Vitendo SACCOS - kukopeshana bila riba

Vitendo SACCOS - kukopeshana bila riba

Zipo taasisi zinazokopesha hapahapa tz moja wapo wanaitwa kutaiba. Wanatumia systema hio ya bila riba. Lkn binafsi naungana na wadau wengine wanaosema ni yaleyale yanabdirishwa majina tuu.
Moja unapewa pesa mkononi kwa makubaliano.
Na nyingine unapewa bidhaa mkononi kwa makubaliano. (IB)

Ukopeshaji wetu ni tofauti.

Tunakopesha kwenye mradi tu ambao nasi tunakuwa wabia. Kwa maana hiyo faida na hasara ni kwa wote.

Pia kwa wanachama tunakopesha mikopo ya dharura zilizoainishwa. Bila riba.

Nakuhakikishia VTS hatuna riba.
 
Ukopeshaji wetu ni tofauti.

Tunakopesha kwenye mradi tu ambao nasi tunakuwa wabia. Kwa maana hiyo faida na hasara ni kwa wote.

Pia kwa wanachama tunakopesha mikopo ya dharura zilizoainishwa. Bila riba.

Nakuhakikishia VTS hatuna riba.
Bi Mrembo, Mzee Abdul akianza kukusanya pesa za mradi wa excavator nijulishe, maana nategemea kusafiri kiduuuchu, ntakuwa kwenye simu sipatikani. Email me.
 
Fursa ya kuwekeza kwa Mtanzania yeyote aliopo ndani na nje ya Tanzania.

Sasa unaweza kuwasiliana na waliokwisha wekeza kwetu na kujipatia majibu mubashara.

Kidole kimoja hakivunji chawa.

Hii nimeipenda.

Mimi shahidi wa kwanza. Nimewekeza miradi yako yote. Wa kwanza ulikuwa wa sand mining nikapata ntaji wangu na 50% faida ndani ya miezi miwili.

Mradi mwengine ni wa bodaboda, nashukuru pesa nilizowekeza zimerudi na sasa nasubiri faida ule wa pili. Ule wa kwanza na kula faida.

Mradi wa sand mining wa pili pia nimewekeza na napata malipo mara kwa mara.

Nnatumai wapo wengine waliowekeza na wapo humu JF wajitokeza waelezee ukweli.

Hongera sana Mzee Abdul kwa kuwa yu muwazi na mkweli naahidi hata pesa yangu ya mwisho ntawekeza kwake.

Ahsante sana Bi Zainab Tamim, keep up the good work ya kum keep busy huyo mzee, day and night. Kwi kwi kwi teh teh teh.
 
Hii nimeipenda.

Mimi shahidi wa kwanza. Nimewekeza miradi yako yote. Wa kwanza ulikuwa wa sand mining nikapata ntaji wangu na 50% faida ndani ya miezi miwili.

Mradi mwengine ni wa bodaboda, nashukuru pesa nilizowekeza zimerudi na sasa nasubiri faida ule wa pili. Ule wa kwanza na kula faida.

Mradi wa sand mining wa pili pia nimewekeza na napata malipo mara kwa mara.

Nnatumai wapo wengine waliowekeza na wapo humu JF wajitokeza waelezee ukweli.

Hongera sana Mzee Abdul kwa kuwa yu muwazi na mkweli naahidi hata pesa yangu ya mwisho ntawekeza kwake.

Ahsante sana Bi Zainab Tamim, keep up the good work ya kum keep busy huyo mzee, day and night. Kwi kwi kwi teh teh teh.

Asante kwa kujitokeza.

We kiajuza huachi ukware, hiyo day and night inahusu nini. Pambaf.
 
Update...

Wadau,

Kwanza tunashukuru AlhamduliLlah mkutano umeenda vizuri na umeisha salama.
Tunafuraha kuwafahamisha wadau wote kuwa mkutano umeenda vizuri kabisa na umefana sana.

Tulianza kwa kukaribishwa na Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Vitendo...

Kisha nikaongea kidogo mimi kuwakaribisha wajumbe wote...

Baada ya hapo ikaanza semina ya ushirika iliotolewa na Afisa Ushirika wa wilaya ya Kibaha, Bwana Msangi. Semina ilikuwa ndefu kidogo lakini ilitoa mwangaza mpana wa nini SACCOS, vipi iongozwe, nini haki za Wana SACCOS na vipi haki zao zinalindwa na kusimamiwa na sheria rasmi za vyama vya ushirika na vipi serikali inasimamia vyama vya ushirika.

Yalizuka maswali mengi kiasi na hususan lilipoongelewa suala la kuendesha saccos kwa riba.

Hatimae kila mtu akaelewa kuwa hakuna tatizo kubwa isipokuwa ni namna tu ya mfumo wa uendeshaji SACCOS bila riba utavyofanyika.

Hilo na mengine yaliojiri mtajionea mkanda wa video.

Baada ya semina ukaanza mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa muda. Ulioendeshwa na kusimamiwa na Afisa Ushirika kama sheria zinavyotaka.

Hatimae tukapata kamati ya uongozi wa muda ya uanzilishi wa Vitendo SACCOS Ltd., kwa mujibu wa Sheria na chini ya usimamizi wa Afisa Ushirika wilaya ya Kibaha.

Kamati hio ya muda ikamteua Katibu wa kwanza wa muda wa Vitendo SACCOS Ltd., chini ya usimamizia wa Afisa Ushirika wilaya ya Kiabaha.


Mambo yote hayo yapo kwenye video na picha. Zitakapokuwa tayari, tutapandisha video YouTube na kwenye tovuti yetu (inayoanadaliwa kwa sasa) tutapandisha video na picha.

Tunakaribisha maswali.

Asanteni na karibuni kujiunga na Vitendo SACCOS Ltd. kwa faida ya wengi.

Abdul Ghafur
Mwenyekiti
Mobile / Whats-app 0625249605
 
Wanachama na Wana hisa wa Vitendo SACCOS wanategemea kuzindua na kuanza kazi miradi yao mitatu mipya hivi karibuni.

Miradi hiyo mitatu yote iliyo nje ya Vitendo SACCOS lakini imebuniwa na Wana VTS na itaendeshwa kwa njia ya kuchangiana mitaji na kugawana faida kwa muda maalum.

Miradi inayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni ni, mradi wa ukumbi wa sinema na mikutano, unaoweza kukaa watu 100, unatambulika kama mradi wa Vitendo Cinema Hall. Huu ni mradi wa muda mfupi kwa waliowekeza. Inatarajiwa kuwa mara tu utakapoanza hivi karibuni, wote waliowekeza kwenye mradi huu kuanza kupata mafao yao na faida ndani ya miezi sita.

Mradi mwingi unaotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni unaojulikana kwa jina la Vitendo Bricks, mradi huu ni wa muda wa kati. Mradi huu utajumuisha utengenezaji wa matofali ya aina tofauti tofauti na pia kwa siku za mwanzoni unatarajiwa kuwa na bidhaa tofauti zinazotokana na mchanga, kokoto na simenti.

Mradi huo pia unatarajiwa kuwa na uwezo wa kutengeneza bidhaa zote za ujenzi zinazotokana na simenti, kokoto na michanga.

Mradi mwengine kuanza hivi karibuni ni mradi wa kijiko (excavator) ya kuchimba na kupakilia mchanga. Mradi huu upo kwenye matayarisho ya mwisho na unategemewa kuanza hivi karibuni. Huu ni mradi unaotarajiwa kuanza kulipa mafao ya wawekezaji na kukamilika ndani ya siku 365 za kazi.

Tunawakaribisha nyote kujiunga na Vitendo SACCOS Ltd. Kwa faida ya wengi.

Vitendo SACCOS imedhamiria kufanya mabadiliko ya uwekezaji Tanzania. Na sasa unaweza kuanza kuwekeza na VTS kwa kuanzia Shillingi 10,000 tu.

Kwa maelezo zaidi, wasiliana nasi kwa simu au whatsapp namba 0625249605.

Ahsanteni sana.
 
Vitendo SACCOS inaendeleaje?

[emoji252] [emoji479]
 
Wish I was with you guys.

Nililiona pilau kwenye picha kwenye group. Count me in Zainab, nitilie pesa za membership, sina access ya account ya Mpesa wala Tigo for now.

Will talk to you on the phone.

Keep it up.
Una updates za hii kitu?
 
Kama nilivyoahidi katika post yangu hii: Fursa ya kuwekeza kwa msingi mdogo kuwa tutafungua mjadala kujadili vipi tunaweza kuanzisha mpango wa kukopa / kukopesha / kuwekeza bila riba.

Duniani kwa sasa kumekuwa na wengi wanaousikia na wengineo wameshaanza kuutumia mpango wa "islamic Banking", lakini si wengi wanaoufahamu unafanyaje kazi ili kuhakikisha unakopa unakopesha na kuwekeza bila kutoa au kupokea riba.

Mpango wa "Islamic Banking" kwa sasa kwa hapa kwetu Tanzania unafanyika kwa njia za benki kubwa kubwa tu na hatujaona ukihusisha vikundi vidogo vya kukopa na kuwekeza kwa njia hiyo isiyokuwa na riba.

Njia sahihi za kukopeshana bila riba zinawezekana kwa vikundi vidogo vidogo na havihitaji ulazima wa kufanya hivyo kupitia benki ambako huwa kuna milolongo na ukiritimba wa hapa na pale.

Mfumo wa "Islamic Banking" umekuwa ni biashara kubwa sana nje ya nchi za Kiislam na haumaanishi kuwa ni Waislam tu wanaoweza kushiriki. Mfumo huu ni kwa yeyote.

Nafungua mjadala huu kwa lengo la kuanzisha kikundi kitakacho anzisha mpango huu rasmi kwa faida ya wengi.

Yeyote anaehisi kuwa anaufahamu au atapenda kushiriki katika mpango huu kuanzia awali anaweza kuwasiliana nami kwa PM au kwa whatsapp 0625249605.

Karibuni Tujadili.

UPDATE 1 (02-05-2017)

Wadau wote,
Ninapenda kuwafahamisha kuwa jana tarehe 1-5-2017 tulikuwa na kikao kuhusu kuanzishwa kwa SACCOS yetu mpya.

Wahudhuriaji walikuwa wa kutosha. Kati yao walikuwepo (wengi wao) ambao ni wawekezaji tayari katika miradi yetu ya awali (nje ya SACCOS tarajiwa), wengine ni wawekezaji watarajiwa. Pia tulimualika Mwenyekiti wa serikali yetu ya mtaa wa Vitendo, ndugu Salehe Dibebile, tulimualika pia na Katibu wa vyama vya ushirika vya kata ya Misugusugu bwana Kussi. Pia tulikuwa na wawekezaji wawili ambao tayari wana miradi yao (nje na yetu) ya machimbo ya michanga.

Kwa kifupi, tulitambulishana, tukajadili ushirika tunaoufikiria na tukakubaliana (bila kuwa na hoja za kupingana). Hoja zilizotamalaki zilikuwa ni za kupeana elimu zaidi ya ushirika na faida zake...

Ikaamuliwa tuuanzishe ushirika haraka iwezekanavyo...

Ikaamuliwa tuanze kwa kukusanya masharti ya saccos tofauti na samples zake, members wote wapitie ili tuweze kuwa na SACCOS yetu tarajiwa haraka iwezekanavyo...

Imeamuliwa pia Abdul Ghafur awe Mwenyekiti wa muda mpaka ushirika wetu utakapo sajiliwa ndiyo kutakapokuwa na masharti ya uchaguzi rasmi. Watakaojiunga wote watakuwa wajumbe mpaka hapo sheria na kanuni rasmi zitakapo patikana.

Pia Imeamuliwa kuanzia sasa kila atakaependa kujiunga kutakuwa na ada ya kiingilo itakayo saidia katika gharama za usajili na mpaka hapo tutapokuwa na masharti na kanuni zetu rasmi zilizopitishwa na wnahama wote kwa ujibu wa sheria...

Ushirika tutakaoanzisha utafata sheria na kanuni zote za nchi na sheria za vyama vya ushirika za Tanzania...

Ushirika hautakuwa na ukomo wa watakaojiunga mpka hapo itakapotangazwa rasmi baada ya kupata kanuni zilizokubalika na wanahama wote, kujiunga kutakuwa wazi kwa yeyote anaekubalika kisheria, awe popote Tanzania au duniani...

Ada ya kiingilo kwa sasa ni shillihgi 10,000 (elfu kumi) ambazo zitatumwa kwa Mwenyekiti wa muda kwa njia ya Mpesa. Namba ni 0756803528 jina Ghafur Abdallah Mohamed.

Mahesabu yote ya chama yatakuwa wazi kwa wanachama wote, kwa sasa yatapatikana kupitia group la whatsapp la waliojiunga.

Kila atakaelipa ataingizwa kwenye group mahususi la whatsapp litalokuwa kwa ajili ya wanachama tu waliojiunga katika ushirika wetu mpya.

Tumeanza kupokea ada za viingilio na hesabu zote zitapatikana kwenye group mpya ya wanachama walioingia kwa kulipia ada...

Uwe popote ulimwenguni unakaribishwa kujiunga kwa faida ya wote.

Group mpya imeshafunguliwa kwa jina la muda Vitendo SACCOS na members wawili waliolipia ada tayari tumepatikana, maelezo zaidi kwenye group mpya...

Ada ya kiingilo ni shillihgi 10,000 (elfu kumi) ambazo zitatumwa kwa Mwenyekiti wa muda kwa njia ya Mpesa. Namba ni 0756803528 jina Ghafur Abdallah Mohamed

Nawajulisha wote watakaotaka kujiunga muanze kwa kulipia ada ili tufanikishe usajili kwa haraka.

Ili kujiunga, (kwa sasa) inatakiwa utupatie jina kamili, namba za simu, email address na ulipo na utume 10,000 kwa Mpesa.

SACCOS ITAENDESHWA KWA KUFATA MFUMO WA ISLAMIC FINANCE AND BANKING SYSTEM.

Tunakaribisha maswali.

Abdul
+255 625 249 605 (whatsapp)
mambo yakoke huko aisee ?

Inaendelea ?
 
Back
Top Bottom