii ilipotamalaki, wabrazil walichoshwa na tabaka la watawala - elite establishment. Na yeyote ambaye alikuwa akihubiri na kupambana na tabaka hilo, wabrazil walimuhusudu na kumpa support mtu huyo.

Falsafa hii ya kisiasa, ndio iliwatawala wabrazil; 'Anyone who is hated by the political system that we despise and the elites who control it, and who promises to burn it and them down to the ground, is on our side.'

Ndipo ilipotokea mwaka 2014, ilipoanzishwa Operesheni ya kupambana na wala rushwa, wakwepa kodi na watakatishaji fedha. Chini ya aliyekuwa Jaji katika mji wa Curitiba, Sergio Moro, (Jaji wa mahakama hii, unaweza mfananisha na Hakimu katika mahakama ya Kisutu hapa nchini kwetu kutokana na unyeti wa kesi zinazopelekwa pale). Kiongozi wa Operesheni hii alikuwa ni Mwendesha Mashtaka Deltan Dellagnol, na iliitwa Operation Car wash [emoji3]. Mamia ya watu walikamatwa, Mamilioni ya dola zililipwa mfano wakuu wa Shirika la mafuta Brazil, Petrobas walilipa takribani $ Mil 700, vigogo walifungwa, na hatimaye kigogo mkubwa zaidi alifungwa, Luiz Inácio Lula da Silva. Huyu alikuwa Rais wa Brazil mwaka 2003 hadi mwaka 2010. Wananchi waliiunga mkono Operesheni hii sababu 'maadui zao'-wala rushwa walikuwa wanaburuzwa mahakamani na Jaji Moro alikuwa ni shujaa wa taifa na 'Mungu Mtu'-kwa lugha yetu, tungesema aliupiga Mwingi.

Kwa sura ya nje, Operesheni hii, ilikuwa ni jambo la kitakatifu. Lakini, ambacho wabrazil hawakujua ni kuwa, hii ilikuwa ni harakati ya kisiasa, ya kumzuia Rais Mstaafu Lula, asiweze gombea uchaguzi wa 2018-ambaye ndiye alikuwa na 'uhakika' wa kushina na chama chake cha Mrengo wa kushoto cha Workers Party. Kufungwa kwake, kulimpa nafasi Jairo Bolsonaro, ambaye chama chake hakikuwa na nguvu, ambaye kihulka ni dikteta mwenye siasa kali za mrengo wa kulia. It went right, Bolsonaro mwaka 2019 alishinda Urais wa Brazil.
View attachment 1875118

Alipoingia Madarakani Bolsonaro, mwaka 2019, alimpa Moro nafasi ya waziri wa katiba na Usalama wa Taifa. Huyu ndiye alikuwa waziri, pengine, mtu mwenye mamlaka na wa kutisha zaidi brazil, sababu ya vyombo vilivyokuwa chini yake. Investigation, law enforcement, policing, domestic intelligence, financial monitoring, and electronic surveillance.

View attachment 1875125

Wakati nasoma kitabu hiki, nilipata mawazo pia, kama nia ilikuwa ni ya kisiasa, haiathiri ukweli kuwa walifanya makosa ya rushwa, seems I was too quick to conclude. Faili alizozitoa mdukuzi huyu kwa Greenwald, ziliibua mambo yafuatayo;

1. Dallagnol alikamata 'vidagaa' ambao walishinikizwa kutoa ushahidi dhidi ya Vigogo, ambao hatimaye walitiwa hatiani. Mfano, Vigogo wa Shirika la Petrobas.

2. Mwendesha Mashtaka (MM) na Jaji walishirikiana kuandaa Ushahidi dhidi ya washatakiwa ambao waliwalenga, na hatimaye jaji mwenyewe kuwafunga.

3. Tatu, walighushi nyaraka ambazo ziliwasilishwa kama ushahidi wa mashtaka.

4. MM na jaji walitengeneza jumbe za kughushi kwa lengo la kumchafua Rais Lula.

5. MM aliharibu ushahidi ambao ungetumiwa na washtakiwa kwenye utetezi wao.

6. MM na jaji walikuwa na mawasiliano wakati wote juu mwendendo wa kesi ambao ni kinyume na Sheria na maadili ya majaji.

Kimsingi, Jaji Moro hakuwa tu anashirikiana na Mwendesha Mashtaka, bali yeye ndiye alikuwa kiongozi, Bosi na Mchora mipango mkuu, wa kuwatia hatiani vigogo ambao mwishoni watamtia hatiani Lula; walifanikiwa. Na hatimaye Lula alifungwa miaka 9. Maana yake hakuweza shiriki uchaguzi, na lengo kuu la kisiasa lilifanikiwa- Bolsonaro alishinda Urais.

Ukipause hapa ukavuta kumbukumbu na kutafakari, unaweza kuona ni jinsi gani hata hapa nchini mwetu, yapo mashataka au Operesheni ambazo licha ya kuonekana zinafanya jambo sahihi lakini zimekuwa na malengo ya kisiasa nyuma yake-hii kwa nchini mwetu iko hasa ndani ya Chama Tawala, si kwa sababu wapinzani ni 'Malaika', bali hawana resources za kufanikisha.

Kisheria, jaji anapaswa awe huru na asiwe na upande wowote (When the judge loses impartiality, he ceases to be a judge.). Pili, Mashtaka yanapaswa yasaidiwe na ushahidi ambao haupaswi kuwa wa kughushi, udanganyifu au umepatikana kwa shurti. Haya yote ukiyaweka kwenye Muktadha unaona kuwa Operesheni hii, ilikuwa ni batili na waliofungea hawakufungwa kihalali. Na ilipaswa punde baada ya taarifa hii kutika, Moro kama waziri alipaswa kuwa amejiuzuru na kushtakiwa. Lakini kwa Brazil ni tofauti, a mafia state. Greenwald alipata mashambulizi ya kila namna, kutoka kwenye Serikali ya Rais Bolsonaro, Bolsonaro mwenyewe, wanaye ambao ni viongozi wakubwa wa kisiasa na propagandists wake, Waziri moro mwenyewe na vyombo vyake anavyo viongoza. Ilichukua zaidi ya mwaka, ndipo Moro alipojiuzuru (kutokana kuibuka hali ya kutiaminiana kisiasa kati yake na Rais Bolsonaro) na na Dellagnol (akitoa sababu ya afya ya familia yake).

Kwenye kitabu hiki, kuna mafunzo mawili makubwa, ambayo yote mawili ni tadhali/angalizo.

1. Operesheni zinazofanywa na vyombo vya dola, zinapswa sana kuwa na mazingira ya kuweza kumulikwa, ili kuhakikisha utii wa sheria.

2. Jamii, inapokuwa ina kiu kubwa ya mabadiliko, inahitaji iwe makini, sababu kuna uwezekano mkubwa wa harakati za kisiasa kutumia fursa hiyo kutimiza azma za kisiasa-madaraka.

Haki huchelewa, lakini baadae hupatikana, Rais Lula alitumia mwaka mmoja na nusu gerezani, na baadae mahakama kumuachia huru.

Nakusihi kisome kitabu hiki katika sura zake zote 9, kina mafunzo makubwa kuhusu mazingira ya uhuru wa vyombo vya habari duniani hasa nchi za Uingereza, Marekani na Brazil, Historia ya Brazil kisiasa-hada jinsi gani Marekani alivyosaidia kuwekwa misingi ya udikteta, ukatili, kutokuheshimu sheria (Sura ya 2), hali ya sasa ya kisiasa na kijamii ya Brazil chini ya Rais Bolsonaro na kumfahamu yeye mwenyewe binafsi (sura ya 5). Ila kama una 75% ya muda wako, basi soma Sura ya Tatu, ya nne, ya sita na ya saba (ambazo ndio hasa zimeelezea kuhusu Ubakaji huu wa misingi ya haki). Kama Una 50% ya muda wako, basi soma sura ya tatu ja ya sita. Kama una muda mchache zaidi, na unataka kupata picha ya jumla, lakini inayojitosheleza, basi soma sehemu ya Utangulizi (Preface), ametoa summary ambayo imeelezea maudhui na story yote kwenye sakata hili. Ila kwa ujumla, ni kitabu chepesi kusoma, kina kurasa 280 tu, na kilivyoandikwa, ni kama unatazama filamu ya kusisimua ya kipelelezi kuhusu siasa.

Red Giant I hope you will this too!
Uchambuz mzr sana mkuu, ningekuwa mpenzi wa siasa siasa ningefaidi sana bt ndo hvyo tena mm na siasa mbali mbali, tuchambulie na vya kina Robert kiyosaki, robin sharma, etc.
 
Uchambuz mzr sana mkuu, ningekuwa mpenzi wa siasa siasa ningefaidi sana bt ndo hvyo tena mm na siasa mbali mbali, tuchambulie na vya kina Robert kiyosaki, robin sharma, etc.
Shukrani mkuu. It's an irony, unaitwa Vladimir Lenin na hupendi siasa[emoji3]
 
Mwezi August nimesoma vitabu vitatu, Cha kwanza ni Collapse chake Jared Diamond ambacho kinaelezea kwanini jamii mbalimbali zilianguka na baadhi zilifanikiwa kusurvive pale zilipokumbwa na madhila mbalimbali ya kimazingira (hiki sijakimaliza, nikimaliza nitakichambua pia); vitabu viwili vyote ni riwaya. Riwaya ya Kwanza ni yake Jeffrey Archer iitwayo Kane and Abel (hii inaelezea watu wawili waliozaliwa kwenye mazingira ya aina mbili tofauti kabisa na kisha kufanikiwa kukutana katika masuala ya kibiashara na hatimaye kuwa na ugomvi mkubwa sana kati yao ma familia zao) na ya pili ni Changes yake Ama Ata Aiddo. Hii ya Changes ndio nitaizungumzia hapa.

CollageMaker_20210917_185526119.jpg


Riwaya hii ya Changes imeandikwa na Mama Ama Ata Aidoo. Mama huyu mghana ni mwanaelimu na mwanaharakati wa usawa wa kifursa kwa wanawake, pia aliwahi kuwa waziri wa elimu wakati wa utawala wa Jerry Rawlings. Kwenye fasihi Afrika, ana mchango mkubwa hasa kwa wanawake ambapo kupitia Taasisi yake ya Mbaasem, anasaidia waandishi wa vitabu wanawake.

Riwaya hii alinipendekezea rafiki yangu mmoja kwenye mtandao wa Twitter baada ya kuona nukuu yake. Nukuu hiyo ilinivutia. Na kuamua kukisoma. Nikuhakikishie ni Riwaya inayofunza sana hasa kwa mwanaume.

Simulizi kwa Ufupi: Katika riwaya hii iliyotoka mwaka 1991, inaemuelezea Esi ambaye ni mwanamke wa kiafrika, msomi wa shahada ya Takwimu na mtumishi wa serikali ya Ghana. Esi ameolewa na Oko, ambaye ni mwalimu. Lakini Esi anachoshwa na maisha ya ndoa kwa sababu mbili moja, anaona kuwa Mmewe anamuhitaji muda mwingi kiasi anaona kuwa anashindwa kufurahia kazi yake kama kusafiri au semina na wafanyakazi wenzake na pili anaona kuwa yeye hana sauti kwenye ndoa kiasi kuwa anaona hata mwili wake hana mamlaka nayo kama vile mmewe kumlazimisha kingono pasi na kutokuwa na utashi—marital rape. Hatimaye Esi anapeana talaka na mmewe. Miezi michache baadae, Esi anaolewa na mwanaume tajiri aitwaye Ali kama mke wa pili. Katika ndoa hii Esi anaishi kwake na anaonana muda mchache na Ali, ambaye anakuwa kwa mkewe wa kwanza muda mwingi, hii inampa uhuru Esi aliokuwa akiukosa kwa Oko. Lakini baadae Esi anajikuta akihisi kuwa kuna jambo analikosa; nalo ni kuwa na mumewe muda mwingi, kukosa mtoto nyumbani na ile hali ya unyumbani. Upweke huu unampa njia panda ambayo anakosa namna ya kuitatua.

Kwanini nimeipenda hii Riwaya. Sababu kuu ni moja, licha ya kuwa mimi ni feminist na Riwaya hii inajaribu kuonyesha jinsi gani wanawake wasomi wanahangaika kufit katika tamaduni za kiafrika, kiislam pamoja na ndoa; lakini mitazamo ya wanawake (sijui kama ni wote) juu ya masuala ya mapenzi, familia na ndoa; ndio sababu ya kuvutiwa na Riwaya hii, na ndio sababu ya kusema, wanaume ndio inatufaa zaidi kuisoma Riwaya hii.

Nyakati nyingi pindi akikumbwa na matatizo au kuwa njia panda, Esi—akiwakilisha usasa— alimkibilia bibi yake. Ni mafunzo ya bibi yake—akiwakilisha mifumo ya kihafidhina.
Wakati Esi akimiani kuwa mwanamke anatakiwa aolewe kwa mapenzi, kwa mtazamo wa kihafidhina, ni kuwa mapenzi hayapaswi kumuongoza mwanamke kwenye kuolewa:

These days, young people don’t seem to know why they marry or should marry.’
‘What are some of the reasons, Nana?’
‘Ah, so you want to know? Esi we know that we all marry to have children
‘But Nana, that is such an old and worn-out idea! Children can be born to people who are not married.’
‘Sure, sure, but to help them grow up well, children need homes with walls, a roof, fire, pots.’
‘Oh Nana. But one person can provide all these things these days for a growing child!’
‘Maybe ... yes... Yes, my lady. We also marry to increase the number of people with whom we can share the joys and the pains of this life.’
‘Nana, how about love?’
‘Love? … Love? … Love is not safe, my lady Silk, love is dangerous. It is deceitfully sweet like the wine from a fresh palm tree at dawn. Love is fine for singing about and love songs are good to listen to, sometimes even to dance to. But when we need to count on human strength, and when we have to count pennies for food for our stomachs and clothes for our backs, love is nothing. Ah my lady, the last man any woman should think of marrying is the man she loves.’

Pia wakati mwingine ndoa hutazamwa kama fadhila anayoitoa kwa mwanaume baada ya jitihada za muda mrefu za kumtongoza.

Esi’s main problem was that she was easily bored. And no woman ever caught a man or held him by showing lack of interest. Esi had known that she would have to work up some enthusiasm in her relationship with men. ‘But how?’ she had kept asking herself. Now looking back she didn’t dare admit, even to herself, that perhaps what she had felt for Oko in the first years of their married life was gratitude more than anything else. Gratitude that in spite of herself he had persisted in courting her and marrying her.
‘Not many women are this lucky …’ Esi could hear her grandmother’s voice. ‘And who told you that feeling grateful to a man is not enough reason to marry him?

Mtazamo huu ulinifikirisha sana, kwa sababu sijaoa, ilinifanya nikumbuke maex wangu walioolewa na kuanza kuanalyse sababu zao za kuolewa; pia mashemji zangu na maisha yao ya ndoa zao, dada zangu na maisha ya ndoa zao na watu wengine ninaowafahamu ambao hunishirikisha masuala yao;

My lady, the world would die of surprise if every woman openly confessed the true reasons why she married a certain man.

It came home to me that, wengi wa wanawake wanaoolewa huwa na agenda zao za siri (si lazima ziwe mbaya), mapenzi huwa ni kisingizio tu.

Nilifanya utafiti wangu binafsi; mfano nilimuuliza nesi ambaye ni rafiki yangu baada ya kushare quotation hii, alicheka na kuniambia, ni kweli kuwa wanawake wengi huolewa kwa fadhila, fedha, huruma au malipizo.

Ni kitabu kilichonifungua sana macho juu ya mitazamo ya wanawake kwenye mapenzi na familia.
 
Back
Top Bottom