Vituko nilivyowahi kuviona kwenye sahili (interviews) vya kukatisha tamaa

Vituko nilivyowahi kuviona kwenye sahili (interviews) vya kukatisha tamaa

Miaka 10 iliyopita nilifanya interview TANROAD Kili, baada ya interview one of the panelist alinijulisha kwa simu kuwa nimepita lakini ningepigiwa simu na wahusika ili uje uanze kazi.

Nilivyokuja kufuatilia nikaambiwa kuna vidada vilikuwa field 3 yrs pale ndio wamechukuliwa na infact tulikuwa nao siku ya interview.
 
interview yangu ya kwanza ilikua kwenye NGO , tulikua watu watano na walitaka watu watatu, nilikua najuana na watu watatu kati ya hao tano, na ndo tuliopita after 3 days tukapewa hadi job offer letters, wakasema watatuambia lini tukareport kazini, tulikaa miezi na miezi tukajasikia tu mbona watu washaanza kazi kitambo na hawakuepo hata kwenye interview , kazi tulioifanyia sisi interview ikaishiwa kufanywa na watu ambao hawakuepo kabisa. [emoji706][emoji706]

Sent from my SM-G9550 using JamiiForums mobile app
Inasikitisha sana asee..


#MaendeleoHayanaChama
 
Kwa uzoefu wangu katika saili nyingi ambazo nimesaili vijana, Taifa hili tuna changamoto kubwa sana ya uelewa wa mambo unakuta mtu kasoma special school na ana Bachelor ya Computer Engineering unamuuliza swali what is Operating System anabaki anashangaa akitoka njee anasema wana watu wao, Binafsi nimeapa nilipata kazi kwa haki na nitatenda haki siku zote japo majaribu ni Mengi na Mikuki ni Mingi, ila kuna vijana wana ufaulu mzuri ila interview wanachemka sana, sikatai uwepo wa upendeleo katika baadhi ya taasisi mbalimbali lakini rai yangu kwa vijana fanya maandalizi vizuri kafanye usaili notion za kusingizia watu wamepangwa achana nazo.

Sent from my SM-N950N using JamiiForums mobile app
 
Pilot
Aircraft engineer
Marine and nautical engineer
Drilling Engineer
Well completion engineer
Fishing engineer
Mining Engineer
Robotic and Automation engineer.
Cyber security expert.
Software developer.
Artificial Intelligence expert.
Reliability and Mechanical Engineer.
ROV operator.
Automation engineer.
Instrumentatio engineer
Electric Engineer.
Mechanical Engineer.
Civil Engineer
nk, nk, nk.

Taifa halitoi direction kwa vijana wasome nini, matokeo yake vijana huishia kutia huruma na kunyenyekea wapumbavu.
Hizo fani za uhandisi zina tatizo gani boss?
 
Nawasalimu wote kwa jina la Jamhuri ya Muungano.

Vijana tunapitia mengi ya kukatisha tamaa, lakini leo niwape machache ya vituko vya sahili nilivyowahi kuviona kwa macho yangu.

1. Tuliitwa kwenye usahili mikoa ya nyanda za juu kusini, basi kwa furaha na kujiamini nikapaki vitu huyooo nikafika siku moja kabla nikaripoti na nikakuta watu wengine, siku ya pili yake tukawahi sana tu,basi wakati tunaendelea kusubili wasahili wakafika na gari aina ya cruiser wakashuka kama saba hivi, sisi tukajua wote ni wasahili, lahaula kumbe wengine ni wasahiliwa kama sisi na tuligundua baada ya kuona wanakuja kukaa kwa wasahiliwa. Baada ya usahili matokeo nakuachia utabiri mwenyewe.

2. Tuliitwa kwenye usahili wa serikali basi wakati tunaendelea kusahiliwa basi kuna kijana sijui wa mkubwa gani akawa ameondoka eneo lile, basi unaambiwa alitafutwa balaa na mwisho wa siku matokeo yumo.

3. Kuna siku tunasubiri usahili,kuna vijana wakawa wanasema wameagizwa kuja hapo kama utani vile,aisee haikuwa utani matokeo yalitujulisha.

4. Tumefanya usahili,matokeo watu ambao hawakuwepo kwenye usahili ndio waajiliwa.

Dah mambo ni mengi sana,ushauri wangu vijana msio na connection mkaze sana na kumuomba Mungu,lakini naamini kila kitu kinawezekana.

Kama una kisa ni ruhusa kuweka.
Mambo ya Usahili yanatisha
 
Ni wiki Tatu zilizopita niliitwa kwenye Interview KCB BANK MAKAO MAKUU DAR nafasi ya CORPORATE AFFAIRS MANAGER,kufika pale tupo Wasailiwa 12 na mmoja yeye anafanyia Usaili akiwa Mwanza(huyu ni staff wa KCB BANK MWANZA)!!![emoji1787]na katika 11 tulio Dar Wasailiwa wawili nao wadada ni wa palepale ndani KCB BANK Maka Makuu[emoji1787]Usaili tuliambiwa saa 8 mchana lakini ukaanza saa 10 jioni(ilikuwa ni Written Interview).Yaani tangu tumefika pale wale wadada(wa HR na Head wa Communications)wakawa wanajizungushazungusha weeee nikajua tu hapa USANII unachezwa!!!kuja kuleta hiko ki-swali Chao chenyewe eti (I)WHAT IS EVENT PLANNING??(II)PROCEDURES ZA EVENT PLANNING(III) EXPLAIN SHORTY ON THOSE PROCEDUCES OF EVENT PLANNING??
yaani ni ki-swali ambacho nilikijibu ndani ya dakika 10 japo wao walisema dakika 30!!!juzi napokea Email kutoka kwa huyo Dada HR anaitwa MONDE LUSHAKO eti nilipata below PASS MARK hivyo sijachaguliwa kwa Oral nilicheka mpaka nikapaliwa na Wine yangu!! [emoji1787][emoji1787] yaani ni wasanii walikuwa na mtu wao wahuni wale[emoji1787][emoji1787]na mimi nina uhakika kile ki-swali chao nilikipata chote 100 kwa 100!!nilimjibu kwenye Email yake kwamba WAMUOGOPE MUNGU na waache tabia ya kusumbua watu waje kwenye Interview wakati nafasi tayari wana mtu wao!!!hebu imagine wengine mpo Dar mnafanya Interview na mwingine(staff wa ndani KCB Bank humohumo) anafanyia Usaili akiwa Mwanza peke yake [emoji1787][emoji1787]na kwa tuliofanyia Dar tulifanya pia na wadada wawili wa palepale KCB BANK tena wakiwa na Uniform za KCB [emoji1787][emoji1787]Nchi ngumu sana hii
 
Miaka 10 iliyopita nilifanya interview TANROAD Kili, baada ya interview one of the panelist alinijulisha kwa simu kuwa nimepita lakini ningepigiwa simu na wahusika ili uje uanze kazi.

Nilivyokuja kufuatilia nikaambiwa kuna vidada vilikuwa field 3 yrs pale ndio wamechukuliwa na infact tulikuwa nao siku ya interview.
Sipati picha ulivyo vunjika moyo.
 
Aisee inahuzunisha kusumbuana hata mahali pa interviews huku wengine wakitoka mbali safari ndefu+fares, huku ukijua kabisa una watu wako(interviewers) wana dhambi sana.
Wanataka jamii ione wanatangaza nafasi za kazi kumbe kazi zenyewe zimejaa.
 
Kwa uzoefu wangu katika saili nyingi ambazo nimesaili vijana, Taifa hili tuna changamoto kubwa sana ya uelewa wa mambo unakuta mtu kasoma special school na ana Bachelor ya Computer Engineering unamuuliza swali what is Operating System anabaki anashangaa akitoka njee anasema wana watu wao, Binafsi nimeapa nilipata kazi kwa haki na nitatenda haki siku zote japo majaribu ni Mengi na Mikuki ni Mingi, ila kuna vijana wana ufaulu mzuri ila interview wanachemka sana, sikatai uwepo wa upendeleo katika baadhi ya taasisi mbalimbali lakini rai yangu kwa vijana fanya maandalizi vizuri kafanye usaili notion za kusingizia watu wamepangwa achana nazo.

Sent from my SM-N950N using JamiiForums mobile app
Heri wewe kama unatenda haki,ubarikiwe na kizazi chako,ila huku nje ni moto.
 
Back
Top Bottom