Vitu 15+ unavyotakiwa kuacha kununua unapotimiza miaka 50

KING MIDAS

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2010
Posts
8,589
Reaction score
16,936
Wasalaam. Leo naongea na wazee wenzangu, team nakataa ndoa na timu tunda kimasihara tafadhalini mtulie.

1. JIEPUSHE KUKIMBIZANA NA FASHENI ZA VIJANA


Sio kila nguo ya vijana itakupendeza. Kumbuka kipindi hiki shape yako inakuwa imebadilika sana na haifanani tena na miili na maumbo ya vijana.

Kubali matokeo anza kuvaa kama umri wako na mwili wako ulivyo.
 
2. ANZA KUVAA NGUO ZISIZOHITAJI KUNYOOSHA, AU NGUO ZINAZO NYOOKA BILA KUPIGA PASI.



Tukatae tukubali, katika umri huu nguza za mwili huwa zimepungua na kamwili kameanza kuchoka na kasi imepungua.

Katik umri huu nguo ambayo kijana anainyosha kwa dakika 2 wewe utainyoosha kwa dakika 7. Bana matumizi ya umeme na uokoe muda.
 
1 Pombe kali
2 Michepuko(miss Buza atakutoa roho)
3 Touch phone(kimeo kinatosha 😂)
4 Raba kali
5 Toyota ist(hadhi ya Uber)
6 Chipsi kuku(nunua vumbi la Kongo)
7 Kulamba ice cream
8 Daladala ikijaa acha iende(utabanwa ujambe🤣)
 
9. USINUNUE NYUMBA KWASABABU NI NYUMBA, JIULIZE ITARUDISHA HIYO HELA BAADA YA MUDA GANI?


Biashara ya majengo (Real Estate) unaweza kufanya popote. Lakini kumbuka thamani ya ardhi imetofautiana kati ya eneo moja hadi nyingine, sababu ikiwa ni vigezo mbalimbali, miundombinu, usalama, neighbourhood na utamaduni wa eneo husika.
Ni ngumu kupata nyumba ya AIRBNB Vingunguti Kiembembuzi
 
1O. ACHA TABIA YA KUNUNULIA WATU POMBE.

Umeingia bar, kila mtu unamwagizia anachokunywa. Tabia ya kujenga heshima bar imekwisha pitwa na wakati. Hela zako tumia vizuri, saidia wahitaji waliopo kwenye jamii inayokuzunguka.
 
11. DALADALA, BAJAJ NA BODABODA NI BIASHARA PASUA KICHWA.


Hata kama watu wako wa karibu wamekushawishi ufanye biashara hii, jiulize mara mbili, je utaweza kukimbizana na watu wenye akili kumi? Avute bangi, anywe gambe, agonge mademu, aweke akiba na ale hapohapo .

Bora ununue trekta, biashara unaongea mwenyewe, dereva unampa posho tu na mafuta.
 
12. USINUNUE KITU SABABU TU RAFIKI YAKO ANACHO.


Enzi za ujana iliitwa FOMO, Fear Of Missing Out. Hii ilikuwa hofu ya kuonekana umeachwa nyuma na fasheni. Muda umeenda sasa, acha kuangalia wenzako watakuonajr,nunua kutokana na mahitaji yako.
 
14. EPUKA KUWATEMBELEA WATOTO WAKO NA KUKAA KWAO KWA MUDA WA SIKU NYINGI.


Ndio ni wanao, watembelee kaa siku mbili rudi kwako. Sio unaenda kwa watoto wako halafu unahamia huko..
Waswahili wanasema hata tamu hukinai. Na pia mwanasanaa mzuri ni yule anayetoka jukwaani wakati mashabiki wa sanaa yake wanaihitaji zaidi.
 
15 JIEPUSHE NA VISERENGETI BOY/ VIBENTEN.

VivuIana Vidogo havina na haviwezi kuwa na mapenzi ya dhati na mijishangazi, vinafuata tu utelezi na Hela. Akiona humpi anaweza hata kukuletea majambazi ndani.
 
16. ACHA KUNUNUA VITU UKIWA BAR

Zimepita sufuri umenunua, imekuja pasi unanunua. Kumbuka, ubora ni jambo la muhimu kuzingatia kabla hujanumua kitu.
Hii itakusaidia kuifanya nyumba yako kutokuwa na makorokoocho mengi yasiyo na kazi wala yasiyo na matumizi.
 
17. PUNGUZA KUNUNUA MARUNDO YA VIPODOZI.


Sasa umri wako umeenda, acha kununua marundo ya vipodozi. Kuwa na vipodozi vyako vichache tu, vitakavyokufanya uonekane nadhifu na simply natural beauty
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…