Rohombaya
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 13,067
- 10,393
Dah....Mkuu ningekushauri ukazanie zaidi kwenye kuagiza magari...lakini kwenye mambo ya ushauri wa kiufundi waachie wataalam...maana unaharibu tu....samahani Mkuu[emoji41]1. Kushuka kwenye mteremko gari ikiwa neutral, hii inasababisha kuzuia oil kusambaa na kusababisha msuguano kukosa kilainishi hicho na kupelekea kusagika kwa baadhi ya sehemu.
2. Kukanyaga mafuta kabla ya kubadilisha gear. Hii ni hasa kwa vijana unawasha gari na kuanza kupiga resi, kitendo hicho husababisha msuguano mkali na unaweza kuharibu sehemu za engine.
3. Kubadilisha gear wakati gari bado inatembea, hakikisha unakamata brake kwanza ndipo ubadilishe gear.
4. Kuweka neutral kweye taa nyekundu kwenye taa za barabarani, watu wengi hufanya hivyo ili kusave mafuta lakini kiasi unachosave ni kidogo sana kulinganisha na gharama ya tatizo unaloweza tengeneza, tumia brake ili gari liendelee kuwa kwenye drive mode, madhara hutokea unapoweka na kutoa neutral.
5. Kuweka parking kabla gari halijasimama kabisa. Hakikisha gari limesimama kabisa ndipo unaweka parking.
6. Kuendesha gari kwa speed ya juu kabla ya engine kupata joto, hasa kipindi cha baridi hakikisha engine imepata joto ili kuwezesha oil kusambaa kwenye sehemu zote.
7. Kuacha mafuta yakiwa machache katika tank, tank la mafuta linatakiwa kuwa full au kuwa nusu lakini sio chini kabisa. kuwa full kunasaidia engine na sehemu nyingine kuwa cool.
Imetolewa na Kimomwe Motors (T) Ltd, waagizaji wa magari. 0746267740
View attachment 1263795
Sent using Beretta ARX 160